Anna Mghwira: Tuendeleze mjadala wa Mikopo ya Elimu ya Juu na tuchukue hatua

Sina hamu na mikopo ya HESLB nimesha omba mara 2 na ku appeal mara 2 bila mafanikio yoyote. Ashukuriwe mungu nipo mwaka wa 3 sasa nategemea kumaliza degree yangu ya Logistics and Transport managemnt mwezi wa 7. Japo nimesoma kwa shida na kudhikika kwa kiasi chake lakini nashukuru namaliza salama.
 
Asante Kitukuu. Katika kuendelea kupata mkono wa umma nimeendesha vipindi vya luninga azam, chanel ten na star tv. Mwitikio ni mzuri. Ninaomba tangazo likitoka tuanze kutoa si


Ndugu Mkwepa Kodi, naona umekwepa na maneno sasa. Sijui kama wengine wamekuelewa. Mimi nimetoka kapa.
Nina maanisha hivi nina mdogo wangu anasoma conas (UDSM) na kasoma shule za kata from kindergarten to university levels yupo mwaka wa kwanza just mwaka huu anasoma kwa kuunga unga since anakaa na dada yake anayemaliza mwaka huu sasa sjajua n vigezo gani vinahuska kuwapa watu mikopo maana walisema sciences wote watapata mikopo.... Na watoto n wa wakulima na sio wafanyakazi wa selikali. Nawasilisha kwa kufanyia marekebisho.
 
Watanzania wengi ni maneno na porojo tu hawana nia ya kuwasomesha Watanzania wenzao. Wamekalia majungu na kutafuna pesa za walipa kodi. Kazi kubwa tuliyonayo Watanzania ni kufahamu kwamba hakuna kitu cha bure, then kila mtu lazima alipe kodi, na wale ambao ni wezi wa pesa za walipa kodi ambao ni dada zetu, shemeji zetu wake/waume zetu na watoto wetu tusiwaonee aibu. Tuwafikishe kwenye vyombo vya dola wachukuliwe hatua kwa sababu tunawafahamu. Jinsi tunavyowachelewesha ndio jinsi tunavyochelewa kuendelea, msumeno lazima ukate kila upande usichague. Tukiwashughulikia wezi wa ndani tutaweza kumsomesha kila Mtanzania.
 
Hata mimi nilikuwa kimya kwa lengo la kuweka mikakati sawa, kukutana na wadau mbalimbali na kuona uwezekano wake kila eneo. Watu wengi wanaunga mkono. Tuanze mara tangazo litakapotoka wiki hii.
Kwa upande wangu najivunia sana we we, Tanzania ingepata watu watano au kumi kama wewe tungekuwa mbali sana. Watu wengi sana wanajua kucritisize tu na kuongea ili wao waonekane bora kuliko wengine, hawajui kuwa sufuria masizi ni asili yake, hata ukisugua kesho yanarudi tena. Ww umeonyesha kitu cha tofauti sana, badala ya kulalamikia serikali kumekuja na njia ya kuwawezesha. We proud of u kwa niaba ya wanafunzi wenzangu. Mungu akubarki sana mama.
 
Huu mpango uwe ni mfuko endelevu wa Vizazi na vizazi, kila mtanzania atakaeguswa achangie na michango iwe ni enedelevu pia, ili taifa letu liweze kusonga mbele kielemu pamoja na kutimiza ndoto za vijana wetu, Mwenyezi mungu ajalie Kheri ndani yake
 
Mama, asante na hongera kwa wazo hilo la kujenga. Mimi ninaomba nitoe ombi langu mahsusi kwako/kwenu kama taasisi, katika utoaji wa hiyo mikopo, muwaangalie kwa jicho la huruma pia na wanafunzi wanaojiunga na elimu ya juu kwa sifa linganifu (equivalents). Kwa kweli imekua ni vigumu mno kupata mkopo toka bodi kama umetokea diploma, imekua ni kana kwamba kuwa na diploma maana yake una ajira tayari au una hela tayari, ninakuomba sana katika vigezo vyenu visibague eti tu kwa sababu mtu katokea diploma ndio asipate mkopo. Ninaongea kama mhanga niliyekwama kuendelea na masomo na ninawajua wenzangu wengi mno waliokumbwa na kadhia hiyo.
Kila la heri, Mungu atalisimamia hili na ninaamini litafanikiwa.
Ni kweli elimu haina mwisho na haina madaraja katika utoaji wake. Kila mwenye nia ya kupata elimu ya kiwango chochote ni budi aipate, kwa hali na mali. Tuombe mfuko uanze mapema, ili tujue una nguvu kiasi gani na unaweza kufanya kiasi gani.
 
Huu mpango uwe ni mfuko endelevu wa Vizazi na vizazi, kila mtanzania atakaeguswa achangie na michango iwe ni enedelevu pia, ili taifa letu liweze kusonga mbele kielemu pamoja na kutimiza ndoto za vijana wetu, Mwenyezi mungu ajalie Kheri ndani yake
Amina. Ndilo ombi na lengo letu pia.
 
Wazo zuri sanaa asante kwa kutoa progress, huu uzi ungekua wa kuikejelii serikali zingekua page 1000plus za replies lakini cha ajabu kitu cha msingi kwa taifa letu watu wanapita tuu
Hakuna tatizo. Tuendelee kujadili. Watu wameonesha mwamko sana hata kama hawachangii hapa, watachangia mara utaratibu utakapokaa vizuri.
 
Nnd
Wazo ni la kialinacha,haya mambo yaliwezekana kwenye vyama vya ushirika vya uchagani na haikuwa bure bali kwa members against makato yao.pia kwa watoto wenye akili sio mabumbumbu, waulize kina mengi, sasa huyu anna anataka mimi nikachangia watoto.wawatu kwa uchungu gani wakati tayari nakatwa.kodi? Hawa ndio wanataka kuongoza nchi kwa misingi ya ujamaa karne hii? Eti huyu mama ndio awe.fund manager wetu, deci? Pole anna this is a daylight.dream, anather project failure, cont me out
Nndondo, una haki ya kutoa maoni yako, na mimi nina haki kushirikisha ualinacha wangu. Ndivyo tulivyo. Walioitikia wakichanga ndipo tutajua kama inawezekana ama la. Ni kweli kuwa elimu inatakiwa kulipiwa kwa kodi zetu, lakini ni kiasi gani hizo na ziko wapi? Mpaka sasa imesaidia wangapi, kama Bodi tu inachukua hao wachache? Kama iko njia ya kuhakikisha kodi zinatosheleza kulipia elimu bure kwa wote, itakuwa vizuri kuipata. Kama hatujaileta hiyo njia tujaribu zingine kwa sababu wanaokosa wanajua walichokosa.
 
Hslb kumejaa rushwa tupu yaaan mpaka uhonge ndo upate mkopo
, maana hakuna cha vgezo wala baby ake na vigezo
 
kuchanga tutachanga ila unakumbuka hela ya tetemeko mama yangu ?
Nakumbuka sana Miss ...ila angalia pia kuwa huu utakuwa mfuko wetu sis wananchi, sisi na watoto / vijana wetu/ sisi na kila anayetaka kujiongeza kielimu lakini anashindwa kwa kukosa hii nyenzo ya malipo yake. Mpaka sasa wamejitokeza wanafunzi wengi ambao hawana mkopo, wanataka mkopo warudi chuo, waongeze maarifa, waongeze kasi yao katika taifa. Ninamini kila mpenda maendeleo wa nchi hii na hata nje ya nchi ataona nia na lengo letu.
 
Naam Tumeanza na hatua zinakuja japo kwa mwendo pole. tuvumiliane. Wanafunzi wengi wamejitokeza baada ya kusikia. Tutatangaza tarehe ya kuzindua....
Wazo zuri sana mfuko uitwe Anna Mghwira Education Support Trust Fund( AESTF) nitawaambia rafiki zangu pale kwa Mfalme kule redsea[/QUOTE
 
Mpaka sasa tunatembea nalo! Tukaze nia mfuko uanze kufanya kazi. Tuombe pia Mungu abariki juhudi hizi. Tangazo linachelewa kiufundi. Likiwa tayari kila kitu kitakaa hewani. Asanteni sana.
UOTE="dudus, post: 19835488, member: 38243"]Wazo zuri sana Mama Mghwira. Ila angalizo, kuna wale ma-plagiarists wazoefu ataibuka RC mmoja (safari hii anaweza kuwa mwingine); ataliteka wazo; litaenezwa kwa propaganda kali halafu mwisho wataliharibu na kujisifia chama cha wanyonge kimejaribu! Kuweni makini na hawa majamaa japo manasema maendeleo hayana itikadi au vyama lakini wao ni mabingwa wa kutafuta sifa kupitia migongo ya wengie japo wazoefu wa kuharibu.[/QUOTE
 
Akhsante sana mama,hoja ya msingi kabisa. Mimi niliwahi kupata wazo kwa ajili ya kuchangia elimu kwa watoto wetu.
Kama serikali inashindwa kutoa mikopo kwa wanafunzi wote wanaostahili,basi tuweke taratibu,sheria au kanuni ambazo zitalazimisha halmashauri husika ambapo mwanafunzi anatoka kuhakikisha mwanafunzi huyo anasomeshwa nao. Na hili kuna Halmashauri wanafanya tayari. Pia kama tunaweza kuchangia sherehe mbalimbali ( mpaka arobaini ya mtoto) na kupatikana mamilioni,kwa nini tusichangishane kwa hawa watoto ambao wamekosa mikopo? Utengenezwe utaratibu tu hata wa kutoa asimilia fulani za michango ya sherehe kwa ajili ya kusaidia hawa vijana. Hili kimsingi ni jukumu la serikali,lakini kama pamoja na kelele zote zilizokwisha pigwa kuhusu wanafunzi wote wenye sifa za kupewa mikopo wapewe,bado wahusika hawaonyeshi kujali. Sasa tuache kuwasaidia vijana wetu kusoma kisa tu si jukumu letu ni la serikali au tuwasaidie ili kujenga Tanzania bora ya kesho.
Kweli kabisa Joel, tusaidie kujenga tanzania mpya bora! Twendeni na mfuko huu kupunguza tatizo. Halmashauri zitakazochukua zitapunguza sehemu nyingine nk. Tupanue wigo, tusifunge njia.
 
Mama yangu umetoa wazo zuri,nachelea kusema watu wanaweza kuchukulia unataka kujijenga kisiasa na kumbuka ulikuwa kwenye kinyang'anyiro cha uraisi.
Kumbuka serikali iliyopo madarakani ilisema watapewa mikopo wale tu waliosoma shule za serikali kwa maana ya kuwa waliosoma private wazazi wao wana uwezo!!!???
Uangalie usije kuwa unataka kuichonganisha serikali na wananchi wake maana tunatofautiana uelewa.
Ili kutoingia kwenye mgogoro,ningeshauri uanzie huko huko serikalini kwa kuwaomba wakukubarie wazo lako.
Naamini,watanzania wengi watakuunga mkono na si wanawake tu kama uluvyoainisha.
Watoto wamebaguliwa, kuna watoto wa watanzania na walipa kodi ndo wanafaidi kodi za wazazi wao!!!!
Hili huwa linatia hasira kama sio kusikitisha....
Hongera mama kwa kuja na hili wazo,simama nali,komaa nalo mpaka uone matunda yake.[/QUOTE

Amina. Twendenipamoja kwa nia moja tu: Kuhakikisha kila anayetaka elimu anaipata kwa kila namna halali.
 
Mama Anna;

Umetoa wazo zuri sana! Umetoa mwelekeo..!

Humu najua watu wataliunga mkono kwa maneno tuu na pongezi kwa wazo zuri..

Nilifikiri huu wito ungefanya event kabisa ili uliadress vizuri..either uitishe Press au kitu kama fundraising na kuwaalika watu wote walengwa..

Humu kuna members kama 400,000 hivi...bado tunataka ifike kwa watu zaidi hata watu 24milion ambao ni nusu ya Population yetu...

Ikiwezekana zihusishwe Taasisi tuu, watu binafsi na NGOs ! Serikali ikae pembeni manake wataleta siasa..! Hili suala wameshindwa kwa sababu watu wako after political gain..

Leo tukishindwa kusomesha hiki kizazi..miaka 50 ijayo hili taifa litapotea kabisa..

[HASHTAG]#Elimukwanza[/HASHTAG]
[HASHTAG]#Uzalendokwanza[/HASHTAG]
[HASHTAG]#Mikopo[/HASHTAG] elimu ya juu
Asante ! Tuendelee tusonge mbele, inawezekana!
 
Elimu bure kutoka Darasa la kwanza mpaka Kidato cha nne, lakini ukifika hapo juu hakuna mikopo sasa hii elimu bure ina maana gani kama siyo danganya toto Maana ya elimu bure ni kupunguza gharama za kusomesha watoto lkn hapo juu mikopo inazuiliwa sasa hapo jamii imesaidikaje kupunguza gharama za kusomesha wakati elimu ya juu ndo gharama kuliko hapa chini basi hapa chini gharama zirudi ili wapate fedha za kukopesha, Tuseme ELIMU bure wamekurupuka...
 
75 Reactions
Reply
Back
Top Bottom