M-mbabe
JF-Expert Member
- Oct 29, 2009
- 13,203
- 23,020
Imeandikwa na Ansbert Ngurumo
MIAKA mitano iliyopita, Rais Jakaya Kikwete aliandika historia kwa kukiri hadharani kwamba Chama Cha Mapinduzi (CCM) kilikuwa kimeshinda uchaguzi kwa mapato haramu.
Ilikuwa hivi. Baada ya miezi minne tu madarakani katika awamu yake ya kwanza, Rais Kikwete alikutana na 'wafadhili' wa CCM), jijini Dar es Salaam, walioisaidia kupata pesa za kampeni mwaka 2005.
Katika kuzungumza nao, Kikwete alisisitiza mambo mawili. Kwanza, aliwaomba wana CCM wasilewe ushindi walioupata mwaka 2005, badala yake wajiandae kwa uchaguzi mkuu unaofuata.
Pili, aliwaasa wanachama wenzake waanze kutafakari namna ya kupata MAPATO HALALI kwa ajili ya kampeni. Hili ndilo lilizua maswali, hasa kwa kuwa lilitoka kinywani mwake baada ya chama kushinda kwa nguvu kubwa ya pesa, huku kikiwa kinashutumiwa kusaidiwa na matajiri kadhaa wanaojihusisha na wizi na ujambazi.
Tunapowapima leo, tunagundua kwamba yote mawili yamewashinda. CCM ilibweteka, ikajidai itatawala milele, ikabaki kuimba ushindi wa kishindo wa mwaka 2005.
Mwenendo na matokeo ya kura katika uchaguzi wa mwaka 2010, vimeonyesha kwamba CCM haitatawala milele. Na baadhi ya wachambuzi wa siasa wanasema kuwa huu ndio umekuwa uchaguzi wa mwisho wa CCM kuwaburuza wananchi.
Dalili zote zinaonyesha kuwa kisipojisuka vema, miaka minne ijayo kitakuwa kimefika kule viliko vyama vingine vya ukombozi barani Afrika. Mapumzikoni. Kitakuwa kinajiandaa upya katika harakati za kujaribu kurejea madarakani.
Lakini hili la pili ndilo limechangia pia katika kuishusha CCM mbele ya umma, na kuwafanya viongozi wake waonekane watu wasioaminika, wenye maneno yasiyofanana na matendo yao; wasio na uwezo wa kutumia kodi zetu kutuletea kile walichotuahidi.
Wakati ule, kuna Watanzania hawakumwelewa Rais Kikwete. Lakini baada ya mapambano ya ufisadi kuanika matukio ya wizi wa EPA na mengine yaliyofanana nayo, leo kila mtu anaelewa vema maana ya kauli ya Rais Kikwete.
Kumbe alikuwa anajua kwamba kampeni zake zilifanikishwa na pesa chafu. Hakutaka litokee tena. Lakini ameshindwa kulizuia.
Maana katika uchaguzi wa mwaka jana (2010), CCM ilipokea michango kutoka kule kule, na hata kutumia baadhi ya ndege zinazomilikiwa na watu wale wale wanaotiliwa shaka.
Aliishia kutamka tu kwamba anakusudia kutunga sheria ya kuzuia wafanyabiashara kuwa wanasiasa, akaishia kuwaomba wafanyabiashara wa aina ile ile wafanikishe kampeni zake.
Kwanini nimekumbuka mambo haya leo? Wiki hii tumekumbushwa dhana ya maamuzi magumu ambayo serikali imekuwa inashindwa kuchukua.
Bahati mbaya, kila mara wapinzani walipokuwa wanazungumza kauli ya kuitaka serikali kuchukua maamuzi magumu, walikuwa wakizomewa na wabunge wa CCM.
Zamu hii kauli ile ile imezungumzwa na mwana-CCM mwenzao, kigogo na mwasisi wa serikali ya awamu ya nne, Waziri Mkuu mstaafu, Edward Lowassa.
Ameitaka serikali iache kuogopa, ichukue maamuzi na ikubali sifa au lawama kwa uamuzi wake.
Nilimsikiliza na kumuona Lowassa akitoa hotuba yake bungeni. Wabunge wengi wa CCM, isipokuwa Samuel Sitta, walikuwa wakimshangilia badala ya kumzomea. Maana yake ni kwamba walikubaliana na kauli yake ile ile wanayoizomea kila inapozungumzwa na wapinzani!
Lakini kikubwa zaidi ni majibu yaliyotolewa na serikali. Ni majibu ya kejeli. Hayaonyeshi umakini. Yanaendekeza uchovu na ubabaishaji ule ule ulioifikisha hapa ilipo.
Serikali, kupitia kwa Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, ilipuuza kauli ya Lowassa na kusisitiza kwamba katika miaka 50 ya historia ya Tanzania huru, hakuna serikali iliyofanya maamuzi magumu kama serikali ya awamu ya nne.
Akataja miradi waliyotekeleza: ujenzi wa shule za kata, umaliziaji wa barabara zilizoachwa na Rais Benjamin Mkapa, ujenzi wa Chuo Kikuu cha Dodoma, kuvunja Baraza la Mawaziri mwaka 2008 na mengine machache.
Katika yote haya, sikuona uamuzi wowote mgumu uliotolewa. Ujenzi wa shule za kata nchi nzima ni uamuzi wa kisera ulioanzishwa na Lowassa mwenyewe, lakini haukuwa umefanyiwa maadalizi ya kina. Si uamuzi mgumu kuanzisha shule nyingi zisizo na walimu, vitabu, maabara, mabweni na vifaa vingine muhimu.
Hata kama ungekuwa uamuzi mgumu, matokeo ya mitihani ya taifa katika shule hizo, hayaonyeshi kama ni jambo la kujivunia kuingiza watoto kwenye shule wakakaa miaka minne bila kuelimika, wakapoteza mwelekeo wa maisha yao kitaaluma.
Badala ya shule za kata, bora wangeanzisha vyuo vichache vya ufundi katika kila wilaya, kwa maandalizi ya kuwapatia wanafunzi stadi za maisha ambazo ni bora kuliko kidato cha nne kisicho na cheti au chenye alama zisizoweza kumsaidia mtoto kuendelea na masomo ya juu.
Kumalizia barabara zilizoanzishwa na Rais Mkapa, tena nyingi kwa kiwango kisichoridhisha, si uamuzi mgumu. Ni wajibu wa serikali. Chuo Kikuu cha Dodoma ni fahari ya taifa, kama ukubwa wa majengo, na wingi wa wanafunzu vitaendana na uwezo na nia ya serikali kukijali na kukiwezesha kufyatua wasomi weledi wanaoendana na mahitaji ya karne ya 21.
Na bado huu si muujiza, wala si uamuzi mgumu. Ni wajibu wa serikali. Ni njia mojawapo ya kutumia kodi za wananchi kwa ajili ya kuendeleza watu wake.
Kama serikali inataka kujitapa kwa maamuzi magumu, mbona taifa liko gizani? Kama inataka kujitapa kwa maamuzi magumu, mbona iliwaogopa mafisadi wa EPA, hata ikawabembeleza warudishe pesa ili isiwashitaki? Kama inataka kujitapa kwa maamuzi magumu mbona ilikiri kwamba Kagoda hawakamatiki?
Kama serikali inataka kujitapa kwa maamuzi magumu mbona ilishindwa kumtia mbaroni aliyekuwa Gavana wa Benki Kuu, Daudi Balali? Mbona ilijidai haijui alikokimbilia? Mbona ilijidai haijui alikodaiwa kuugulia? Mbona ilishindwa kumfuata kokote aliko na kumrejesha ili awe shahidi katika kesi ya wizi wa EPA?
Kama serikali inajitapa kwa maamuzi magumu, mbona taifa linakabiliwa na njaa?
Siamini kwamba haya ninayojadili ndiyo maamuzi magumu aliyokuwa amekusudia Lowassa bungeni, lakini ni wazi kwamba Lowassa ametupatia fursa ya nyongeza kuibana serikali ifanye maamuzi magumu. Na kama hayo iliyofanya ndiyo inaita maamuzi magumu, basi hatuna serikali!
Kuvunja Baraza la Mawaziri si uamuzi mgumu. Kwa kawaida, anayeunda baraza hilo ndiye ana wajibu wa kulivunja. Lakini Rais Kikwete hajavunja Baraza la Mawaziri. Ilikuwa lazima livunjike baada ya Lowassa kujiuzulu.
Kama rais angetaka heshima ya kuvunja Baraza la Mawaziri, angemfukuza kazi Lowassa. Alishindwa kumfukuza Waziri Mkuu, hadi Spika wa Bunge wa wakati huo, Samuel Sitta na Mwenyekiti wa Kamati Teule ya Bunge iliyochunguza sakata la Richmond, Dk. Harrison Mwakyembe, walipomsaidia kumshauri Lowassa apime na kutafakari hatima yake kisiasa.
Kwa hiyo, kimantiki, haukuwa uamuzi wa serikali, bali wa Bunge. Maana kama serikali ingekuwa na uwezo wa kufanya maamuzi hayo, isingeliacha Bunge liifikishe mahali pa kuivua nguo na kuidhalilisha.
Ingekuwa heri kama Pinda angepuuza kabisa hoja hii, kuliko kuthubutu kuijibu kwa kutoa kauli inayozidi kushusha heshima ya serikali mbele ya umma. Lakini kama tunakubaliana kwamba haya aliyotaja ndiyo maamuzi magumu ya serikali ya awamu ya nne, basi serikali haijaanza kazi!
Maamuzi magumu yangeturudisha kule kule alikoanzia rais mwaka 2006, kusafisha mifumo ya chama tawala na serikali na kujijengea uhalali wa kutawala kwa heshima na ridhaa ya wananchi. Wamelazimisha ushindi mwaka jana, na sasa wanatawala kwa kulazimisha. Je, na huu tuuite uamuzi mgumu?
MIAKA mitano iliyopita, Rais Jakaya Kikwete aliandika historia kwa kukiri hadharani kwamba Chama Cha Mapinduzi (CCM) kilikuwa kimeshinda uchaguzi kwa mapato haramu.
Ilikuwa hivi. Baada ya miezi minne tu madarakani katika awamu yake ya kwanza, Rais Kikwete alikutana na 'wafadhili' wa CCM), jijini Dar es Salaam, walioisaidia kupata pesa za kampeni mwaka 2005.
Katika kuzungumza nao, Kikwete alisisitiza mambo mawili. Kwanza, aliwaomba wana CCM wasilewe ushindi walioupata mwaka 2005, badala yake wajiandae kwa uchaguzi mkuu unaofuata.
Pili, aliwaasa wanachama wenzake waanze kutafakari namna ya kupata MAPATO HALALI kwa ajili ya kampeni. Hili ndilo lilizua maswali, hasa kwa kuwa lilitoka kinywani mwake baada ya chama kushinda kwa nguvu kubwa ya pesa, huku kikiwa kinashutumiwa kusaidiwa na matajiri kadhaa wanaojihusisha na wizi na ujambazi.
Tunapowapima leo, tunagundua kwamba yote mawili yamewashinda. CCM ilibweteka, ikajidai itatawala milele, ikabaki kuimba ushindi wa kishindo wa mwaka 2005.
Mwenendo na matokeo ya kura katika uchaguzi wa mwaka 2010, vimeonyesha kwamba CCM haitatawala milele. Na baadhi ya wachambuzi wa siasa wanasema kuwa huu ndio umekuwa uchaguzi wa mwisho wa CCM kuwaburuza wananchi.
Dalili zote zinaonyesha kuwa kisipojisuka vema, miaka minne ijayo kitakuwa kimefika kule viliko vyama vingine vya ukombozi barani Afrika. Mapumzikoni. Kitakuwa kinajiandaa upya katika harakati za kujaribu kurejea madarakani.
Lakini hili la pili ndilo limechangia pia katika kuishusha CCM mbele ya umma, na kuwafanya viongozi wake waonekane watu wasioaminika, wenye maneno yasiyofanana na matendo yao; wasio na uwezo wa kutumia kodi zetu kutuletea kile walichotuahidi.
Wakati ule, kuna Watanzania hawakumwelewa Rais Kikwete. Lakini baada ya mapambano ya ufisadi kuanika matukio ya wizi wa EPA na mengine yaliyofanana nayo, leo kila mtu anaelewa vema maana ya kauli ya Rais Kikwete.
Kumbe alikuwa anajua kwamba kampeni zake zilifanikishwa na pesa chafu. Hakutaka litokee tena. Lakini ameshindwa kulizuia.
Maana katika uchaguzi wa mwaka jana (2010), CCM ilipokea michango kutoka kule kule, na hata kutumia baadhi ya ndege zinazomilikiwa na watu wale wale wanaotiliwa shaka.
Aliishia kutamka tu kwamba anakusudia kutunga sheria ya kuzuia wafanyabiashara kuwa wanasiasa, akaishia kuwaomba wafanyabiashara wa aina ile ile wafanikishe kampeni zake.
Kwanini nimekumbuka mambo haya leo? Wiki hii tumekumbushwa dhana ya maamuzi magumu ambayo serikali imekuwa inashindwa kuchukua.
Bahati mbaya, kila mara wapinzani walipokuwa wanazungumza kauli ya kuitaka serikali kuchukua maamuzi magumu, walikuwa wakizomewa na wabunge wa CCM.
Zamu hii kauli ile ile imezungumzwa na mwana-CCM mwenzao, kigogo na mwasisi wa serikali ya awamu ya nne, Waziri Mkuu mstaafu, Edward Lowassa.
Ameitaka serikali iache kuogopa, ichukue maamuzi na ikubali sifa au lawama kwa uamuzi wake.
Nilimsikiliza na kumuona Lowassa akitoa hotuba yake bungeni. Wabunge wengi wa CCM, isipokuwa Samuel Sitta, walikuwa wakimshangilia badala ya kumzomea. Maana yake ni kwamba walikubaliana na kauli yake ile ile wanayoizomea kila inapozungumzwa na wapinzani!
Lakini kikubwa zaidi ni majibu yaliyotolewa na serikali. Ni majibu ya kejeli. Hayaonyeshi umakini. Yanaendekeza uchovu na ubabaishaji ule ule ulioifikisha hapa ilipo.
Serikali, kupitia kwa Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, ilipuuza kauli ya Lowassa na kusisitiza kwamba katika miaka 50 ya historia ya Tanzania huru, hakuna serikali iliyofanya maamuzi magumu kama serikali ya awamu ya nne.
Akataja miradi waliyotekeleza: ujenzi wa shule za kata, umaliziaji wa barabara zilizoachwa na Rais Benjamin Mkapa, ujenzi wa Chuo Kikuu cha Dodoma, kuvunja Baraza la Mawaziri mwaka 2008 na mengine machache.
Katika yote haya, sikuona uamuzi wowote mgumu uliotolewa. Ujenzi wa shule za kata nchi nzima ni uamuzi wa kisera ulioanzishwa na Lowassa mwenyewe, lakini haukuwa umefanyiwa maadalizi ya kina. Si uamuzi mgumu kuanzisha shule nyingi zisizo na walimu, vitabu, maabara, mabweni na vifaa vingine muhimu.
Hata kama ungekuwa uamuzi mgumu, matokeo ya mitihani ya taifa katika shule hizo, hayaonyeshi kama ni jambo la kujivunia kuingiza watoto kwenye shule wakakaa miaka minne bila kuelimika, wakapoteza mwelekeo wa maisha yao kitaaluma.
Badala ya shule za kata, bora wangeanzisha vyuo vichache vya ufundi katika kila wilaya, kwa maandalizi ya kuwapatia wanafunzi stadi za maisha ambazo ni bora kuliko kidato cha nne kisicho na cheti au chenye alama zisizoweza kumsaidia mtoto kuendelea na masomo ya juu.
Kumalizia barabara zilizoanzishwa na Rais Mkapa, tena nyingi kwa kiwango kisichoridhisha, si uamuzi mgumu. Ni wajibu wa serikali. Chuo Kikuu cha Dodoma ni fahari ya taifa, kama ukubwa wa majengo, na wingi wa wanafunzu vitaendana na uwezo na nia ya serikali kukijali na kukiwezesha kufyatua wasomi weledi wanaoendana na mahitaji ya karne ya 21.
Na bado huu si muujiza, wala si uamuzi mgumu. Ni wajibu wa serikali. Ni njia mojawapo ya kutumia kodi za wananchi kwa ajili ya kuendeleza watu wake.
Kama serikali inataka kujitapa kwa maamuzi magumu, mbona taifa liko gizani? Kama inataka kujitapa kwa maamuzi magumu, mbona iliwaogopa mafisadi wa EPA, hata ikawabembeleza warudishe pesa ili isiwashitaki? Kama inataka kujitapa kwa maamuzi magumu mbona ilikiri kwamba Kagoda hawakamatiki?
Kama serikali inataka kujitapa kwa maamuzi magumu mbona ilishindwa kumtia mbaroni aliyekuwa Gavana wa Benki Kuu, Daudi Balali? Mbona ilijidai haijui alikokimbilia? Mbona ilijidai haijui alikodaiwa kuugulia? Mbona ilishindwa kumfuata kokote aliko na kumrejesha ili awe shahidi katika kesi ya wizi wa EPA?
Kama serikali inajitapa kwa maamuzi magumu, mbona taifa linakabiliwa na njaa?
Siamini kwamba haya ninayojadili ndiyo maamuzi magumu aliyokuwa amekusudia Lowassa bungeni, lakini ni wazi kwamba Lowassa ametupatia fursa ya nyongeza kuibana serikali ifanye maamuzi magumu. Na kama hayo iliyofanya ndiyo inaita maamuzi magumu, basi hatuna serikali!
Kuvunja Baraza la Mawaziri si uamuzi mgumu. Kwa kawaida, anayeunda baraza hilo ndiye ana wajibu wa kulivunja. Lakini Rais Kikwete hajavunja Baraza la Mawaziri. Ilikuwa lazima livunjike baada ya Lowassa kujiuzulu.
Kama rais angetaka heshima ya kuvunja Baraza la Mawaziri, angemfukuza kazi Lowassa. Alishindwa kumfukuza Waziri Mkuu, hadi Spika wa Bunge wa wakati huo, Samuel Sitta na Mwenyekiti wa Kamati Teule ya Bunge iliyochunguza sakata la Richmond, Dk. Harrison Mwakyembe, walipomsaidia kumshauri Lowassa apime na kutafakari hatima yake kisiasa.
Kwa hiyo, kimantiki, haukuwa uamuzi wa serikali, bali wa Bunge. Maana kama serikali ingekuwa na uwezo wa kufanya maamuzi hayo, isingeliacha Bunge liifikishe mahali pa kuivua nguo na kuidhalilisha.
Ingekuwa heri kama Pinda angepuuza kabisa hoja hii, kuliko kuthubutu kuijibu kwa kutoa kauli inayozidi kushusha heshima ya serikali mbele ya umma. Lakini kama tunakubaliana kwamba haya aliyotaja ndiyo maamuzi magumu ya serikali ya awamu ya nne, basi serikali haijaanza kazi!
Maamuzi magumu yangeturudisha kule kule alikoanzia rais mwaka 2006, kusafisha mifumo ya chama tawala na serikali na kujijengea uhalali wa kutawala kwa heshima na ridhaa ya wananchi. Wamelazimisha ushindi mwaka jana, na sasa wanatawala kwa kulazimisha. Je, na huu tuuite uamuzi mgumu?