The Sheriff
JF-Expert Member
- Oct 10, 2019
- 617
- 1,792
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres akiwa mjini Paris Ufanransa wakati wa ufunguzi wa kongamano la kimataifa la Paris kwa ajili ya Amani jana, amesema kuzuia vyanzo vote vinavyosababisha uvunjifu wa amani duniani ndio dawa mujarabu ya kulinda na kudumisha amani ya dunia kuliko kukabili machafuko wakati yameshatokea.
Ameongeza kuwa ingawa ukilinganisha na migogoro mikubwa ya karne zilizopita hali ya sasa inaonekana kuwa ni ya amani zaidi, lakini ukweli ni kwamba “Bado tuko mbali kuwa na ile tunayoiita amani ya kweli, hali halisi ni ya sintofahamu na changamoto kubwa’’
Katika ulingo wa kimataifa Guterres ametaja hatari tano (5) zinazoikabili dunia hivi sasa akisema:
Mosi, Tunaona hatari ya mgawanyiko wa kiuchumi, kiteknolojia na kijiografia.
Pili, Tunapaswa kuangalia katika ngazi ya kitaifa mgawanyiko wa kijamii na tofauti zilizopo.
Tatu, tunashuhudia wimbi la maandamano kote duniani, na kama kila hali ni tofauti basi amesema kuna mambo mawili ambayo yanashabihiana:
Na tano, wanataka haki zao za binadamu na uhuru wa msingi vitekelezwe na kuzingatiwa kwa wote.
Ameongeza kuwa ingawa ukilinganisha na migogoro mikubwa ya karne zilizopita hali ya sasa inaonekana kuwa ni ya amani zaidi, lakini ukweli ni kwamba “Bado tuko mbali kuwa na ile tunayoiita amani ya kweli, hali halisi ni ya sintofahamu na changamoto kubwa’’
Katika ulingo wa kimataifa Guterres ametaja hatari tano (5) zinazoikabili dunia hivi sasa akisema:
Mosi, Tunaona hatari ya mgawanyiko wa kiuchumi, kiteknolojia na kijiografia.
Pili, Tunapaswa kuangalia katika ngazi ya kitaifa mgawanyiko wa kijamii na tofauti zilizopo.
Tatu, tunashuhudia wimbi la maandamano kote duniani, na kama kila hali ni tofauti basi amesema kuna mambo mawili ambayo yanashabihiana:
- Kwanza kabisa tunashuhudia ongezeko la kutoaminiana baina ya raia na taasisi za kisiasa na viongozi, usawa wa kijamii uko katika tishio kubwa.
- Pili, tunashuhudia athari za utandawazi unaohusiana na maendeleo ya kiteknolojia zikiongeza pengo la usawa katika jamii.
Na tano, wanataka haki zao za binadamu na uhuru wa msingi vitekelezwe na kuzingatiwa kwa wote.