Anna Mghwira: Tuendeleze mjadala wa Mikopo ya Elimu ya Juu na tuchukue hatua

Tuvumiliane kidogo, kukamilisha taratibu zote, inachukua muda kidogo kwa upande wetu.Asante

Mama, nimeanza kupata wasiwasi kidogo juu ya hili zoezi jema uliloliasisi, kwa vyovyote vile iwavyo ni lazima tutambue kwamba muda si rafiki yetu, tunapaswa kupewa utaratibu wa kuchangia mapema iwezekanavyo ili tuwe na muda mrefu wa kuikusanya hiyo michango na hivyo angalau tupate kiasi kikubwa cha fedha na kusaidia idadi kubwa zaidi ya wanafunzi.

Ninaendelea kusisitiza kwamba ninatambua umuhimu wa maandalizi mazuri kabla kuanza michango, lakini ni lazima tujue kwamba adui yetu ni muda, muda hautusubiri hata kama tunachofanya ni kitu muhimu (maandalizi).

Kwa mwaka huu wa masomo (2017/2018) ninategemea vilio kuongezeka zaidi, japokua mimi sio mtabiri ila hata kwa hisia tu.
Baada ya kuipitia hotuba ya bajeti ya wizara ya elimu kwa mwaka huu, imesisitizwa kwamba bodi ya mikopo itaendelea kutoa mikopo kwa wanafunzi wanaostahili tu.
Hofu yangu inakuja hapo kwenye NANI ANASTAHILI ? Kwa mujibu wa bodi na uzoefu wa mwaka jana, ni wazi waombaji waliosoma shule binafsi, waliosoma masomo ya sanaa na watakaochaguliwa kozi zisizo za kipaumbele watamwaga machozi yao tena mwaka huu (kwa bahati nzuri) kama kiwango cha mwaka au (kwa bahati mbaya) zaidi ya mwaka jana.

Please mum, don't tell us to wait any longer.

Ni katika kukumbushana tu. Nakutakia muda mwema.
 
Ninaikumbuka vema kauli ya mama Salma Kikwete kuwa nanukuu: " Mtoto wa mwenzio ni mtoto wako." Leo watoto wa wenzetu wameingia tatizo la kukosa mikopo ya elimu ya juu; tuwasaidie kama watoto wetu.

Ninapenda kuwaomba akina mama wote nikianza na Mhe mama Salma Kikwete aliyeasisi usemi na hatua hii, tushirikiane kunusuru maisha ya elimu ya watoto walioko vyuoni wenye sifa ya kuwa na mikopo lakini hawakufanikiwa kupata mkopo. Tuwahamasishe vijana waliobakia mitaani na majumbani kujiunga na vyuo vikuu kuanua akili zao changa kukidhi ushindani wa sasa kimaisha.

Naomba akina mama wote viongozi, wazazi, walezi, wafanya bishara, waajiriwa, wanaharakati bila kujali itikadi zetu za aina yoyote tusimame kama wanawake wazazi wenye nia kuejnga taifa la watu walioelimika tuunde mfuko wa kuwasiadia watoto wetu wafanikiwe kumaliza masomo yao kwa ujenzi wa taifa letu.

Nikitoka na mama Kikwete ninaomba wake za marais wote waliopita kuanzia na mama Karume (mzee marehemu na Rais aliyemaliza mda wake) mpaka mama Janet Magufuli anayenivutia sana kwa kuonesha moyo wa amani sana kwa taifa letu.

Baada ya hao nimuombe mama Anna Makinda na wabunge wanawake wote waliopo na waliomaliza tangu uhuru wa nchi yetu tuungane kumsaidia kila mtoto wa Tanzania mwenye uwezo wa kusoma asome.

Kisha kwa niaba ya wanawake wafanya bishara niombe kitengo cha wanawake cha TCCIA, Baraza la Biashara la wanawake...tukubali wito huu: Tuungane kama wazazi na walezi chini ya kauli mbiu: Mtoto wa mwenzio ni mtoto wako...tuunde mfuko wa elimu kwa ajili ya vijana wetu.

Niombe vyama vya wana-taaaluma: waalimu, madaktari, wahandisi, watumishi wa umma, mabenki, makampuni yote ya ndani na ya kigeni, asasi za kiraia za ndni na za kimataifa, balozi zetu zote, tuungane kuunda chombo hiki kuwasaidia vijana wetu.

Nimeguswa sana na mahangaiko ya vijana wa vyuo vikuu. Ninawashukuru wachache waliofika kwangu kueleza changamoto zao. Mmenihamasisha kuchangia kidogo elimu yenu lakini ninaomba hili liwe suala la kitaifa.

Ninaomba wanawake wenzangu popote tulipo tuwasiliane tuunde umoja huu kuwaimarisha na kuwapa tumaini vijana na janga la kukosa elimu ya juu kama wana sifa za kuipata.

Tuweke kando siasa, dini, kabila, ukanda ama aina yoyote ya kigezo kufanikisha jambo hili. Ninawashukru sana. Kesho kuna wanafunzi watashindwa kufanya mitihani kwa kukosa ada kidogo tu ya laki kuanzia 5-8. Mfuko wa mama Salma, Mfuko wa mama Mkapa wa Fursa sawa kwa wote, Taasisi ya Benjamini mkapa, Taasisi ya Jakaya Kikwete, Taasisi ya Mwalimu Nyerere, na zingine, tusaidiane kukamilisha azima hii. Na mimi nimeanzisha Taasisi ya Mama Anna Mghwira kwa ajili ya kushughulikia masuala ya aina hii.

Nitawashukuru sana kwa niaba ya vijana wetu, tuenzi elimu yao kwa kuunganisha nguvu zetu hivi. Mnisamehe kwa kuandika mtandaoni. Nimejaribu njia za kawaida za simu sikufanikiwa sana. Hapa ninajua kila moja atapata taarifa. Mapungufu yangu yasizuie jambo hili kutendeka. Jinsi tulivyo changia madawati, sasatuchangie elimu ya juu.

Niombe wizara na Bodi ya mikopo ya wanafunzi kutoa ushirikiano tutakapouhitaji utaalamu muwe nasi bega kwa bega.

Mungu atubariki wote, aibariki Tanzania.

Asanteni tena, ni mimi mama Anna Mghwira
kuna wanafunz wengine wa elimu ya juu n wanafaika wa mikopo na walipostpone mwaka na taarifa ambayo tunapata et kwamba kwa huu mwaka ambao tumerud chuo hatuwwez kupewa mkopo naomba wahusika watuangalie katka hlo lina ukweli au#loanboard
 
Hongera Mama Kwa Uteuzi, Sasa Ukafanyekazi Siasa Basi.. Mambo mengi yalisemwa na mengi yakaendelea kusemwa katika siasa za nchi yetu Mh. Rais akakuteua wewe. Nakuomba uache siasa ufanyekazi. Mh makonda anafanyakazi hana siasa siasa. Ufanye hivyo uache siasa
 
Ninaikumbuka vema kauli ya mama Salma Kikwete kuwa nanukuu: " Mtoto wa mwenzio ni mtoto wako."
Leo Mama Kikwete AMEGEUKA nguzo ya chumvi. Hamtetei tena Mtotowa Kike. Anasema anayepata mimba shuleni ASISOME! Na wewe Mama Mghwira umeteuliwa katika nafasi ambayo, kwa mujibu wa katiba CCM, utahudhuria, KISHERIA, vikao vukuu vya Mkoa vya chama "kisichokuwa chako". Hawa wamama walioheshimika, mbona WANATUANGUSHA?
 
Hongera Mama Kwa Uteuzi, Sasa Ukafanyekazi Siasa Basi.. Mambo mengi yalisemwa na mengi yakaendelea kusemwa katika siasa za nchi yetu Mh. Rais akakuteua wewe. Nakuomba uache siasa ufanyekazi. Mh makonda anafanyakazi hana siasa siasa. Ufanye hivyo uache siasa
Cheo chenyewe ni cha kisiasa, sema akafanye siasa safi.
 
Mama umetuangusha, hiyo ilani ya CCM uliyopewa leo kipindi cha uchaguzi si ulikuwa unaipinga? Je yale matatizo uliyokuwa unayasema kwa ilani hiyo utayatatua? Some of us tulikuona kama kiongozi wa kipekee lakini ki ukweli umetuangusha
 
Mama umetuangusha, hiyo ilani ya CCM uliyopewa leo kipindi cha uchaguzi si ulikuwa unaipinga? Je yale matatizo uliyokuwa unayasema kwa ilani hiyo utayatatua? Some of us tulikuona kama kiongozi wa kipekee lakini ki ukweli umetuangusha
ukweli ni kwamba tatizo tumbo Singojr:
 
ukweli ni kwamba tatizo tumbo Singojr:
Yaani huwezi kuamini yule mama niliyemuona kichwa another hope kwa watanzania wanyonge leo kasmile akipewa ilani kandamizi. Ilani isiyo na hata mpango ya katiba mpya. Ataenda lakini hii itamuwinda i wish fahamu zimrudie mapema.
 
Jamani huu Uzi ni mahsusi kuhusu masuala ya mikopo (hata kama aliyeuanzisha ndiye mteuliwa), kama mna hoja, pongezi, malalamiko na madukuduku kuhusu uteuzi wake tafadhali nendeni kwenye nyuzi zingine (ziko nyingi sana zinazohusu uteuzi wake) mkazungumzie huko. Uzi huu si sahihi sana kwa jambo hilo, tusijaribu kupoteza maudhui ya huu Uzi.
 
Nakutakia utekelezaji mwema wa ilani ya CCM. Kumbe hukua mwenzetu kila la kheri katika majukumu yako mapya.
 
Jamani huu Uzi ni mahsusi kuhusu masuala ya mikopo (hata kama aliyeuanzisha ndiye mteuliwa), kama mna hoja, pongezi, malalamiko na madukuduku kuhusu uteuzi wake tafadhali nendeni kwenye nyuzi zingine (ziko nyingi sana zinazohusu uteuzi wake) mkazungumzie huko. Uzi huu si sahihi sana kwa jambo hilo, tusijaribu kupoteza maudhui ya huu Uzi.
Kama haamini katika ilani ya aliyoitetea na kuzunguka nayo nchi zima. Tutamwamini vipi kwa thread ya JF
 
Kwenye siasa hakuna adui wala rafiki wa kudumu


Anything can happen..

Mwacheni mama Anna akapige kazi..
 
Kama haamini katika ilani ya aliyoitetea na kuzunguka nayo nchi zima. Tutamwamini vipi kwa thread ya JF
Bora mmuunge mkono tuu akatende haki...sidhani kama atarudi nyuma

Ila lazima muelewe wanasiasa wana nia moja siku zote...

Watanzania tunapaswa kujifunza na kuelewa hili..

Mwisho wa siku ninyi msioelewa wanasiasa ndio mnakufa kwa presha.

If you can't fight them, join them- Ndicho alichokifanya Mama Anna.

All the Best to her..
 
Kama haamini katika ilani ya aliyoitetea na kuzunguka nayo nchi zima. Tutamwamini vipi kwa thread ya JF

Nilikua nazungumzia maudhui ya huu Uzi ukilinganisha na kinachojaribu kujadiliwa hapa, nimeshauri muende kwenye nyuzi kadhaa zinazozungumzia huo uteuzi (zipo, tena nyingi tu). Hapa panapaswa kuachwa pashughulike na namna ya kuwasaidia wahanga wa gharama za elimu ya juu. Kuhusu hayo masuala ya ilani, anachokiamini aliyeteuliwa na mengineyo mengi yanayokwenda pamoja na uteuzi wake yakajadiliwe kwenye nyuzi husika. Nilimaanisha hivyo tu mkuu.
 
Wazo zuri, na uwezo kupitia kwa wananchi wapenda maendeleo upo. Serikali kukwepa jukumu la kugharimia elimu ya juu ni ubinafsi wa viongozi wetu, na mgawanyo usio sawa wa raslimali zetu. Mafanikio ya elimu ya vijana wetu ndio mafanikio ya taifa. Elimu bure ya msingi mpaka f4 si mzigo mkubwa kwa familia. Uwezo kulipia chuo kikuu ni mgumu. Wingi wa mikopo inayotajwa kutolewa na sesikali ina mapambio, kuna wengi wamepata %ge ndogo sana. Wazo hili likijitangaza kwa wananchi, wengi watahamasika kuchangia. Mchango wa sh 1000 tu kwa mwezi, kwa watu 1m, kwa mwaka 1, mfuko wako utakuwa sh 12bn za kusomesha watoto elfu 6 kwa 2m.
 
Back
Top Bottom