Anxiety as CCM top organ holds meeting

BAK

JF-Expert Member
Feb 11, 2007
124,790
288,005
The CCM-NEC will also seek members' views on legal steps and disciplinary action to take against three former ministers who were involved in the $170 million Richmond Development Company scandal, in which the company was supposed to supply 100MW power to the national grid.

The NEC committee - which includes Mzee Rashid Kawawa, second Prime Minister of Tanzania, retired presidents Ali Hassan Mwinyi and Benjamin Mkapa - will most likely seek stern measures against the former ministers in President Jakaya Kikwete's government.

The three, Edward Lowassa, former prime minister, Nazir Karamagi, former minister for energy and minerals and Dr Ibrahim Msabaha, former minister for the East African Community, have been called to Butiama to explain what happened and why disciplinary action should not be taken against them.
 
Mimi sitegemei kitu toka huo mkutano wa CCM, labda suala la muafaka wa Zanzibar. Lakini mambo ya maendeleo kwa Mtanzania, hayo tusahau kwamba yataletwa na serikali ya CCM.

Kwasasa muhimu kwa mtu mmoja mmoja kutimiza wajibu wake huku juhudi zikifanywa za kuilazimisha serikali iache kuwaibia wananchi.

Kinachoendelea sasa ni sawa na baba kuiba uji wa mwanawe, huyo mtoto atakua kweli? Au ni sawa na daktari kuiba dawa za mgonjwa wake, kuna kupona hapo kweli?

Tusiwategemee sana hawa viongozi wetu maana wengi wao ni wasanii. Hata ukiongea nao, unagundua hapa tuna kazi kubwa sana mpaka tuje tupate maendeleo.

Wengine tunaombea kwa njia yoyote ile, serikali ya CCM ianguke. Tatizo tu ni je kweli kuna huo uwezekano kwasasa? Tusije tukawa fisi anayetegemea mkono wa mwanadamu utadondoka. Lazima tutengeneze mazingira ya kweli ambayo yataifanya CCM ianguke. JF ni sehemu moja wapo pa kuwaelemisha Watanzania jinsi viongozi wao walivyo fake. Bahati mbaya JF inawakilisha labda asilimia kumi tu ya walengwa. Tatizo ni namna ya kuwafikia hao asilimia 90.

Vyama vya upinzani na civil socities zinazunguka mjini tu na kuwaacha CCM wanatamba huko vijijini ambako ndio kuna wananchi wengi.

Kama CCM kweli wanataka kuwajibika basi Hosea, Mwanyika na wengine wote waliotajwa kwenye Richmond wawajibishwe mara moja, kabla ya kuanza na EPA.
 
Mimi sitegemei kitu toka huo mkutano wa CCM, labda suala la muafaka wa Zanzibar.


hata hilo suala la muafaka wa Zanzibar sidhani kama litapatiwa ufumbuzi hii ni kwa jinsi CCM walivyo na uchoyo wa madaraka lakini utekelezaji hanma kitu
 
Mimi sitegemei kitu toka huo mkutano wa CCM, labda suala la muafaka wa Zanzibar. Lakini mambo ya maendeleo kwa Mtanzania, hayo tusahau kwamba yataletwa na serikali ya CCM.

Kwasasa muhimu kwa mtu mmoja mmoja kutimiza wajibu wake huku juhudi zikifanywa za kuilazimisha serikali iache kuwaibia wananchi.

Kinachoendelea sasa ni sawa na baba kuiba uji wa mwanawe, huyo mtoto atakua kweli? Au ni sawa na daktari kuiba dawa za mgonjwa wake, kuna kupona hapo kweli?

Tusiwategemee sana hawa viongozi wetu maana wengi wao ni wasanii. Hata ukiongea nao, unagundua hapa tuna kazi kubwa sana mpaka tuje tupate maendeleo.

Wengine tunaombea kwa njia yoyote ile, serikali ya CCM ianguke. Tatizo tu ni je kweli kuna huo uwezekano kwasasa? Tusije tukawa fisi anayetegemea mkono wa mwanadamu utadondoka. Lazima tutengeneze mazingira ya kweli ambayo yataifanya CCM ianguke. JF ni sehemu moja wapo pa kuwaelemisha Watanzania jinsi viongozi wao walivyo fake. Bahati mbaya JF inawakilisha labda asilimia kumi tu ya walengwa. Tatizo ni namna ya kuwafikia hao asilimia 90.

Vyama vya upinzani na civil socities zinazunguka mjini tu na kuwaacha CCM wanatamba huko vijijini ambako ndio kuna wananchi wengi.

Kama CCM kweli wanataka kuwajibika basi Hosea, Mwanyika na wengine wote waliotajwa kwenye Richmond wawajibishwe mara moja, kabla ya kuanza na EPA.


Mtanzania umesema yote sina la kuongeza na watanzania waendelee na matatizo yao tu hakuna lolote litafanyika .
 
Mimi mshangao wangu ni kuhusiana na fisadi Mkapa ambaye bado ni mwanachama hai wa CCM. Mbona yeye haitwi kujieleza kuhusu biashara yake aliyokuwa anaifanya wakati akiwa Rais wa Tanzania na pia kujieleza ni katika mazingira yapi yeye pamoja na Yona walikuwa wamiliki wa Kiwira Coal Mining? Waliinunua kwa kiasi gani na walimlipa nani na zabuni ya kutangazwa kuuzwa KCM ilitangazwa lini na wapi na nani waliohusika na kufanya maamuzi ya nani mshindi wa zabuni hiyo?

Au ndio ule ule unafiki wa CCM kwamba kuna wengine ndani ya chama hicho ni UNTOUCHABLES? Kama haki kutendeka basi iwaguse wote wanaohusika na ufisadi, vinginevyo itakuwa yale yale ya kuwaacha mafisadi wakiwa wanapeta na mabilioni ya ufisadi wao.
 
Hili sio suala la kichama, sasa kwa mtaji huu polisi na mahakama wana kazi gani? Hivi ni viini macho tu kwa wananchi ili kutuzuga kuwa they are taking this matter seriously. Kama nawaona vile watakavyochoma mbuzi, kula bia na kuserebuka and they have 'created' a very good excuse to escape from their wives!- Now I know why they chose Butiama, what a nice-quiet location!
 
Hili sio suala la kichama, sasa kwa mtaji huu polisi na mahakama wana kazi gani? Hivi ni viini macho tu kwa wananchi ili kutuzuga kuwa they are taking this matter seriously. Kama nawaona vile watakavyochoma mbuzi, kula bia na kuserebuka and they have 'created' a very good excuse to escape from their wives!- Now I know why they chose Butiama, what a nice-quiet location!

Polisi na mahakama kazi yao ni kuhakikisha mafisadi ndani ya chama na siri kali wanalindwa ipasavyo na lolote baya haliwafiki. Si unaona mafisadi waliokupua $133 billion hata kutajwa majina yao watu wanaogopa eti kwa kisingizio kwamba nchi "italipuka!" Nchi italipuka kuwataja mafisadi waliokupua shilingi bilioni 133 za walipa kodi!? :confused:
 
Polisi na mahakama kazi yao ni kuhakikisha mafisadi ndani ya chama na siri kali wanalindwa ipasavyo na lolote baya haliwafiki. Si unaona mafisadi waliokupua $133 billion hata kutajwa majina yao watu wanaogopa eti kwa kisingizio kwamba nchi "italipuka!" Nchi italipuka kuwataja mafisadi waliokupua shilingi bilioni 133 za walipa kodi!? :confused:

IGP Mwema alisema hata katika hostage situation huwa kuna negotiators wanaojitahidi kutafuta muafaka na watekaji! Sasa mimi ninachojiuliza katika hii EPA situation nani ni mateka, nani ni Mtekaji na nani Negotiator?Tunadanganyana tu kila siku na hii serikali yetu afu kila siku tunatengeneza tume, zinaleta ripoti hatuzifanyii kazi na badala yake tunatengeneza tume zingine ili kupitia mapendekezo ya tume zingine duh!!! It's all crap to me!
Wanafanya ufisadi kwa matumizi mabaya kuchunguza ufisadi... UFISADI JUU YA UFISADI!
 
Mimi mshangao wangu ni kuhusiana na fisadi Mkapa ambaye bado ni mwanachama hai wa CCM. Mbona yeye haitwi kujieleza kuhusu biashara yake aliyokuwa anaifanya wakati akiwa Rais wa Tanzania na pia kujieleza ni katika mazingira yapi yeye pamoja na Yona walikuwa wamiliki wa Kiwira Coal Mining? Waliinunua kwa kiasi gani na walimlipa nani na zabuni ya kutangazwa kuuzwa KCM ilitangazwa lini na wapi na nani waliohusika na kufanya maamuzi ya nani mshindi wa zabuni hiyo?

Au ndio ule ule unafiki wa CCM kwamba kuna wengine ndani ya chama hicho ni UNTOUCHABLES? Kama haki kutendeka basi iwaguse wote wanaohusika na ufisadi, vinginevyo itakuwa yale yale ya kuwaacha mafisadi wakiwa wanapeta na mabilioni ya ufisadi wao.

KWAHIYO KISA KIZIMA CHA TOPIC YAKO NI KUSHANGAA KUWEPO KWA MKAPA KTK KUWAHUKUMU AKINA NGOYAI?!!!! CHAMA KITARUDI KTK MSTARI UPENDE USIPENDE,NYUNDO ILIGONGWA KABLA KUGONGWA,KUWA NA SUBIRA.
 
Mimi mshangao wangu ni kuhusiana na fisadi Mkapa ambaye bado ni mwanachama hai wa CCM. Mbona yeye haitwi kujieleza kuhusu biashara yake aliyokuwa anaifanya wakati akiwa Rais wa Tanzania na pia kujieleza ni katika mazingira yapi yeye pamoja na Yona walikuwa wamiliki wa Kiwira Coal Mining? Waliinunua kwa kiasi gani na walimlipa nani na zabuni ya kutangazwa kuuzwa KCM ilitangazwa lini na wapi na nani waliohusika na kufanya maamuzi ya nani mshindi wa zabuni hiyo?

Au ndio ule ule unafiki wa CCM kwamba kuna wengine ndani ya chama hicho ni UNTOUCHABLES? Kama haki kutendeka basi iwaguse wote wanaohusika na ufisadi, vinginevyo itakuwa yale yale ya kuwaacha mafisadi wakiwa wanapeta na mabilioni ya ufisadi wao.

KWAHIYO KISA KIZIMA CHA TOPIC YAKO NI KUSHANGAA KUWEPO KWA MKAPA KTK KUWAHUKUMU AKINA NGOYAI?!!!! CHAMA KITARUDI KTK MSTARI UPENDE USIPENDE,NYUNDO ILIGONGWA KABLA KUGONGA,KUWA NA SUBIRA.
 
Kuna mtu mmoja alisema hivi kimzaha mzaha tu lakini nadhani maneno haya yana uzito mkubwa, ili hii nchi ipate mwelekeo tofauti itabidi kwanza majority sio wote ya viongozi waliopo wafe kwa wakati mmoja ili kusiwe na watu wa kocorrupt akili mpya zinazozaliwa. Watu wapya wapewe nafasi ya kuanza upya bila ya watu wakuwaambia sisi tulifanyaga hivi kumbe ni madudu matupu.

Na hii habari ya kulindana sijui itaisha lini, haipo kwa wakubwa tu hata kwa watu wa chini. Mtu yupo radhi afukuzwe kazi kwa makosa ya mtu mwingine, mtu hawezi kusema ukweli hata kama anajua ukweli utamuokoa ni heri azame na yeye.

hali hii itatucost sana especially viongozi wetu wanapotuzamisha sisi wote kwa sababu wnalindana.
 
Lazima ujue kuwa CCM ina wenyewe na ina wasindikizaji, kama wengine (wasindikizaji) wanajidai kuingia kwenye kundi la wenyewe na kutaka kuwa-overtake, huwa wanashikishwa adabu. Kuna possibility kubwa kuwa wengine hata wakifanya kosa lolote hawatafanywa kitu, hapa ndio utajua kuwa chama kina wenyewe. Na kama ikizungumzwa kuhusu Mkapa itagusiwa tu, na wala hawatakwenda in deep!
 
Kwa chama cha mapinduzi mimi nadhani kikao cha Butiama ilikua ni nafasi tosha kabisa kama wataitumia nafasi hiyo ipasavyo ili kurudisha imani imani kwa watanzania.

Chama kama chama hatuhitaji kiingilie kazi za kipolisi hapana isipokua kuwavua uanachama kwa wahusika waliohusika na ufisadi wa Richmond.Hii pekeyake inaweza kuonyesha kwamba CCM wanaungana na Bunge la Muungano katika kuleta maendeleo na hawataki mzaha juu ya vita vya kupambana na mafisadi.

Lakini kama ushoga utatawala huko Butiama then tusitegemee kitu kipya kutoka kwa wana CCM
 
Hapa Kijijini sioni kama kuna jipya humu litakalojitokeza kwani NEC huwa inaandaliwa ajenda na Kamati Kuu .

Wajumbe wa kamati kuu ni pamoja na Rostam Aziz, Yusuph Mkamba, Benjamini Mkapa yule mr clean,Andrew Chenge tena mwenyekiti wa kamati ya maadili ambayo kama ni kweli wangekuwa na cha kupeleka kamati kuu wanagekuwa tayari wameshawaita na kuwahoji .

Pia humo kuna wengi tuu mafisadi sasa sijui lets wait and see kama kuna jipya hapa kiijijini kwetu.
 
Kwa chama cha mapinduzi mimi nadhani kikao cha Butiama ilikua ni nafasi tosha kabisa kama wataitumia nafasi hiyo ipasavyo ili kurudisha imani imani kwa watanzania.

Chama kama chama hatuhitaji kiingilie kazi za kipolisi hapana isipokua kuwavua uanachama kwa wahusika waliohusika na ufisadi wa Richmond.Hii pekeyake inaweza kuonyesha kwamba CCM wanaungana na Bunge la Muungano katika kuleta maendeleo na hawataki mzaha juu ya vita vya kupambana na mafisadi.

Lakini kama ushoga utatawala huko Butiama then tusitegemee kitu kipya kutoka kwa wana CCM

Makamba juzi alinukuliwa akisema kuwa ccm hawaendi kuomba msamaha kwa Nyerere ni mizimu yake butiama kama vile wengine wanavyodai. For now nategemea kuwa mengi yatakuwa the same. I wish kungekuwa na wanaccm wengi kama Mama Malecela ambao wako radhi kumtosa hata tingatinga mwenyewe ili kulinda maslahi ya nchi!
 
I beg to differ, huko Butiama, kuna jambo na kuna watu watarudi mahututi, maana kipigo walichopewa mawaziri bungeni na wabunge wa CCM, siamini kwamba huko kuna usalama,

Lakini I could be wrong pia!
 
anxiety as ccm top organ holds meeting...........halafu kinachoongelewa ni biskuti ! duh...watu siku wajanja wanaanzisha halafu wao haoooooooo..tim !
 
Back
Top Bottom