Antony Mtaka aambiwe kwamba sera ya elimu ni ya kitaifa na siyo mkoa kwa mkoa

Bila hata kujua kiwango cha elimu ya mkuu wa mkoa wa Dodoma, mara moja naona makosa ya kiutendaji aliyonayo. Kwanza, yaonekana ni mtu asiyejua kuchagua maneno. Pili, hakujua mchakato upi uboreshe kiwango cha elimu mkoani kwake, siyo ufaulu anaotafuta. Elimu inaendeshwa kitaifa na siyo ki-mkoa.

Haiingii akilini kwamba mkuu wa mkoa anataka kuboresha ufaulu wa wanafunzi kwa kupambana na waziri wa elimu, kwa makambi ya elimu. Ili iweje?

Elimu ni mchakato wa miaka 7 kwa shule za msingi, miaka 4 sekondari, n.k. Kama kuna uzembe ktk miaka ya elimu, Mtaka anawezaje kuboresha uzembe huo kwa makambi ya miezi miwili? Yaani sasa hivi aanze, kufika septemba darasa la 7 wafaulu mtihani. Ni elimu gani hiyo?

Sera ya elimu ipo ili kudhibiti mawazo mfu kama haya ya akina Mtaka.
Kwani walioua Elimu ya nchi hii kitaifa ni akina nani zaidi ya Serikali na mawaziri wake?

Muacheni Mtaka ajaribu njia mbadala ili tumpime mafanikio yake.
 
Bila hata kujua kiwango cha elimu ya mkuu wa mkoa wa Dodoma, mara moja naona makosa ya kiutendaji aliyonayo. Kwanza, yaonekana ni mtu asiyejua kuchagua maneno. Pili, hakujua mchakato upi uboreshe kiwango cha elimu mkoani kwake, siyo ufaulu anaotafuta. Elimu inaendeshwa kitaifa na siyo ki-mkoa.

Haiingii akilini kwamba mkuu wa mkoa anataka kuboresha ufaulu wa wanafunzi kwa kupambana na waziri wa elimu, kwa makambi ya elimu. Ili iweje?

Elimu ni mchakato wa miaka 7 kwa shule za msingi, miaka 4 sekondari, n.k. Kama kuna uzembe ktk miaka ya elimu, Mtaka anawezaje kuboresha uzembe huo kwa makambi ya miezi miwili? Yaani sasa hivi aanze, kufika septemba darasa la 7 wafaulu mtihani. Ni elimu gani hiyo?

Sera ya elimu ipo ili kudhibiti mawazo mfu kama haya ya akina Mtaka.
Umeshindwa kuzungumzia mapungufi ya sera ya elimu tuliyo nayo na Nini kifanyike unakuja kuleta siasa uchwara za wanasiasa wa kibongo.

Acheni siasa. Mimi pia ni mdau wa elimu ,Kuna shule moja Ina mwalimu mmoja biology anafundisha form one to four, mwingine chemistry anafundisha form one to four, physics form one to four. Baadhi ya madarasa yana mikondo miwili mpaka mitatu wastani wa vipindi vinne Kwa SoMo Kwa kila mkondo ndani ya week moja,Siku 194 za masomo.

Katika Hali ya kawaida tu huyu mwalimu hawezi fundisha vipindi vyote Kwa ufasaha hata kupelekea kutomaliza mada Kwa muda unaostahili, mtihani wa mwisho unakuja na coverage ya syllabus yote. Hapo ndio wengine wakaja na haya mawazo ya kuwepo na Kambi wakati wa likizo.

Ukiwa kiongozi Kupanga ni kuchagua usiruhusu kuwepo Kwa Kambi hizo au ufuate sera ya elimu Inayo waweka pembeni wanafunzi Hawa wa shule za kata kama hii.

Ila nionavyo na Kwa experience niliyo nayo RC yupo sahihi zaidi ni mzalendo zaidi kuliko wewe uliyekaa tu kwenye keyboard kupost vitu ambavyo hujafanyia utafiti or tayali umemezwa na siasa uchwara za ku shambulia watu Kwa masrahi Fulani.
 
Kosa la mtaka ni nn sasa? Maana sera ya elimu kitaifa ni kufaulu mitihani. Mtaka amekuja na mbinu ya kufaulu hio mitihan. Ww unakataa, kwa nn sasa?
Kwamba kufaulu ni kuweka kambi ya miezi miwili? Acheni ku support vitu vya kijinga yaani pale kambini mtoto anafundishwa kukariri na sio kumwandaa na mapambano halisi ya mitihani.
 
Haiingii akilini kwamba mkuu wa mkoa anataka kuboresha ufaulu wa wanafunzi kwa kupambana na waziri wa elimu, kwa makambi ya elimu. Ili iweje?
Sidhani ama ulimwelewa vyema huyu mwamba! Ni vyema ungetafakuru maneno yake badala yakukurupuka kumkandia! Alichosema Huyu mwamba ndio ukweli ambao wa Tz tunatakiwa kuchukua hatua badala y akumeza haya yanayosemwa na hawa mawaziri.
 
Mkuu robinson crusoe , kwanza naheshimu mawazo yako ila sikubaliani na wewe. Kwenye hili la makambi, mimi nasimama na RC Mtaka. Kiongozi mzuri hapimwi kwa jinsi anavyo jua kuongea, bali hupimwa kwa matokeo chanya ya utendaji wake. Kwa wanao ijua Simiyu kabla ya RC Mtaka na Simiyu ya Mtaka ndio watanielewa.
Shuhudia hapa
P


Mayalla, uko sahihi kabisa. Watu wanapenda kufanya mambo kwa mazoea. Solutions za matatizo ndani ya mikoa hazipaswi kuwa one-size-fits-all. A unique situation needs a unique response.

Huwezi kuwasaidia wanafunzi wanaochechemea kwa kutumia utaratibu uleule uliozalisha wanafunzi wanaochechemea!
 
Sidhani ama ulimwelewa vyema huyu mwamba! Ni vyema ungetafakuru maneno yake badala yakukurupuka kumkandia! Alichosema Huyu mwamba ndio ukweli ambao wa Tz tunatakiwa kuchukua hatua badala y akumeza haya yanayosemwa na hawa mawaziri.
That is rubbish of you! aliporejea kutomsikiliza waziri ulielewa anamaanisha nini?
 
Nchi yetu tuna tatizo na tatizo lenyewe sio dogo ni la kimfumo.Mtu akiwa mkweli anaanza kubanwa kwa mfumo lakini Ukweli unabaki uuwazi. Kwa mfano Kuna watu wanategemea mawaziri au wabunge walete hoja za maana kuhusu kuboresha elimu yetu hasa shule za sekondari za kata na msingi.Hili haliwezekani kwa sababu viongozi wakubwa wote HAWANA IMANI na elimu inayotolewa katika shule za kata lakini pia viongozi wengi wanamiliki shule za private. Mtaka alisema Ukweli anapigwa mawe kimfumo.
Tatizo Ni yeye mwenyewe....baada kusema ukweli kwa Imani yake hakujiamini Hadi kujitokeza kuomba msamaha. Mimi ninasema Hivi.....watu waoga hawatatufikisha popote, Ni Bora wakaachia nafasi zao zipate watu wa kauli na vitendo. Sasa mtu umeongea pointi hadi muda wote unashangilia ....kwa kiasi kikubwa ukatoa elimu ikawaingia watu wako. Kesho wewe uliye Jemedari wa kuhamasisha unaanza kujiumauma kuomba msamaha . Unadhani utaelewekaje......halafu ukute uliemuhamasisha kesho katekeleza kwa wito wako...ansbughudhiwa wakati ulishamruka kuomba msamaha. Nasema waoga wapishe
 
Back
Top Bottom