Msanii
Platinum Member
- Jul 4, 2007
- 22,603
- 29,745
Kwa mtazamo wangu ni kwamba, JPM ni mwanasiasa mwerevu sana.
Anachokipigania kwa ajili ya nchi yake ni uhakika wa ukuaji wa uchumi na kuiondoa nchi kutoka dimbwi la umaskini.
Anaishi kwa vitendo hasa ahadi anazotoa anatimiza. Lazima na ni kweli wapo maadui wa ndani na nje ya CCM. Maadui hao ndiyo wale majizi na mafisadi waliotufikisha kwenye pembe ya shimo la ufukara na uchumi wa hovyo.
Naweka shilingi yangu kwa JPM kuwa atarudi madarakani kwa kishindo na safari hii mazuri yatazidi uzuri
Sent using Jamii Forums mobile app
Anachokipigania kwa ajili ya nchi yake ni uhakika wa ukuaji wa uchumi na kuiondoa nchi kutoka dimbwi la umaskini.
Anaishi kwa vitendo hasa ahadi anazotoa anatimiza. Lazima na ni kweli wapo maadui wa ndani na nje ya CCM. Maadui hao ndiyo wale majizi na mafisadi waliotufikisha kwenye pembe ya shimo la ufukara na uchumi wa hovyo.
Naweka shilingi yangu kwa JPM kuwa atarudi madarakani kwa kishindo na safari hii mazuri yatazidi uzuri
Uchaguzi unakaribia watu hawataki kuvunja katiba wanamsubiri alivunje bunge waanze kumrarua kutoka pande zote.
Sio ndani ya vyombo vya usalama,
Sio ndani ya ccm wala ndani ya upinzani wote watapeleka mashambulizi juu ya hoja za Usalama wa taifa na utekaji wa watu, kuanguka kwa Uchumi, Ajira kwa vijana je amejipanga kuzuia ili gharika? wakina bashite wana msaada wowote?
Eti anakubalika kama anakubalika kwa nini anabana wapinzani ndani ya chama na nje?
Eti anapendwa sasa nawaambia subiri muone anavyopendwa ndani ya systemu ya nchi.
Nashauri aanze kufungasha vilago kwenda chato.
Sent using Jamii Forums mobile app