Anne Makinda enough is enough tumechoka na Bunge lako la hovyo!

Mazoko

JF-Expert Member
Jul 10, 2009
674
184
http://feedproxy.google.com/~r/co/l...o.html?utm_source=feedburner&utm_medium=emailNasema wazi Anne Makinda hana la kujivunia na pengine hata wanahistoria hawana la kuandika juu ya mwanasiasa huyo ambaye ni dhahiri sasa nyota yake inazidi kufifia kila sekunde.
Yanayoendelea na yatakayoendelea kutoka Bungeni ni ushahidi wa wazi wa udhaifu wa spika Makinda, Job Ndugai, Jenista Mhagama na Simbachamwene ambao kwa nyakati tofauti wameonyesha dhahiri kuwa sasa wameshindwa kazi.
Sitaki kuibua malumbano yasiyo na tija bali nataka niweke wazi kuwa tatizo si wapinzani bali udhaifu wa Makinda na wasaidizi wake.
Ni mwehu gani leo hii hakumbuki mikiki ya Dr Slaa wakati wa spika Sitta? je yalitokea haya tunayoyaona sasa? je nikisema Sitta “KAMFUNIKA” Makinda nitakuwa naongopa? NARUDIA TENA tatizo ni Makinda na wasaidizi wake!
Tangu awali wenye kuona mbali walitoa angalizo kuwa spika aliyechaguliwa kwa kigezo cha jinsia “HAFAI” na leo hii wote tu mashahidi kuwa sasa “MAKINDA ANAWABEBA WALIOMBEBA” amelivuruga Bunge na kweli limevuruga .
Kawafanya wapinzani kuwa na roho ya “KUPAMBANA” dhidi yake na wasaidizi wake na kwa bahati mbaya hana uwezo wa kulitatua hili si yeye wala “wasaidizi wake”
Watanzania hawapaswi kushangaa “eti wabunge wanataka kupigana” nini cha ajabu? au Deo Filikunjombe kutaka “kupigwa makofi?” lipi la ajabu? Lema, Msigwa na Lissu kutolewa nje ya Bunge? nini cha ajabu? pendekezo la wabunge kupimwa akili? haya yote hayana budi kutokea, hebu jaribu kufikiria haya yasipotokea watanzania mtaamini vipi kuwa “HII NI NCHI LEGELEGE?”


Mungu Ibariki Tanzania, Amin
 
Nasema wazi Anne Makinda hana la kujivunia na pengine hata wanahistoria hawana la kuandika juu ya mwanasiasa huyo ambaye ni dhahiri sasa nyota yake inazidi kufifia kila sekunde.
Yanayoendelea na yatakayoendelea kutoka Bungeni ni ushahidi wa wazi wa udhaifu wa spika Makinda, Job Ndugai, Jenista Mhagama na Simbachamwene ambao kwa nyakati tofauti wameonyesha dhahiri kuwa sasa wameshindwa kazi.
Sitaki kuibua malumbano yasiyo na tija bali nataka niweke wazi kuwa tatizo si wapinzani bali udhaifu wa Makinda na wasaidizi wake.
Ni mwehu gani leo hii hakumbuki mikiki ya Dr Slaa wakati wa spika Sitta? je yalitokea haya tunayoyaona sasa? je nikisema Sitta "KAMFUNIKA" Makinda nitakuwa naongopa? NARUDIA TENA tatizo ni Makinda na wasaidizi wake!
Tangu awali wenye kuona mbali walitoa angalizo kuwa spika aliyechaguliwa kwa kigezo cha jinsia "HAFAI" na leo hii wote tu mashahidi kuwa sasa "MAKINDA ANAWABEBA WALIOMBEBA" amelivuruga Bunge na kweli limevuruga .
Kawafanya wapinzani kuwa na roho ya "KUPAMBANA" dhidi yake na wasaidizi wake na kwa bahati mbaya hana uwezo wa kulitatua hili si yeye wala "wasaidizi wake"
Watanzania hawapaswi kushangaa "eti wabunge wanataka kupigana" nini cha ajabu? au Deo Filikunjombe kutaka "kupigwa makofi?" lipi la ajabu? Lema, Msigwa na Lissu kutolewa nje ya Bunge? nini cha ajabu? pendekezo la wabunge kupimwa akili? haya yote hayana budi kutokea, hebu jaribu kufikiria haya yasipotokea watanzania mtaamini vipi kuwa "HII NI NCHI LEGELEGE?"


Mungu Ibariki Tanzania, Amin

Unasema kweli. Lakini ujue kuwa huyu ameletwa na watu kwa masilahi yao. Unategemea nini?
 
Back
Top Bottom