Anthony Joshua kurejea ulingoni Jumamosi hii

screpa

JF-Expert Member
Sep 10, 2015
10,792
15,693
Baada ya kuwa nje ya ulingo kwa mwaka mzima, hatimaye bingwa wa ndondi wa uzito wa juu duniani anayeshikilia mikanda ya WBA, WBO na IBF anatarajiwa kurudi tena ulingoni jumamosi hii. Sikuhiyo atakuwa anatetea ubingwa wake dhidi ya mbulgaria Kubrat Pulev ambaye IBF walimrate kama no1 Challenger hivyo pambano hilo ni 'IBF mandatory'.

Pambano hilo kwa AJ ni la kwanza baada ya lile la marudiano dhidi ya Mmexico Andy Ruiz lililofanyika Saudi Arabia mwishoni mwa mwaka jana na kufanikiwa kuirejesha mikanda yake. Rekodi zao ni kama zinavyoonekana pichani, wote wakiwa wamepoteza mara moja; AJ akipoteza dhidi ya Andy Ruiz na Pulev akipoteza dhidi ya W.Klistchko.

eddiehearn_20201208_173950_0.jpg
tale-of-tape-long-aj-rublev-v4.jpg
 
Aj anashinda kweupe tu jamaa mzito sana mikono
Yes AJ ana nafasi kubwa ya kumpiga tena kwa KO. Japo kwenye heavyweight lolote linaweza kutokea, one punch can change everything
 
Huyo Pulev hana lolote, ni mzito na AJ anajua anaenda kuchukua points tu hapo tena kwa KO

Alishapigwa na Vladimir Klitschko...
Na sipendagi style yake anapenda sana kupiga jab then anakuhug, but hiyo style inawork kwa hao heavyweight wadogo kama kina Chisora, kwa magiant kama AJ sidhani kama itawork ukizingatia AJ anapiga combination so hatapata chance ya kufanya hivyo
 
Huyo Pulev hana lolote, ni mzito na AJ anajua anaenda kuchukua points tu hapo tena kwa KO

Alishapigwa na Vladimir Klitschko

AJ apigane na Tyson Fury au Deontay Wilder ndio tumpime hapo.
Tyson Fury ndio kipimo tosha, huyo Wilder hana lolote kelele nyingi tu.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom