Anna Abdallah naye ni fisadi?

BAK

JF-Expert Member
Feb 11, 2007
124,792
287,994
Ni kipi kilichomfanya huyu mama amshambulie Anne Kilango? Anne Kilango alizungumza nini kibaya ndani ya Bunge hata kikamgusa vibaya Anna Abdallah? Je, Anna Abdallah amewahi kushiriki kwenye ulaji wa kifisadi? Je, mumewe Pius Msekwa ambape aliwahi kuwa Spika wa Bunge na sasa Naibu Mwenyekiti wa CCM ni fisadi? aliwahi kushiriki kwenye ulaji au mradi wowote ambao machoni mwa Watanzania ulikuwa na harufu harufu ya kifisadi?

Anna Abdallah amshambulia Kilango

na Martin Malera, Dodoma
Tanzania Daima~Sauti ya watu

MJADALA wa Bajeti ya 2008/09 jana uligeuka sehemu ya malumbano, baada ya mbunge na mwanasiasa mzoefu na kiongozi wa juu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) kuamua kujibu mapigo ya hoja zilizotolewa na mwanaCCM mwenzake.

Katika hali ambayo haikutarajiwa, Mbunge wa Viti Maalum, Anna Abdallah, alitumia muda wake mwingi kuchangia bajeti hiyo kujibu kauli kali zilizotolewa juzi na Mbunge mwenzake wa CCM, Anne Kilango Malecela (Same Mashariki) kuhusu wizi wa mabilioni ya shilingi kutoka Akaunti ya Malipo ya Madeni ya Nje (EPA) na Benki Kuu (BoT).

Akionekana dhahiri kutofautiana na Kilango, mbunge huyo alipinga katakata kuwapo kwa watu wanaotisha wenzao au wabunge waoga kuchangia mjadala wa bajeti ndani ya bunge hilo.

Alisema suala la wizi wa fedha za EPA halipaswi kuwagawa wabunge kwani tukio hilo ni kilio cha kila mbunge na si cha watu wachache kwani hakuna mbunge anayeshabikia ufisadi.

Abdallah, ambaye ni mke wa Makamu Mwenyekiti wa CCM, Pius Msekwa, alisema kila mbunge anataka fedha hizo zirejeshwe, lakini kinachowatofautisha ni kwa baadhi ya wabunge kuweza kuzungumzia suala hilo kwa mbwembwe.

Huku akishangiliwa na baadhi ya wabunge kwa nguvu kiasi cha kuvuruga hotuba yake mara kadhaa, mbunge huyo ambaye pia ni Mwenyekiti wa Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT) ambayo ni jumuiya ya CCM, alitaka suala hilo kutowagawa wabunge.

"Suala la EPA lisitugawe wabunge humu ndani. Kila mbunge anataka fedha hizo zirejeshwe, tofauti yetu ni kwamba wengine wanazungumza sana, tena kwa mbwembwe nyingi, wengine wanazungumza kwa upole, lakini nia yetu ni moja," alisema Abdallah.

Mbali ya hilo, aliwataka wabunge waliokuwa wakishangilia kwa nguvu kwa kupigapiga meza zao, kutulia kwani walikuwa wakimmalizia muda wake na kusema: "Jamani, nani hapa anaogopa? Hatuogopi kitu, tena hakuna anayetishwa kwani lengo letu ni moja." Abdallah ambaye amewahi kushika nyadhifa mbalimbali ndani ya chama na serikali, alivirukia vyombo vya habari kwa kuviweka kwenye kundi moja na kuviita chama cha siasa kisicho na usajili, kwa kuwa ndivyo vinavyofanya wabunge wanaonekana wana mtafaruku ndani ya Bunge, kwamba kuna kundi linashabikia ufisadi na lingine halishabikii.

Ingawa hakutaja jina la mbunge yeyote aliyedai kulizungumzia suala la EPA kwa mbwembwe, lakini ni dhahiri alikuwa akimlenga Kilango ambaye juzi alizungumzia fedha za EPA kwa ukali wakati akichangia mjadala wa hotuba ya bajeti.

Akizungumza kwa kujiamini na sauti ya juu juzi, Kilango alisema yuko tayari kufa kupigania fedha za EPA ambazo ni zaidi ya sh bilioni 133, zirejeshwe kama alivyoagiza Rais Jakaya Kikwete, vinginevyo bungeni ‘patakuwa hapatoshi'.

Kilango, ambaye pia ni Mwenyekiti wa Kamati ya Maadili ya CCM Taifa na mmoja wa wabunge waliokuwa mstari wa mbele kulaani ufisadi katika kashfa ya Richmond iliyosababisha mawaziri watatu kujiuzulu, akiwemo aliyewahi kuwa Waziri Mkuu, Edward Lowassa, alizungumzia pia ufisadi mwingine wa zaidi ya sh bilioni 216 zilizokopwa mwaka 1992 kupitia Mpango wa Uagizaji Bidhaa Nje (Import Support), na kutaka nazo zirejeshwe mara moja.

Kilango ambaye pia ni mke wa mwanasiasa mkongwe, John Malecela, katika hotuba yake ya juzi iliyowafurahisha wengi, alisema vitisho dhidi yake haviwezi kamwe vikamfanya abadili msimamo wake kwa madai kuwa anafanya hivyo kwa maslahi ya serikali, chama chake cha CCM na kwa wananchi wa Jimbo la Same Mashariki, waliomtuma kuwawakilisha bungeni.

"Mheshimiwa Spika, Mwanafalsafa wa Kigiriki, Socrates siku moja alipokuwa sokoni, alihubiri kuwa watu wengi makini duniani huwa wako tayari kufa kwa ajili ya kile wanachokiamini, ukweli na haki. Alipotakiwa kuikana kauli yake, alisema hawezi, wakampa sumu, akanywa, akafa kwa kusimamia ukweli.

"Mheshimiwa Spika, tumebaki kulalamikia ufinyu wa mapato ya ndani, lakini tumesahau kuwa fedha nyingi zinaliwa na kikundi cha watu wachache, watu wameiba fedha za EPA, rais anataka fedha hizo zirejeshwe, na mimi nasema siogopi vitisho, fedha hizo zisiporudishwa, hapa patachimbika, patakuwa hapatoshi hapa, Mheshimiwa Spika," alisema Mama Kilango.

Katika hali inayoonyesha mgawanyiko wa dhahiri miongoni mwa wabunge wa CCM ndani ya Bunge, hasa linapofika suala la ufisadi mkubwa, baadhi ya wabunge waliozungumza na Tanzania Daima nje ya Bunge kwa sharti la kutotajwa majina yao, walishangazwa na hatua ya Anna Abdallah kuonyesha kutofautiana na Anne Kilango waziwazi katika suala la ufisadi wa fedha za EPA.

"Mama Anna kama angetaka kuunga mkono hoja ya Mama Kilango, asingesema eti wapo wanaozungumza kwa mbwembwe kuhusu suala la EPA. Hapo anaonyesha hakufurahishwa na hoja ya Mama Kilango ama kwa sababu za kutotaka kumjengea umaarufu zaidi au kwa sababu anazozijua," alisema mmoja wa wabunge wa Mkoa wa Dar es Salaam.

Hata hivyo, wabunge wengine waliungana na Mama Anna Abdallah na kumtetea.

Mbunge mmoja alisema ni kweli kwamba wabunge wote wa CCM wana uchungu, na kwamba hakuna sababu ya Mama Kilango juzi kuelezea kuwa yupo tayari kufa kana kwamba yeye pekee ndiye mwenye uchungu na fedha hizo.

Mjadala wa hotuba hiyo ya Bajeti ya Waziri wa Fedha, ilihitimishwa jana kwa Bunge kupitisha bajeti hiyo.
 
Maoni ya Wabongo na hata wasio wabongo kuhusu sakata hili

HAPA NAONA KUNA JAMBO.
MSEKWA ALIDHALILISHWA NA WANA MTANDAO AKAUKOSA USPIKA. MALECELA ALIDHALILISHWA NA WANA MTANDAO AKAUKOSA URAISI. WAKE ZAO WANALUMBANA, KUNA NINI?
ANA ABADLAH AMEKAA SANA SERIKALINI, ANAONA BARIDI KUKAA NJE, LAZIMA AJIKOMBE ILI MABADALIKO YANAYOKUJA MUDA SI MREFU APATE NAFASI YA KURUDI.

KILANGO KASEMA KWELI, NDANI YA CCM TUNATISHWA SANA NA KUNDI LA EPA.

Wasalaam
Mbunge wa Zamani Kidogo
Ujerumani

na MASALAKULANGWA, GERMANY, - 21.06.08 @ 08:40 | #17771

Mimi si mtaalam sana wa siasa zetu za Tanzania.Mama Malechela ni mbunge wa kuchaguliwa na wapiga kura kwa hiyo lazima awe mkali kutetea maslahi ya wananchi,Mama Msekwa ni mbunge wa viti maalum hana deni.Mama Msekwa unapashwa kusoma alama za nyakati,huko unakotaka kuturudisha wenzio ndiyo tumeshaanza kutoka,nakuhurumia,waachie vijana!!
Felicitation Mama Malechela!!!!KUNA MTU ALISEMA JANA,KAMA KUNA WABUNGE WANAONA WATU CCM HAWATAKI KUBADILIKA,JUMP OUT ANZISHA CHAMA MTAWABWAGA CCM 2010.

na David Villa, Tanzania, - 21.06.08 @ 08:47 | #17775

Ana hataki mabadiliko bali anataka iwe kama kawaida ya kila siku. Anataka 'wasiseme' akiamini mambo yatajiweka sawa yenyewe. Anasahau mambo yamefika hapo kwa sababu serikali ya CCM na wabunge kwa ujumla wamekua hawasemi na kwamba wengi watishika na kukosa nafasi zao au kupanda nafasi zao.

na David, Dar. TZ, - 21.06.08 @ 08:53 | #17778

ANNA ABDALLAH huna jipya la kutueleza sasa hivi nia yetu hatutaki watanzania tuwe na ile kasumba ya bunge kutumika kama muhuri tu.Kwa kifupi wabunge hususa wa CCM mmeonyesha woga ktk suala la EPA .Mwache kilango aseme ukweli ndio maana mnapewa vitabu vya bajeti halafu mnasomewa bagdet speech inayotofautiana na vitabu mnakaa kimya tu .hamuoni ni aibu tupu kwa serikali.Sijui wahisani watatuelewa vipi.Ingekuwa ni nchi zilizo endelea waziri wa fedha angetakiwa ajiuzulu mara moja lakini kwa bongo hiyo ni sawa tu ,bustard

na adili, uk, - 21.06.08 @ 09:06 | #17783

Mama Anna ni mmoja wa viongozi wa kale ambao hawataki kubadilika! Tangu nchi hii ipate uhuru yeye na mme wake wamekuwepo serikalini na hawataki kuachia vizazi vipya! Wote wawili ni mbumbumbu wanaoabudu u miungu watu na wanaona kuwa wao pekee ndio wanatakiwa kubaki mabwana na jamii nyingine iendelee kuwa matwana!
Anna na Mme wake Msekwa ni waasisi wa kilichokuwa kikiitwa Siasa ni kilimo, yaani wao walikuwa wakipiga domo kaya la siasa huku wananchi wakilima, wakiwashibisha hadi kusaza na kulewa kiasi cha kupindukia ndiyo maana wanajaribu kuwashangaa wanaotaka haki!
Anna na Mmewe ni waanzilishi wa siasa za kudumu kwa fikra sahihi za mwenyekiti wa chama na ni wafuasi wazuri wa jamii ya Kingunge, wakifuata msimamo wa CCM wa kuongea ukweli ndani ya vyumba na kuuacha humo ukioza huku wananchi wakiendelea kupata taabu!
Umefika wakati wazee hawa waachie ngazi na waanze kuona ukweli ambao watanzania wanautaka!
Kwani inahitaji shule gani kujua kuwa wabunge na hata watu wengine wanaosema ukweli katika nchi yetu wanatishwa na pengine kuuawa! Labda nitoe mfano tena ambao ni tofauti na wabunge: yule mwanafunzi anayetoka katika jimbo la mmewe Anna alipatwa na nini baada ya kumuuliza yule mungu wa CCM kuhusu swala la viongozi wa CCM kushika mambo zaidi ya mawili? Yule mkemia Mkuu wa zamani marehemu Fupi alipatwa na nini alipotaka kuongea suala la ubovu wa chakula cha Mhindi? yuko wapi mwandishi Stan Katabaro wa lile gazeti la mfanyakazi?
Ifike wakati tukubaliane na ukweli usiohitaji ushabiki wa kisiasa ili nchi isonge mbele! Hapa Korea watu ni waaminifu na hakuna anayefanya ujinga unaotokea huko kwetu! Ipo haja ya kuhamishia baadhi ya adhabu zinazotolewa hapa huko kwetu ili kukomesha hayo madudu! Baadhi ya wabunge kama Ndesamburo wanaojua uzuri wa adhabu hizi wanahitaji kuungwa mkono ili na sisi tuanze kuzitumia!

na LCD, Pyongyang, DRPK, - 21.06.08 @ 09:08 | #17784

anna abdallah wewe ni ********* tu huna jipya tumekuchoka kama huogopi ulikuwa wapi mpaka mwenzio aseme kwenda zako akili zako zimezeeka

na ***** lee - 21.06.08 @ 09:14 | #17787

MHESHIMIWA MAMA ANNA ABDALLAH KUMBUKA YAFUATAYO KUTHIBITISHA KAMA KWELI UNA UCHUNGU NA NCHI;

1. ULIPOKUWA WIZARA YA UJENZI KUNA TETESI YA RUSHWA KUBWA KATIKA UJENZI WA BARABARA. KWELI ULICHUKIA UFISADI? ANGALUA MAGUFULI HATUKUSIKIA HATA HARUFU

2. ULIPOKUWA WIZARA YA AFYA, NI KWELI WEWE NI MWENZETU MWENYE KUCHUKIA RUSHWA? HATUYAONI HAYO KWA ALIYEKURITHI PROFESSOR MWAKYUSA.

3. MWACHE MAMA MALECELA ASEME. CCM WAKATI WA AWAMU YA 3 MLIINGIA KWA MBWEMBWE, MMEUZA NCHI HALAFU MNASEMA WENGINE WANASEMA KWA MBWEMBWE. MNASEMA KWA UPOLE MMEFANYA NINI? SI NINYI MLIUZA NCHI.

WAACHE WANAHABARI WAFANYE KAZI YAO. MLIPOKUWA MNASHABIKIWA NA RADIO TZ, TVT, UHURU NA MZALENDO, NAVYO VILIKUWA VYAMA VISIVYOSAJILIWA.

na B.J.M, DSM, - 21.06.08 @ 09:16 | #17789

hawa wabunge wa viti maaalum kweli wengine hawana machungu kabisa.sasa huyu mama alikua wapi asizungumze siku zote.mama kilango kazungumza sasa yeye anamkosoa kuwa kazungumza kwa mbwebwe, mama nanihi ulikua wapi siku zote wewe.hizi mbwembwe ndio tunazitaka maana wengine masikio yao wametia pamba, wewe endelea kukaa kimya na kula hela za wananchi kwa kutochangia kitu huko bungeni!!mama kilango tupo pamoja mama!!!

na lucas, ar,, - 21.06.08 @ 09:17 | #17791

huyu mama nilimuangalia wakati akitoa mchango wake bungeni. Hakuwa mwenyewe. kulikuwa na nguvu fulani sio dumba ( dizaini ya mtandao wa mafisadi)uliokuwa ndani yake.

hawana kwa kuwa ni kundi lenye nguvu na ushawishi mkubwa ndio limemtumia mama huyu, ambaye sikumbuki kama mipango yake ya kufunga ndoa na msekwa ilifanikiwa kutokana na pingamizi la mke mkubwa wa msekwa.

kundi hilo kwa kuwa haziivi na spika, na kwa kuwa spika alipigilia msumari baada ya kauli ya mama malecela kw amaneneo kuwa wana bahati ya kuwa na spika asiyeogopa, liliamua kumwandaa mama Msekwa.

huyu ameandaliwa pengine kwa ahadi kwamba siku moja anaweza kurudi serikali licha ya madudu yote aliyofanya akiwa wizara ya afya.

anachopaswa kuelewa kuwa UWT yao kwanza imekufa,haina kitu haina chake umebakia kuwa mkusanyiko wa mafisadi wasioweza kuwasaidia wanawake na watoto wa taifa hili.

badala ya kumsakama mama malecela, yeye katiikamchango wake angejielekeza kuishambulia serikali kwa kushindwa kutoa huduma kwa watanzania hali inayosababisha mmomonyoko wa maandili.

mwenyekiti wa umoja wa wanawake wa tanzania haoni kwamba taifa linaelekea kusiko kwenyewe?, huoni aibu unapokutana na vibinti vinavyotembea uchi, vijana wanaotumia mihardarati au hata kukemea mauaji ya wakongwe na maalbino ni mama wa aina gani wewe?



na mashilatu, ngara, - 21.06.08 @ 09:22 | #17796

Anna Abdallah,

Hujui maumivu makubwa mliyoleta ninyi wazee wetu ambao mlitugeuka ghafla kwenye awamu ya pili. Afadhali nyamaza.

Hamuwezi tena mkatufunga kitambaa usoni. Mnachukia ufisadi ninyi kweli? Mbona yote haya yalifanyika wakati mko mwenye BARAZA la MAWAZIRI? IPTL, NETGROUP, TTCL (badala ya kuuzwa kwa 120bn mkauza kwa 60bn), KIWIRA COAL MINE.

na NJETILE, DSM, - 21.06.08 @ 09:25 | #17797

ANNA ABDALLAHI NIKO TAYARI KUKUCHANGIA PESA ZA MATIBABU YA AKILI NCHI YEYOTE DUNIANI

na MOSHI, DAR , - 21.06.08 @ 09:25 | #17798

Utu uzima tena ndiyo unao msumbua tumsamehe hajui alitendalo,yeye baada ya kuchangia hojo anajibu hoja nyie hamoni kama kituko? anjibu hoja ye mkullo? pili kilango mbunge kupitia jimbo yeye ubunge wa hisani tofati nyingine ndiyo maana nasema huyu mama ameshachoka hana jipya.

na kassim,tegeta, dar,tz, - 21.06.08 @ 09:39 | #17807

LCD hapo juu mawazo yako tunayaheshimu. Lakini Tanzania haina lakuiga kutoka DPRK. Huko Bunge lao ni la rubber stamp, nchi inaendeshwa na mtu mmoja. Adhabu zao hazilingani na makosa, mtu anauliwa kwa kukataa kumuabudu Great Leader na Dear Leader. Akina Ann Kilango wa huko wameuliwa zamani. Ufisadi mkubwa ni kudhulumu roho ya mtu, eti kwa tofauti za kisiasa.

na Kassim., Ughaibuni., - 21.06.08 @ 09:46 | #17811

Anna nakuita!(nilisema toka jana ni jina la mwanangu)sikiliza wewe umeisha zeeka kama unataka heshima yako idumu pumzika,huna la kuchangia nyamaza tafadhari,unataka yatokee au yakukute kama ya miaka hiyooo ulipokuwa mkuu wa wilaya ya kahama??nyamaza tafadhari kumbukumbu bado tunazo,halafu kwa wasio mjua Anna Abdalah huyo mama amezaa na nusu ya viongozi serikali!!hata pius msekwa siyo mumewe wa ndoa,alivunja ndoa ya msekwa ndiyo anishi nae mpaka leo,kumbuka mama hata uhusiano wa mzee msekwa na mzee kawawa si mzuri (na wala hawaongei wala kusalimiana) kwa ajili yako!!uliwagombanisha kwa kuwachukua wote! sasa unasema kuna watu wanaosema sana tena kwa mbwembwe!!wacha mama kilango aseme kwa mbwembwe hata kwa machozi ikiwezekana,tutamsikiliza wewe unasema kwa njia gani emu tulia weee KIZEEE acha vijana wachape kazi,wewe huna la kuongea bungeni hesabu zako kubwa ni kuchukua viongozi mmoja baada ya mwingine na ukizidi tutakupaka zaidi,kama huna la kuongea bungeni si unyamaze!!?? wacha watu waongeee kwa mbwembwe si wanauhakika na wanachokisema!!wewe mama vipi akili zako ziko sawasawa kweli??watu wanazungumza mambo muhimu ya nchi wewe,unaleta uzuri!!(WADAU SAMAHINI KAMA NIMETUMIA KAULI YOYOTE YA KUWAUDHI,HUYU "AJUZA" AMENIKERA SANAA HANA ADABU)halafu wewe Anna kwanza ulimjibu kilango kama nani bungeni??ilitakiwa ajibiwe na waziri muhusika,au bado unaota uwaziri??FUNGA DOMO LAKO WEEE KIZEEE

na mwana wa matonya, leeds uk, - 21.06.08 @ 09:55 | #17813

Wewe Anna umesahau hapa Magu tulivyo kufanyizia, sasa endelea kulopoka kuwa hutishiki na mtu kama hutalala nje tena.
Wenzio wanauchungu na nchi yao wewe unaendekeza umbea na kutumiwa na hao Mafisadi wenzio, hatuwezi kukuvumilia kwa hilo, koma ukomae kutoa kauli za kipuzi kwenye masilahi ya nchi.

na Pipi, Magu, - 21.06.08 @ 10:15 | #17820

Mama Ana Abdalah, unachokiongea hakiingii akilini wala masikioni mwetu kabisa. Wewe inaonekana unafagilia UFISADI kwa staili fulani fulani, na kama ni kweli basi tunakuomba unyamaze kimya. Sisi tunamtaka Mama Anne Kilango Malechela, hongera sana, tuko nyuma yako na tuna enzi hotuba zako. Endelea kushika nyayo za huyu Mgiriki SOCRATES ambaye alikufa kwa kukutetea haki. Achana na akina Ana abdalah. ALUTA CONTINUA!!

na hamisi, Tanzania, - 21.06.08 @ 10:40 | #17824

ANNA, KAA KIMYA, KAA PEMBENI, NINI ULICHOFANYA WEWE HATA KIKAKUPANDISHA CHATI WAKATI UKIWA SERIKALINI??? HAAAAAKUNA!! NINI UMEISHACHANGIA BUNGENI KIKAKUPANDISHA CHATI?? HAAAKUNA
SABABU WEWE SI MUBUNIFU (IQ NDOGO) HIVYO MWACHE KILANGO NA HISIA ZAKE ZA KUJIELEZA NAWE KAA NA ZAKO.
WEWE NA WABUNGE WOTE WALIOKUSHANGILIA HUKO BUNGENI NI RUBBER STAMP.MNALITIA TAIFA HASARA BURE KUWA BUNGENI HAKUNA CHA MAANA MNACHOWEZA KUCHANGIA NI KUVUTA POSHO NK.

na msekwa junior, japani, - 21.06.08 @ 10:46 | #17826


Kweli watanzania naona sasa tumechoka kikweli na ufisadi. Mawazo ya watanzania nayaheshimu.
Anne KIlango Malechela Kaza buti mama ni wachache wenye moyo na ujasiri ulionao. Tuwakilishe watanzania. Kufa si ajabu. Watakuwa wamekutanguliza tu. Hakuna atayeishi milele. Ni bora ufe kishujaa kuliko kuendelea kutetea uzembe na uozo uliopo.
Ni aibu na fedheha kusoma na kusikia mambo yanayofanyika na kutendeka. Tusiishi kinafiki jamani tuwe wawazi na wakweli. Mungu atuwezeshe tubadike jamani.

na c3, Dk, - 21.06.08 @ 10:53 | #17828

Nadhani ifike wakati sheria ya kuwawekea vipindi visivyozidi viwili wabunge,tukifanya hivyo aina ya wabunge kama mama Anna Abdallah Msekwa [Kawawa] haitakuwapo.Historia inaanza kuonyesha kuwa hawa wabunge wa viti maalumu hawana habari na wananchi kama alivyo mama Anna Abdallah Msekwa [Kawawa]kwasababu hawapigiwi kura moja kwa moja na wananchi badala yake wanaabudu sana chama kwakuwa ndicho kilichowapeleka bungeni na siyo wananchi kama alivyo mama Anne Kilango Malechela mbunge wa kuchaguliwa na wananchi[jimbo la Same].Mama Anna Abdallah Msekwa [Kawawa] anasema pia kuna vyama vya siasa visivyo rasm [magazeti] vinawachonganisha wabunge,hivi huyu mama mbona anapenda kukurupuka [kuropoka] anataka yale magazeti ya enzi za chama kimoja yanayosifu kila upuuzi na uchafu wa wanasiasa uhuru,mzalendo,radio tanzania na TVT ?????.

na G KABONDE, ARUSHA,TANZANIA, - 21.06.08 @ 11:07 | #17830

Huyu mama alikuwa kwenye mabunge mengi ya zamani yaliyozea kubweteka na kutufikisha hapa tulipo, inaonekana hajui anachokisema mfano anashambulia vyombo vya habari hebu tujiulize, siku hizi tvt, itv, star tv, radio wanatuletea matukio live, tunaona wenyewe yeye anadai vyombo vya habari vinapotosha, kweli jambo linaloonekana zahiri yeye anashambulia vyombo vya habri, kaishiwa huyu hana jipya, hata hivyo hana wa kuwazungumzia maana ni mbunge wa viti maalum, aidha anaweza kuwa anamtetea mumewe maana si ndio vikongwe vya chama visivyo na jipy

na Peter, TZ, - 21.06.08 @ 11:11 | #17831

KUNA UWEZEKANO HUO ANNA MWENYEWE AKAWA NI MUHUSIKA WA UFISADI.KAULI YAKE YA KWAMBA WABUNGE WOTE WANACHUKIA UFISADI SI KWELI.MLE NDANI KUNA MAFISADI WENGI TU.WANAWEZA KUWA SI WAHUSIKA WA FEDHA ZA EPA MOJA KWA MOJA,LAKINI WENGI WAO NI WAHUSIKA KWA MIKATABA MIBOVU KAMA RICHMOND.WANGEKUWA NA UCHUNGU NA NCHI TZ ISINGEKUWA HAPO ILIPO.WALIOSAINI MKATABA WA IPTL WAMO HUMO,KUNUNUA RADA WAMO HUMU BUNGENI

na lugayila, Norway, - 21.06.08 @ 11:18 | #17832

****** huyu mama kazoea kudandia wanaume wenye madaraka kaanzia kwa Kawawa kaishia kwa Msekwa.Kwanza tujiulize ana mwakilisha nani bungeni !,amekaa nje ya madaraka ya kiserekali anajikomba ili arudishwe madarakani maana hakuzoea kukaa uraiani.Kazeeka mwili na akili atumie busara akacheze na wajukuu ambao kwa kiasi fulani wamekosa upendo wa bibi.

na Halfan M, Sanawari,Tz, - 21.06.08 @ 11:24 | #17833

Mama ANA Msekwa(Kawawa)Huna jipya.Tunataka watu wanaochangamka bungeni kama Mama Kilango siyo wewe unaongea kama umelala.Umeishiwa huna chako.Subiri 2010 utaona joto ya jiwe.
Ghalib

na ghalib, Tanzania, - 21.06.08 @ 11:25 | #17834

Mama ANNA MSEKWA KAWAWA hata aibu huna muda wote ulikuwa umesinzia mpaka Mama Kilango alipokupurukusha na kiwewe chako kukakutuma kuongea kitu amabacho kimedihirisha kuwa kweli akili yako imechoka, tumechoka kukusikia wewe na waume zako miaka nenda rudi hamna jipya jiondoeni kabla hatujawaonjesha joto ya jiwe 2010, sisi wananchi tumewachoka

na Shaban mizuki, Tanzania, - 21.06.08 @ 11:34 | #17836

Du!!! lahaullah!!! Jamani kumbe ili upate mafanikio kwenye siasa kwa akina mama ni lazima uliwe uroda na wakubwa!!. Kumbe ndiyo maana akina mama wengi wanasiasa ndoa zao mgogoro na pia wengi ni manung'ayembe!!! Hii ni kali. Haya bwana lakini angalieni maana siku hizi ukimwi unatisha.



na Mwanaharakati, Tanzani, - 21.06.08 @ 11:51 | #17838

Kassim unayejiita wa Ughaibuni!
unajua unachokiongea au unasiliza ya vyombo vya habari vya magharibi? Kwa taarifa yako mimi ninafanya kazi inayonifanya nizunguke karibu dunia nzima hivyo ninazijua taratibu nyingi za mataifa ambayo ninafika mwenyewe na kujionea na sio kusikia kama wewe! taja nchi ulipo nitakwambia yanayotokea Ikulu ya hapo. Mimi siambiwi nianaona mwenyewe!

na LCD, Pyongyang, DRPK, - 21.06.08 @ 12:03 | #17840

Anna Abdalla, wewe ni kilaza mkubwa. Ni miongoni mwa MAFISADI wakubwa wa hii nchi. Uliwahi kushika nyidhifa nyingi serikalini hukufanya chochote. Wizara ya afya ilikushinda.....wakati wa utawala wako huduma ya afya ilikuwa mbovu hakuna mfano; vifo vya akina mama vilikuwa zaidi ya 600, na upande wa vifo vya watoto balaa tupu (>250). Ulipokuwa waziri wa ujenzi...hakuna barabara hata moja ya lami iliyojengwa. Kwa jinsi tulivyoufahamu utumishi wako kwa umaa....wewe hukuwa UNAFAA, na kwa sasa HUFAI, na HUTAFAA popote pale. Twambie Watanzania ni lini ulisimama na kukemea RUSHWA!? Wewe hufai...acha kutukumbusha siasa zako za kitoto zilizojaa woga na rushwa. Wacha mama Anna Kilango aseme ukweli. Na tunamwombea kwa mungu awe na afya njema na aendelee kusema ukweli juu ya ufisadi wako na chama chako cha chukua chako mapema.
Kauli ya Anna Abdalla ni ya KULAANIWA. Anatumia nafasi yake ya kuwa Bungeni kuwatisha wanamapinduzi wetu walio na uchungu na matumizi mabaya ya rasilimali zetu na madudu ya serikali ya Kikwete. Tunachotaka nchi yetu ipige hatua kimaendeleo. Anna Abdalla na wenzako waliokutuma hamuwezi kuturudisha nyuma kwa kuendeleza siasa zenu za kuwapaka mafuta watanzania kwa kilemba cha ukoka. Tunafahamu utumbo ulivyofanyika sehemu zote, pia tunawafahamu vilaza wote hapo Bungeni mlivyo jawa na imani ya ndiyo mzee, na jinsi mnavyoendekeza ushirikina.Anna huna jipya, na huna cha kujivunia katika utumishi wako serikalini na hata katika ubunge wako. Wewe ni miongoni mwa wabunge waliokunywa dawa za kidumu chama, na zidumu vifkra za mwenyekiti
Sasa Watanzania tumeamka,tuna kila sababu ya kujua matumizi ya rasilimali zetu, hivyo Anna Abdalla acha kutuletea umbea na ushambenga wako bungeni. Wacha wabunge wachache wenye nia ya kumkomboa mtanzania wafanye kazi walizotumwa na Mungu na wapiga wao....Akina mama walisha kufa sana sasa tunasema imetosha, watoto wadogo walisha kufa sana, sasa tunasema basi imetosha, tulisha kosa sana barabara nzuri na madawa katika zahanati na hospitali; tunasema sasa basi. Tunachotaka ni maendeleo yanayomjali mtanzania si kuendelea kuneemesha vitumbo vya wachache.
Mama Anna Kilango na Wenzako wachache hapo Bungeni, Jamii inafahamu vitisho na ugumu wa kutimiza nia yenu nzuri na hii kazi ya kutete maslahi ya umma. Akina Anna Abdalla wako wengi hapo Bungeni na nje ya Bunge. Tunawafahamu fika kwa majina, kwa tabia zao, na mienendo yao ya kinafiki. Tunawaomba msife moyo na wala msirudi nyuma kwa sababu ya vitisho na kauli za kukatisha tamaa kama alivyofanya mama mtu mzima hovyo..Anna Abdalla na Kingunge aliyemvamia Jaji mstaafu mzee Sinde Warioba. Tunawategemea kuwa ni vielelezo bora si tu kwa utawala, bali pia ni wapigania haki na wapenda maendeleo ya nchi yetu iliyo tajiri wa rasilimali lakini masikini wa kutupwa.

na Elizabethy , Malawi, - 21.06.08 @ 12:03 | #17841

Wewe Mama Anna Abdallah huna jipyaq la kutueleza sisi watanzania, ningekushauri tu ukapumzike uwaache wapigania walalahohi waendeleze mapambano, kwanza wewe umeshashika nyazifa mbalmbali serikalini lakini hakuna kitu chochote ulichofanya zaidi ya kuagiza machine feki za kupima ukimwi,huo wote ni wivu unaokusumbua hivyo unabaki kutapatapa au na wewe ni fisadi?

na just, Arusha, - 21.06.08 @ 12:16 | #17844

wewe Ana nani kakuchagua kwanza kuingia humo bungeni? wewe na wenzako ndiyo mmetufikisha hapa ondoa kichefuchefu kaa kando kampikie ******** mwenzio Msekwa.

na JOHN MKAMA, NANSIO, - 21.06.08 @ 12:22 | #17845

huyo anna kwanza ni fisadi wa mapenzi,pili anatamani kuwa na chenge ili watumie zile fedha za ufisadi, tatu alijigonga kwa balali lakini balali almshiti kwakuwa amezeeka.nne sura yake inaonyesha ni ***** wa wanaume na ***** wa fedha za hao wanaume.tyano yupo hapo dodoma ili kutoa burudani kwa wabunge ndio maana hana uchungu wowote na nchi hii anabiashara yake anaqyo ijua na mpaka kumaliza bunge hapo ni milionea.anna koma kuongea maneno yako ya kitoto na ya kipuuzi na waambie walio kutuma kwamba muda wa kigumu chama cha mapinduzi badala ya kidumu umefika sura mbaya we'

na limbandula, ruvuma, - 21.06.08 @ 12:26 | #17848

Ni kweli kwamba ufisadi sikitu bora, na ni wajibu wa kila mtu kukataa kwa juhudi kubwa, lakini watanzania tusisahau kuwa rushwa nayo ni adui mwingine tena jasiri zaidi.Nia ya kweli inatakiwa na si maneno matupu,huyu mama Kilango anapoiga kelele tu,je ipo nia ya kwlei au na wewe unataka uonekane halafu upate uwaziri katika mabadiliko yajayo? maana tunao ushahidi wa kutosha watu wanaopiga kelele wakiwa wabunge wakiingia kwenye system wanakumbatia rushwa na ufisadi,Anna Kilango tuambie umefanya nini hadi sasa kwa ajili ya nchi hii, na je utafanya nini siku za usoni, si kutishia kuwa bungeni patachimbika, huo ni ubabaishaji.Waziri wa fedha amesema kuwa fedha za EPA hazikuwa za serikali,sasa hebu mhoji waziri kama fedha hazikuwa za serikali ilikuwaje serikali ikatuma wakaguzi wa mahesabu waliogudua wizi huo?na kama ni wa wafanyabishara walichanga, malengo yalitimia, kama la kwa nini?Anna Kilango jenga hoja kwa mantiki si kupiga kelele za kioga, ooh eti siogopi NEC, hayo mambo ya NEC yanakujaje bungeni? mliyaongea huko NEC basi nenda tena huko NEC kawaambie maana si kila mtanzania ni mwana CCM, habari za NEC wengine haziwahusu kabisa, tunataka haki ifanyike na si ushabiki wa makelele.Na hata hao waliochangia hapo juu wengi wenu mna chuki binafsi, tafuteni ukweli halafu haki, si kusema-sema tu ovyo.

na tony, Bologna, Italia., - 21.06.08 @ 12:31 | #17852

LCD wa Pyongyang DPRK, mimi naishi Washington DC, na sina haja ya kujua Ikulu au White House kunapita nini. Nnachosema ni kwamba hakuna la Tanzania kujifunza huko DPRK. Soma tena maoni yangu na utanifahamu. Inaonyesha unajua mengi kwa kuitembea dunia, kwanza niambie maana ya DRPK. Mimi naijua DPRK, Democratic People's Republic of Korea? Kila la heri.

na Kassim. - 21.06.08 @ 12:35 | #17854

UKALI WA NINI KILANGO MALECELA TOA HOJA ZAKO KWA BUSARA ACHA KUUDHI WENGINE NANI ANYEOGOPA? KAMA KUNA ANAYEOGOPA BASI MTAJE. KAULI ZAKO NI NZURI LAKINI UNAPOZITOA KWA JAZBA NA KUWAPONDA WENGINE TUNAONA UNATAKA UMAARUFU TU

na william kasembe, arusha , - 21.06.08 @ 12:38 | #17855

MAMA ANNA TUNAKUJUA MTETEZI WA MAFISADI. UMAARUFU WAKO NI WA KUKAA MUDFA MREFU KATIKA UONGOZI BILA FAIDA YOYOTE. HUKO KWENU MTWARA NA LINDI NI SEHEMU YA MWISHO KI MAENDELEO, UMEWAFANYIA NINI WANANCHI WA KWENU? HATA BARABARA YA KWENU NI MBOVU KULIKO ZOTE TANZANIA.KAZI YA KUJIPENDEKEZA UNAIWEZA LAKINI HUWATENDEI HAKI WATU WAKO, MWACHE MAMA KILANGO ATETEE WATU WAKE.KAMA WEWE HUONI UMUHIMU KAA KIMYA, YEYE KATUMWA NA WATU WAKE WA SAME, LABDA WASEME KAMA HAWAKUMTUMA VINGINEVYO KAULI YAKO INAWAFURAHISHA MAFISADI WENZAKO HAO WALIOKUWA WAKIKUSHANGILIA BUNGENI, HUKU NJE TUKO PAMOJA NA MAMA KILANGO.

na kadala, Tegeta, - 21.06.08 @ 12:38 | #17856

Anna umeishiwa weye nenda Ukerewe, hata kwenu Masasi umekufasidi! Waziri uliokuwa huna huruma na maslai ya nchi isipokuwa tumbo lako binafsi. Ukuwe sasa na sio wakati wa kulindana.

na Msemakweli Kadinda, Tanganyika, - 21.06.08 @ 12:38 | #17857

Huyo Anna Abdallah Mwongo mkubwa, she is a liar. Atasemaje wabunge wote wanataka pesa za EPA zirudi wakati kuna wabunge wanaotuhumiwa kuwa mafisadi. E.g. Chenge.

Wewe mama unajifanya kuongea kwa unyenyekevu kumbe mnafiki mkubwa unatetea mafisadi. Kwani wewe unakichwa cha panzi. Kuna wabunge kama akina Serukamba yule taahira wa Kigoma hujui kuwa anatetea mafisadi.

Wabunge wanaochukizwa na ufisadi ni wachache tu nao ni Anne Kilango, Malecela, Mwakyembe, Sherukindo, Kimaro na wengine wachache wa CCM. Wewe Anna Abdallah haumo kwenye watu hao. Wabunge wengine ni akina Zitto, Slaa, Hamadi Rashid na wengine wa upinzani.

Maneno uliyotumia kuwa Anne Kilango kaongea kwa mbwembwe ni maneno aliyotumia Lowasa dhidi ya Mwakyembe pale aliposema kuwa, alisoma ripoti ya kamati ya Richmond kwa mbwembwe.

Usituzuge hapa wewe mama upo upande wa wanaotetea mafisadi. Sisi wananchi tumekujua.

na Kim, MN, - 21.06.08 @ 12:39 | #17858

We Mama Abdallah nyamaza kabisa, kwanza huna msimamo thats y una waume wawili na unatuabisha wanawake wenzio. Kama huna point kaa kimya acha wanaojua kilichowapeleka bungeni waongee. U have been warming up chairs bungeni for a long time, huchoki tu? Watanzania wanaamka wewe unawarudisha usingizini, hatuko tayari kukuunga mkono. Inaelekea na wewe ni fisadi, eti wote tunakemea..ulikuwa wapi usiongee hadi akuanzishie Mama Kilango? Hawa ndio wabunge ambao hawatakiwi kuwepo bungeni, unahongwa fedha za watanzania na ngono juu. Mama Kilango kaza buti..nakuaminia! achana na hiki kizee..Na hao wenzio waliokupigia makofi u never kno waliona unaongea pumba wakaamua kukukalisha chini kwa style hiyo..or else na wenyewe hatuwafagilii. Sijui nani anatoa mapendekezo ya viti maalum jamani!! Huyu Mama hatufai..pliz 2010 tusione sura yako Bungeni tunataka damu mpya. Acha vyombo vya habari vitupe habari zinazotuhusu maana wewe sasa sio mtanzania, huna uchungu na wananchi kabisa.

na Mtu, Australia, - 21.06.08 @ 13:07 | #17862

Anne Kilango Malecela PLEASE DON`T FORGET TO TAKE YOUR MEDICATION .YOU ARE DANGER KWA WANANCHI NA BUNGE KWA UJUMLA

na ROGER, mwanza, - 21.06.08 @ 13:14 | #17864

Wewe Anna bado unadhani watanzania wanakubaliana wanaotetea wafisadi au wanopinga wale wanaonyamazisha wanopinga Ufisadi.Wewe umekuwa katika CCM miaka mingi na waziri umetusaidia nini? au umetetea lipi?. Umekuwa ukipokea posho lako na kuendelea kutetea na wakubwa na wala rushwa.Unataka kuwanyamazisha akina mama wanaoinukia na kutaka kututetea sisi watanzania tupate haki zetu.Wewe mama tumewachoka wapifisadi wa CCM. Mimi nadhani nawe labda unamgao au nawe ni mfisadi. Mimi nilitegemea uungane naye mama Kilago mwana mapinduzi lakini unaendelea kutetea watuumiwa wa ufisadi wa akina Mkapa na wenzake ambao wameuza nchi( madini). Umenisikitisha kweli.( Tafadhali naomba mhariri umtumie mawazo yetu, aone mawazo yetu wasomaji, tulivyosikitishwa na kauli zake bungeni.Hata nami niliye nje ya nchi ninaposima mawazo yake naona huyu Anna hapashwi kuitwa mtanzania mzalendo, yeye hajaona umaskini ulioletwa na ufisadi na haoni uchumi ulivyo poromoka kutokana na rushwa, na ni kwa sababu yeye ana Shangigi na posho inayotokana na walipa fedha za walipa kodi ambao ni maskini).

na S.Kazima, Italia, - 21.06.08 @ 13:21 | #17866

ANNA ABDALLAH can u prove to us what kind of develpment you have done to Tanzanians apart from bitching in the house of parliament

na sauda, moro, - 21.06.08 @ 13:25 | #17868

Au huyu Anna Abdalla ni kati ya wale waliohusika kuchukua zile pesa za import support? Hiki kibibi bado kinafanya nini humo bungeni, Hivi JK alikisoa watu wa kuwapa hicho kiti kweli. These old figures hazina jipya. Kawawa umesikia habari ya huyu mama!!

na Twalipo jr - 21.06.08 @ 13:26 | #17869

MAMA ANA ABDALA,WATANZANIA TUMECHOKA,MWACHE MAMA ANA KILANGO MALECHELA ASEME KWA UKALI, TENA TUNATAKA TUWACHAPE VIBOKO MAFISADI. NAONA KWELI MAMA ANA ABDALA ANASHINIKIZO LA MTANDAO WA UFISADI, HATUFAI
UNATAKA WATU WASEME POLE POLE WAKATI NCHI IMEUZWA? AU UNAHUSIKA? UNAJUA MACHUNGU WANAYOYAPATA WATANZANIA? UNAKUMBUKA LINI UMESHINDA NA NJAA? AU MWANAO KUKOSA ADA? UNAJUA KUNA WAKINAMAMA TANZANIA WANAZAA NJIANI KWA KUKOSA HOSPITALI KARIBU? UNAJUA VIJANA WAKITANZANIA WANVYOPATA SHIDA ALAFU UNASEMA MAMA ANNA KILANGO MALECHELA AZUNGUMZE POLEPOLE!JAMANI WEWE ANA ABDALAH NA HUO MTANDAO WA UFISADI ONDOKENI,MNATUKERA,HATUWATAKI!

na kweli, Dar, - 21.06.08 @ 13:26 | #17870

Wachangiaji hivi huyu mama Anna Abdallah Msekwa Kawawa mbona ana macho kama mchawi.J K wa Bagamoyo ebu mpeleke Mwanza akawe mkuu wa mkoa tuone kama ataweza kuzuia vifoo vya walee bibi wazee wenye macho mekundu {macho ya kichawi kama ya mrs Msekwa Kawawa}

na RUTA Br, sweden, - 21.06.08 @ 13:29 | #17872

Anna Abdallah ifuatayo ndiyo orodha ya mabwana zako uliozaa nao huko NEC,
Marehemu John Mhavile(alikuwa mkuu wa mkoa dar(Mzee Rashid Kawawa,na mwisho ukavunja ndoa ya Mh Pius Msekwa!!kwahiyo wachangiaji naomba huyu SHANGINGI WA NEC mumsamehe,kwahiyo historia yake hapo nafikiri mmeishamjua ni mtu wa namna gani,kwahiyo kauli ile ya kusema eti wabunge wote wanataka fedha za epa zirudi si kweli,eti tofauti kauli wengine wanazunguza kwa kupaza sauti wengine taratibu,hivi niwaulize toka lini TAPELI mkaongea nae kwa sauti ya kumbembeleza!!?huyu SHANGINGI VIPI!!?tunajua INAKUUMAkwa sababu kaka yako ,Mh Mkapa anahusika na swala la ufisadi sisi hatujali sema usemavyo lakini siku zinakuja mtajibu tu wewe na kaka yako,kama umechoka pumzika usilete kidomodomo halafu huna unachojua,niungane na mchangiaji mmoja hapo juu aliyetoa wazo kuwa hata wabunge wawekewe kikomo cha kukombea ubunge kama ilivyo kwa urais,maana huyu mama akili zimechoka

na tinoh, athens greece, - 21.06.08 @ 13:47 | #17877

RUTA wa Sweden, na Twalip wa jr, na mtu mwanamke wa Australia kumbe huyu mama anaitwa mama Anna Abdallah-Msekwa Kawawa! Ka Makubwa.

Sasa ni wazi kuwa mama huyu ni fisadi tayari. Anawanaume wawili kwa mpigo. Hii kali.

Mama Anne Kilango Malecela wewe kaza Buti, kamua mafuta twende, tupo pamoja, tunataka kuona pesa za EPA na Richmond zinarudi zote by July mwaka huu. Na wasije kukusanya pesa hizo kwenye wizara halafu watufanyie usanii kuwa zimerudi.

Ubarikiwe sana mama Anne Kilango Malecela.

Anna Abdallah Gharika ya mwenyezi Mungu inakusubiri, upatilizwe mbali na hukumu ya Mungu.

na lm, hj, - 21.06.08 @ 13:48 | #17878

Huyu Mama ni mnafiki sana anapaswa kutoka hata nje ya Bunge, kusini hakuna barabara yeye anakalia kusema kuwa anauchungu hapo hakuna uchungu hata kidogo.

na masalakulanga, KUZIMU, - 21.06.08 @ 14:03 | #17881

Anna Abdallah msekwa mhaville kawawa mwisho wako nahao mafisadi unaowatetea ni 2010 tutawatoa kwa nguvu ya hoja,tabia yako inajulikana wazi kwa watanzania, tulikuwa tunakumezea tu, sasa umechokoza nyuki ni afadhali urudi kwenu kusini ukalime korosho.

na jus, ar, - 21.06.08 @ 14:03 | #17882

picha kwenye ukarasa wa mbele wa daily news 21/06/08 inaonesha huyo mama maneno aliyosema sio yake ,angalieni picha hiyo na labda kumchaya ndio pia kamwambia kwamba waandishi wa habari ni chama kisichosajiliwa !pengine ndio alivyokuwa akifanya hiyo kazi wakati alipokuwa akifanya redio tz

na abdulla, kijiwe, - 21.06.08 @ 14:26 | #17883

Jamani ninyi watanzania mumerongwa na nani
mbona munakua wajinga sana kwanini huyu mama Ana munashidwa kumushuguikia kabisa
mumuue kabisa hafai katika maisha ya watanzania kwanza ni ****** kisha Fisadi

atawamailiza kwa ukimyi pia akili yake ni mbaya sana

kwanini munashidwa kumuonesha mulango wa Minibwe akatibiwe
sisi hapa zambia watu kama hao tunawo

pole sana ndugu zangu watanzania likini munatutia aibu munalala sana naomba muamke kabisa muondoe CCM madarakani
tutawa unga mkono kama mutaomba

na Zambia1, zambia, - 21.06.08 @ 14:29 | #17885

Ama kweli watanzania tunayo kazi. Watu wa aina ya huyu mama kumbe tunao wengi hata ndani ya bunge. Kitendo cha baadhi ya wabunge kushabikia manene ya huyu mama inaonesha wazi kuna wabungu wanaokerwa na jitihada za wapigania haki za wananchi wa Tanzania. Kwa kweli hii vita ni ngumu inahitaji msaada mkubwa wa Mungu. Mama kilango usichoke, Mungu yu pamoja nawe.

na Mwinjanga, Uholanzi, - 21.06.08 @ 14:31 | #17886

NYETI ZA ANNA ABDALAH........

wajameni huyu mama kwenye jimbo lake walimfukuza kabisa walimwambia asijaribu kugombea hatapata kura ilikuwa mwaka 2000 then akaenda CCM-UWT kwavile yeye ni mwenyekiti wa UWT-CCM akalobi akapata ubunge wa viti maalum.

ukweli ni kwamba kisiasa amefilisika sana kwani kama mtakumbuka huyu yuko kwenye siasa toka enzi za nyerere na ndiyo aliwagombanisha kawawa na msekwa kwa mambo yake ya kutojiheshimu

me namshangaa badala ya yeye kuachia siasa vijana kama shyrose bhaji yeye ameng'ang'ana tu ubunge kila mtu anamshangaa...

na dunia, Dar, - 21.06.08 @ 14:41 | #17891

kama wabunge wa kuteuliwa ndo zao hizi basi mi sioni kwanini wanaendelea kulipwa mshahara unaotoka kwa wapiga kura.

na swerejr, beijing,zhongguo, - 21.06.08 @ 14:42 | #17892
 
Kuna mengi ambayo Anna Msekwa amefanya na ni suala la muda tu kila kitu kitakuwa wazi.

Mama Malecela hakusema chochote kibaya na zaidi alikuwa anasema nini watanzania wengi wanahitaji. Tunajua kabisa kuwa uwasilishaji wa hotuba hutofautiana kati ya askari na mwalimu, daktari na wakili lakini lazima tutambue kuwa bungeni kuna wengi wasiowakilisha umma bali wanawakilisha waliowapigia ;kula'

Napingana kabisa na kauli ya kuwajali wapiga 'kura' na kuusahau umma wa watanzania, wenye nchi. Kilango hawezi kutishwa na umma (sio wapiga 'kura') upo unashirikiana naye bega kwa bega.



Watapinga kwa mengi huku wakisema hasemi kwa madiodo lakini wakikutana pamoja wanapiga mayowe ya kushabikia ufisadi. Umma unataka pesa zake
 
Du ameshambuliwa kweli bibi wa watu. Angepumzika akalee vitukuu. Mmesahau mme wake Msekwa alikuwa mwenyekiti wa Vodacom (Rostam) na ikaleta maneno pale bungeni!!! Wote ni mafisadi tu.Amepitwa nawakati aachie young blood wafanye mambo.Aache wivu.
 
Tatizo ni kwamba hatujui bado kuwa ni nani mwenye kutakiwa kutoa boriti jichoni mwake na ni nani mwenye kuona kibanzi!

WOTE wanafuata kauli za sahihi za mwenyekiti wa chama na katibu waliosema hakuna mafisadi wa kushitakiwa ila kuna pesa za kurudishwa ambazo ziliibiwa bila watu hao kuwa wezi bali watuhumiwa huru ambao wengine hufa wakiwa huru na hivyo kuwa marehemu wasio na MAKOSA!
 
Sasa pia naunganisha na Makampuni Yasio lipa Kodi tume tajiwa Voda ni Mojawapo, na share holders ni Rostam na wengineo, pili nakumbuka Msekwa alipewa Uwenyekiti wa Bodi ya VODa wakati akiwa Spika, alipoambiwa ni mgongano wa madaraka akalia, mimi sina kazi nyingine na karibuni nitaacha uspika.
sasa naona mambo yalivyo , ni kwamba wabunge wetu, hususana wachama tawala wanapitisha sheria ya kitu walicho na maslahi nacho.
Kwahiyo hapo hela inatoka kwa wananchi zinakwenda kwa viongozi, kwa kitu walicho pitisha wenyewe Bungeni
 
Tatizo ni kwamba hatujui bado kuwa ni nani mwenye kutakiwa kutoa boriti jichoni mwake na ni nani mwenye kuona kibanzi!

WOTE wanafuata kauli za sahihi za mwenyekiti wa chama na katibu waliosema hakuna mafisadi wa kushitakiwa ila kuna pesa za kurudishwa ambazo ziliibiwa bila watu hao kuwa wezi bali watuhumiwa huru ambao wengine hufa wakiwa huru na hivyo kuwa marehemu wasio na MAKOSA!

Kaka Mushi umenena,

hapa jambo ambalo lipo wazi ni kwamba Uongozi wa juu kAbisa wa CCM umeamua kusimama kidete na kuwakingia kifua mafisadi na kuwasafisha. CCM kama Chama na JK akiwa kama Mwenyekiti wa CCM, Amiri Jeshi Mkuu na Raisi wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania ameamua kusimama imara kuhakikisha ya kwamba Wahujumu Uchumi Mafisadi wanakula 'pepo' kw
Jasho la Watanzania.

Mama Kilango amekuwa muwazi na kusimama kidete na kukemea wazi hili suala la EPA. alichofanya ni Ushujaa, kaamua kugoma kuwa kibaraka wa Mafisadi na kuongelea kile ambacho anakiamini kwa uhuru na uchungu, akiwa Mtanzania kwanza... amekuwa sauti ya wananchi na kulia kilio chao! wazalendo tupo nyuma yake.

Wabunge wa CCM nashindwa kuwaelewa. nilikuwa nategemea kwamba wao kabla ya yote wanajitambua kwamba ni Watanzania, wanaomuwakilisha yule Mlalahoi wa Kasulu na Ipinda. sikutegemea kama Anna Abdallah angeweza nyanyuka na kumkebehi Mh. Kilango kwa Hotuba yake ya jana. wote tunajua wabunge wote wanataka pesa za EPA zirudi. Lakini je ni kweli? na sidhani kama kitu pekee ni kurudi kwa pesa, je Mafisadi kuhukumiwa maana huu ni uhalifu na uhujumu uchumi!

Tulipoingia vitani na Uganda Mwalimu Nyerere katika kutangaza vita alisema; "NIA TUNAYO, SABABU TUNAZO NA UWEZO TUNAO WA KUMPIGA NDUI AMINI"... je mama Anna Abdallah alipoongea kwa niaba ya wabunge wote kwamba wote wanataka pesa irudi, alifikiria hayo mambo Matatu? Nia, Sababu na Uwezo!

Mama Kilango Watanzania Tupo Nyuma Yako.

MAPAMBANO YANAENDELEA!
 
Kaka Mushi umenena,

hapa jambo ambalo lipo wazi ni kwamba Uongozi wa juu kAbisa wa CCM umeamua kusimama kidete na kuwakingia kifua mafisadi na kuwasafisha. CCM kama Chama na JK akiwa kama Mwenyekiti wa CCM, Amiri Jeshi Mkuu na Raisi wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania ameamua kusimama imara kuhakikisha ya kwamba Wahujumu Uchumi Mafisadi wanakula 'pepo' kw
Jasho la Watanzania.

Mama Kilango amekuwa muwazi na kusimama kidete na kukemea wazi hili suala la EPA. alichofanya ni Ushujaa, kaamua kugoma kuwa kibaraka wa Mafisadi na kuongelea kile ambacho anakiamini kwa uhuru na uchungu, akiwa Mtanzania kwanza... amekuwa sauti ya wananchi na kulia kilio chao! wazalendo tupo nyuma yake.

Wabunge wa CCM nashindwa kuwaelewa. nilikuwa nategemea kwamba wao kabla ya yote wanajitambua kwamba ni Watanzania, wanaomuwakilisha yule Mlalahoi wa Kasulu na Ipinda. sikutegemea kama Anna Abdallah angeweza nyanyuka na kumkebehi Mh. Kilango kwa Hotuba yake ya jana. wote tunajua wabunge wote wanataka pesa za EPA zirudi. Lakini je ni kweli? na sidhani kama kitu pekee ni kurudi kwa pesa, je Mafisadi kuhukumiwa maana huu ni uhalifu na uhujumu uchumi!

Tulipoingia vitani na Uganda Mwalimu Nyerere katika kutangaza vita alisema; "NIA TUNAYO, SABABU TUNAZO NA UWEZO TUNAO WA KUMPIGA NDUI AMINI"... je mama Anna Abdallah alipoongea kwa niaba ya wabunge wote kwamba wote wanataka pesa irudi, alifikiria hayo mambo Matatu? Nia, Sababu na Uwezo!

Mama Kilango Watanzania Tupo Nyuma Yako.

MAPAMBANO YANAENDELEA!

Nakubali mkuu lakini ni lazima tuwe makini...HAWA CCM WATAJIDAI KUPINGANA ILI KUIBUA MIJADALA YA KUWAPUMBAZA WANANCHI!

Hawezi kuikosoa ccm kwa kwenda kinyume na makubaliano yao wakati akiwa ndani ya chama hicho cha kimafia!

Nilichukizwa sana pale niliposikia ETI HUYU MAMA KAPATA UMAARUFU MKUBWA KWA KUDAI PESA ZIRUDISHWE..Sasa kama TANZANIA HAIJAROGWA...Hiyo kauli ya kurudishwa fedha amabzo tayari zilisharudishwa ni ya kumpa mtu umaarufu na kusema anawatetea wanyonge?

Mama akidai mashtaka yafunguliwe na watuhumiwa waanze kuhojiwa na bunge huku ripoti ya EPA ikijadiliwa..Then nitakubali moja kwa moja kuwa ana nia nzuri.

Zaidi ya hapo..Kwetu sisi waelewa ni USANII MTUPU kwasababu alipiga kura pamoja na MAFISADI...Kura ya kuipitisha bajeti ya kifisadi,Pia amekubaliana na mwenyekiti wao kwa pamoja kuwa hakuna mafisadi na kwamba pesa zilizoibiwa ziliibiwa kihalali na watuhumiwa huru ambao wengine wanakufa wakiwa huru na hivyo msisitizo wa mapenzi ya Mungu kuwa ccm ni safi unaendelea kuwepo.
 
Sina kumbu kumbu ya kazi ambayo Anna Abdallah akiwahi kuifanya kwa ufanisi. So, she has survived kwa kujikomba-komba na ndicho alichokifanya ktk mchango wake.
Badal ya kujadili hoja ya Bajeti kama mwenzake, yeye anajadili maoni ya Anne!
 
huyu mama anataka kuchanganya watu kama alivyokuwa anamchanganya kawawa na msekwa. ni hallot hana lolote apuuzwe kama bata

bado ana ndoto za kujikomba ili msekwa labda aje amrithi jk
 
Maoni yangu ni kwamba WOTE WALIOIPITISHA BAJET YA KIFISADI NI MAFISADI PIA!
Niliwaonya wabunge kuwa wasikubali mafisadi wachangie bajeti...Sasa wamefanya yale yasiyotarajiwa na wazalendo..WAMEKAA NAO MEZA MOJA NA KUAMUA KUWA TANZANIA IELEKEE WAPI NA HUKU UWAJIBISHWAJI UKIWA HAKUNA NA KUSAFISHANA KWA MASLAHI YA CHAMA...WATOKE HUMO KAMA KWELI NI WAZALENDO HALAFU WAZUNGUMZIE YALE WANANCHI WANAYOTAKA KUSIKIA...MAFISADI WAKAMATWE MARA MOJA..PERIOD!
KWELI TUTAMKUMBUKA MZEE WA KIRARACHA!
 
Kamalaya hako kamwanamke ka-Anna Abdallah Mhavile Kawawa Msekwa..............nasikia hata kuna tuvijana nato tunajilia kidogokidogo, kanavikamatia tu!!!!
 
Tuanze hivi:

(1) CCM ni mali ya Kikwete akisaidiana na Msekwa na Makamba (unaweza kuwa na tafasiri yako tofauti ila ukweli utabaki huo); beneficiaries wakubwa kutokana na ushindi wa CCM watakuwa ni ndugu na marafiki wa Kikwete, Msekwa na Makamba.

(2) Ufisadi ni tatizo kubwa sana kwa CCM ambalo linaweza kufanya ishindwe kwenye uchaguzi ujao. Endapo CCM ikishindwa basi hilo litakuwa ni balaa kwa ndugu na marafiki wa vigogo hao watatu niliowataja hapo juu.

(3) Anne Abdallah ni mke wa Msekwa. Je kwa maslahi yake inabidi akae upande upi? dhidi ya ufisadi au upande wa ufisadi?

Kumbuka kuwa kwenye swala la kuku kuvuka barabara, Raisi George Bush wa Marekani alisema hivi: "Iwe kuku kavuka barabara au la sisi hatujali, tunachoitaka kujua ni kama kuku huyo yuko upande wetu wa barabara au yuko upande wa pili. Akiwa upande wa pili basi atakuwa ni adui wetu."
 
Huyu Mwanamke anajiona ni mungu mtu, ana tabia ya kutumia mabavu na madaraka aliyonayo katika kuendesha maisha yake. Amekuwa ndani ya serikali miaka nenda miaka rudi mpaka sasa amesahau kwamba yeye ni mtumishi wa wananchi. Ni mchawi na mpenda majungu wa hali ya juu.
Ingekuwa ni wakati muafaka akakaa kimya kama hana la kusema.
 
Maoni ya Wabongo na hata wasio wabongo kuhusu sakata hili

HAPA NAONA KUNA JAMBO.
MSEKWA ALIDHALILISHWA NA WANA MTANDAO AKAUKOSA USPIKA. MALECELA ALIDHALILISHWA NA WANA MTANDAO AKAUKOSA URAISI. WAKE ZAO WANALUMBANA, KUNA NINI?
ANA ABADLAH AMEKAA SANA SERIKALINI, ANAONA BARIDI KUKAA NJE, LAZIMA AJIKOMBE ILI MABADALIKO YANAYOKUJA MUDA SI MREFU APATE NAFASI YA KURUDI.

KILANGO KASEMA KWELI, NDANI YA CCM TUNATISHWA SANA NA KUNDI LA EPA.

Wasalaam
Mbunge wa Zamani Kidogo
Ujerumani

na MASALAKULANGWA, GERMANY, - 21.06.08 @ 08:40 | #17771

Mimi si mtaalam sana wa siasa zetu za Tanzania.Mama Malechela ni mbunge wa kuchaguliwa na wapiga kura kwa hiyo lazima awe mkali kutetea maslahi ya wananchi,Mama Msekwa ni mbunge wa viti maalum hana deni.Mama Msekwa unapashwa kusoma alama za nyakati,huko unakotaka kuturudisha wenzio ndiyo tumeshaanza kutoka,nakuhurumia,waachie vijana!!
Felicitation Mama Malechela!!!!KUNA MTU ALISEMA JANA,KAMA KUNA WABUNGE WANAONA WATU CCM HAWATAKI KUBADILIKA,JUMP OUT ANZISHA CHAMA MTAWABWAGA CCM 2010.

na David Villa, Tanzania, - 21.06.08 @ 08:47 | #17775

Ana hataki mabadiliko bali anataka iwe kama kawaida ya kila siku. Anataka 'wasiseme' akiamini mambo yatajiweka sawa yenyewe. Anasahau mambo yamefika hapo kwa sababu serikali ya CCM na wabunge kwa ujumla wamekua hawasemi na kwamba wengi watishika na kukosa nafasi zao au kupanda nafasi zao.

na David, Dar. TZ, - 21.06.08 @ 08:53 | #17778

ANNA ABDALLAH huna jipya la kutueleza sasa hivi nia yetu hatutaki watanzania tuwe na ile kasumba ya bunge kutumika kama muhuri tu.Kwa kifupi wabunge hususa wa CCM mmeonyesha woga ktk suala la EPA .Mwache kilango aseme ukweli ndio maana mnapewa vitabu vya bajeti halafu mnasomewa bagdet speech inayotofautiana na vitabu mnakaa kimya tu .hamuoni ni aibu tupu kwa serikali.Sijui wahisani watatuelewa vipi.Ingekuwa ni nchi zilizo endelea waziri wa fedha angetakiwa ajiuzulu mara moja lakini kwa bongo hiyo ni sawa tu ,bustard

na adili, uk, - 21.06.08 @ 09:06 | #17783

Mama Anna ni mmoja wa viongozi wa kale ambao hawataki kubadilika! Tangu nchi hii ipate uhuru yeye na mme wake wamekuwepo serikalini na hawataki kuachia vizazi vipya! Wote wawili ni mbumbumbu wanaoabudu u miungu watu na wanaona kuwa wao pekee ndio wanatakiwa kubaki mabwana na jamii nyingine iendelee kuwa matwana!
Anna na Mme wake Msekwa ni waasisi wa kilichokuwa kikiitwa Siasa ni kilimo, yaani wao walikuwa wakipiga domo kaya la siasa huku wananchi wakilima, wakiwashibisha hadi kusaza na kulewa kiasi cha kupindukia ndiyo maana wanajaribu kuwashangaa wanaotaka haki!
Anna na Mmewe ni waanzilishi wa siasa za kudumu kwa fikra sahihi za mwenyekiti wa chama na ni wafuasi wazuri wa jamii ya Kingunge, wakifuata msimamo wa CCM wa kuongea ukweli ndani ya vyumba na kuuacha humo ukioza huku wananchi wakiendelea kupata taabu!
Umefika wakati wazee hawa waachie ngazi na waanze kuona ukweli ambao watanzania wanautaka!
Kwani inahitaji shule gani kujua kuwa wabunge na hata watu wengine wanaosema ukweli katika nchi yetu wanatishwa na pengine kuuawa! Labda nitoe mfano tena ambao ni tofauti na wabunge: yule mwanafunzi anayetoka katika jimbo la mmewe Anna alipatwa na nini baada ya kumuuliza yule mungu wa CCM kuhusu swala la viongozi wa CCM kushika mambo zaidi ya mawili? Yule mkemia Mkuu wa zamani marehemu Fupi alipatwa na nini alipotaka kuongea suala la ubovu wa chakula cha Mhindi? yuko wapi mwandishi Stan Katabaro wa lile gazeti la mfanyakazi?
Ifike wakati tukubaliane na ukweli usiohitaji ushabiki wa kisiasa ili nchi isonge mbele! Hapa Korea watu ni waaminifu na hakuna anayefanya ujinga unaotokea huko kwetu! Ipo haja ya kuhamishia baadhi ya adhabu zinazotolewa hapa huko kwetu ili kukomesha hayo madudu! Baadhi ya wabunge kama Ndesamburo wanaojua uzuri wa adhabu hizi wanahitaji kuungwa mkono ili na sisi tuanze kuzitumia!

na LCD, Pyongyang, DRPK, - 21.06.08 @ 09:08 | #17784

anna abdallah wewe ni ********* tu huna jipya tumekuchoka kama huogopi ulikuwa wapi mpaka mwenzio aseme kwenda zako akili zako zimezeeka

na ***** lee - 21.06.08 @ 09:14 | #17787

MHESHIMIWA MAMA ANNA ABDALLAH KUMBUKA YAFUATAYO KUTHIBITISHA KAMA KWELI UNA UCHUNGU NA NCHI;

1. ULIPOKUWA WIZARA YA UJENZI KUNA TETESI YA RUSHWA KUBWA KATIKA UJENZI WA BARABARA. KWELI ULICHUKIA UFISADI? ANGALUA MAGUFULI HATUKUSIKIA HATA HARUFU

2. ULIPOKUWA WIZARA YA AFYA, NI KWELI WEWE NI MWENZETU MWENYE KUCHUKIA RUSHWA? HATUYAONI HAYO KWA ALIYEKURITHI PROFESSOR MWAKYUSA.

3. MWACHE MAMA MALECELA ASEME. CCM WAKATI WA AWAMU YA 3 MLIINGIA KWA MBWEMBWE, MMEUZA NCHI HALAFU MNASEMA WENGINE WANASEMA KWA MBWEMBWE. MNASEMA KWA UPOLE MMEFANYA NINI? SI NINYI MLIUZA NCHI.

WAACHE WANAHABARI WAFANYE KAZI YAO. MLIPOKUWA MNASHABIKIWA NA RADIO TZ, TVT, UHURU NA MZALENDO, NAVYO VILIKUWA VYAMA VISIVYOSAJILIWA.

na B.J.M, DSM, - 21.06.08 @ 09:16 | #17789

hawa wabunge wa viti maaalum kweli wengine hawana machungu kabisa.sasa huyu mama alikua wapi asizungumze siku zote.mama kilango kazungumza sasa yeye anamkosoa kuwa kazungumza kwa mbwebwe, mama nanihi ulikua wapi siku zote wewe.hizi mbwembwe ndio tunazitaka maana wengine masikio yao wametia pamba, wewe endelea kukaa kimya na kula hela za wananchi kwa kutochangia kitu huko bungeni!!mama kilango tupo pamoja mama!!!

na lucas, ar,, - 21.06.08 @ 09:17 | #17791

huyu mama nilimuangalia wakati akitoa mchango wake bungeni. Hakuwa mwenyewe. kulikuwa na nguvu fulani sio dumba ( dizaini ya mtandao wa mafisadi)uliokuwa ndani yake.

hawana kwa kuwa ni kundi lenye nguvu na ushawishi mkubwa ndio limemtumia mama huyu, ambaye sikumbuki kama mipango yake ya kufunga ndoa na msekwa ilifanikiwa kutokana na pingamizi la mke mkubwa wa msekwa.

kundi hilo kwa kuwa haziivi na spika, na kwa kuwa spika alipigilia msumari baada ya kauli ya mama malecela kw amaneneo kuwa wana bahati ya kuwa na spika asiyeogopa, liliamua kumwandaa mama Msekwa.

huyu ameandaliwa pengine kwa ahadi kwamba siku moja anaweza kurudi serikali licha ya madudu yote aliyofanya akiwa wizara ya afya.

anachopaswa kuelewa kuwa UWT yao kwanza imekufa,haina kitu haina chake umebakia kuwa mkusanyiko wa mafisadi wasioweza kuwasaidia wanawake na watoto wa taifa hili.

badala ya kumsakama mama malecela, yeye katiikamchango wake angejielekeza kuishambulia serikali kwa kushindwa kutoa huduma kwa watanzania hali inayosababisha mmomonyoko wa maandili.

mwenyekiti wa umoja wa wanawake wa tanzania haoni kwamba taifa linaelekea kusiko kwenyewe?, huoni aibu unapokutana na vibinti vinavyotembea uchi, vijana wanaotumia mihardarati au hata kukemea mauaji ya wakongwe na maalbino ni mama wa aina gani wewe?



na mashilatu, ngara, - 21.06.08 @ 09:22 | #17796

Anna Abdallah,

Hujui maumivu makubwa mliyoleta ninyi wazee wetu ambao mlitugeuka ghafla kwenye awamu ya pili. Afadhali nyamaza.

Hamuwezi tena mkatufunga kitambaa usoni. Mnachukia ufisadi ninyi kweli? Mbona yote haya yalifanyika wakati mko mwenye BARAZA la MAWAZIRI? IPTL, NETGROUP, TTCL (badala ya kuuzwa kwa 120bn mkauza kwa 60bn), KIWIRA COAL MINE.

na NJETILE, DSM, - 21.06.08 @ 09:25 | #17797

ANNA ABDALLAHI NIKO TAYARI KUKUCHANGIA PESA ZA MATIBABU YA AKILI NCHI YEYOTE DUNIANI

na MOSHI, DAR , - 21.06.08 @ 09:25 | #17798

Utu uzima tena ndiyo unao msumbua tumsamehe hajui alitendalo,yeye baada ya kuchangia hojo anajibu hoja nyie hamoni kama kituko? anjibu hoja ye mkullo? pili kilango mbunge kupitia jimbo yeye ubunge wa hisani tofati nyingine ndiyo maana nasema huyu mama ameshachoka hana jipya.

na kassim,tegeta, dar,tz, - 21.06.08 @ 09:39 | #17807

LCD hapo juu mawazo yako tunayaheshimu. Lakini Tanzania haina lakuiga kutoka DPRK. Huko Bunge lao ni la rubber stamp, nchi inaendeshwa na mtu mmoja. Adhabu zao hazilingani na makosa, mtu anauliwa kwa kukataa kumuabudu Great Leader na Dear Leader. Akina Ann Kilango wa huko wameuliwa zamani. Ufisadi mkubwa ni kudhulumu roho ya mtu, eti kwa tofauti za kisiasa.

na Kassim., Ughaibuni., - 21.06.08 @ 09:46 | #17811

Anna nakuita!(nilisema toka jana ni jina la mwanangu)sikiliza wewe umeisha zeeka kama unataka heshima yako idumu pumzika,huna la kuchangia nyamaza tafadhari,unataka yatokee au yakukute kama ya miaka hiyooo ulipokuwa mkuu wa wilaya ya kahama??nyamaza tafadhari kumbukumbu bado tunazo,halafu kwa wasio mjua Anna Abdalah huyo mama amezaa na nusu ya viongozi serikali!!hata pius msekwa siyo mumewe wa ndoa,alivunja ndoa ya msekwa ndiyo anishi nae mpaka leo,kumbuka mama hata uhusiano wa mzee msekwa na mzee kawawa si mzuri (na wala hawaongei wala kusalimiana) kwa ajili yako!!uliwagombanisha kwa kuwachukua wote! sasa unasema kuna watu wanaosema sana tena kwa mbwembwe!!wacha mama kilango aseme kwa mbwembwe hata kwa machozi ikiwezekana,tutamsikiliza wewe unasema kwa njia gani emu tulia weee KIZEEE acha vijana wachape kazi,wewe huna la kuongea bungeni hesabu zako kubwa ni kuchukua viongozi mmoja baada ya mwingine na ukizidi tutakupaka zaidi,kama huna la kuongea bungeni si unyamaze!!?? wacha watu waongeee kwa mbwembwe si wanauhakika na wanachokisema!!wewe mama vipi akili zako ziko sawasawa kweli??watu wanazungumza mambo muhimu ya nchi wewe,unaleta uzuri!!(WADAU SAMAHINI KAMA NIMETUMIA KAULI YOYOTE YA KUWAUDHI,HUYU "AJUZA" AMENIKERA SANAA HANA ADABU)halafu wewe Anna kwanza ulimjibu kilango kama nani bungeni??ilitakiwa ajibiwe na waziri muhusika,au bado unaota uwaziri??FUNGA DOMO LAKO WEEE KIZEEE

na mwana wa matonya, leeds uk, - 21.06.08 @ 09:55 | #17813

Wewe Anna umesahau hapa Magu tulivyo kufanyizia, sasa endelea kulopoka kuwa hutishiki na mtu kama hutalala nje tena.
Wenzio wanauchungu na nchi yao wewe unaendekeza umbea na kutumiwa na hao Mafisadi wenzio, hatuwezi kukuvumilia kwa hilo, koma ukomae kutoa kauli za kipuzi kwenye masilahi ya nchi.

na Pipi, Magu, - 21.06.08 @ 10:15 | #17820

Mama Ana Abdalah, unachokiongea hakiingii akilini wala masikioni mwetu kabisa. Wewe inaonekana unafagilia UFISADI kwa staili fulani fulani, na kama ni kweli basi tunakuomba unyamaze kimya. Sisi tunamtaka Mama Anne Kilango Malechela, hongera sana, tuko nyuma yako na tuna enzi hotuba zako. Endelea kushika nyayo za huyu Mgiriki SOCRATES ambaye alikufa kwa kukutetea haki. Achana na akina Ana abdalah. ALUTA CONTINUA!!

na hamisi, Tanzania, - 21.06.08 @ 10:40 | #17824

ANNA, KAA KIMYA, KAA PEMBENI, NINI ULICHOFANYA WEWE HATA KIKAKUPANDISHA CHATI WAKATI UKIWA SERIKALINI??? HAAAAAKUNA!! NINI UMEISHACHANGIA BUNGENI KIKAKUPANDISHA CHATI?? HAAAKUNA
SABABU WEWE SI MUBUNIFU (IQ NDOGO) HIVYO MWACHE KILANGO NA HISIA ZAKE ZA KUJIELEZA NAWE KAA NA ZAKO.
WEWE NA WABUNGE WOTE WALIOKUSHANGILIA HUKO BUNGENI NI RUBBER STAMP.MNALITIA TAIFA HASARA BURE KUWA BUNGENI HAKUNA CHA MAANA MNACHOWEZA KUCHANGIA NI KUVUTA POSHO NK.

na msekwa junior, japani, - 21.06.08 @ 10:46 | #17826


Kweli watanzania naona sasa tumechoka kikweli na ufisadi. Mawazo ya watanzania nayaheshimu.
Anne KIlango Malechela Kaza buti mama ni wachache wenye moyo na ujasiri ulionao. Tuwakilishe watanzania. Kufa si ajabu. Watakuwa wamekutanguliza tu. Hakuna atayeishi milele. Ni bora ufe kishujaa kuliko kuendelea kutetea uzembe na uozo uliopo.
Ni aibu na fedheha kusoma na kusikia mambo yanayofanyika na kutendeka. Tusiishi kinafiki jamani tuwe wawazi na wakweli. Mungu atuwezeshe tubadike jamani.

na c3, Dk, - 21.06.08 @ 10:53 | #17828

Nadhani ifike wakati sheria ya kuwawekea vipindi visivyozidi viwili wabunge,tukifanya hivyo aina ya wabunge kama mama Anna Abdallah Msekwa [Kawawa] haitakuwapo.Historia inaanza kuonyesha kuwa hawa wabunge wa viti maalumu hawana habari na wananchi kama alivyo mama Anna Abdallah Msekwa [Kawawa]kwasababu hawapigiwi kura moja kwa moja na wananchi badala yake wanaabudu sana chama kwakuwa ndicho kilichowapeleka bungeni na siyo wananchi kama alivyo mama Anne Kilango Malechela mbunge wa kuchaguliwa na wananchi[jimbo la Same].Mama Anna Abdallah Msekwa [Kawawa] anasema pia kuna vyama vya siasa visivyo rasm [magazeti] vinawachonganisha wabunge,hivi huyu mama mbona anapenda kukurupuka [kuropoka] anataka yale magazeti ya enzi za chama kimoja yanayosifu kila upuuzi na uchafu wa wanasiasa uhuru,mzalendo,radio tanzania na TVT ?????.

na G KABONDE, ARUSHA,TANZANIA, - 21.06.08 @ 11:07 | #17830

Huyu mama alikuwa kwenye mabunge mengi ya zamani yaliyozea kubweteka na kutufikisha hapa tulipo, inaonekana hajui anachokisema mfano anashambulia vyombo vya habari hebu tujiulize, siku hizi tvt, itv, star tv, radio wanatuletea matukio live, tunaona wenyewe yeye anadai vyombo vya habari vinapotosha, kweli jambo linaloonekana zahiri yeye anashambulia vyombo vya habri, kaishiwa huyu hana jipya, hata hivyo hana wa kuwazungumzia maana ni mbunge wa viti maalum, aidha anaweza kuwa anamtetea mumewe maana si ndio vikongwe vya chama visivyo na jipy

na Peter, TZ, - 21.06.08 @ 11:11 | #17831

KUNA UWEZEKANO HUO ANNA MWENYEWE AKAWA NI MUHUSIKA WA UFISADI.KAULI YAKE YA KWAMBA WABUNGE WOTE WANACHUKIA UFISADI SI KWELI.MLE NDANI KUNA MAFISADI WENGI TU.WANAWEZA KUWA SI WAHUSIKA WA FEDHA ZA EPA MOJA KWA MOJA,LAKINI WENGI WAO NI WAHUSIKA KWA MIKATABA MIBOVU KAMA RICHMOND.WANGEKUWA NA UCHUNGU NA NCHI TZ ISINGEKUWA HAPO ILIPO.WALIOSAINI MKATABA WA IPTL WAMO HUMO,KUNUNUA RADA WAMO HUMU BUNGENI

na lugayila, Norway, - 21.06.08 @ 11:18 | #17832

****** huyu mama kazoea kudandia wanaume wenye madaraka kaanzia kwa Kawawa kaishia kwa Msekwa.Kwanza tujiulize ana mwakilisha nani bungeni !,amekaa nje ya madaraka ya kiserekali anajikomba ili arudishwe madarakani maana hakuzoea kukaa uraiani.Kazeeka mwili na akili atumie busara akacheze na wajukuu ambao kwa kiasi fulani wamekosa upendo wa bibi.

na Halfan M, Sanawari,Tz, - 21.06.08 @ 11:24 | #17833

Mama ANA Msekwa(Kawawa)Huna jipya.Tunataka watu wanaochangamka bungeni kama Mama Kilango siyo wewe unaongea kama umelala.Umeishiwa huna chako.Subiri 2010 utaona joto ya jiwe.
Ghalib

na ghalib, Tanzania, - 21.06.08 @ 11:25 | #17834

Mama ANNA MSEKWA KAWAWA hata aibu huna muda wote ulikuwa umesinzia mpaka Mama Kilango alipokupurukusha na kiwewe chako kukakutuma kuongea kitu amabacho kimedihirisha kuwa kweli akili yako imechoka, tumechoka kukusikia wewe na waume zako miaka nenda rudi hamna jipya jiondoeni kabla hatujawaonjesha joto ya jiwe 2010, sisi wananchi tumewachoka

na Shaban mizuki, Tanzania, - 21.06.08 @ 11:34 | #17836

Du!!! lahaullah!!! Jamani kumbe ili upate mafanikio kwenye siasa kwa akina mama ni lazima uliwe uroda na wakubwa!!. Kumbe ndiyo maana akina mama wengi wanasiasa ndoa zao mgogoro na pia wengi ni manung'ayembe!!! Hii ni kali. Haya bwana lakini angalieni maana siku hizi ukimwi unatisha.



na Mwanaharakati, Tanzani, - 21.06.08 @ 11:51 | #17838

Kassim unayejiita wa Ughaibuni!
unajua unachokiongea au unasiliza ya vyombo vya habari vya magharibi? Kwa taarifa yako mimi ninafanya kazi inayonifanya nizunguke karibu dunia nzima hivyo ninazijua taratibu nyingi za mataifa ambayo ninafika mwenyewe na kujionea na sio kusikia kama wewe! taja nchi ulipo nitakwambia yanayotokea Ikulu ya hapo. Mimi siambiwi nianaona mwenyewe!

na LCD, Pyongyang, DRPK, - 21.06.08 @ 12:03 | #17840

Anna Abdalla, wewe ni kilaza mkubwa. Ni miongoni mwa MAFISADI wakubwa wa hii nchi. Uliwahi kushika nyidhifa nyingi serikalini hukufanya chochote. Wizara ya afya ilikushinda.....wakati wa utawala wako huduma ya afya ilikuwa mbovu hakuna mfano; vifo vya akina mama vilikuwa zaidi ya 600, na upande wa vifo vya watoto balaa tupu (>250). Ulipokuwa waziri wa ujenzi...hakuna barabara hata moja ya lami iliyojengwa. Kwa jinsi tulivyoufahamu utumishi wako kwa umaa....wewe hukuwa UNAFAA, na kwa sasa HUFAI, na HUTAFAA popote pale. Twambie Watanzania ni lini ulisimama na kukemea RUSHWA!? Wewe hufai...acha kutukumbusha siasa zako za kitoto zilizojaa woga na rushwa. Wacha mama Anna Kilango aseme ukweli. Na tunamwombea kwa mungu awe na afya njema na aendelee kusema ukweli juu ya ufisadi wako na chama chako cha chukua chako mapema.
Kauli ya Anna Abdalla ni ya KULAANIWA. Anatumia nafasi yake ya kuwa Bungeni kuwatisha wanamapinduzi wetu walio na uchungu na matumizi mabaya ya rasilimali zetu na madudu ya serikali ya Kikwete. Tunachotaka nchi yetu ipige hatua kimaendeleo. Anna Abdalla na wenzako waliokutuma hamuwezi kuturudisha nyuma kwa kuendeleza siasa zenu za kuwapaka mafuta watanzania kwa kilemba cha ukoka. Tunafahamu utumbo ulivyofanyika sehemu zote, pia tunawafahamu vilaza wote hapo Bungeni mlivyo jawa na imani ya ndiyo mzee, na jinsi mnavyoendekeza ushirikina.Anna huna jipya, na huna cha kujivunia katika utumishi wako serikalini na hata katika ubunge wako. Wewe ni miongoni mwa wabunge waliokunywa dawa za kidumu chama, na zidumu vifkra za mwenyekiti
Sasa Watanzania tumeamka,tuna kila sababu ya kujua matumizi ya rasilimali zetu, hivyo Anna Abdalla acha kutuletea umbea na ushambenga wako bungeni. Wacha wabunge wachache wenye nia ya kumkomboa mtanzania wafanye kazi walizotumwa na Mungu na wapiga wao....Akina mama walisha kufa sana sasa tunasema imetosha, watoto wadogo walisha kufa sana, sasa tunasema basi imetosha, tulisha kosa sana barabara nzuri na madawa katika zahanati na hospitali; tunasema sasa basi. Tunachotaka ni maendeleo yanayomjali mtanzania si kuendelea kuneemesha vitumbo vya wachache.
Mama Anna Kilango na Wenzako wachache hapo Bungeni, Jamii inafahamu vitisho na ugumu wa kutimiza nia yenu nzuri na hii kazi ya kutete maslahi ya umma. Akina Anna Abdalla wako wengi hapo Bungeni na nje ya Bunge. Tunawafahamu fika kwa majina, kwa tabia zao, na mienendo yao ya kinafiki. Tunawaomba msife moyo na wala msirudi nyuma kwa sababu ya vitisho na kauli za kukatisha tamaa kama alivyofanya mama mtu mzima hovyo..Anna Abdalla na Kingunge aliyemvamia Jaji mstaafu mzee Sinde Warioba. Tunawategemea kuwa ni vielelezo bora si tu kwa utawala, bali pia ni wapigania haki na wapenda maendeleo ya nchi yetu iliyo tajiri wa rasilimali lakini masikini wa kutupwa.

na Elizabethy , Malawi, - 21.06.08 @ 12:03 | #17841

Wewe Mama Anna Abdallah huna jipyaq la kutueleza sisi watanzania, ningekushauri tu ukapumzike uwaache wapigania walalahohi waendeleze mapambano, kwanza wewe umeshashika nyazifa mbalmbali serikalini lakini hakuna kitu chochote ulichofanya zaidi ya kuagiza machine feki za kupima ukimwi,huo wote ni wivu unaokusumbua hivyo unabaki kutapatapa au na wewe ni fisadi?

na just, Arusha, - 21.06.08 @ 12:16 | #17844

wewe Ana nani kakuchagua kwanza kuingia humo bungeni? wewe na wenzako ndiyo mmetufikisha hapa ondoa kichefuchefu kaa kando kampikie ******** mwenzio Msekwa.

na JOHN MKAMA, NANSIO, - 21.06.08 @ 12:22 | #17845

huyo anna kwanza ni fisadi wa mapenzi,pili anatamani kuwa na chenge ili watumie zile fedha za ufisadi, tatu alijigonga kwa balali lakini balali almshiti kwakuwa amezeeka.nne sura yake inaonyesha ni ***** wa wanaume na ***** wa fedha za hao wanaume.tyano yupo hapo dodoma ili kutoa burudani kwa wabunge ndio maana hana uchungu wowote na nchi hii anabiashara yake anaqyo ijua na mpaka kumaliza bunge hapo ni milionea.anna koma kuongea maneno yako ya kitoto na ya kipuuzi na waambie walio kutuma kwamba muda wa kigumu chama cha mapinduzi badala ya kidumu umefika sura mbaya we'

na limbandula, ruvuma, - 21.06.08 @ 12:26 | #17848

Ni kweli kwamba ufisadi sikitu bora, na ni wajibu wa kila mtu kukataa kwa juhudi kubwa, lakini watanzania tusisahau kuwa rushwa nayo ni adui mwingine tena jasiri zaidi.Nia ya kweli inatakiwa na si maneno matupu,huyu mama Kilango anapoiga kelele tu,je ipo nia ya kwlei au na wewe unataka uonekane halafu upate uwaziri katika mabadiliko yajayo? maana tunao ushahidi wa kutosha watu wanaopiga kelele wakiwa wabunge wakiingia kwenye system wanakumbatia rushwa na ufisadi,Anna Kilango tuambie umefanya nini hadi sasa kwa ajili ya nchi hii, na je utafanya nini siku za usoni, si kutishia kuwa bungeni patachimbika, huo ni ubabaishaji.Waziri wa fedha amesema kuwa fedha za EPA hazikuwa za serikali,sasa hebu mhoji waziri kama fedha hazikuwa za serikali ilikuwaje serikali ikatuma wakaguzi wa mahesabu waliogudua wizi huo?na kama ni wa wafanyabishara walichanga, malengo yalitimia, kama la kwa nini?Anna Kilango jenga hoja kwa mantiki si kupiga kelele za kioga, ooh eti siogopi NEC, hayo mambo ya NEC yanakujaje bungeni? mliyaongea huko NEC basi nenda tena huko NEC kawaambie maana si kila mtanzania ni mwana CCM, habari za NEC wengine haziwahusu kabisa, tunataka haki ifanyike na si ushabiki wa makelele.Na hata hao waliochangia hapo juu wengi wenu mna chuki binafsi, tafuteni ukweli halafu haki, si kusema-sema tu ovyo.

na tony, Bologna, Italia., - 21.06.08 @ 12:31 | #17852

LCD wa Pyongyang DPRK, mimi naishi Washington DC, na sina haja ya kujua Ikulu au White House kunapita nini. Nnachosema ni kwamba hakuna la Tanzania kujifunza huko DPRK. Soma tena maoni yangu na utanifahamu. Inaonyesha unajua mengi kwa kuitembea dunia, kwanza niambie maana ya DRPK. Mimi naijua DPRK, Democratic People's Republic of Korea? Kila la heri.

na Kassim. - 21.06.08 @ 12:35 | #17854

UKALI WA NINI KILANGO MALECELA TOA HOJA ZAKO KWA BUSARA ACHA KUUDHI WENGINE NANI ANYEOGOPA? KAMA KUNA ANAYEOGOPA BASI MTAJE. KAULI ZAKO NI NZURI LAKINI UNAPOZITOA KWA JAZBA NA KUWAPONDA WENGINE TUNAONA UNATAKA UMAARUFU TU

na william kasembe, arusha , - 21.06.08 @ 12:38 | #17855

MAMA ANNA TUNAKUJUA MTETEZI WA MAFISADI. UMAARUFU WAKO NI WA KUKAA MUDFA MREFU KATIKA UONGOZI BILA FAIDA YOYOTE. HUKO KWENU MTWARA NA LINDI NI SEHEMU YA MWISHO KI MAENDELEO, UMEWAFANYIA NINI WANANCHI WA KWENU? HATA BARABARA YA KWENU NI MBOVU KULIKO ZOTE TANZANIA.KAZI YA KUJIPENDEKEZA UNAIWEZA LAKINI HUWATENDEI HAKI WATU WAKO, MWACHE MAMA KILANGO ATETEE WATU WAKE.KAMA WEWE HUONI UMUHIMU KAA KIMYA, YEYE KATUMWA NA WATU WAKE WA SAME, LABDA WASEME KAMA HAWAKUMTUMA VINGINEVYO KAULI YAKO INAWAFURAHISHA MAFISADI WENZAKO HAO WALIOKUWA WAKIKUSHANGILIA BUNGENI, HUKU NJE TUKO PAMOJA NA MAMA KILANGO.

na kadala, Tegeta, - 21.06.08 @ 12:38 | #17856

Anna umeishiwa weye nenda Ukerewe, hata kwenu Masasi umekufasidi! Waziri uliokuwa huna huruma na maslai ya nchi isipokuwa tumbo lako binafsi. Ukuwe sasa na sio wakati wa kulindana.

na Msemakweli Kadinda, Tanganyika, - 21.06.08 @ 12:38 | #17857

Huyo Anna Abdallah Mwongo mkubwa, she is a liar. Atasemaje wabunge wote wanataka pesa za EPA zirudi wakati kuna wabunge wanaotuhumiwa kuwa mafisadi. E.g. Chenge.

Wewe mama unajifanya kuongea kwa unyenyekevu kumbe mnafiki mkubwa unatetea mafisadi. Kwani wewe unakichwa cha panzi. Kuna wabunge kama akina Serukamba yule taahira wa Kigoma hujui kuwa anatetea mafisadi.

Wabunge wanaochukizwa na ufisadi ni wachache tu nao ni Anne Kilango, Malecela, Mwakyembe, Sherukindo, Kimaro na wengine wachache wa CCM. Wewe Anna Abdallah haumo kwenye watu hao. Wabunge wengine ni akina Zitto, Slaa, Hamadi Rashid na wengine wa upinzani.

Maneno uliyotumia kuwa Anne Kilango kaongea kwa mbwembwe ni maneno aliyotumia Lowasa dhidi ya Mwakyembe pale aliposema kuwa, alisoma ripoti ya kamati ya Richmond kwa mbwembwe.

Usituzuge hapa wewe mama upo upande wa wanaotetea mafisadi. Sisi wananchi tumekujua.

na Kim, MN, - 21.06.08 @ 12:39 | #17858

We Mama Abdallah nyamaza kabisa, kwanza huna msimamo thats y una waume wawili na unatuabisha wanawake wenzio. Kama huna point kaa kimya acha wanaojua kilichowapeleka bungeni waongee. U have been warming up chairs bungeni for a long time, huchoki tu? Watanzania wanaamka wewe unawarudisha usingizini, hatuko tayari kukuunga mkono. Inaelekea na wewe ni fisadi, eti wote tunakemea..ulikuwa wapi usiongee hadi akuanzishie Mama Kilango? Hawa ndio wabunge ambao hawatakiwi kuwepo bungeni, unahongwa fedha za watanzania na ngono juu. Mama Kilango kaza buti..nakuaminia! achana na hiki kizee..Na hao wenzio waliokupigia makofi u never kno waliona unaongea pumba wakaamua kukukalisha chini kwa style hiyo..or else na wenyewe hatuwafagilii. Sijui nani anatoa mapendekezo ya viti maalum jamani!! Huyu Mama hatufai..pliz 2010 tusione sura yako Bungeni tunataka damu mpya. Acha vyombo vya habari vitupe habari zinazotuhusu maana wewe sasa sio mtanzania, huna uchungu na wananchi kabisa.

na Mtu, Australia, - 21.06.08 @ 13:07 | #17862

Anne Kilango Malecela PLEASE DON`T FORGET TO TAKE YOUR MEDICATION .YOU ARE DANGER KWA WANANCHI NA BUNGE KWA UJUMLA

na ROGER, mwanza, - 21.06.08 @ 13:14 | #17864

Wewe Anna bado unadhani watanzania wanakubaliana wanaotetea wafisadi au wanopinga wale wanaonyamazisha wanopinga Ufisadi.Wewe umekuwa katika CCM miaka mingi na waziri umetusaidia nini? au umetetea lipi?. Umekuwa ukipokea posho lako na kuendelea kutetea na wakubwa na wala rushwa.Unataka kuwanyamazisha akina mama wanaoinukia na kutaka kututetea sisi watanzania tupate haki zetu.Wewe mama tumewachoka wapifisadi wa CCM. Mimi nadhani nawe labda unamgao au nawe ni mfisadi. Mimi nilitegemea uungane naye mama Kilago mwana mapinduzi lakini unaendelea kutetea watuumiwa wa ufisadi wa akina Mkapa na wenzake ambao wameuza nchi( madini). Umenisikitisha kweli.( Tafadhali naomba mhariri umtumie mawazo yetu, aone mawazo yetu wasomaji, tulivyosikitishwa na kauli zake bungeni.Hata nami niliye nje ya nchi ninaposima mawazo yake naona huyu Anna hapashwi kuitwa mtanzania mzalendo, yeye hajaona umaskini ulioletwa na ufisadi na haoni uchumi ulivyo poromoka kutokana na rushwa, na ni kwa sababu yeye ana Shangigi na posho inayotokana na walipa fedha za walipa kodi ambao ni maskini).

na S.Kazima, Italia, - 21.06.08 @ 13:21 | #17866

ANNA ABDALLAH can u prove to us what kind of develpment you have done to Tanzanians apart from bitching in the house of parliament

na sauda, moro, - 21.06.08 @ 13:25 | #17868

Au huyu Anna Abdalla ni kati ya wale waliohusika kuchukua zile pesa za import support? Hiki kibibi bado kinafanya nini humo bungeni, Hivi JK alikisoa watu wa kuwapa hicho kiti kweli. These old figures hazina jipya. Kawawa umesikia habari ya huyu mama!!

na Twalipo jr - 21.06.08 @ 13:26 | #17869

MAMA ANA ABDALA,WATANZANIA TUMECHOKA,MWACHE MAMA ANA KILANGO MALECHELA ASEME KWA UKALI, TENA TUNATAKA TUWACHAPE VIBOKO MAFISADI. NAONA KWELI MAMA ANA ABDALA ANASHINIKIZO LA MTANDAO WA UFISADI, HATUFAI
UNATAKA WATU WASEME POLE POLE WAKATI NCHI IMEUZWA? AU UNAHUSIKA? UNAJUA MACHUNGU WANAYOYAPATA WATANZANIA? UNAKUMBUKA LINI UMESHINDA NA NJAA? AU MWANAO KUKOSA ADA? UNAJUA KUNA WAKINAMAMA TANZANIA WANAZAA NJIANI KWA KUKOSA HOSPITALI KARIBU? UNAJUA VIJANA WAKITANZANIA WANVYOPATA SHIDA ALAFU UNASEMA MAMA ANNA KILANGO MALECHELA AZUNGUMZE POLEPOLE!JAMANI WEWE ANA ABDALAH NA HUO MTANDAO WA UFISADI ONDOKENI,MNATUKERA,HATUWATAKI!

na kweli, Dar, - 21.06.08 @ 13:26 | #17870

Wachangiaji hivi huyu mama Anna Abdallah Msekwa Kawawa mbona ana macho kama mchawi.J K wa Bagamoyo ebu mpeleke Mwanza akawe mkuu wa mkoa tuone kama ataweza kuzuia vifoo vya walee bibi wazee wenye macho mekundu {macho ya kichawi kama ya mrs Msekwa Kawawa}

na RUTA Br, sweden, - 21.06.08 @ 13:29 | #17872

Anna Abdallah ifuatayo ndiyo orodha ya mabwana zako uliozaa nao huko NEC,
Marehemu John Mhavile(alikuwa mkuu wa mkoa dar(Mzee Rashid Kawawa,na mwisho ukavunja ndoa ya Mh Pius Msekwa!!kwahiyo wachangiaji naomba huyu SHANGINGI WA NEC mumsamehe,kwahiyo historia yake hapo nafikiri mmeishamjua ni mtu wa namna gani,kwahiyo kauli ile ya kusema eti wabunge wote wanataka fedha za epa zirudi si kweli,eti tofauti kauli wengine wanazunguza kwa kupaza sauti wengine taratibu,hivi niwaulize toka lini TAPELI mkaongea nae kwa sauti ya kumbembeleza!!?huyu SHANGINGI VIPI!!?tunajua INAKUUMAkwa sababu kaka yako ,Mh Mkapa anahusika na swala la ufisadi sisi hatujali sema usemavyo lakini siku zinakuja mtajibu tu wewe na kaka yako,kama umechoka pumzika usilete kidomodomo halafu huna unachojua,niungane na mchangiaji mmoja hapo juu aliyetoa wazo kuwa hata wabunge wawekewe kikomo cha kukombea ubunge kama ilivyo kwa urais,maana huyu mama akili zimechoka

na tinoh, athens greece, - 21.06.08 @ 13:47 | #17877

RUTA wa Sweden, na Twalip wa jr, na mtu mwanamke wa Australia kumbe huyu mama anaitwa mama Anna Abdallah-Msekwa Kawawa! Ka Makubwa.

Sasa ni wazi kuwa mama huyu ni fisadi tayari. Anawanaume wawili kwa mpigo. Hii kali.

Mama Anne Kilango Malecela wewe kaza Buti, kamua mafuta twende, tupo pamoja, tunataka kuona pesa za EPA na Richmond zinarudi zote by July mwaka huu. Na wasije kukusanya pesa hizo kwenye wizara halafu watufanyie usanii kuwa zimerudi.

Ubarikiwe sana mama Anne Kilango Malecela.

Anna Abdallah Gharika ya mwenyezi Mungu inakusubiri, upatilizwe mbali na hukumu ya Mungu.

na lm, hj, - 21.06.08 @ 13:48 | #17878

Huyu Mama ni mnafiki sana anapaswa kutoka hata nje ya Bunge, kusini hakuna barabara yeye anakalia kusema kuwa anauchungu hapo hakuna uchungu hata kidogo.

na masalakulanga, KUZIMU, - 21.06.08 @ 14:03 | #17881

Anna Abdallah msekwa mhaville kawawa mwisho wako nahao mafisadi unaowatetea ni 2010 tutawatoa kwa nguvu ya hoja,tabia yako inajulikana wazi kwa watanzania, tulikuwa tunakumezea tu, sasa umechokoza nyuki ni afadhali urudi kwenu kusini ukalime korosho.

na jus, ar, - 21.06.08 @ 14:03 | #17882

picha kwenye ukarasa wa mbele wa daily news 21/06/08 inaonesha huyo mama maneno aliyosema sio yake ,angalieni picha hiyo na labda kumchaya ndio pia kamwambia kwamba waandishi wa habari ni chama kisichosajiliwa !pengine ndio alivyokuwa akifanya hiyo kazi wakati alipokuwa akifanya redio tz

na abdulla, kijiwe, - 21.06.08 @ 14:26 | #17883

Jamani ninyi watanzania mumerongwa na nani
mbona munakua wajinga sana kwanini huyu mama Ana munashidwa kumushuguikia kabisa
mumuue kabisa hafai katika maisha ya watanzania kwanza ni ****** kisha Fisadi

atawamailiza kwa ukimyi pia akili yake ni mbaya sana

kwanini munashidwa kumuonesha mulango wa Minibwe akatibiwe
sisi hapa zambia watu kama hao tunawo

pole sana ndugu zangu watanzania likini munatutia aibu munalala sana naomba muamke kabisa muondoe CCM madarakani
tutawa unga mkono kama mutaomba

na Zambia1, zambia, - 21.06.08 @ 14:29 | #17885

Ama kweli watanzania tunayo kazi. Watu wa aina ya huyu mama kumbe tunao wengi hata ndani ya bunge. Kitendo cha baadhi ya wabunge kushabikia manene ya huyu mama inaonesha wazi kuna wabungu wanaokerwa na jitihada za wapigania haki za wananchi wa Tanzania. Kwa kweli hii vita ni ngumu inahitaji msaada mkubwa wa Mungu. Mama kilango usichoke, Mungu yu pamoja nawe.

na Mwinjanga, Uholanzi, - 21.06.08 @ 14:31 | #17886

NYETI ZA ANNA ABDALAH........

wajameni huyu mama kwenye jimbo lake walimfukuza kabisa walimwambia asijaribu kugombea hatapata kura ilikuwa mwaka 2000 then akaenda CCM-UWT kwavile yeye ni mwenyekiti wa UWT-CCM akalobi akapata ubunge wa viti maalum.

ukweli ni kwamba kisiasa amefilisika sana kwani kama mtakumbuka huyu yuko kwenye siasa toka enzi za nyerere na ndiyo aliwagombanisha kawawa na msekwa kwa mambo yake ya kutojiheshimu

me namshangaa badala ya yeye kuachia siasa vijana kama shyrose bhaji yeye ameng'ang'ana tu ubunge kila mtu anamshangaa...

na dunia, Dar, - 21.06.08 @ 14:41 | #17891

kama wabunge wa kuteuliwa ndo zao hizi basi mi sioni kwanini wanaendelea kulipwa mshahara unaotoka kwa wapiga kura.

na swerejr, beijing,zhongguo, - 21.06.08 @ 14:42 | #17892

Ndugu zangu Watanzania, huyu mama tunamfahamu tangu kabla hajafanyiziwa alivyokuwa mkuu wa Wilaya. Kazivuruga Wizara za Ujenzi, Afya na sasa anatetea MAFISADI.Hivi asiyejua kuwa huyu mama ni fisadi mkubwa ni nani? Jaribuni kumuuliza alivyokuwa Wizara ya Ujenzi wakati huo, yale malori ya Serikali aliyanunua kwa shilingi ngapi. Tunazotaarifa kuwa vijana waliokuwa wanajipendekeza kwake ili wapewe madaraka walikuwa wanamfanyia mpango anayachukuwa kwa bei ya kutupwa! Madudu yake akiwa Wizara ya afya ndio hayo Prof. anajitahidi kupambana nayo hadi leo. Huyu mama hana jipya hao wanaume aliyonao wanamchanganya.Wanamapinduzi tuendelee kumekucha, Mama Anne usirudi nyuma kaza kamba tuko nyuma yako. Watu wazima hawana aibu, watoto wa shule zetu wanachangia tundu moja la choo wao hawajali, wanakalia mawe (afadhali yangekuwa hata matofali) hawajali, wanapata shida ya usafiri wao wanapita na mashangingi hawajali. Hivi wamejiuliza hizo pesa za EPA zingeweza kusaidia kujenga madarasa mangapi au hata shule mpaya na vyuo mbali mbali vingapi? Nashauri, hizo pesa wanazosema zinarudi, ziundiwe kamati inayoongozwa na watu waadilifu kama Prof. Mmari, Afande Mwema na wengine watakaopendekezwa na wakereketwa wenzangu, WAZISIMAMIE ILI ZITUMIKE KUMALIZA MATATIZO KATIKA SHULE ZETU MBALI MBALI, IKIWA NI PAMOJA NA KUJENGA SHULE ZA KUTOSHA NCHI NZIMA NA KUZIPATIA WALIMU NA VITENDEA KAZI VYA KUTOSHA NA KUONDOA KERO YA USAFIRI KWA WANAFUNZI. Nasema hivyo kwa sababu, hizi pesa ni zawadi ambayo Mwenyezi Mungu ameamua kutuonyesha. Wajanja walisha tuingiza mkenge. Kwa kufanya hivyo watoto na wajukuu zetu watakuja kusimuliwa siku za usoni kuwa ziliwahi kuibwa pesa za Serikali na zipofanikiwa kurejeshwa, Rais wa wakati huo akaamua zitumike kuondoa kero kwenye jamii kwa kuagiza pesa zote zitumike kuboresha mfumo wa elimu.

mkereketwa,Kigoma
[/COLOR]
 
Kweli hatuwapendi wanawake! Mama Anna Abdallah kama vile mwenzake Anne Kilango wanastahili kupimwa kwa yale wayafanyao na wanayoyasemwa na si kuhusisha historia zao binafsi! Anna Abdallah ni mbunge ambaye ametofautiana na mbunge mwenzake. Ndiyo demokrasi. Ni haki yake. Tusikimbile kumtukana matusi ati kwa vile hatukubaliani na aliyoyasema.
 
Mimi si mtaalam sana wa siasa zetu za Tanzania.Mama Malechela ni mbunge wa kuchaguliwa na wapiga kura kwa hiyo lazima awe mkali kutetea maslahi ya wananchi,Mama Msekwa ni mbunge wa viti maalum hana deni.Mama Msekwa unapashwa kusoma alama za nyakati,huko unakotaka kuturudisha wenzio ndiyo tumeshaanza kutoka,nakuhurumia,waachie vijana!!
Felicitation Mama Malechela!!!!KUNA MTU ALISEMA JANA,KAMA KUNA WABUNGE WANAONA WATU CCM HAWATAKI KUBADILIKA,JUMP OUT ANZISHA CHAMA MTAWABWAGA CCM 2010.

na David Villa, Tanzania, - 21.06.08 @ 08:47 | #17775
 
Tangu mama huyu alipoikamata UWT wanawake wengi MAKINI hawako huko wanafanya kupita tu wakati wa UCHAGUZI kuchukua VITI MAALUM. Waulize kina Mama Mongela watakueleza Ana Abdallah Msekwa ni nani. Tunaofahamu kidogo alivyofika hapo alipo hatumshangai kwa kauli zake Bungeni wiki iliyopita. Mwanamke wa SHOKA Nchi hii ni yeye tu; akijitokeza mwingine ni lazima amkalie kooni. Anazo nguvu nyingi sana kwa wanaume MAFISADI( kwa maana halisi ya neno lenyewe) wa CCM.
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom