Mwanamaji
JF-Expert Member
- Apr 20, 2013
- 2,896
- 4,495
Tuvumiliane kidogo, kukamilisha taratibu zote, inachukua muda kidogo kwa upande wetu.Asante
Mama, nimeanza kupata wasiwasi kidogo juu ya hili zoezi jema uliloliasisi, kwa vyovyote vile iwavyo ni lazima tutambue kwamba muda si rafiki yetu, tunapaswa kupewa utaratibu wa kuchangia mapema iwezekanavyo ili tuwe na muda mrefu wa kuikusanya hiyo michango na hivyo angalau tupate kiasi kikubwa cha fedha na kusaidia idadi kubwa zaidi ya wanafunzi.
Ninaendelea kusisitiza kwamba ninatambua umuhimu wa maandalizi mazuri kabla kuanza michango, lakini ni lazima tujue kwamba adui yetu ni muda, muda hautusubiri hata kama tunachofanya ni kitu muhimu (maandalizi).
Kwa mwaka huu wa masomo (2017/2018) ninategemea vilio kuongezeka zaidi, japokua mimi sio mtabiri ila hata kwa hisia tu.
Baada ya kuipitia hotuba ya bajeti ya wizara ya elimu kwa mwaka huu, imesisitizwa kwamba bodi ya mikopo itaendelea kutoa mikopo kwa wanafunzi wanaostahili tu.
Hofu yangu inakuja hapo kwenye NANI ANASTAHILI ? Kwa mujibu wa bodi na uzoefu wa mwaka jana, ni wazi waombaji waliosoma shule binafsi, waliosoma masomo ya sanaa na watakaochaguliwa kozi zisizo za kipaumbele watamwaga machozi yao tena mwaka huu (kwa bahati nzuri) kama kiwango cha mwaka au (kwa bahati mbaya) zaidi ya mwaka jana.
Please mum, don't tell us to wait any longer.
Ni katika kukumbushana tu. Nakutakia muda mwema.