Anne Kilango Malecela: Kuna mkanganyiko kwenye suala la kodi ya majengo. Ieleweke anayelipa ni nani

beth

JF-Expert Member
Aug 19, 2012
3,877
6,326
Mbunge wa Jimbo la Same Mashariki, Anne Kilango Malecela, ametaka suala la kulipa kodi kwenye majengo kuangaliwa vizuri akisema, "Mkaliangalie vizuri huko mtaani. Tusidanganyane, kuna mkanganyiko!"

Ameshauri jambo hilo kuwekwa vizuri kwa Wananchi na kueleweka anayelipa Kodi hiyo ni nani kati ya mwenye nyumba na mpangaji badala ya kusema ulipaji kodi umekuwa rahisi.
 
Mbunge wa Jimbo la Same Mashariki, Anne Kilango Malecela, ametaka suala la kulipa kodi kwenye majengo kuangaliwa vizuri akisema, "Mkaliangalie vizuri huko mtaani. Tusidanganyane, kuna mkanganyiko!"

Ameshauri jambo hilo kuwekwa vizuri kwa Wananchi na kueleweka anayelipa Kodi hiyo ni nani kati ya mwenye nyumba na mpangaji badala ya kusema ulipaji kodi umekuwa rahisi
1. Kama mbunge alipaswa aseme na kupendekeza nini kifanyike. Kusema tu waende wakaangalie kwa sababu mitaani halieleweki. Sijui anataka wakaangalie nini sasa maana wao ndiyo wameshaliangalia na kuja na utaratibu huo...

2. Ukweli ni kuwa kwa namna lilivyoletwa na litakavyotekelezwa (kama halitafanyiwa mabadiliko), hii haiwezi kuwa KODI YA MAJENGO bali ni bora iitwe KODI YA LUKU yaani kila mwenye LUKU ya umeme...

3. Ni kwa sababu, siyo kila LUKU YA UMEME imewekwa kwenye Jengo. Kuna watu wana LUKU na wameziweka kwenye miti Mf. Mafundi seremala, mashine za kupasua mbao nk nk

4. Aidha huko vijijini kuna LUKU zimewekwa kwenye nyumba za nyasi na matembe (zilizoezekwa kwa miti na udongo). Hawa kuwalipisha kodi ya Jengo siyo sawa hata kidogo tena kwa kiwango sawa na mwenyewe nyumba ya thamani ya Tshs. 300,000,000...!!
 
...

4. Aidha huko vijijini kuna LUKU zimewekwa kwenye nyumba za nyasi na matembe (zilizoezekwa kwa miti na udongo). Hawa kuwalipisha kodi ya Jengo siyo sawa hata kidogo tena kwa kiwango sawa na mwenyewe nyumba ya thamani ya Tshs. 300,000,000...!!
... zimewekwa categories sio just kulipa kwa kuwa una Luku.
 
Mwigulu anataka Wapangaji ndio walipe Kodi za Wenye Nyumba😆
Sio Mwigulu ila siku zote TRA wanachukua kodi ya jengo toka kwa mpangaji ..... ukihitaji kupata leseni ya biashara popote iwe halmashauri, viwanda na biashara au mamlaka zingine ni lazima uambatanishe Tax Clearance Certificate ambayo utaipata baada ya kuwa ume submit mkataba wa pango la sehemu ya biashara bila kujalisha kwamba mwenye nyumba alishalipa kodi au lah! ila TRA pamoja na makadirio ya kodi watakupa invoice yenye 10% ya gharama ya pango kwa mwaka... uilipe.
 
Huu ni mwanya wa kulipa kodi, tusirudi nyuma, kama mnataka kodi ya jengo irudi poa tu, ila hii kodi ya luku ibaki
 
Sio Mwigulu ila siku zote TRA wanachukua kodi ya jengo toka kwa mpangaji ..... ukihitaji kupata leseni ya biashara popote iwe halmashauri, viwanda na biashara au mamlaka zingine ni lazima uambatanishe Tax Clearance Certificate ambayo utaipata baada ya kuwa ume submit mkataba wa pango la sehemu ya biashara bila kujalisha kwamba mwenye nyumba alishalipa kodi au lah! ila TRA pamoja na makadirio ya kodi watakupa invoice yenye 10% ya gharama ya pango kwa mwaka... uilipe.
Sio kama inayoongelewa hapa ni Kodi ya Nyumba
 
Halafu baadaye wanakuja kushangaa hii sheria ilipitaje....tuna shida sana ss watz
 
1. Kama mbunge alipaswa aseme na kupendekeza nini kifanyike. Kusema tu waende wakaangalie kwa sababu mitaani halieleweki. Sijui anataka wakaangalie nini sasa maana wao ndiyo wameshaliangalia na kuja na utaratibu huo...

2. Ukweli ni kuwa kwa namna lilivyoletwa na litakavyotekelezwa (kama halitafanyiwa mabadiliko), hii haiwezi kuwa KODI YA MAJENGO bali ni bora iitwe KODI YA LUKU yaani kila mwenye LUKU ya umeme...

3. Ni kwa sababu, siyo kila LUKU YA UMEME imewekwa kwenye Jengo. Kuna watu wana LUKU na wameziweka kwenye miti Mf. Mafundi seremala, mashine za kupasua mbao nk nk

4. Aidha huko vijijini kuna LUKU zimewekwa kwenye nyumba za nyasi na matembe (zilizoezekwa kwa miti na udongo). Hawa kuwalipisha kodi ya Jengo siyo sawa hata kidogo tena kwa kiwango sawa na mwenyewe nyumba ya thamani ya Tshs. 300,000,000...!!

Mawaziri na wabunge nao kutolipa kodi stahiki nayo waiona je?
 
Sio Mwigulu ila siku zote TRA wanachukua kodi ya jengo toka kwa mpangaji ..... ukihitaji kupata leseni ya biashara popote iwe halmashauri, viwanda na biashara au mamlaka zingine ni lazima uambatanishe Tax Clearance Certificate ambayo utaipata baada ya kuwa ume submit mkataba wa pango la sehemu ya biashara bila kujalisha kwamba mwenye nyumba alishalipa kodi au lah! ila TRA pamoja na makadirio ya kodi watakupa invoice yenye 10% ya gharama ya pango kwa mwaka... uilipe.
Mi simkubali Mwigulu ila katika hili ni seme ukweli Wala halina utata.

Mfano, wakati flani nilikua branch manager mahali ilikua tukitaka ku lease ofisi (fremu/jengo) lazima kwenye ile Kodi ikatwe withhold tax sasa mwenye nyumba huwa haelewi hivo ilibidi sisi wenyewe tujiongeze kwakuilipa wenyewe

so naona ni ishu ya makubaliano kati mwenye nyumba na mpangaji.
 
Mi simkubali Mwigulu ila katika hili ni seme ukweli Wala halina utata.

Mfano, wakati flani nilikua branch manager mahali ilikua tukitaka ku lease ofisi (fremu/jengo) lazima kwenye ile Kodi ikatwe withhold tax sasa mwenye nyumba huwa haelewi hivo ilibidi sisi wenyewe tujiongeze kwakuilipa wenyewe

so naona ni ishu ya makubaliano kati mwenye nyumba na mpangaji.
Makubaliano hayo ni nadra sana kufanyika unless mpangaji uwe na uwelewa huo.
 
Back
Top Bottom