OMARI Mohamed (22), mkazi wa Yombo jijini Dar es Salaam, amefikishwa katika Mahakama ya Wilaya ya Temeke kujibu, shtaka la kutaka kumuua msichana baada ya kukataa kumwingilia kinyume na maumbile.
Akisoma hati ya mashitaka, Inspekta Isaya Mwanga mbele ya Hakimu Aziza Kalili wa mahakama hiyo alidai kuwa,mshitakiwa alitenda kosa hilo Oktoba 10, mwaka huu katika majira ya saaa 2 usiku huko Yombo Kilakala.
Alidai baada ya mshitakiwa kumwambia mlalamikaji kuwa alikuwa anahitaji kumwingilia kinyume na maumbile mlalamikaji alikataa kufanyiwa kitendo hicho na ndipo Omari alimchoma kisu cha tumbo, mgongoni na kwenye ubavu jambo ambalo lilimsababishia kuzirai na kupoteza fahamu papohapo.
Alidai hali hiyo ilimfanya mlalamikaji apoteze fahamu papohapo na kukimbizwana wasamaria wema katika hospitali ya Taifa Muhimbili kwa matibabu zaidi.
Mlalamikaji baada ya siku mbili aliweza kupata fahamuna kueleza umma jinsi ilivyokuwa na mshitakiwa kwenda kukamatwa
Hata hivyo mshtakiwa alipotakiwa kujibu shtaka hilo, alikana na alipelekwa rumande kwa kukosa dhamana, na kesi imeahirishwa hadi Januari 7, mwaka huu itakapotajwa tena.
Source: www.Nifahamishe.com
Akisoma hati ya mashitaka, Inspekta Isaya Mwanga mbele ya Hakimu Aziza Kalili wa mahakama hiyo alidai kuwa,mshitakiwa alitenda kosa hilo Oktoba 10, mwaka huu katika majira ya saaa 2 usiku huko Yombo Kilakala.
Alidai baada ya mshitakiwa kumwambia mlalamikaji kuwa alikuwa anahitaji kumwingilia kinyume na maumbile mlalamikaji alikataa kufanyiwa kitendo hicho na ndipo Omari alimchoma kisu cha tumbo, mgongoni na kwenye ubavu jambo ambalo lilimsababishia kuzirai na kupoteza fahamu papohapo.
Alidai hali hiyo ilimfanya mlalamikaji apoteze fahamu papohapo na kukimbizwana wasamaria wema katika hospitali ya Taifa Muhimbili kwa matibabu zaidi.
Mlalamikaji baada ya siku mbili aliweza kupata fahamuna kueleza umma jinsi ilivyokuwa na mshitakiwa kwenda kukamatwa
Hata hivyo mshtakiwa alipotakiwa kujibu shtaka hilo, alikana na alipelekwa rumande kwa kukosa dhamana, na kesi imeahirishwa hadi Januari 7, mwaka huu itakapotajwa tena.
Source: www.Nifahamishe.com