Anna Tibaijuka utaweza utapeli wa viwanja wizara yako? Anza na katibu wa sasa

Pdidy

JF-Expert Member
Nov 22, 2007
50,462
21,334
Sidhan nimekuwa nikiifwatilia sana hii wizara
wapo waliosema imempata mkunaji lakiini binafsi nasubiri kwanza,wapo waliokuja kwa kasi tukadanganywa nyumba zinarudi walizoiba viwanja vinarudi ikabaki historia kama ya adam na hawa


Mamam yangu kipenzi nakupenda sana ila nimepata mshtuko sana hii wizara imejaa matapeli kuanzia katibu wako mpaka chini wamegawana na familia zao nahisi ungeanza na hawa kwanza ili wa chini waanze kukutajia wengine
 
hata mimi ni wasiwasi wangu wizala hii imejaa rushwa na uzulumaji mkubwa sana! I WISH AFANIKIWE NI WIZALA NGUMU SANA.
 
yap tumpe mda,naamini hatatolet down,labda afuate matakwa ya wanamtandao lakini kama atakuja na sera zake kama zile za un aaaaaaah anaweza hana tabu mama wa mtu
mapiduziiiii daimaaaaa
 
nani kati yao msafi asimame? (QUOTE).

Haya ni maneno ya kwenye Biblia. Usije ukawa wewe ni Makamba ambaye ni bingwa wa kunukuu BIBLIA. Anadhani akinukuu BIBLIA kwenye mikutano ndiyo anavutia umati.
 
Awali ya yote nimwombe mwanzisha mada anithibitishie kama anamufahamu na kumuelewa vema Katibu Mkuu wa Hiyo wizara! Usicheze na Patrick bwana! Kaingia hapo Wizarani Mwaka huu tu lkn tayari amemudu kupunguza urasimu kwa kiwango kikubwa. Hati unapata ndani ya miezi mi3, wafanyakazi wa wizara wanaogundulika kuhodhi viwanja wananyanganywa, miradi ya viwanja 20,000 Dsm amehusika sana kuifanikisha huku akipunguza upendeleo na rushwa ktk upatikanaji. Ni utendaji wa huyu KM uliowakimbiza wafanyakazi wazembe wakiwemo Wahadhiri wa UCLAS walizoeakutumia Wizara kama kijiwe au anwani yao.
 
Hata Mama Magreth Sitta alipopewa wizara ya Elimu watu walisema sasa walimu wamepata mkombozi lakin nini kilichotokea. Wasiwasi wangu hata huyo Mama Tibaijuka anaweza kua controlled na mafisadi na asifanye tunayotarajia.
 
Awali ya yote nimwombe mwanzisha mada anithibitishie kama anamufahamu na kumuelewa vema Katibu Mkuu wa Hiyo wizara! Usicheze na Patrick bwana! Kaingia hapo Wizarani Mwaka huu tu lkn tayari amemudu kupunguza urasimu kwa kiwango kikubwa. Hati unapata ndani ya miezi mi3, wafanyakazi wa wizara wanaogundulika kuhodhi viwanja wananyanganywa, miradi ya viwanja 20,000 Dsm amehusika sana kuifanikisha huku akipunguza upendeleo na rushwa ktk upatikanaji. Ni utendaji wa huyu KM uliowakimbiza wafanyakazi wazembe wakiwemo Wahadhiri wa UCLAS walizoeakutumia Wizara kama kijiwe au anwani yao.

Lakini pamoja na kugawa viwanja 20000 pesa zetu zimeliwa bila kutufikishia miundombinu toka 2006 hadi sasa kama tulivyoahidiwa pale Mwongozo kigamboni. Mwache ahukumiwe
 
Lakini pamoja na kugawa viwanja 20000 pesa zetu zimeliwa bila kutufikishia miundombinu toka 2006 hadi sasa kama tulivyoahidiwa pale Mwongozo kigamboni. Mwache ahukumiwe

mams,
Hapa si unaongelea mambo mawili tofauti? Kulipa ada na kupata kiwanja na pili kufikishiwa miundombinu ambayo ni kazi ya Wizara nyingine japo ndani ya serikali moja! Au sijakupata?
 
Kama Hapa Tanzania tungekuwa na Ma KM 10 kama KM wa sasa wa Ardhi hii nchi ingekuwa inapiga maendeleo kama China, Watu wanahama bila kupenda, Asante Patrick Rutabanzibwa.
 
hata mama magreth sitta alipopewa wizara ya elimu watu walisema sasa walimu wamepata mkombozi lakin nini kilichotokea. Wasiwasi wangu hata huyo mama tibaijuka anaweza kua controlled na mafisadi na asifanye tunayotarajia.


kabisa na natamani nmsikie atutajie kile kiwanja pale pembeni ya salendar club ni cha nani
 
Nyie mnaomsifia Katibu Mkuu Patrick Rutabanzibwa hamumfahamu sawasawa. Huyu jamaa ni mrasimu sana na ni mnafiki na mtu wa kujipendekeza kwa wakubwa ndio maana Wizara zote alikopitia hakuna maamuzi ya maana yaliyofanyika. Tangia ameingia Wizara ya Ardhi hakuna jipya kafanya; mazuri yote yanayoonekana ni ya mtangulizi wake, mama Sijaona.
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom