Anguko la Ndugai: Somo la Katiba, viongozi na nchi

Nyerere alianza uongozi wakati mgumu kuliko wote waliofuata.
Hakuwa na wasomi, hakuwa na infrastructure na hakuwa na resources za kutosha

Tukiangazia mengi aliyofanya na ni 'kashfa' kubwa kumweka katika mizani na mwingine.
Rekodi ya Nyerere katika taifa hili ni 'unique'

Kuchukua nchi yenye dini tofauti na makabila tofauti na kuiuanganisha ni jambo gumu sana

Nigeria na majirani Kenya au Uganda, miaka 60 bado zimwi la ukabila na udini linawatesa sana. Tanzania tulishaondoka huko aliyeanza kuturudisha huko ni Magufuli

Ukishaanza kuwatazama wananchi kwa jicho la dini na makabila tayari unawagawa
Mfano rahisi tu, JPM alikuwa na salam za kidini. Hili ni jambo baya sana , Tanzania ni SECULAR country. Kuna dini tofauti , watu wenye dini za asili, Wasio na dini na Wasioamini

Kusalimia kwa Ukristo na Uislam ni kutenga makundi mengine na kuyajengea makundi mawili umuhimu usio na sababu wala maana. Nchi yetu ina raia wenye dini lakini serikali haina dini.

Kilichoshangaza wakati wa JPM kila jambo lilihusisha viongozi wa dini.
Hili likajenga utamaduni wa kuamini Wakristo na Waislam, utaratibu unaoiumiza Nigeria

Lakini pia teuzi zake zilitiliwa shaka, kuna kiongozi mmoja alitoa takwimu (kukamatwa) akionyesha namna udini ulivyotamalaki. Ingawa nia yake haikuwa na dhamira njema lakini likuwa ngumu kumpinga alikuwa na takwimu!!

Nyerere, katika kumaliza ukanda udini na ukabila alianzisha mifumo ya elimu iliyokuwa ghali lakini leo tunaona manufaa yake.

Watoto wa Mkoa wa Mara walisoma Tanga, wale wa Kilimanjaro walisoma Dodoma, Wa Mwanza walikwenda Mtwara , na wa Kigoma walikwenda Mbeya.

Mchanganyiko huu uliwafanya watu waone ni wamoja na wanaweza kuishi sehemu yoyote Tanzania bila tatizo. Ndiyo maana leo kuna Wasukuma Kilimanjaro na Wabondei Shinyanga.

JPM alikuja na sera ya chuki dhidi ya kanda ya kaskazini akiwataka ''wasubiri maendeleo'
Hilo limeamsha hasira si kwa kanda moja bali nyingine wakihisi kuwa Rais kutoka eneo fulani ana influence maendeleo ya eneo jingine '' positive au negative'' na si nchi kwa ujumla

Kulikuwa na sababu gani za Rais wa nchi anayetegemewa kuwaleta wananchi pamoja kutoa kauli ya kibaguzi namna ile?

Hivi ikitokea vita kama ile ya Kagera kuna kuchagua nani aende? Kwanini basi watu watengwe.

Na kuna kosa gani watu wa eneo fulani kujiletea maendeleo?

Tukiachilia mbali Nyerere kafanya nini kwa kitu kimoja kimoja, kuunganisha Taifa ilikuwa kazi muhimu sana inayomtofautisha na waliomfuata, hawakuwa na kazi hiyo na pengine walianza kuibomoa kwa kauli za reja reja na za kibaguzi

Kumweka Nyerere na mwingine katika mizani kuna matokeo mawili;
Kumtusi sana Nyerere au kumdhalilisha sana aliyesimama katika mizani na Nyerere
Hii ligi ya nani bora umeianzisha wewe, na wewe ndio unayeiendeleza.

Hasa unapolazimisha Nyerere na Magufuli sijui unatoa wapi hoja hiyo.

Lakini pia hilo kwavile linapita sana kichwani mwako ulipaswa ujiulize mara mbilimbili KWANINI MAGUFULI Vs NYERERE, na si Mwinyi, Mkapa wala Kikwete?

Binafsi sijawahi sikia Mkapa/Mwinyi wala Kikwete Vs Nyerere, ila tu Magufuli na Nyerere.

Katika nafasi zao na nyakati zao tofauti, hao ndio viongozi pekee walioonesha kujali, kuheshimu na kulinda Rasilimali za Taifa kwa kiasi kikubwa sana kuliko wengine.

Nafasi ya Nyerere haiwezi kukaliwa na MTU mwingine yeyote, lakini chini yake hutamkosa Magufuli. Huo ukweli mnaujua ila tu mnamchukia, mnaumia.

Atazaliwa Tena na Tena.
 
Hii ligi ya nani bora umeianzisha wewe, na wewe ndio unayeiendeleza.
Huko nyuma (kasome) ulisisitiza JPM kufanya makubwa kuliko viongozi waliotangulia.
Utakumbuka nilikuuliza ni kipi tofauti alichofanya ambacho hakikufanywa na viongozi wengine?
Hasa unapolazimisha Nyerere na Magufuli sijui unatoa wapi hoja hiyo.
Soma kauli iliyotangulia, aliyeleta ulinganifu ni wewe, nilikuonya kumweka Magufuli katika mizani na viongozi wengine ni tatizo, nikakueleza kuwa Magufuli alikuwa 'unconventional leader'
Lakini pia hilo kwavile linapita sana kichwani mwako ulipaswa ujiulize mara mbilimbili KWANINI MAGUFULI Vs NYERERE, na si Mwinyi, Mkapa wala Kikwete?
Yes kwasababu wewe na wafuasi wa JPM mnamlinganisha JPM na JK Nyerere
Nilisema ukishaweka mizani ya JPM na kiongozi mwingine, JPM ni loser
Binafsi sijawahi sikia Mkapa/Mwinyi wala Kikwete Vs Nyerere, ila tu Magufuli na Nyerere.
Hao walitembelea zama zao. Wanaomlinganisha JPM na JKN ndio wamekaribisha mjadala.
Hutasikia Mwinyi, Mkapa au Kikwete wakijifaragua kwa ulinganifu na Nyerere
Katika nafasi zao na nyakati zao tofauti, hao ndio viongozi pekee walioonesha kujali, kuheshimu na kulinda Rasilimali za Taifa kwa kiasi kikubwa sana kuliko wengine.
Nyerere na Magufuli hawakutani popote kwa nyakati zozote, walikuwa na mitazamo tofauti.
Watu hufanya makosa kuwalinganisha kwa sifa, tabia, hulka au utendaji.

Nyerere ni kiongozi aliyeamini kuongoza watu. Mwalimu alisikiliza watu wanataka nini na kwanini. Nyerere aliamini katika utu na ubinadamu na kuwa tayari kukiri makosa.
Mauaji ya vikongwe Shinyanga yalionyesha sura yake katika kujali utu , haki na ubinadamu

Mwalimu alivuka mipaka kutetea walionewa kwa kuweka mbele ubinadamu
Alipinga uonevu wa Wapalestina, Ukoloni Africa na kwingineko duniani.

Msimamo ulishadidiwa na uwepo wa Tanzania NAM ikutoa nafasi ya kukemea /kushauri bila woga

Msimamo wa Nyerere duniani haukuwa na shaka, alichaguliwa kuwa miongoni mwa viongozi 6 duniani kusimamia suala la kupunguza silaha kali 'Disarmament' akishirikiana na majina makubwa kama Bi Indira Gandhi na Wolf Palme

JKN alikuwa kiongozi aliyeaminiwa kuandika mpango uliojulikana kama South-South Commission

Ukiachilia hayo alikuwa mwenyekiti wa nchi za mstari mbele 'frontline states'

Katika siasa za ndani Nyerere hakuwa tofauti, alikemea uonevu na udhalilishaji

Nyerere hakupenda kuabudiwa au tajwa au kupewa misifa, alipofanya vizuri alisema 'Tumefanya'

Katika domestic politics sifa yake kuu ilikuwa umoja wa kitaifa.

Alipenda Watanzania watazamane kama Watanzania.
Baraza lake la mawaziri lilizingatia technical know how.
Mwalimu hakuendekeza Ukanda au Ukabila na alilaani vitu hivyo

Nyerere aliwahi kusema ''madini yaachwe watanzania watakapokuwa tayari watachimba'
Hakugawa madini au vitalu vya wanyama, alihifadhi mapori ya nchi n.k.

Utaweza kumuona MwalimU Nyerere kila mahali iwe kitaifa, kikanda, Africa au Dunia yote

Sifa hizo ndizo zinamtofautisha na Magufuli

Magufuli alikuwa mtawala, hakupenda kusikiliza watu alipenda kusikilizwa.
JPM alipenda kuabudiwa , kusifiwa na kupambwa, waliomjua walimpamba leo wanamruka kimanga. Walimpendeza kwa kumwambia tuna viwanda 3000 ambavyo havipo
Wakamwamia uchumi unakua sana leo wanatuambia mabenki yalikufa n.k.

Magufuli hakujali utu au ubinadamu , alijali vitu zaidi, hakuchukia uonevu wala ujasiri wa kukemea uonevu na ilionekana alipenda kuutumia ili kuogopwa.

Hakuwa mvumilivu na hukupenda kusahihishwa wala kukoselewa. Alikuwa na sifa za Mtawala

Magufuli hana rekodi yoyote katika nyanja za kimataifa.

Kwa sehemu kubwa aliondoa nchi katika eneo hilo si kwasababu kuna manufaa bali hakuona umuhimu wa kuwa sehemu ya kimataifa. JPM si mtu Diplomasia na haikuielewa dunia vizuri pengine kwa mapungufu ya kujisomea au kusikiliza habari.

Siasa za ndani hakufanya vizuri, aliligawa Taifa vibaya katika misingi ya Udini/ Ukanda na Ukabila.

Alitukuza vitu hivyo kwa kujua au kutokuja madhara yake ya muda mrefu.
Hakuwa kiongozi wa kuunganisha na laiti nchi ingeingia vitani wakati wake Taifa lilikuwa limegawanyika vibaya. Chuki dhidi ya kanda na watu fulani au imani fulani havikumsaidia

Ukimweka katika mizani na Mwalimu, unamtafutia JPM dhalili isiyo na sababu
Nafasi ya Nyerere haiwezi kukaliwa na MTU mwingine yeyote, lakini chini yake hutamkosa Magufuli. Huo ukweli mnaujua ila tu mnamchukia, mnaumia.

Atazaliwa Tena na Tena.
Ni kweli nafasi ya Nyerere haikaliwi na mtu mwingine yeyote, na katika ''colum' yenye jina la Nyerere juu chini yake hawezi kuwa Magufuli, nisome hapo juu utaelewa
 
Huko nyuma (kasome) ulisisitiza JPM kufanya makubwa kuliko viongozi waliotangulia.
Utakumbuka nilikuuliza ni kipi tofauti alichofanya ambacho hakikufanywa na viongozi wengine?
Kwanza hakuna sehemu nimetumia hiyo kauli ya "kuliko viongozi waliotangulia", rejea zipo tuwekee.
Soma kauli iliyotangulia, aliyeleta ulinganifu ni wewe, nilikuonya kumweka Magufuli katika mizani na viongozi wengine ni tatizo, nikakueleza kuwa Magufuli alikuwa 'unconventional leader'
Hats kama hiyo kauli ingekuwa ni sahihi, KUMCHAGUA KWAKO NYERERE KATI YA WANNE WALIOTANGULIA KUNAONESHA TAYARI UFANANO WA HAO WAWILI.

Kwanini hukumchagua Mwinyi, Mkapa, au Kikwete Ila tu NYERERE? Chaguo lako linajibu hoja ya kuwa ni NYERERE tu anayeweza kuwa juu ya MAGUFULI.
Yes kwasababu wewe na wafuasi wa JPM mnamlinganisha JPM na JK Nyerere
Nilisema ukishaweka mizani ya JPM na kiongozi mwingine, JPM ni loser
Onesha wapi alitajwa NYERERE!
Hao walitembelea zama zao. Wanaomlinganisha JPM na JKN ndio wamekaribisha mjadala.
Hutasikia Mwinyi, Mkapa au Kikwete wakijifaragua kwa ulinganifu na Nyerere
Onesga wapi JKN alitajwa humu ndani kwa kumlinganisha na MAGUFULI?

Hakika, inahitaji CV kubwa sana kana ya NYERERE ili kuifunika ya MAGUFULI
Nyerere na Magufuli hawakutani popote kwa nyakati zozote, walikuwa na mitazamo tofauti.
Watu hufanya makosa kuwalinganisha kwa sifa, tabia, hulka au utendaji.
Kuwa na Mitazamo tofauti sio tatizo, Wajibu mmojawapo Mkuu wa Rais ni Kulinda na Kusimamia Rasilimali za Umma na Masilahi ya Taifa. Katika hilo anayemkaribia NYERERE ni JPM.
Nyerere ni kiongozi aliyeamini kuongoza watu. Mwalimu alisikiliza watu wanataka nini na kwanini. Nyerere aliamini katika utu na ubinadamu na kuwa tayari kukiri makosa.
Mauaji ya vikongwe Shinyanga yalionyesha sura yake katika kujali utu , haki na ubinadamu
UTU ni jambo lililokuzidi kimo, si sahihi wewe kulisenea. Kuishi Utu ni Kuishi nje ya Mihemko/Hisia, ziwe tamu au chungu.
Mwalimu alivuka mipaka kutetea walionewa kwa kuweka mbele ubinadamu
Alipinga uonevu wa Wapalestina, Ukoloni Africa na kwingineko duniani.
Nyakati za sasa hilo halina nafasi, usikariri. Katika Nyakati zake Nyerere alikuwa sahihi.
Msimamo ulishadidiwa na uwepo wa Tanzania NAM ikutoa nafasi ya kukemea /kushauri bila woga.
Waliotuletea Utegemezi wa Kisera ndio wa kulaumiwa katika hilo. Si Mwinyi, Mkapa wala Kikwete, hata Samia abayeweza kukemea chochote huko nje. Ni MAGUFULI peke yake aliyekuwa na uthubutu kuchallenge Mataifa makubwa. Masikini Jeuri, wengine ni timu hewala baba.

Msimamo wa Nyerere duniani haukuwa na shaka, alichaguliwa kuwa miongoni mwa viongozi 6 duniani kusimamia suala la kupunguza silaha kali 'Disarmament' akishirikiana na majina makubwa kama Bi Indira Gandhi na Wolf Palme
Hukuwa na haja ya kuandika mengi.
JKN alikuwa kiongozi aliyeaminiwa kuandika mpango uliojulikana kama South-South Commission

Ukiachilia hayo alikuwa mwenyekiti wa nchi za mstari mbele 'frontline states'
Jani uliloshika halikusaidii, maji mengi sana.
Katika siasa za ndani Nyerere hakuwa tofauti, alikemea uonevu na udhalilishaji

Nyerere hakupenda kuabudiwa au tajwa au kupewa misifa, alipofanya vizuri alisema 'Tumefanya'

Katika domestic politics sifa yake kuu ilikuwa umoja wa kitaifa.
Still mtaani kuna minong'ono ya Mfumo Kristo (nadhani unamjua Mzee Mohammed Said)
Still kuna minong'ono ya kutengwa kwa makabila makubwa katika nafasi ya juu.

Yote hayo muasisi ni Nyerere, ndivyo wanavyodai. MADAI YAO NI SAWA NA YAKO KWA MAGUFULI.
MTI WENYE MATUNDA.
Alipenda Watanzania watazamane kama Watanzania.
Wazanzibari bado wapo Leo...
Baraza lake la mawaziri lilizingatia technical know how.
Mwalimu hakuendekeza Ukanda au Ukabila na alilaani vitu hivyo
Rejea hapo juu...
Nyerere aliwahi kusema ''madini yaachwe watanzania watakapokuwa tayari watachimba'
Hakugawa madini au vitalu vya wanyama, alihifadhi mapori ya nchi n.k.
Semea nafsi yako sasa yupi walau aliliishi hili walau kwa mbali....
Utaweza kumuona MwalimU Nyerere kila mahali iwe kitaifa, kikanda, Africa au Dunia yote

Sifa hizo ndizo zinamtofautisha na Magufuli
Kinachowatofautisha zaidi ni Nyakati tu na Mazingira, Mengi Jpm ameyaishi.
Magufuli alikuwa mtawala, hakupenda kusikiliza watu alipenda kusikilizwa.
JPM alipenda kuabudiwa , kusifiwa na kupambwa, waliomjua walimpamba leo wanamruka kimanga. Walimpendeza kwa kumwambia tuna viwanda 3000 ambavyo havipo.
Hatujawahi kusema hana madhaifu hakika.
Wakamwamia uchumi unakua sana leo wanatuambia mabenki yalikufa n.k.
Ukimwambia bibi aliyenunua sabuni sh 500 wakati wa MAGUFULI kuwa uchumi ulianguka, Ila umekua leo abaponunua sabuni sh 700, atakulaani.
Magufuli hakujali utu au ubinadamu , alijali vitu zaidi, hakuchukia uonevu wala ujasiri wa kukemea uonevu na ilionekana alipenda kuutumia ili kuogopwa.
UTU na mihemko havichangamani.
Hakuwa mvumilivu na hukupenda kusahihishwa wala kukoselewa. Alikuwa na sifa za Mtawala.
Ipo tofauti ya Bezo, Matusi, Ukosoaji na Ushauri.
Magufuli hana rekodi yoyote katika nyanja za kimataifa.
IPO, ana Rekodi Chafu Kimataifa, ya Kuchukiwa. Na hakika hiyo ndio TUNAMTAKA.
Kwa sehemu kubwa aliondoa nchi katika eneo hilo si kwasababu kuna manufaa bali hakuona umuhimu wa kuwa sehemu ya kimataifa.
JPM si mtu Diplomasia na haikuielewa dunia vizuri pengine kwa mapungufu ya kujisomea au kusikiliza habari.
Msipumbaze watu, HAKUNA MAHUSIANO YA KAKA NA DADA KIMATAIFA, ILA TU BIASHARA. UNATOA NINI UNAPATA NINI BASI.

Punguzeni kubeba FIKRA ZA WAUZA NCHI.
Siasa za ndani hakufanya vizuri, aliligawa Taifa vibaya katika misingi ya Udini/ Ukanda na Ukabila.
Hapa watakuwa wanafanana na JKN(kwa hoja za Mfumo Kristo za Mohammed Said)
Alitukuza vitu hivyo kwa kujua au kutokuja madhara yake ya muda mrefu.
Hakuwa kiongozi wa kuunganisha na laiti nchi ingeingia vitani wakati wake Taifa lilikuwa limegawanyika vibaya. Chuki dhidi ya kanda na watu fulani au imani fulani havikumsaidia
Acheni Uongo, FIKA KILIMANJARO leo ukapime hiyo chuki.

Mnabeba Chuki za Kufikirika, Msikazimishe vitu vusivyokuwepo.
Ukimweka katika mizani na Mwalimu, unamtafutia JPM dhalili isiyo na sababu
Na Mwinyi, Mkapa, Kikwete Je?
Ni kweli nafasi ya Nyerere haikaliwi na mtu mwingine yeyote, na katika ''colum' yenye jina la Nyerere juu chini yake hawezi kuwa Magufuli, nisome hapo juu utaelewa
Sifikiri hata kana mwenyewe umekielewa ukichoandika.

Tumempoteza SHUJAA HAKIKA.
 
Hats kama hiyo kauli ingekuwa ni sahihi, KUMCHAGUA KWAKO NYERERE KATI YA WANNE WALIOTANGULIA KUNAONESHA TAYARI UFANANO WA HAO WAWILI.
Hoja hapa ni moja JPM alikuwa 'unconventional leader' tofauti na Mwinyi, Mkapa na Kikwete
Nyerere alikuwa 'unique' miongoni mwao na anabaki kuwa standard
AHM, BWM na JMK waliheshimu katiba na taratibu kama alivyofanya Nyerere

Wafuasi wa JPM humlinganisha na JK Nyerere na hilo ni kosa!
Kwanini hukumchagua Mwinyi, Mkapa, au Kikwete Ila tu NYERERE? Chaguo lako linajibu hoja ya kuwa ni NYERERE tu anayeweza kuwa juu ya MAGUFULI.
Wala Nyerere hawezi kuwa katika 'row au column' moja na Magufuli. Hakuna ufanano wala ulinganifu. Kumlinganisha na JKN ni kumweka katika std na hapo habari inakwisha mapema
Hakika, inahitaji CV kubwa sana kana ya NYERERE ili kuifunika ya MAGUFULI
CV za wawili hao zina kitu kimoja kinachofanana, wote waliwahi kuishi magogoni Ikulu! only
Waliotuletea Utegemezi wa Kisera ndio wa kulaumiwa katika hilo. Si Mwinyi, Mkapa wala Kikwete, hata Samia abayeweza kukemea chochote huko nje. Ni MAGUFULI peke yake aliyekuwa na uthubutu kuchallenge Mataifa makubwa. Masikini Jeuri, wengine ni timu hewala baba.
Well, JPM haku challenge ! alionekana wa wajabu . Unaamini mataifa ya Magharibi yana vita ya uchumi na Tanzania! Matifa hayo yajibu nini kuhusu kupima mafenesi na mbuzi kwa kutumia 'calibrated equipment'. Mataifa ya magharibi ya m-challenge kwa kutovaa barakoa ! etc etc
Hukuwa na haja ya kuandika mengi.
Of course hupendi kuona CV ya Nyerere ilivyoshiba lakini ndiyo CV iliyopo
Utaifananisha na ile ya flyover ! my foot
Still mtaani kuna minong'ono ya Mfumo Kristo (nadhani unamjua Mzee Mohammed Said)
Still kuna minong'ono ya kutengwa kwa makabila makubwa katika nafasi ya juu.
Yote hayo muasisi ni Nyerere, ndivyo wanavyodai. MADAI YAO NI SAWA NA YAKO KWA MAGUFULI.
MTI WENYE MATUNDA.
Tumejadili sana mfumo kristo na mwasisi wake, hakuweza ku substantiate mfumo huo ulikuwaje.
Kinyume chake tulionyesha jinsi Nyerere alivyotaifisha shule na Hospitali katika kujenga Taifa lenye fursa sawa. Mwasisi yupo jamii forum, mfuate umuulize alipokwama na leo hazungumzii tena Nyerere alifanya kitu kuleta uwiano. Kinachoitwa mfumokristo ni matokeo ya Historia ya nchi kwa kuzingatia ukoloni na dini na usambazaji wa huduma kama elimu na afya.
Wazanzibari bado wapo Leo...
Tena Uzanzibar umeibuka baada ya Mwalimu.
Kinachowatofautisha zaidi ni Nyakati tu na Mazingira, Mengi Jpm ameyaishi.
Hapana! Nyerere na Magufuli ni Mlima Kilimanjaro na kichuguu! Magufuli hana sifa za kubeba viatu vya Mwalimu, hilo si jema kulisema lakini ndio ukweli. 10-0
Hatujawahi kusema hana madhaifu hakika.
Yes alikuwa na madhaifu mengi na ya hatari. Kugawa Taifa kwa msingi ya udini, kuingiza dini katika shughuli za umma, kutenga dini na makundi mengine akiamini Uislam na Ukristo ni kitu kibaya sana. Huko tulishapita na hakuchaguliwa kuwa Sheikh au Padre! so awful

Kwanyanyasa watu wa kanda zingine ni kitendo kibaya sana, ni kuligawa Taifa kwa ukanda , ukabila. Matokeo yake yanaliumiza Taifa sasa hivi. Huu ukanda unaongelewa kaasisi JPM

Kubagua Walipa kodi kwa itikadi za kisiasa ni kitendo kibaya sana. Kwamba, Rais wa nchi anajiapiza kuwanyima maendeleo watu wanaolipa kodi anayotumia! pathetic

sipumbaze watu, HAKUNA MAHUSIANO YA KAKA NA DADA KIMATAIFA, ILA TU BIASHARA. UNATOA NINI UNAPATA NINI BASI.
Yes na JPM hakuliona hilo. JPM alisema hovyo majirani wakaataa mahindi yetu,hakuwa na Diplomacy. Hakutangamana na dunia, alikuwa na ''fantasy world''

Si kwamba alifanya kwa lengo , ni upungufu tu wa kuielewa dunia, kujisomea, wigo wa mawazo n.k. Sidhani kama alisoma hata gazeti jingine zaidi ya Uhuru!

Communication skills ilikuwa challenge kwake! ilimkwaza kutokana na knowledge hafifu
Aliweza ku compensate deficiency katika communication skills kwa kufoka foka
 
Hoja hapa ni moja JPM alikuwa 'unconventional leader' tofauti na Mwinyi, Mkapa na Kikwete
Nyerere alikuwa 'unique' miongoni mwao na anabaki kuwa standard
AHM, BWM na JMK waliheshimu katiba na taratibu kama alivyofanya Nyerere
Being Conventional au Unconventional sio hoja hapa. HOJA KUU ni yupi kati ya Watano aliyeheshimu, kulinda na kuthamini RASILIMALI ZA TAIFA NA USTAWI WAKE?
Baada ya Nyerere, kutomuweka MAGUFULI ni Kujitoa ufahamu.
Wafuasi wa JPM humlinganisha na JK Nyerere na hilo ni kosa!
Hawafanani Uzito, lakini si kweli kwamba hakuna wanachofanana tena pakubwa tu.
Wala Nyerere hawezi kuwa katika 'row au column' moja na Magufuli. Hakuna ufanano wala ulinganifu. Kumlinganisha na JKN ni kumweka katika std na hapo habari inakwisha mapema
Ingekwisha mapema wewe leo usingemchagua Nyerere out of 5 kubattle na MAGUFULI.

Matendo yako yanakuvua Nguo.
CV za wawili hao zina kitu kimoja kinachofanana, wote waliwahi kuishi magogoni Ikulu! only
Dhati, Ujasiri, Uthubutu, Uzalendo, Kujitambua, Uafrika, Wajibu, UTU, nk.... Tofauti yao kubwa ni Sifa na Upole.
Well, JPM haku challenge ! alionekana wa wajabu . Unaamini mataifa ya Magharibi yana vita ya uchumi na Tanzania! Matifa hayo yajibu nini kuhusu kupima mafenesi na mbuzi kwa kutumia 'calibrated equipment'. Mataifa ya magharibi ya m-challenge kwa kutovaa barakoa ! etc etc
Porojo!
Of course hupendi kuona CV ya Nyerere ilivyoshiba lakini ndiyo CV iliyopo
Utaifananisha na ile ya flyover ! my foot
Hakuna ayekataa CV ya Nyerere. Sasa hamia kwa hao wengine.
Tumejadili sana mfumo kristo na mwasisi wake, hakuweza ku substantiate mfumo huo ulikuwaje.
Tambua hutofautiani na Mohammed Said.
Kinyume chake tulionyesha jinsi Nyerere alivyotaifisha shule na Hospitali katika kujenga Taifa lenye fursa sawa.
Bora huko kuna mpaka matendo yaliyotafsiriwa vibaya, ila wewe leo unakuja na porojo za ALISEMA, Fulani naye SI KASEMA.
Mwasisi yupo jamii forum, mfuate umuulize alipokwama na leo hazungumzii tena Nyerere alifanya kitu kuleta uwiano.
Wewe ni copy yake hapa, sina haja ya kumfuata. Na aliyekuambia hazungumzii tena amekudanganya.
Kinachoitwa mfumokristo ni matokeo ya Historia ya nchi kwa kuzingatia ukoloni na dini na usambazaji wa huduma kama elimu na afya.
Unajaribu kupotosha hoja za watu... Hoja zao ni kuwa Nyerere ndio Muasisi.

Ni rahisi tu ndugu, shutuma zao dhidi ya Ukanda na Ukabila na Udini wa Nyerere ni Mfu sawa na zenu juu ya MAGUFULI.
Na ndio kimbilio LA losers mara nyingi.
Tena Uzanzibar umeibuka baada ya Mwalimu.
Mpaka Karume mwenyewe akiwahi kutamka Kulivua Koti. KWANINI UNAKUWA MUONGO MOONGO?
Hapana! Nyerere na Magufuli ni Mlima Kilimanjaro na kichuguu! Magufuli hana sifa za kubeba viatu vya Mwalimu, hilo si jema kulisema lakini ndio ukweli. 10-0
Sema ni nani kati ya 6 mwenye sifa zinazomzidi MAGUFULI kubeba viatu vyav. Nyerere katika KULINDA TAIFA NA RASILIMALI ZAKE?
Yes alikuwa na madhaifu mengi na ya hatari. Kugawa Taifa kwa msingi ya udini, kuingiza dini katika shughuli za umma, kutenga dini na makundi mengine akiamini Uislam na Ukristo ni kitu kibaya sana. Huko tulishapita na hakuchaguliwa kuwa Sheikh au Padre! so awful
POROJO. Hoja za Kulazimisha.
Kwanyanyasa watu wa kanda zingine ni kitendo kibaya sana, ni kuligawa Taifa kwa ukanda , ukabila. Matokeo yake yanaliumiza Taifa sasa hivi.
Let's ushahidi wa Manyanyaso hayo.
Huu ukanda unaongelewa kaasisi JPM
Mtaani kuna kasumba ya kuwa Nyerere alikataa watu kutoka kanda ile na makabila yale kutoingia ikulu.
Kubagua Walipa kodi kwa itikadi za kisiasa ni kitendo kibaya sana. Kwamba, Rais wa nchi anajiapiza kuwanyima maendeleo watu wanaolipa kodi anayotumia! pathetic
Sema wepi huko kulitokea hilo? Ni kanda gani haikufanyiwa chochote na MAGUFULI?
Yes na JPM hakuliona hilo. JPM alisema hovyo majirani wakaataa mahindi yetu,hakuwa na Diplomacy.
Mlizoea kujipendekeza hovyohovyo kwa masters wenu. Mfano wako wa mahindi ni hovyo kabisa, KWANINI sasa waliendelea kununua baada nasi kuwapa kibano?

FIKRA ZENU ZA KUJIPENDEKEZA NA KUJINYENYEKEZA ZINAKERA SANA. HERI KIZAZI CHENU KIPOTEE HARAKA. MMEJAA FIKRA ZA KITUMWATUMWA .
Hakutangamana na dunia, alikuwa na ''fantasy world''
YES, Tusipokuwa na Uthubutu wa Kujenga our own WORLD hata aje nani hatutajitegemea kamwe.
Si kwamba alifanya kwa lengo , ni upungufu tu wa kuielewa dunia, kujisomea, wigo wa mawazo n.k. Sidhani kama alisoma hata gazeti jingine zaidi ya Uhuru!
Muijuao dunia vizuri mmekuwa watumwa na vibaraka wa Ukoloni. Yule asiyeijua dunia vizuri ameishi akijinasua mitego ya Ukoloni huo.

ANGUKO KUU LA TAIFA HILI SI UKOLONI BALI WATU WENYE FIKRA KAMA ZAKO. NINYI NI AIBU KABISA.
Communication skills ilikuwa challenge kwake! ilimkwaza kutokana na knowledge hafifu
Aliweza ku compensate deficiency katika communication skills kwa kufoka foka
Hilo halibatilishi wala kuhalalisha chochote. Muhimu alilinda TAIFA na RASILIMALI zake.
 
Being Conventional au Unconventional sio hoja hapa. HOJA KUU ni yupi kati ya Watano aliyeheshimu, kulinda na kuthamini RASILIMALI ZA TAIFA NA USTAWI WAKE? Baada ya Nyerere, kutomuweka MAGUFULI ni Kujitoa ufahamu.
Wote wanne waliotangulia walilinda rasilimali za asili , uchumi na rasilimali watu.
JPM alifanana na wengine katika kipengele cha rasilimali za asili.

Rasilimali za uchumi bado hatujui 1.5T ipo wapi wala 70B zilizokwenda Mwanza zipo wapi

Hatuna rekodi ya Nyerere, Mwinyi , Mkapa au Kiwekete kuondoka madarakani na chochote
Hawafanani Uzito, lakini si kweli kwamba hakuna wanachofanana tena pakubwa tu.
Eleza Nyerere na Magufuli wanafanana wapi ukiachilia kwamba wote waliishi Magogoni!
Dhati, Ujasiri, Uthubutu, Uzalendo, Kujitambua, Uafrika, Wajibu, UTU, nk.... Tofauti yao kubwa ni Sifa na Upole.
Miaka 24 Nyerere hayupo. Hakuna mahali, Bank, Taasisi au mtu binafsi aliyejitokeza kusema Nyerere aliondoka na Fuba la Pesa au kutumia rasilimali za Taifa kujenga kwao miradi hovyo kama Burigi kwa wivu tu wa kaskazini na Airport isiyo na kazi

Kama ujasiri na uthubutu ni kutojulikana Trilioni za rasilimali zilipo, sina comment
Hakuna ayekataa CV ya Nyerere. Sasa hamia kwa hao wengine.
CV ya Mkapa hailingani na Magufuli. Mkapa hapewi credit za kutosha, ni kiongozi aliyekuza uchumi aliyeheshimu utawala, watu na ubinadamu
Ni rahisi tu ndugu, shutuma zao dhidi ya Ukanda na Ukabila na Udini wa Nyerere ni Mfu sawa na zenu juu ya MAGUFULI.Na ndio kimbilio LA losers mara nyingi.
Ni hivi Mwalimu aliunganisha Taifa kwa ujumla wake, Magufuli aligawa Taifa kwa ujumla wake.period
Sema ni nani kati ya 6 mwenye sifa zinazomzidi MAGUFULI kubeba viatu vyav. Nyerere katika KULINDA TAIFA NA RASILIMALI ZAKE?
AH, BWM, JMK wanabeba viatu vya mwalimu, mikono inaweza kuwa michafu, inasafishika.

JPM mikono yake haifanani na alichosimamia mwalimu, utu, ubinadamu na kuthamini damu ya mwanadamu. Kwa mikono ipi JPM atabeba viatu vya Mwlaimu? please
Let's ushahidi wa Manyanyaso hayo.
Kushika kipaza sauti na kuwaambia Watanzania ''Kanda ya kaskazini watusubiri' ni manyanyaso

Hao wa kaskazini ni walipa kodi, maendeleo ni jitihada zao leo wanakuwaje raia wa kigeni kwenye ardhi yao? Kauli hiyo haijawahi kutolewa na Marais wanne waliotangulia hata kwa bahati mbaya.
Sema wepi huko kulitokea hilo? Ni kanda gani haikufanyiwa chochote na MAGUFULI?
Ipi unauliza wakati alisema ''Kaskazini Wasubiri'?
HERI KIZAZI CHENU KIPOTEE HARAKA. MMEJAA FIKRA ZA KITUMWATUMWA .
Aha! sema tu maana ndiyo sera aliyowaachia. Ukitofautiana na mwenzako kimawazo poteza.Sera ilifanya kazi na mnataka iendelee! Yes! tesa, ua, poteza .
YES, Tusipokuwa na Uthubutu wa Kujenga our own WORLD hata aje nani hatutajitegemea kamwe.
Fantasy world ni tofauti na own world! JPM alikuwa na the former
Yule asiyeijua dunia vizuri ameishi akijinasua mitego ya Ukoloni huo.
Eeee! kwa siri you mean! Deni la Taifa lilikuwa sana nyakati zake, tukiangalia nyaraka alifanya kazi na Wakoloni. Tofauti na wengine yeye aliwananga hadharani nyuma ya pazia akiwa peti peti!
ANGUKO KUU LA TAIFA HILI SI UKOLONI BALI WATU WENYE FIKRA KAMA ZAKO. NINYI NI AIBU KABISA.
Hilo halibatilishi wala kuhalalisha chochote. Muhimu alilinda TAIFA na RASILIMALI zake.
Anguko kuu la Taifa ni ku bet katika kupata viongozi, tukishindwa kuchuja.
Tukawapa uwezo wasio nao na kuwaamini kwa kelele na tambo zao!
Tukashindwa kuchuja werevu na Washamba
 
Wote wanne waliotangulia walilinda rasilimali za asili , uchumi na rasilimali watu.
JPM alifanana na wengine katika kipengele cha rasilimali za asili.
Kwamba MAGUFULI amefanana na Mwinyi katika kulinda Uchumi Wetu, Amefanana na Mkapa katika kulinda Madini Yetu, amefanana na Kikwete katika kulinda Gas Yetu!?

Hongereni, sasa mnakaribia kuuza Ngorongoro pia kama Loliondo mkimuenzi Nyerere.

WANAFIKI.
Rasilimali za uchumi bado hatujui 1.5T ipo wapi wala 70B zilizokwenda Mwanza zipo wapi
Hakuna kitu kinaitwa RASILIMALI za Uchumi halafu kiwe nje ya Madini, Mazao, Utalii, Uvuvi, Biashara, nk....

UNA HOJA ZA KULAZIMISHA.
Hatuna rekodi ya Nyerere, Mwinyi , Mkapa au Kiwekete kuondoka madarakani na chochote
Mtoe Mwinyi na Nyerere, hao wengine walitumia sheria kuibia TAIFA. Wizi wao unaonekana kupitia jamaa zao, Rostam nk...

Sasa tuamvie wewe, T 1.5 unaiona wapi? Au walimfukia nayo?

UNAFIKI.
Eleza Nyerere na Magufuli wanafanana wapi ukiachilia kwamba wote waliishi Magogoni!
Nimeshataja mengi, Mihemko yako inakufanya usione na kurudiarudia maswali.
Miaka 24 Nyerere hayupo. Hakuna mahali, Bank, Taasisi au mtu binafsi aliyejitokeza kusema Nyerere aliondoka na Fuba la Pesa au kutumia rasilimali za Taifa kujenga kwao miradi hovyo kama Burigi kwa wivu tu wa kaskazini na Airport isiyo na kazi
Hawa wengine sasa..... Loliondo, IPTL, Richmond, Gas, Visiwa kupigwa Chenji, Ngorongoro, bado kitaa kina fununu za Vituo vya Mafuta, Kampuni za Usafiri(wahujumu reli) Hotels, Estates, Utukufu wa Watoto wao,..nk..

Yaani unajisahulisha hata Account Uswis? Mpaka Balali?

Yoye hayo bado mnataka mtufumbe macho!! HAMTAWEZA KUTUDANGANYA TENA, WEZI.
Kama ujasiri na uthubutu ni kutojulikana Trilioni za rasilimali zilipo, sina comment
Porojo.
CV ya Mkapa hailingani na Magufuli. Mkapa hapewi credit za kutosha, ni kiongozi aliyekuza uchumi aliyeheshimu utawala, watu na ubinadamu
Still 2021 yaliyotokea Zanzibar unayajua, Mikataba ya hovyo kwwnye madini mingi ilianza Nate. Ubinafsishaji hovyo...

UKIUZA NCHI WAJOMBA ZENU ULAYA watawasifia kukua kwa Uchumi, na NINYI huku mtashangilia kwa vifijo.

Enslaved totally.
Ni hivi Mwalimu aliunganisha Taifa kwa ujumla wake, Magufuli aligawa Taifa kwa ujumla wake.period
Porojo.
AH, BWM, JMK wanabeba viatu vya mwalimu, mikono inaweza kuwa michafu, inasafishika.
Kujitoa Ufahamu tu.... Kamsafishe Mkapa Zanzibar, Kikwete kwa Mwangosi.

JPM mikono yake haifanani na alichosimamia mwalimu, utu, ubinadamu na kuthamini damu ya mwanadamu. Kwa mikono ipi JPM atabeba viatu vya Mwlaimu? please
Mihemko yako tu. Hakuna damu iliyo juu ya Masilahi ya TAIFA hata hivyo.
Kushika kipaza sauti na kuwaambia Watanzania ''Kanda ya kaskazini watusubiri' ni manyanyaso.
Lete matendo nje ya kauli...USIJITOE UFAHAMU.
Hao wa kaskazini ni walipa kodi, maendeleo ni jitihada zao leo wanakuwaje raia wa kigeni kwenye ardhi yao? Kauli hiyo haijawahi kutolewa na Marais wanne waliotangulia hata kwa bahati mbaya.
Porojo.
Ipi unauliza wakati alisema ''Kaskazini Wasubiri'?
Porojo.
Aha! sema tu maana ndiyo sera aliyowaachia. Ukitofautiana na mwenzako kimawazo poteza.Sera ilifanya kazi na mnataka iendelee! Yes! tesa, ua, poteza .
Asili itaamua juu yenu.... Wakati huo mifupa yetu itashuhudia Ukuu wa FIKRA za MAGUFULI zikineemesha Taifa.
Fantasy world ni tofauti na own world! JPM alikuwa na the former
Ni upofu wenu tu kutoona.
Eeee! kwa siri you mean! Deni la Taifa lilikuwa sana nyakati zake, tukiangalia nyaraka alifanya kazi na Wakoloni. Tofauti na wengine yeye aliwananga hadharani nyuma ya pazia akiwa peti peti!
Nilishakuambia, Nitarudia. MAHUSIANO YOYOTE YA TAIFA NA TAIFA NI BIASHARA. Ninyi ndio mnaoshangaza kudai aliua MAHUSIANO ya KIMATAIFA huku mnasema kaenda kukopa sana huko.

ALIFANYA BIASHARA, HAKUWA MTU WA KULIALIA KAMA WEWE NA NDUGU ZAKO.

Miradi aliyoianzisha, na pesa aliyokopa, sisi vinaendana kwa kiasi kikubwa.

Msisahau NINYI mlikopa ili muibe mpeleke Uswis hela.
Anguko kuu la Taifa ni ku bet katika kupata viongozi, tukishindwa kuchuja.
Tukawapa uwezo wasio nao na kuwaamini kwa kelele na tambo zao!
Tukashindwa kuchuja werevu na Washamba
Heri yako wewe Born Town, Nyakati NI zako sasa, Furahi Wizi wako.
 
Kwamba MAGUFULI amefanana na Mwinyi katika kulinda Uchumi Wetu, Amefanana na Mkapa katika kulinda Madini Yetu, amefanana na Kikwete katika kulinda Gas Yetu!?
Kipi unadhani JPM alikuwa nacho cha ziada? Mapato yatokanayo kama zile 1.5T na 70B vipi?
Hongereni, sasa mnakaribia kuuza Ngorongoro pia kama Loliondo mkimuenzi Nyerere
Mtoe Mwinyi na Nyerere, hao wengine walitumia sheria kuibia TAIFA. Wizi wao unaonekana kupitia jamaa zao, Rostam nk...
Eeee! kama walifanya hivyo ilikuwa mbaya sana, si wangetumia Watoto wa Dada! pengine ingependeza.
Sasa tuamvie wewe, T 1.5 unaiona wapi? Au walimfukia nayo?
CAG Assad hakuwahi kujibiwa, CAG Kichere hawakuwahi kujibiwa. Siyo mimi ni maandiko na yapo
Yaani unajisahulisha hata Account Uswis? Mpaka Balali?
Wizi hauhalalishwi na wizi mwingine. Tunazungumzia zama za Mwendazake
Unaposema X alifanya unatuambia ni haki Y kufanya. Two wrongs don't make a right
Ndiyo maana tunasema Nyerere halinganishwi na Magufuli kwasababu ni std si wengine
Still 2021 yaliyotokea Zanzibar unayajua, Mikataba ya hovyo kwwnye madini mingi ilianza Nate. Ubinafsishaji hovyo...
Yes BWM amesimama na kukiri makosa, ameandika kitabu na kukiri makosa. Kuna mambo yanatokea bila kudhamiria lakini kukiri ni Uungwana.

Nyerere aliwahi kuzungumzia na kukiri makosa kwa mauji ya vikongwe Shinyanga

Magufuli aliwahi kuzungumzia nini kwa mauji yaliyotokea yakiwemo ya watu kuokotwa baharini na mitoni? Watu wanaua kwa sababu za kisiasa hakuwahi kukemea hata siku moja.
Kutofautiana kimawazo ilikuwa ni jinai na hukumu yake unaijua kama ulivyosema '' poteza''

Hiyo ndiyo tofauti ya Utu, Ubinadamu na kujali baina ya viongozi .
Yes, unajua huna hoja. Mwenda alikuwa na chuki na watu wa kaskazini! chuki tu bila sababu
Kachukua kipaza sauti na kuliambia Taifa '' Wa kaskazini watubiri'' Hakuwahi kusema wasubiri kulipa kodi. Maendeleo ni zao la juhudi za watu, kuchukia juhudi za watu ni chuki mbaya sana
Nilishakuambia, Nitarudia. MAHUSIANO YOYOTE YA TAIFA NA TAIFA NI BIASHARA.
Of course yes , lakini kujifungia ni mbaya , kuwananga hadharani na kukopa kwa siri ni unafiki
Ni uongo kama ule COVID kuletwa kwa kutumia Barakoa!
Ni uongo kama ule wa BANK kutoa migao serikalini , Mwigulu anasema zilikuwa zinakufa
Miradi aliyoianzisha, na pesa aliyokopa, sisi vinaendana kwa kiasi kikubwa.
Yes, lakini 1.5T na 70B zilitumika katika miradi gani? Zipo wapi? CAG Assada & Kichere
Msisahau NINYI mlikopa ili muibe mpeleke Uswis hela.
Hoja ni moja 1.5T na 70B zipo wapi?
 
Kipi unadhani JPM alikuwa nacho cha ziada?
Hakuuza Loliondo wala Ngorongoro, hakuingia mikataba ya kimangungo kama ile ya gas na madini. Mbali zaidi walau alijaribu kuitafuta mikataba ya madini yenye tija kwa TAIFA. Walau alionesha kukerwa na wezi wetu, na Umma unajua wizi huo sasa.
Tofauti wewe na timu yako ya walamba miguu ya wazungu.
Mapato yatokanayo kama zile 1.5T na 70B vipi?
Kamuulize Assad sasa leo aseme zilitokaje kwanza na zilikuwa wapi. Naona mnafanana mwaenda mwasononekea nyadhifa mlizokosa. Kila siku majungumajungu.

Mshauri mzee aondoe chuki iliyojaa kifuani, atapasuka kifua.
Eeee! kama walifanya hivyo ilikuwa mbaya sana, si wangetumia Watoto wa Dada! pengine ingependeza.
Tuoneshe hao watoto wa Dada walichonacho. 1.5 T ni karibia nusu ya utajiri wa Mo. Tuoneshe mtoto wa Dada mwenye nao. Au hata acc za nje labda.

Mkubwa mzima unajenga hoja kwa stori za vijiweni na kuzirudiarudia.

Halafu hapa chini unadai Wizi hauhalalishi wizi mwingine.
CAG Assad hakuwahi kujibiwa, CAG Kichere hawakuwahi kujibiwa. Siyo mimi ni maandiko na yapo
Timu yako ihitimishe majibu sasa leo, MAGUFULI hayupo tena, semeni zipo kwenye mfuko wa nani T1.5? Au Mama Janet amezifunga kwa kitenge?
Wizi hauhalalishwi na wizi mwingine. Tunazungumzia zama za Mwendazake
Unaposema X alifanya unatuambia ni haki Y kufanya. Two wrongs don't make a right
Ndiyo maana tunasema Nyerere halinganishwi na Magufuli kwasababu ni std si wengine
Usijitoe ufahamu ndugu, Hapa hatuhalalishi wizi kwa wizi. Hoja ilikuwa kati ya hao yupi anastahili kufuata baada ya Nyerere. Nawe ukasema MAGUFULI hafai kwa porojo za T1.5 za kusadikika, ila wa acc Uswis ukaonapoa tu.

Unafiki.

Yes BWM amesimama na kukiri makosa, ameandika kitabu na kukiri makosa. Kuna mambo yanatokea bila kudhamiria lakini kukiri ni Uungwana.
Leo umekuwa mpaka na uwezo wa kujua dhati ya mtu eti.

Je, tuseme MAGUFULI naye angeandika kuomba radhi baada ya kustaafu, INGEBADILISHA NINI KWAKO? Mbona unapenda sana michezo ya kitotototo?
Nyerere aliwahi kuzungumzia na kukiri makosa kwa mauji ya vikongwe Shinyanga

Magufuli aliwahi kuzungumzia nini kwa mauji yaliyotokea yakiwemo ya watu kuokotwa baharini na mitoni? Watu wanaua kwa sababu za kisiasa hakuwahi kukemea hata siku moja.
Kutofautiana kimawazo ilikuwa ni jinai na hukumu yake unaijua kama ulivyosema '' poteza''
Assad yupo hai, Zitto, Wewe, Mbowe,na wengineo wengi tu. Mbona hawakupotezwa?

Hiyo ndiyo tofauti ya Utu, Ubinadamu na kujali baina ya viongozi .
Mtumwa kujali mbwa wa bwana wake si UTU ni WENDAWAZIMU.
Yes, unajua huna hoja. Mwenda alikuwa na chuki na watu wa kaskazini! chuki tu bila sababu
Kachukua kipaza sauti na kuliambia Taifa '' Wa kaskazini watubiri'' Hakuwahi kusema wasubiri kulipa kodi. Maendeleo ni zao la juhudi za watu, kuchukia juhudi za watu ni chuki mbaya sana
POROJO.
Of course yes , lakini kujifungia ni mbaya , kuwananga hadharani na kukopa kwa siri ni unafiki
Hawakukataa walionangwa kutoa mikopo, uumie wewe eti. Hamjitambui hakika.
Ni uongo kama ule COVID kuletwa kwa kutumia Barakoa!
Ni uongo kama ule wa BANK kutoa migao serikalini , Mwigulu anasema zilikuwa zinakufa
Hivi unafahamu nini juu ya UTUMWA WA KIFIKRA?
Kuna kagonjwa kengine huko kutoka kwa Nyani wa Afrika, jiandae kupeleka mwili wako huo, maana umekosa FIKRA sahihi za kuuendesha.
Yes, lakini 1.5T na 70B zilitumika katika miradi gani? Zipo wapi? CAG Assada & Kichere

Hoja ni moja 1.5T na 70B zipo wapi?
Assad anaenda anaweweseka huko kila siku anamuota Magufuli. Waliomtuma hawakumwambia kuwa atakutana na maji marefu. Pole yenu.
 
Back
Top Bottom