Anza kujitizama wewe kwanza

Surya

JF-Expert Member
Jun 7, 2015
8,378
12,573
Wana JF mie sina mengi ya kusema ila nina jambo moja tu la kusema kwenu. Ugumu huu wa maisha na kushindwa kwa mipango mbalimbali ambayo tunaipanga na kuifanyia kazi hapa duniani ni majibu tosha kua sisi sio wakamilifu. Mimi sio mkamilifu wewe pia sio mkamilifu.

Tuanze kujitizama sisi wenyewe matendo na tabia zetu. Mawazo na fikra zetu je yapo sahihi wakati wote? Hua tunakosea au hatukosei jambo.

Jambo kubwa ninalopenda kukusisitiza binadamu mwenzangu ni kwamba tujarbu kuzifundisha akili zetu zipate uelewa wa mambo, TUPENDE KUJIFUNZA.

Tupende kuja hapa jukwaa na kufundisha mambo mbali mbali ya kimaisha, huku tukiendelea kutafuta mbinu za kupata pesa huko uliko.

Tutumie utandawazi na teknologia hii ya mawasiliano kama nyenzo ya kujifunzia vitu mbali mbali. Tusipende kuangalia watu wakichekesha vitu visivyo na maudhui yoyote wala tusipende kusikiliza matatizo ya watu pasipo kuchambua kuna maudhui gani.

Tupende kujifunza ili hata mimi Surya wa mwaka huu, nibadilike na kuongeza kitu akilini ili mwaka ujao apatikane Surya mwingine.

Ni hayo tu.
 
Kama kifaru angekuwa n mchoraji kila picha ambayo angechora ingekuwa na pua yake katikati ya hio picha, 7bu pua imezidi usawa wa macho.

Unaona dunia vile ulivyo, ila ukiamua kubadili mtizamo wako inawezekana kabisa. Namna bora ya kujifunza n kutana wigo wa vitu unajua.

Mwsho;
Ujinga wa karne hii s kutojua soma na kuandika ila n kutokuwa tayari kulearn, kurelearn, na kuunlearn
 
Kama kifaru angekuwa n mchoraji kila picha ambayo angechora ingekuwa na pua yake katikati ya hio picha, 7bu pua imezidi usawa wa macho.

Unaona dunia vile ulivyo, ila ukiamua kubadili mtizamo wako inawezekana kabisa. Namna bora ya kujifunza n kutana wigo wa vitu unajua.

Mwsho;
Ujinga wa karne hii s kutojua soma na kuandika ila n kutokuwa tayari kulearn, kurelearn, na kuunlearn
True kabisa.
 
Kama kifaru angekuwa n mchoraji kila picha ambayo angechora ingekuwa na pua yake katikati ya hio picha, 7bu pua imezidi usawa wa macho.

Unaona dunia vile ulivyo, ila ukiamua kubadili mtizamo wako inawezekana kabisa. Namna bora ya kujifunza n kutana wigo wa vitu unajua.

Mwsho;
Ujinga wa karne hii s kutojua soma na kuandika ila n kutokuwa tayari kulearn, kurelearn, na kuunlearn
Dah hapo mwisho umemaliza na msemo wa mwandishi mashuhuri Alvin toffler kwenye. Kitabu chake cha future shock...I wish kila mtu angesoma hicho kitabu..Dah big up Mkuu
 
Kila mtu angechukua Muda akajitafakari japo dakika 10 kwa siku...Ingemsaidia sana..Tafakari matendo yako, tafakari maneno Yake...tafakari siku yako.

Tatizo hua tunasubiria tupate changamoto ndo tuanze kujitafakari Kwamba pale nilikosea....

Watu wasio tafakari..hu play victims huwalaumu wengine..hutegemea wengine wajitoe Sana kwao..

Usisahau pia kutafakari wema Wa Mungu maishani mwako...HILI.latakiwa kuwa lwa kwanza..

You will continue making the same mistakes untill you learn the lesson.
 
Kwa hiyo mkuu unatuambia kwamba tuache kutafuta connection pindi zinapoleak
 
Back
Top Bottom