Anguko la Ndugai: Somo la Katiba, viongozi na nchi

Nguruvi3

Platinum Member
Jun 21, 2010
15,389
31,337
Hatimaye Spika aliyeongoza kwa 'mkono wa chuma'' anguko lake limetimia. Mh. anaondoka akiacha historia ya Spika wa kwanza kujiuzulu tangu uhai wa Taifa hili

Spika asingeweza kutekeleza majukumu yake kwa fyongo yake na dhalili aliyopata Fyongo si alichosema ni kile alichofanya baada ya kusema. Hakusimama na kauli yake

Shinikizo la kuondoka lilitoka makundi ya jamii yakiona amepoteza imani au kudhalilika, Wapo wanaolaumu Mhimili wa serikali umeshinikiza Spika aondolewe

Inaweza kuwa ''kweli '' lakini kuna ubaya gani ikiwa mhimili hauwezi kufanya kazi na Spika? Ni Ndugai huyo huyo aliyewahi kusema ' ni lazima mihimili ifanye kazi pamoja''

Hoja si nani kashinikiza Spika ajiuzulu, hoja ni utaratibu uliotumika kumshinikiza aondoke

CCM ingeweza kumwita na kumlazimisha aondoke na angekataa ingechukua kadi. Spika anapigiwa kura na Wabunge ndivyo katiba inavyosema, wengi ni CCM

Ndugai aliamini kuishi kwa 'kupendelewa, mapenzi ya chama, kupendwa n.k.' na si katiba

Laiti katiba ingesema Spika haondolewi na chama baada ya kuchaguliwa Ndugai asingekuwa alivyo. Ndugai alitetea katiba mbovu iliyokuwa nzuri kwake leo Jan 06 ni shubiri

Mh Ndugai aliongoza harakati za ''kumdhalilisha'' CAG, kikatiba ana ulinzi wa kuondolewa. Ndugai hakuruhusu kuhoji utataribu kwasababu alikuwa 'darling' wa CCM na serikali.

Mh alijisahau na kudhani ni mteule wa Mungu na si Mtanzania au mwanaCCM

Hili la Spika si kwamba linaonyesha matundu ya mihimili bali ubovu wa Katiba. Viongozi hujisahau wanapokuwa madarakani, wengi wamkuwa wahanga wa katiba hii

Wabunge na viongozi wa serikali ni watetezi wa katiba hii wakidhani itawalinda milele. Wasichojua ubovu wa katiba unawaathiri vizazi vyao vya leo kesho na keshokutwa

Anguko la 'mbabe' ni fundisho la kujenga misingi ya nchi inayolindwa kisheria na si fadhila. Watu wasilalamike mhimili mmoja kuwa na nguvu, waangalie namna ya kurekebisha nguvu hizo ki uwiano. Alipoondolewa CAG kibabe hakuna aliyejali.

Leo kaondoka Spika huku mhimili ''mwingine'' ukitiliwa shaka sana kama unatumika. Ni wajibu wa mihimili mingine kujijengea ulinzi wa kisheria kupitia Katiba yasijitokeze tena.

Malumbano hayana majibu isipokuwa jambo moja, mifumo yetu inahitaji marekebisho. Tume huru ya uchaguzi haitatupa majibu ya mifumo mibovu, leo kuna mtu ana majibu tofauti na jana ! Tume huru ya uchaguzi haitaweka uwiano sawa wa mihimili

Leo tofauti na jana Mh Ndugai anaifikiria katiba zaidi kuliko tume huru ya uchaguzi

Tupitie maoni ya wananchi ya Rasimu ya Warioba tutengeneza utaratibu mpya-KATIBA. KATIBA ni msumeno unaokata mbele na nyuma, hauchagui siku wala tarehe

KATIBA ni nyaraka yetu, vyama ni mapito tu! tutengeneze katiba inayojenga mifumo imara

Turudi kwa Mzee Warioba tudurusu nyaraka yake, maana kama ninyi viongozi msiojifunza fanyeni ziara Kongwa mtaelewa tunachosema

Tusemezane
 
HATUJIFUNZI KUTOKANA NA MAKOSA

Watanzania hawajifunza kutokana na makosa

Mchakato wa Katiba iliyozaa rasimu ya Warioba ulianzishwa na Rais JK na si Wabunge, Taasisi au NGO, baada ya shinikizo la Wapinzani.

Kuanzisha mchakato kulipaswa kuanze na mjadala , tunataka nini kwa namna gani na kwanini
Matokeo ya kufanya mambo bila utaratibu yalitufikisha tulipokwama. Wahuni wakaua mchakato

Makosa hayo yanajurudia kwa kile kinachooitwa 'task force' ya kuunda tume huru ya uchaguzi

Wazo hilo limesukumizwa tu na ni mpango wa maalum wenye lengo maalum kwa ajili ya kikundi tu
Viongozi wanaofanya haya ni Wasomi wakubwa wasiotarajiwa hata kwa bahati mbaya

Kwa bahati mbaya sana wasomi wa nchi yetu wanaishi kwa kujipendekeza na si taaluma zao
Kujipendekeza kunaletea Taifa matatizo. Leo Spika Ndugai kaachia ngazi baada ya kuvunja sheria nyingi sana zikiwemo za kuruhusu Wabunge wasio na vyama mmoja mmoja na kwa makundi

Kinachoonekana ni kwamba hata taratibu nyingine hakuzijua. Barua ya Spika isiyoeleza lini anaachia Uspika ni kielelezo kimoja cha taasisi zinavyoendeshwa kwa matakwa na si miongozo.

Spika ameadhibiwa kwa 'kutoa maoni ', hilo aliwezi kuwa kosa kwani kama Mbunge na Raia ana haki na uhuru huo. Kilichomponza ni kukengeuka kusingizia media na kuomba msahama.
Lakini pia haki ya maoni ni zao la mbegu aliyopanda yeye mwenyewe

Kumwita CAG Assad kwa kutoa maoni ni moja ya mbegu hizo.

Ni mbegu hizo hizo alizokuwa nazo Waziri Nape za kudumaza uhuru wa habari kabla ya dhambi hiyo kumrudi mbele ya mtutu

Ni ni mbegu hiyo ya kuminya uhuru wa maoni aliyokuwa nayo Mwenezi wa wakati huo Polepole
Alizuia watu kukusanyika akisema ni utamaduni wa nchi kana kwamba nchi inaongozwa na mila na desturi na si sheria

Dhambi hiyo imemrudi, amefungiwa kutoa maoni kupitia kipindi chake kwa tuhuma kutoka kusikojulikana na kuhukumiwa na chombo kile kile alichokitumia yeye na wenzake kuminya uhuru wa maoni.

Mifano hiyo inatosha kueleza kuwa mifumo yetu ni mibovu na inahitaji kurekebishwa

Viongozi wasichukue dhamana za wananchi kwa matakwa yao kama hili la kuunda kikosi kazi cha tume huru ya uchaguzi. Tatizo letu si tume huru ni katiba mpya

Tunahitaji kuweka mihimili huru na kuweka uzio kwa wanaotoa huduma za mihimili.

Mfano, Spika aondolewe na Bunge na asiwe na wadhifa wa kichama kama mjumbe wa CC
Spika asiweze kugombea nafasi nyingine kama Urais au umakamu baada ya kipindi chake

Jaji mkuu na Majaji wasiruhusiwe kugombea nafasi za kisiasa baada ya utumishi wao

Taasisi nyeti za nchi ziwe huru na kuwajibika maeneo zaidi ya maoja ikiwa ni pamoja na kuwathibitisha watendaji na kutangaza nafasi kwa kuomba na sifa ili kuondoa fadhila

Kwa uchache, tunahitaji kudurusu katiba kupitia rasimu ya Warioba ambayo msingi wake ni maoni ya Wananchi. Hizi habari za kikosi kazi hazitasaidia kuondoa mapungufu zitaahirisha matatizo

Tuna matatizo makubwa sana ya kimfumo.

Hivi kikosi kazi cha tume huru kitakuja na suluhu ya matatizo ya muungano?
Hivi kikosi kazi kitatuhakikishia uhuru wa maoni bila kuadhibiwa au kudhulimiwa?

Tusemezane
 
KWANINI KUJIUZULU KWA NDUGAI KUWE HABARI KUBWA

Habari za Spika Ndugai zimekuwa kubwa katika vyombo vya habari na mitandaoni.
Spika ni kiongozi wa Mhimili na 'watatu' nafasi ya Urais ikiwa itatokea isivyotarajiwa.

Kujiuzulu Ndugai kunatukumbusha PM Lowassa alipojiuzulu, hivyo Rais kulihutubia Taifa!!
Rais alisema ''Nchi imetetemeka''

Nchi ya Japan imebadili PM Watatu katika miaka 2 tu na zaidi ya 5 katika miaka 10.

Miezi michache iliyopita Israel haikuwa na PM kutokana na ugumu wa majority ktk Knesset

India ilikaa miezi 3 bila PM baada ya uchaguzi kama ilivyowahi kuwa UK kwa wiki 3.

Katika muda wote serikali za nchi hizo ziliendelea na hakukuwa na tatizo lolote

Siri kubwa ni mifumo imara ya nchi , viongozi wakihudumu kwa kuingia na kutoka.

Kwa Tanzania hamaki inatokana na kutokuwa na mifumo , hata iliyopo hatuitumii vema

Kiongozi wa NCCR Mh. Mbati ameonyesha matundu ya kujiuzulu kwa Spika akisema kwa mujibu wa Katiba ya Spika anajiuzulu Bungeni, amechaguliwa na Wabunge si CCM

Mbatia anasema, barua ya Ndugai kwa Katibu mkuu wa CCM ina uchechefu.

Kwa mshangao Mbatia anahoji Katibu Mkuu wa CCM naye kamwandikia Katibu wa Bunge.
Mbatia ameeleza ukiukwaji wa Katiba akionyesha vifungu husika na wapi vimekiukwa

Kwa fikra za kawaida haifikiriki Spika anawajibika kwa chama chake na si Taasisi ya Bunge

Kiapo cha Spika na Wabunge ni kwa utii wa nchi na si chama.

Utaratibu alioutumia Spika Ndugai na Katibu wa Bunge unaeleza tatizo la mfumo

Spika ni mkuu wa Mhimili wa kutunga sheria.
Ikiwa Mh Mbatia atakuwa sahihi ni aibu kwa Ndugai. Ni aibu kwa katibu wa Bunge na Katibu mkuu wa CCM. Kwamba, inakuwaje hawaelewi taratibu!!

Kama Mbatia yu sahihi haitakuwa mara ya kwanza kwa Ndugai kukiuka taratibu.
Bunge limeendeshwa kwa Ubabe badala ya Sheria , kanuni hekma na Busara.

Muda wote Ndugai akiharibu taratibu hakukuwepo njia 'mechanism' ya kumwajibisha

Ndugai alieleza Chadema hawajui taratibu wakati anawapokea ''Wabunge uchochoroni''.

Ndugai akaandika sheria zinazotumika kwa tukio la kabla ya sheria kutungwa.
Kwamba vyama viambatanishe nakala za vikao na uzuzu wa aibu usioelezeka

Hoja ya Mh Mbati haina tofauti na ya wakili aliyeeleza kukiukwa Katiba baada ya Rais kuapishwa kufuatia kifo cha Rais JPM , kwamba Rais alipaswa kuvunja Baraza

Hoja zinazogusa katiba ya sasa ni nyingi sana

Wapo wanaohoji Mhimili wa Mahakama na Bunge kutokuwa na Bajeti zinazojitegemea

Wapo wanaouliza Takukuru chini ya Ofisi ya Rais ina uwezo gani wa kufanyia kazi 'grand corruption' tatizo kubwa kwa mataifa hasa nchi Masikini.

Wapo wanaohoji muungano na malalamiko ya pande zote

Wapo wanaohoji viongozi wa baadhi ya vyombo wana ulinzi upi dhidi ya mkono wa dola utakaowaweka huru kutimiza majukumu yao bila kuingiliwa na Mhimili uliojichimbia!
Jaji mkuu na Mahakama, Spika na Bunge, DPP na DC, Takukuru na NEC n.k.

Ikiwa hatutakaa chini na kutengeneza mifumo inayojiendesha na kuendesha nchi bila kutegemea 'personality' tutaendelea kuhamaki kila siku yakitokea ya Spika.

Hatuhitaji hamaki tunatarajia yatokee tusiyotegemea na wakati ukifika kama ilivyokuwa mwaka jana nchi ijiendeshe kwa mifumo. Ikitokea ya Ndugai nchi ijiendeshe bila Tatizo

Njia rahisi ni kuejea maoni ya Wananchi kupitia Rasimu ya Warioba! Tuwe na katika mpya

Wapo wanaohoji kwanini iliyopo tumeshindwa kuitetea, tutajadili
 
KWANINI KATIBA YA JMT (1977) HAIWEZI KUTETEWA AU KUJITETEA!

Wasomi na Wazee wenye heshima zao katika jamii wamehoji iwapo katiba mpya ni muhimu.
Hoja ni kwamba katiba iliyopo inakiukwa, mbona hakuna anayeitetea? Mpya itasaidia nini?

Hoja inatumika kuzima dai la katiba mpya.Ni hoja dhaifu sana na ya kupuuzwa , haina
Inatolewa kupotosha kwa makusudi, hawajui au ni kwa kukosa maono kwa uzuzu

Mhimili wa Serikali unatoa ukuu kutoka katiba inayompa Rais wa JMT madaraka ya teuzi hadi umiliki wa vyombo vya dola. Ni katika hali hiyo, katiba ya sasa haiwezi kujitetea inapokiukwa

Rais ni mteuzi wa RC , DC na Wakurgenzi wa miji na majiji. Serikali za mitaa ambazo kimsingi ni za wananchi zipo chini ya Ofisi ya Rais.

Taasisi kama Mahakama, DCI, DPP, Takukuru , Msajili wa vyama na NEC zina wateule wa Rais.

Rais ni mteuzi wa Wajumbe wa Tume ya uchaguzi (NEC) kikatiba.
Sheria inamruhusu kuteua na kutengua Wajumbe muda wowote bila kuulizwa.

Rasi JK alibadili wajumbe wiki mbili kabla ya uchaguzi yeye akiwa mshiriki wa Uchaguzi.
Kuna kosa lipi ikiwa alilotenda ikiwa katiba inamruhusu? Hakuwa na kosa, katiba haikujitetea!

Ilipobaini kimaadili na kiroho haikuwa sahihi, ni nani angepeleka suala hilo Mahakamani?
Katiba iliyompa uwezo haina uwezo wa kujitetea Mahakamani! Haina hoja dhidi ya Rais. Hana kosa

Sheria za Uchaguzi zinasema matokeo ya uchaguzi wa Rais hayawez kuhojiwa mahakamani.
Kunapokuwa na tatizo, katiba inawezaje kujitetea dhidi ya sheria zinazozuia katiba kujitetea?

Ilipohojiwa Wakurugenzi ambao ni Wateule wa Rais na Mwenyekiti wa CCM kusimamia chaguzi Mahakama kuu ilisema '' watu hao wanakula viapo hivyo ni sawa''

Kwamba Mhimili wa mahakama unaamini kiapo kinamfanya mhusika awe muadilifu bila mahakama kujiuuliza ni mara ngapi viapo vinakiukwa mahakamani, nyumba za dini n.k.
Ni moja ya hukumu zilizotilia shaka sana na kuondoa Imani ya Mhimili huo
Katika hukumu kama hiyo, katiba ya sasa inajitetea wapi tena inapokiukwa?

Uchaguzi wa 2020 hakuna kesi iliyokwenda Mahakamani watu has upinzani kupoteza imani na Mahakama kwa kujua katiba haiwezi kujitetea na hakuna anayeweza kuitetea .

Chombo kinachoweza kusimamia haki wakati 'katiba inajitetea'' kinatiliwa shaka
Katika mazingira hayo nani mwingine anaweza kuitetea katiba hii?

Miaka mitano kuelekea 2020 kulikuwa na marufuku ya ''mikutano'' . Katiba inatoa haki kwa vyama kufanya siasa chini ya sheria ya Msajili wa vyama. Msajili hakusimama kutetea sheria za ofisi yake. Ni vipi basi watu watarajie katiba inaweza kujitetea au kutetewa na mwananchi baki?

Kiongozi wa UVCCM alitoa maneno katika mkutano wa kisiasa akichagiza watu kuuwawa.

Kauli zake zilikiuka sheria za nchi zikiwa na uhalifu , na ingalikuwa tofauti, chama husika kingefutwa au kuitwa kujieleza kwa Msajili wa vyama.

Msajili wa vyama hakuzungumzia, Polisi hawakuzungumzia, DCI na DPP hawakuzungumzia!

Wote walikaa kimya kwasababu UVCCM ni tawi la CCM ambaye Mteuzi ni M/Kiti na Rais wa JMT

Viongozi walikaa kimya kwasababu kumgusa kiongozi wa UVCCM ni kumgusa liyewateua

Katika hali hiyo katiba inayoeleza uvunjwaji wa sheria inajisimamia au kujitetea au kutetewa na nani? Wenye dhamana hawathubutu ni 'mkulima au mvuvi au fundi cherehani' gani anayeweza?

Tunasema hivi Katiba ya sasa ni dhaifu sana kiasi kwamba haiwezi kujitetea au kutetewa.

Wenye hoja kwanini Wananchi hawawezi kuitetea, wajiulize tena wakifikiri sawa sawa!

Tusemezane
 
SOMO LA UONGOZI

Anguko la Ndugai limepotea haraka sana katika duru za habari likifunikwa na Nafasi ya Uspika

Shinikizo la Ndugai kujiuzulu kutoka kwa jamii linaeleza amii ilimuangalia kwa kauli na matendo

Imekuwa kana kwamba 'alikua anatafutiwa sababu''

Sehemu kubwa ya jamii ilifurahia anguko bila kujali ni sababu zipi hasa! bali ameondoka

Hii ni mara ya pili Mh Ndugai anakumbana na maswahibu yanayomhusu yeye binafsi na jamii .
Akiwa India anaugua sehemu ya jamii ilionyesha upendo na nyingine ikibaki bila huruma

Mh Ndugai ni kiongozi aliyejitengenezea mazingira anayokutana nayo.

Ukimlinganisha na Maspika kama Mh Sitta(RIP), Msekwa, Sapi(RIP), Mang'enya (RIP) na Makinda , Mh Ndugai alikosa unyenyekevu kwa jamii na mwenye majivuno na Ubabe

Ubabe na kukosa unyenyekevu si kwa makundi asiyokubaliana nayo, hata CCM walimuona hivyo.

Mh Alipenda kuona nafasi ya Uspika kama cheo kinachomruhusu kufanya lolote na chochote bila kuulizwa hata kama ni kinyume na sheria , kanuni au tamaduni.

Vyama vingi vipo kabla yake , maspika watatu wlaihudumu kwa nyakati tofauti. Maspika hao hawakuwa watimilifu kama tulivyo wanadamu wote lakini hawakuwa watu wa kutweza, kujikweza, jeuri

Mifano michache tu

Aliagizwa awatoe Wapinzani nje ya Bunge washughulikiwe, na alifanya hivyo
Askari wa Bunge walizoa Wabunge mzobemzobe kitendo cha nadra skwa maspika waliopita.

Ndugai aliruhusu Mbunge aliyejiuzulu Cecil Mwambe aendelee kukaa Bungeni si kwa mujibu wa sheria bali kwa takwa na jeuri yake tu kama Spika. Ujumbe wake ulikuwa rahisi, mtanifanya nini!

Ndugai aliruhusu Wabunge waliofukuzwa chama, Lijualikali na Silinde waendelee kukaa Bungeni si kwa mujibu wa sheria bali kwa jeuri yake tu. Mtanifanya nini! Hakuna anayeweza

Mh Ndugai akaruhusu Wabunge 19 nje ya utaratibu , akawapisha uani na kutamka bungeni wataendelea na Bunge. Ujumbe ukiwa ule ule, mtanifanya nini

Mh Ndugai katika kudharau wananchi na nchi akatunga sheria ya kufikisha katazo la Wabunge kutoka katika vyama liambatane na vikao vya chama.

Mh akajigeuza kuwa mshauri wa vyama, hakimu wa migogoro ya vyama na Spika.
Sheria ikatumika kurudi nyuma, kichekesho. Mh aliamini katika 'mtanifanya nini'

Katika hali ya unafiki, Mh aliyewatimua Wabunge wanawake wengine kwa nusu ya vipindi vya mwaka eti alisimama na kusema vyama vyao vinawanyanyasa.

Mh Ndugai akatuhumiwa kukataza malipo ya Mbunge TL, akasimama na kusema hajui alipo.

Ndugai akasiamama kutangaza nafasi ya jimbo akijua ni kufanya hivyo ni kukiuka utu wa mwanadamu. Ndugai hakumbuki alipokuwa India ndivyo TL alivyokuwa naye pia.
Kwasababu tu ya ubabe na jeuri '' mtanifanya nini akaamua ' atakavyo bila chembe ya utu

Mh Ndugai akageuza chombo cha umma kama eneo takatifuukisema lolote lisilompendeza utaitwa na kamati zake. Ndivyo alivyomdhalilisha CAG akimwita Bungeni na kuonyesha picha za kumdhalilisha akiingia getini na kupekuliwa kama mwizi

Kila aliyesema lolote kuhusu chombo cha wananchi(Bunge) Ndugai aligeuza kama mali yake na awaye aliitwa au kusemwa hadharani kama ilivyotokea karibu kwa Jenerali Ulimwengu.

Mh Ndugai bila kujali stara ya kiti chake akaingia mizozo na Waliokuwa wabunge na kutaja madeni mbele ya Bunge, hakujali heshima ya kiti, aliendekeza ubabe na jeuri 'mtanifanya nini''

Kutokana na hali aliyojijengea hata yalipomkuta madhila hakuna aliyesimama naye.
Marafiki walijitenga kunasibishwa naye kwa hulka yake na si kauli, wakamwacha mpweke.

Akiwa mkiwa na ametengwa, jamii ikapata fursa iliyoisubiri kwa muda, shinikizo aondoke

Hata waliomchagiza katika majivuno, jeuri na ubabe nao pia wamemtenga.

Mh ataendelea kuwa Mbunge na atapata masilahi yake kwa maisha yake yote.
Atakuwa na kila kitu ndani , nje na popote atakapokuwa.

Jambo moja tu hatakuwa nalo, ni 'amani ya roho' kwa jicho la jamii. Atakuwa mpweke sana

Funzo, unapokuwa kiongozi popote pale chukua fursa hiyo kwa mtazamo wa Utumishi
Uongozi usikutie kiburi, jeuri, majivuno na dharau.

Uongozi ni dhamana tu lakini kubwa katika uongozi ni unyenyekevu, upendo na heshima kwa wale unaowaongoza ili siku ukiondoka usemwe kwa mema na jamii ikutazame kwa jicho la kheri!

Tusemzane






 
SOMO LA UONGOZI

Anguko la Ndugai limepotea haraka sana katika duru za habari likifunikwa na Nafasi ya Uspika

Shinikizo la Ndugai kujiuzulu kutoka kwa jamii linaeleza amii ilimuangalia kwa kauli na matendo

Imekuwa kana kwamba 'alikua anatafutiwa sababu''

Sehemu kubwa ya jamii ilifurahia anguko bila kujali ni sababu zipi hasa! bali ameondoka

Hii ni mara ya pili Mh Ndugai anakumbana na maswahibu yanayomhusu yeye binafsi na jamii .
Akiwa India anaugua sehemu ya jamii ilionyesha upendo na nyingine ikibaki bila huruma

Mh Ndugai ni kiongozi aliyejitengenezea mazingira anayokutana nayo.

Ukimlinganisha na Maspika kama Mh Sitta(RIP), Msekwa, Sapi(RIP), Mang'enya (RIP) na Makinda , Mh Ndugai alikosa unyenyekevu kwa jamii na mwenye majivuno na Ubabe

Ubabe na kukosa unyenyekevu si kwa makundi asiyokubaliana nayo, hata CCM walimuona hivyo.

Mh Alipenda kuona nafasi ya Uspika kama cheo kinachomruhusu kufanya lolote na chochote bila kuulizwa hata kama ni kinyume na sheria , kanuni au tamaduni.

Vyama vingi vipo kabla yake , maspika watatu wlaihudumu kwa nyakati tofauti. Maspika hao hawakuwa watimilifu kama tulivyo wanadamu wote lakini hawakuwa watu wa kutweza, kujikweza, jeuri

Mifano michache tu

Aliagizwa awatoe Wapinzani nje ya Bunge washughulikiwe, na alifanya hivyo
Askari wa Bunge walizoa Wabunge mzobemzobe kitendo cha nadra skwa maspika waliopita.

Ndugai aliruhusu Mbunge aliyejiuzulu Cecil Mwambe aendelee kukaa Bungeni si kwa mujibu wa sheria bali kwa takwa na jeuri yake tu kama Spika. Ujumbe wake ulikuwa rahisi, mtanifanya nini!

Ndugai aliruhusu Wabunge waliofukuzwa chama, Lijualikali na Silinde waendelee kukaa Bungeni si kwa mujibu wa sheria bali kwa jeuri yake tu. Mtanifanya nini! Hakuna anayeweza

Mh Ndugai akaruhusu Wabunge 19 nje ya utaratibu , akawapisha uani na kutamka bungeni wataendelea na Bunge. Ujumbe ukiwa ule ule, mtanifanya nini

Mh Ndugai katika kudharau wananchi na nchi akatunga sheria ya kufikisha katazo la Wabunge kutoka katika vyama liambatane na vikao vya chama.

Mh akajigeuza kuwa mshauri wa vyama, hakimu wa migogoro ya vyama na Spika.
Sheria ikatumika kurudi nyuma, kichekesho. Mh aliamini katika 'mtanifanya nini'

Katika hali ya unafiki, Mh aliyewatimua Wabunge wanawake wengine kwa nusu ya vipindi vya mwaka eti alisimama na kusema vyama vyao vinawanyanyasa.

Mh Ndugai akatuhumiwa kukataza malipo ya Mbunge TL, akasimama na kusema hajui alipo.

Ndugai akasiamama kutangaza nafasi ya jimbo akijua ni kufanya hivyo ni kukiuka utu wa mwanadamu. Ndugai hakumbuki alipokuwa India ndivyo TL alivyokuwa naye pia.
Kwasababu tu ya ubabe na jeuri '' mtanifanya nini akaamua ' atakavyo bila chembe ya utu

Mh Ndugai akageuza chombo cha umma kama eneo takatifuukisema lolote lisilompendeza utaitwa na kamati zake. Ndivyo alivyomdhalilisha CAG akimwita Bungeni na kuonyesha picha za kumdhalilisha akiingia getini na kupekuliwa kama mwizi

Kila aliyesema lolote kuhusu chombo cha wananchi(Bunge) Ndugai aligeuza kama mali yake na awaye aliitwa au kusemwa hadharani kama ilivyotokea karibu kwa Jenerali Ulimwengu.

Mh Ndugai bila kujali stara ya kiti chake akaingia mizozo na Waliokuwa wabunge na kutaja madeni mbele ya Bunge, hakujali heshima ya kiti, aliendekeza ubabe na jeuri 'mtanifanya nini''

Kutokana na hali aliyojijengea hata yalipomkuta madhila hakuna aliyesimama naye.
Marafiki walijitenga kunasibishwa naye kwa hulka yake na si kauli, wakamwacha mpweke.

Akiwa mkiwa na ametengwa, jamii ikapata fursa iliyoisubiri kwa muda, shinikizo aondoke

Hata waliomchagiza katika majivuno, jeuri na ubabe nao pia wamemtenga.

Mh ataendelea kuwa Mbunge na atapata masilahi yake kwa maisha yake yote.
Atakuwa na kila kitu ndani , nje na popote atakapokuwa.

Jambo moja tu hatakuwa nalo, ni 'amani ya roho' kwa jicho la jamii. Atakuwa mpweke sana

Funzo, unapokuwa kiongozi popote pale chukua fursa hiyo kwa mtazamo wa Utumishi
Uongozi usikutie kiburi, jeuri, majivuno na dharau.

Uongozi ni dhamana tu lakini kubwa katika uongozi ni unyenyekevu, upendo na heshima kwa wale unaowaongoza ili siku ukiondoka usemwe kwa mema na jamii ikutazame kwa jicho la kheri!

Tusemzane
Nguruvi leo nimefurahi sana baada ya kuona andiko lako. Miaka michache iliyopita ulikuwa miongoni mwa watu walioleta uhai wa fikra kwa kujadili mambo muhimu ya taifa leo. Wakati wa JPM jukwaa hili ni kama lilikuwa kimya. Wengine walitishwa wakatishika, wengine walinunuliwa wakawa wapiga zumari wa JPM, wengine ..........
Yaliyopita si ndwele tugange yajayo.

1. Nikimuona Tulia naona kivuli cha matendo hasi ya JPM na matendo hasi ya Ndugai wewe unasemaje?

2. Ile kazi ya Ndugai ya kuhariri hotuba za wapinzani, kuwafukuza wapinzani bungeni kama vibaka, kuwadhalilisha, kuwaonea, kuwazushia, kuwachonganisha na wananchi, kuwanyima mafao yao nk, kwa fikra "watanifanya nini" unadhani itaisha?

3. Nimeona maamuzi mabaya yamepitishwa na Bunge la Ndugai na kisha Ndugai akalalamika nje ya bunge eg tozo, Kuna chochote chanya tutegemee

4. Vipi kuhusu wabunge covid 19?
 
kamili
Kabla sijapitia hoja zako naomba nikukumbushe siku za nyuma

Tulikuwa na Bunge la chama kimoja tangu 1965.CCM ikiundwa Bunge ni la chama kimoja.
Miaka ya 80 na 90, Wabunge walitishia kuzuia bajeti kwasababu bei ya mchele
Utakumbuka Bunge la akina Mlagala Njelu Kasaka na G55 na hoja ya Tanganyika

Vyama vingi vikaja hoja zikaibuliwa, Bunge la Hayati Samuel Sitta 'standard and speed''
Hoja alizotumia Rais JPM ni matokeo ya michango na hoja za Wapinzani Bungeni.
JPM alizifanyia kazi kwa manufaa mapana ya Taifa

Moja ya 'dhambi kubwa' alizofanya JPM ni kutoa amri ya kufuta upinzani 2020.
Kazi hiyo aliyomshirikisha Spika Ndugai ya kuwashughulikia Wapinzani.
Bila aibu Ndugai akalifanya Bunge Idara akiusakama upinzani

Bunge likatoka katika majukumu ya msingi na kuwa ''baraza la CCM'' na kituo cha kushughulikia Wapinzani. Mfano, Ndugai ku qualify kazi za Wabunge akisema '' Hai sasa ina Mbunge'' ! kichekesho Bunge likapoteza mvuto kabisa mbele ya umma

Ndugai hakutaka hotuba za Wapinzani eti yeye kama Spika anazifanyia editing.
Kwa kauli ni '' uhuni'' wa juu. Akimsaidi Ndugai ni Naibu wake Tulia Akson

Tulia alikuwa Naibu akiteuliwa na JPM na pengine kutayarishwa kuwa Spika.
JPM alishauriwa kuwa Spika kutoka Wateuliwa haileti picha nzuri! Tulia akawa Naibu

Tulia alifaya kazi chini ya Ndugai, msaidizi mzuri sana kwa maana ya kutekeleza ajenda za Ndugai, kufifisha mijadala asiyotaka , kukabiliana na Wapinzani na kila alilotaka Ndugai

Uteuzi wa Uspika umezingatia kuwa alikuwa Naibu mtu mwingine angekuwa na wakati mgumu kuwa na Naibu mzoefu.

Pili, ni mwanamke na karata inayochezwa sana siku hizi.
Na mwisho anajulikana atatimiza malengo kusudiwa kama atakavyoamrishwa

Ni kwa manti hiyo, hatukuona haja ya kumjadili Tulia. Hatutegemei
Kwa makusudi ya mjadala naomba nipitie hoja zako nzuri ulizoleta
1. Nikimuona Tulia naona kivuli cha matendo hasi ya JPM na matendo hasi ya Ndugai wewe unasemaje?
Nimeeleza alipotokea na alivyopanda na kuwa hapo alipo.
2. Ile kazi ya Ndugai ya kuhariri hotuba za wapinzani, kuwafukuza wapinzani bungeni kama vibaka, kuwadhalilisha, kuwaonea, kuwazushia, kuwachonganisha na wananchi, kuwanyima mafao yao nk, kwa fikra "watanifanya nini" unadhani itaisha?
Ni zao la Ndugai hakuna jipya.
3. Nimeona maamuzi mabaya yamepitishwa na Bunge la Ndugai na kisha Ndugai akalalamika nje ya bunge eg tozo, Kuna chochote chanya tutegemee
Ndugai alikuwa anatafuta umaarufu kwa njia za ajabu ajabu, ni aibu sana
4. Vipi kuhusu wabunge covid 19?
Wabunge COVID-19 watakuwepo, wanalipwa na serikali na imeridhika waendelee.

Tulia hatakuwa na Jipya, siku hizi ni '' uanamke' ni qualification kuhoji ni kuwanyanyasa.
Ndugai aliwalinda kinyume cha sheria. NEC wanaujua ataigusa serikali iliyowaajiri?

Tulidhani, Wabunge wanawake wangetetea pesa zinazowalipa COVID-19 ni nyingi katika Bilioni zitumike kununua vifaa vya uzazi '' delivery kit' kwa wanawake wa Tanzania vijijini ambako hata wembe wa kukatia kitovu cha mtoto ni mtihani

Pesa wanazolipwa COVID zingeweza kujenga shule za Bweni za wasichana kila Kanda.
Pesa zingeweza kujenga visima na kupunguza adha kwa wanawake na familia vijijini
Pesa zingeweza kutibu wanawake wenye matatizo ya ''njia ya mkojo'' VVF kutokana na sababu mbali mbali zikiwemo tatizo la uzazi. Wengi wapo na hawamudu gharama

Pesa za COVID zingeweza kununua ' sanitary pad'' taulo za kike kwa wanafunzi wa kike bure

Lakini kuna unafiki wa matumizi ya neno ''wanawake''
kwa Wabunge wanawake na Mh Tulia hawawezi kuwaondoa COVID, ni ''Wenzao''

Kuna unaifiki kwamba kumuendeleza mwanamke ni kumpa cheo.Ukweli ni kuwa kwa wanawake wanataka fursa kwa si vyeo .

Wanawake wanaohitaji fursa ni mamilioni ukilinganisha na wanaopata 'vyeo' kwa jina la ''Wanawake wanaweza''. Wanawake wenyewe wameachwa wakiteseka bila fursa, jina la wanawake linatumika kuneemesha wenye vyeo na wasiowasemea au kuwatetea wengi

Hii ni mada tutakaoijadili nilichotaka kukuambia hapa ni kuwa Tulia ni zao la JPM na Ndugai, hakuna jipya .
 
kamili
Kabla sijapitia hoja zako naomba nikukumbushe siku za nyuma

Tulikuwa na Bunge la chama kimoja tangu 1965.CCM ikiundwa Bunge ni la chama kimoja.

Miaka ya 80 na 90, Wabunge walitishia kuzuia bajeti kwasababu bei ya mchele
Utakumbuka Bunge la akina Mlagala Njelu Kasaka na G55 na hoja ya Tanganyika

Vyama vingi vikaja hoja zikaibuliwa, Bunge la Hayati Samuel Sitta 'standard and speed''
Hoja alizotumia Rais JPM ni matokeo ya michango na hoja za Wapinzani Bungeni.
JPM alizifanyia kazi kwa manufaa mapana ya Taifa

Moja ya 'dhambi kubwa' alizofanya JPM ni kutoa amri ya kufuta upinzani 2020.
Kazi hiyo aliyomshirikisha Spika Ndugai ya kuwashughulikia Wapinzani.
Bila aibu Ndugai akalifanya Bunge Idara akiusakama upinzani

Bunge likatoka katika majukumu ya msingi na kuwa ''baraza la CCM'' na kituo cha kushughulikia Wapinzani. Mfano, Ndugai ku qualify kazi za Wabunge akisema '' Hai sasa ina Mbunge'' ! kichekesho Bunge likapoteza mvuto kabisa mbele ya umma

Ndugai hakutaka hotuba za Wapinzani eti yeye kama Spika anazifanyia editing.
Kwa kauli ni '' uhuni'' wa juu. Akimsaidi Ndugai ni Naibu wake Tulia Akson

Tulia alikuwa Naibu akiteuliwa na JPM na pengine kutayarishwa kuwa Spika.
JPM alishauriwa kuwa Spika kutoka Wateuliwa haileti picha nzuri! Tulia akawa Naibu

Tulia alifaya kazi chini ya Ndugai, msaidizi mzuri sana kwa maana ya kutekeleza ajenda za Ndugai, kufifisha mijadala asiyotaka , kukabiliana na Wapinzani na kila alilotaka Ndugai

Uteuzi wa Uspika umezingatia kuwa alikuwa Naibu mtu mwingine angekuwa na wakati mgumu kuwa na Naibu mzoefu.

Pili, ni mwanamke na karata inayochezwa sana siku hizi.
Na mwisho anajulikana atatimiza malengo kusudiwa kama atakavyoamrishwa

Ni kwa manti hiyo, hatukuona haja ya kumjadili Tulia. Hatutegemei
Kwa makusudi ya mjadala naomba nipitie hoja zako nzuri ulizoleta

Nimeeleza alipotokea na alivyopanda na kuwa hapo alipo.

Ni zao la Ndugai hakuna jipya.

Ndugai alikuwa anatafuta umaarufu kwa njia za ajabu ajabu, ni aibu sana

Wabunge COVID-19 watakuwepo, wanalipwa na serikali na imeridhika waendelee.

Tulia hatakuwa na Jipya, siku hizi ni '' uanamke' ni qualification kuhoji ni kuwanyanyasa.
Ndugai aliwalinda kinyume cha sheria. NEC wanaujua ataigusa serikali iliyowaajiri?

Tulidhani, Wabunge wanawake wangetetea pesa zinazowalipa COVID-19 ni nyingi katika Bilioni zitumike kununua vifaa vya uzazi '' delivery kit' kwa wanawake wa Tanzania vijijini ambako hata wembe wa kukatia kitovu cha mtoto ni mtihani

Pesa wanazolipwa COVID zingeweza kujenga shule za Bweni za wasichana kila Kanda.
Pesa zingeweza kujenga visima na kupunguza adha kwa wanawake na familia vijijini
Pesa zingeweza kutibu wanawake wenye matatizo ya ''njia ya mkojo'' VVF kutokana na sababu mbali mbali zikiwemo tatizo la uzazi. Wengi wapo na hawamudu gharama

Pesa za COVID zingeweza kununua ' sanitary pad'' taulo za kike kwa wanafunzi wa kike bure

Lakini kuna unafiki wa matumizi ya neno ''wanawake''
kwa Wabunge wanawake na Mh Tulia hawawezi kuwaondoa COVID, ni ''Wenzao''

Kuna unaifiki kwamba kumuendeleza mwanamke ni kumpa cheo.Ukweli ni kuwa kwa wanawake wanataka fursa kwa si vyeo .

Wanawake wanaohitaji fursa ni mamilioni ukilinganisha na wanaopata 'vyeo' kwa jina la ''Wanawake wanaweza''. Wanawake wenyewe wameachwa wakiteseka bila fursa, jina la wanawake linatumika kuneemesha wenye vyeo na wasiowasemea au kuwatetea wengi

Hii ni mada tutakaoijadili nilichotaka kukuambia hapa ni kuwa Tulia ni zao la JPM na Ndugai, hakuna jipya .
Naaam nimeelewa, nakubali uchambuzi wako, asante sana.
Nina mengi ya kuuliza kuhusu siasa za utawala huu wa CCM (sina hakika kama ni uongozi) lakini nisikukatishe endelea kwanza na mada yako ya msingi " Anguko la Ndugai........
 
Nina mengi ya kuuliza kuhusu siasa za utawala huu wa CCM (sina hakika kama ni uongozi) lakini nisikukatishe endelea kwanza na mada yako ya msingi " Anguko la Ndugai........
Hakuna tatizo kama una hoja au swali tujadili bila shaka

Kuhusu Anguko la Ndugai, kuna mengi yanayomhusu
Kwanza, sidhani ni sahihi kumjadili Tulia Akson pekee bila kuliangalia Bunge

Katika taasisi dhaifu nchini Bunge ni mojawapo. Udhaifu wa Bunge ulitengenezwa na Mh Ndugai.

Kwamba, aligeuza Bunge kama Taasisi 'binafsi' na kwamba yeye ni mwamba.
Alitumia kamati za Bunge kudhalilisha watu kama alivyofanya kwa CAG Mh Musa Assad

Ndugai aliwashambulia Wabunge akiwatoa nje na kila aina ya vituko katika kulifanya Bunge dhaifu

Kutokana na udhaifu alioutengeneza, Bunge halikuwa na nguvu na hivyo pia kwa Wabunge

Kuna msemo unaosema '' ukipanda mahindi utavuna mahindi''. Kilichomtokea Mh Ndugai

Wakati anapata msuko suko uliopelekea kujiuzulu, hakuna Mbunge hata mmoja aliyesimama naye

Kwa maana kuwa kati ya Wabunge 320 aliyejitokeza kumtetea au basi kumuombea msamaha.

Wabunge katika Bunge dhaifu wakauonyesha udhaifu wao kwa Spika wa Bunge dhaifu na Ndugai akavuna kile alichopanda, yaani udhaifu alioujenga

Tusijisahau kuongelea Ndugai na Tulia, tujiulize udhaifu wa Bunge unatokana na nini?
Bunge lililopo ni la ''chama kimoja'' tunajua lilivyopatikana kwa ile dhambi ya uchaguzi wa 2020

Tunarudi kule kule 'ukipanda mahindi utavuna mahindi' . Uchaguzi wa 2020 ndio umezaa Bunge hili na Spika huyu na Naibu Spika aliyepo.

Turudi kwa rasimu ya Warioba!
 
Tumjadili Ndugai, ili tusije jikwaa tena, lakini tumjadili zaidi Tulia maana utendaji wake una athari kubwa kwa taifa. Japo sioni kama tunaweza ondoa kisiki kinachosababisha kujikwaa tena.

Sitaki kuwa mpiga ramli au msoma nyota, lakini naona bunge lililozingirwa na giza la kivuli cha maelekezo ya rais. Naona dhana ya bunge kuwatetea watu inapotea na badala yake bunge la kutetea serikali, lakini haswa CCM.

Maana kauli ya Tulia kuhusu ukuu wa rais jumlisha Tulia alivyojikuta bungeni jumlisha wabunge wa sasa walivyopatikana .............
 
Tumjadili Ndugai, ili tusije jikwaa tena, lakini tumjadili zaidi Tulia maana utendaji wake una athari kubwa kwa taifa. Japo sioni kama tunaweza ondoa kisiki kinachosababisha kujikwaa tena.
Sitaki kuwa mpiga ramli au msoma nyota, lakini naona bunge lililozingirwa na giza la kivuli cha maelekezo ya rais. Naona dhana ya bunge kuwatetea watu inapotea na badala yake bunge la kutetea serikali, lakini haswa CCM. maana kauli ya Tulia kuhusu ukuu wa rais jumlisha Tulia alivyojikuta bungeni jumlisha wabunge wa sasa walivyopatikana .............
Kamili, hakuna ''haramu'' inayozaa halali.

Uongozi wa nchi si kama 'money laundering' kwamba unakuwa na pesa chafu ukaisifisha, no way.

Bunge lililopo lilipatikana kwa njia za mbovu. Mwaka 2020 hatukuwa na uchaguzi! ulikuwa ubabe wa kufuta upinzani. Rais JPM aliwaambia Wabunge nani angeingia bungeni kama si yeye!
Aliwaambia wazi na wote walikaa kimya. Ulikuwa ni ukweli mchungu lakini ni ukweli

Kupatikana kwa Mh Ndugai na sasa Mh. Tulia Akson ni zao la bunge lililioletwa na JPM kwa kauli zake. Kwamba walifika pale kwasababu ya JPM.

Katika mazingira hayo unategemea Tulia atakuwa na ubora gani?
Unategemea Ndugai angekuwa na ubora gani?

Tatizo si Tulia au Ndugai, ni Bunge la CCM na madhara yake kwa Taifa ni makubwa sana.
Huwezi kumpata 'mtakatifu na Mwadilifu' aliyeingia mjengoni kwa njia zisizo za kiadilifu

Turudi kwenye rasimu ya Warioba, tufanyie kazi maoni ya Wananchi. Hapo ndipo jibu lilipo
 
Wapo wanaolaumu Mhimili wa serikali umeshinikiza Spika aondolewe
Inaweza kuwa ''kweli '' lakini kuna ubaya gani ikiwa mhimili hauwezi kufanya kazi na Spika?
Suala la CAG kutokukubalika na awamu fulani ya Awamu ya uongozi wa nchi hii kiasi cha kutafutwa CAG mwingine ilikuwa nongwa kweli.

Lakini kwa Spika na awamu fulani nyingine si nongwa!!! Ha ha ha haa Mna mambo Mengi sana nyie!
 
Suala la CAG kutokukubalika na awamu fulani ya Awamu ya uongozi wa nchi hii kiasi cha kutafutwa CAG mwingine ilikuwa nongwa kweli. Lakini kwa Spika na awamu fulani nyingine si nongwa!!! Ha ha ha haa Mna mambo Mengi sana nyie!
Hakukuwa na hoja hizi kwamba "Kuna ubaya gani ikiwa Mhimili hauwezi kufanya kazi na CAG?"

Na kiuhalisia huo ndio Ukomavu wa hoja na uhalisia wa serikali.
Ajabu ni unapokataa hilo kwa yule na kukubali hilohilo kwa huyu, na kutaka uungwe mkono.

Hawa ndugu zetu wanashangaza sana. Mimi kinachoniumiza zaidi ni kuona wanajivunia na kuonea Fahari Fikra zao potofu, na kujivisha Ukuu.
 
Hakukuwa na hoja hizi kwamba "Kuna ubaya gani ikiwa Mhimili hauwezi kufanya kazi na CAG?"

Na kiuhalisia huo ndio Ukomavu wa hoja na uhalisia wa serikali.
Ajabu ni unapokataa hilo kwa yule na kukubali hilohilo kwa huyu, na kutaka uungwe mkono.

Hawa ndugu zetu wanashangaza sana. Mimi kinachoniumiza zaidi ni kuona wanajivunia na kuonea Fahari Fikra zao potofu, na kujivisha Ukuu.
Kwanza, hoja inajengwa juu ya hoja au inabomolewa na hoja si vingnevyo

Maoni ya wengine hata kama hayapendezi hayawezi kuwa potofu, kuheshimu maoni ni uungwana

Kuhusu CAG hapa mjadala ni kitu gani, naona methali na mafumbo. Niweke rekodi vizuri kwanza

Ofisi ya CAG ni 'entity' siyo sehemu ya Mhimili wowote na hilo linathibitishwa na ukweli kuwa kuondolewa kwa CAG kunahitaji tume ya Kijaji kutoka common Wealth

Tangu tumepata Uhuru hataujawahi kuona CAG akiingiliwa kikazi kama ilivyotokea awamu ya 5

Rais JPM alimwita CAG Musa Assad Ikulu na kumshtukiza azungumzie Trilion 1.5 alizosema hazionekani katika mahesabu. CAG Assad hakusema zimeibwa, alisema hazikuonekana

Hii ina maana moja kwamba Serikali ya Magufuli ilikuwa na dhima ya kueleza zipo wapi!

Serikali haikufanya hivyo, badala yake Magufuli akamwita CAG na kumweka ''On the spot'

Rais Magufuli akaenda kumteua CAG Kichere kabla ya muda wa CAG Assad kwisha akisingizia Umri wa kustaafu! Ililikuw kosa la kukiuka taratibu za uteuzi wa CAG na kusema uongo

Siku CAG Kichere anaapishwa, Magufuli akamwambia ' na wewe usiende ukajifanya ni mhimili'' (rekodi zipo you tube) , akithibitisha chuki yake dhidi ya CAG Assad kwa vile tu alifanya kazi kwa mujibu wa taratibu kinyume na matakwa yake.

Zipo kumbu kumbu Rais Magufuli akisema '' Sasa tumepata CAG'' katika mwendelezo ule ule wa kuonyesha hasira zake dhidi ya CAG Assad kwasababu tu aliuliza ziko wapi 1.5 Trilioni.

Majuzi CAG Kichere katoa taarifa na hiyo ndiyo inajadiliwa.
CAG Kichere kama CAG Assad wanalindwa na sheria za kazi zao ni makosa kuwatuhumu kama wao

Kinachotakiwa na wale walioumizwa na taarifa ya CAG ni kuonyesha ubovu wake

Mfano, CAG kahoji katika utawala wa Rais JPM kuna Bilioni 70 zilizopelekwa Mwanza
Zitto wa ACT Wazalendo anauliza pesa hizo zilikwenda kufanya nini?

Kinachotakiwa si kuhoji taarifa ya CAG au hoja ya Zitto bali majibu ya Bilioni 70 zilikwendaje.

Ofisi ya CAG imeonyesha 'madudu' ni haki wananchi kuelewa madudu hayo yametokeaje.

Hivyo, sioni kuna biasness au controversy ya aina yoyote na kama ipo wekeni ijadiliwe
Wasomaji wanategemea kuona hoja zikijibiwa kwa hoja.
 
Kwanza, hoja inajengwa juu ya hoja au inabomolewa na hoja si vingnevyo

Maoni ya wengine hata kama hayapendezi hayawezi kuwa potofu, kuheshimu maoni ni uungwana

Kuhusu CAG hapa mjadala ni kitu gani, naona methali na mafumbo. Niweke rekodi vizuri kwanza

Ofisi ya CAG ni 'entity' siyo sehemu ya Mhimili wowote na hilo linathibitishwa na ukweli kuwa kuondolewa kwa CAG kunahitaji tume ya Kijaji kutoka common Wealth

Tangu tumepata Uhuru hataujawahi kuona CAG akiingiliwa kikazi kama ilivyotokea awamu ya 5

Rais JPM alimwita CAG Musa Assad Ikulu na kumshtukiza azungumzie Trilion 1.5 alizosema hazionekani katika mahesabu. CAG Assad hakusema zimeibwa, alisema hazikuonekana

Hii ina maana moja kwamba Serikali ya Magufuli ilikuwa na dhima ya kueleza zipo wapi!

Serikali haikufanya hivyo, badala yake Magufuli akamwita CAG na kumweka ''On the spot'

Rais Magufuli akaenda kumteua CAG Kichere kabla ya muda wa CAG Assad kwisha akisingizia Umri wa kustaafu! Ililikuw kosa la kukiuka taratibu za uteuzi wa CAG na kusema uongo

Siku CAG Kichere anaapishwa, Magufuli akamwambia ' na wewe usiende ukajifanya ni mhimili'' (rekodi zipo you tube) , akithibitisha chuki yake dhidi ya CAG Assad kwa vile tu alifanya kazi kwa mujibu wa taratibu kinyume na matakwa yake.

Zipo kumbu kumbu Rais Magufuli akisema '' Sasa tumepata CAG'' katika mwendelezo ule ule wa kuonyesha hasira zake dhidi ya CAG Assad kwasababu tu aliuliza ziko wapi 1.5 Trilioni.

Majuzi CAG Kichere katoa taarifa na hiyo ndiyo inajadiliwa.
CAG Kichere kama CAG Assad wanalindwa na sheria za kazi zao ni makosa kuwatuhumu kama wao

Kinachotakiwa na wale walioumizwa na taarifa ya CAG ni kuonyesha ubovu wake

Mfano, CAG kahoji katika utawala wa Rais JPM kuna Bilioni 70 zilizopelekwa Mwanza
Zitto wa ACT Wazalendo anauliza pesa hizo zilikwenda kufanya nini?

Kinachotakiwa si kuhoji taarifa ya CAG au hoja ya Zitto bali majibu ya Bilioni 70 zilikwendaje.

Ofisi ya CAG imeonyesha 'madudu' ni haki wananchi kuelewa madudu hayo yametokeaje.

Hivyo, sioni kuna biasness au controversy ya aina yoyote na kama ipo wekeni ijadiliwe
Wasomaji wanategemea kuona hoja zikijibiwa kwa hoja.
Nitangulize kuomba radhi labda kwa kutamka Mawazo Potofu. Hata kama itabaki kuwa hivyo kwangu lakini ninajua kuwa wapo wengi ambao wanaweza wasipendezwe na kauli hiyo hadharani. Mniwie Radhi.
 
Kuhusu CAG hapa mjadala ni kitu gani, naona methali na mafumbo. Niweke rekodi vizuri kwanza

Ofisi ya CAG ni 'entity' siyo sehemu ya Mhimili wowote na hilo linathibitishwa na ukweli kuwa kuondolewa kwa CAG kunahitaji tume ya Kijaji kutoka common Wealth

Tangu tumepata Uhuru hataujawahi kuona CAG akiingiliwa kikazi kama ilivyotokea awamu ya 5

Rais JPM alimwita CAG Musa Assad Ikulu na kumshtukiza azungumzie Trilion 1.5 alizosema hazionekani katika mahesabu. CAG Assad hakusema zimeibwa, alisema hazikuonekana

Hii ina maana moja kwamba Serikali ya Magufuli ilikuwa na dhima ya kueleza zipo wapi!

Serikali haikufanya hivyo, badala yake Magufuli akamwita CAG na kumweka ''On the spot'

Rais Magufuli akaenda kumteua CAG Kichere kabla ya muda wa CAG Assad kwisha akisingizia Umri wa kustaafu! Ililikuw kosa la kukiuka taratibu za uteuzi wa CAG na kusema uongo

Siku CAG Kichere anaapishwa, Magufuli akamwambia ' na wewe usiende ukajifanya ni mhimili'' (rekodi zipo you tube) , akithibitisha chuki yake dhidi ya CAG Assad kwa vile tu alifanya kazi kwa mujibu wa taratibu kinyume na matakwa yake.

Zipo kumbu kumbu Rais Magufuli akisema '' Sasa tumepata CAG'' katika mwendelezo ule ule wa kuonyesha hasira zake dhidi ya CAG Assad kwasababu tu aliuliza ziko wapi 1.5 Trilioni.

Majuzi CAG Kichere katoa taarifa na hiyo ndiyo inajadiliwa.
CAG Kichere kama CAG Assad wanalindwa na sheria za kazi zao ni makosa kuwatuhumu kama wao

Kinachotakiwa na wale walioumizwa na taarifa ya CAG ni kuonyesha ubovu wake

Mfano, CAG kahoji katika utawala wa Rais JPM kuna Bilioni 70 zilizopelekwa Mwanza
Zitto wa ACT Wazalendo anauliza pesa hizo zilikwenda kufanya nini?

Kinachotakiwa si kuhoji taarifa ya CAG au hoja ya Zitto bali majibu ya Bilioni 70 zilikwendaje.

Ofisi ya CAG imeonyesha 'madudu' ni haki wananchi kuelewa madudu hayo yametokeaje.

Hivyo, sioni kuna biasness au controversy ya aina yoyote na kama ipo wekeni ijadiliwe
Wasomaji wanategemea kuona hoja zikijibiwa kwa hoja.
Shida yako Mkuu uko westernized mno. Ni nani au ni nini unafikiri kinaweza kuwa juu ya Ustawi wa Taifa letu? Je, ni UN, Common Wealth, AU, CAG, Bunge, Rais, Katiba, au Mahakama?

Nilishawahi kukuuliza hapo nyuma, Kama wapo wanaokiuka Katiba ya Nchi ili kulinda matumbo yao, UPI ni Ubaya wa Kukiuka Katiba ya Nchi au taratibu zozote ili kulinda Ustawi wa Umma?

Halafu kama unasema ni "entity huru" na bado unadai imeingiliwa, kwanini haikutumia Uhuru wake kutoingiliwa? Tunawaeleza kila siku ila hamsiki, Dhana ya Uhuru ni "KIINI MACHO" na bado mtaendelea kuhubiri huo Uhuru hewa.

CAG akiwa na ripoti iliyokamilika, anaitwa kuitolea maelezo, wewe unadai Ameshtukizwa, HOW? Ilihitajika maandalizi gani kati huu ulimwengu wa kidigitali? Acha chuki Mkuu.

Nafasi yako ilikuwa kuhoji ukiwa katikati ya Assad na Magufuli, lakini unapompa Usahihi wore Assad na kudai ni Chuki za Magufuli, inakufanya tukushangae sana na ndio maana wakati mwingine tunatumia maneno Makali kwa mitazamo ya aina yako.

Kama Assad ailiweza kuingiliwa na Magufuli, Kichere pia, ni nini kinakufanya uone kuwa Kichere hawezi kuingiliwa na mhimili katika awamu hii? You keep no benefit of doubt, Je, wewe ndio Kichere mwenyewe au ndio Rais?

Kuna kundi linaonesha Chuki za wazi kwa Magufuli, na kila Siku linajaribu kumpaka matope (wewe ukiwemo). Ni kundi hilo hilo linalozunguka huku na huko kutoa Shutuma Hasi kwa Magufuli. SASA UTUSIDIE LABDA, TUNAWEZAJE KUTOFAUTISHA SHUTUMA ZA CHUKI NA ZILE HALISI KUTOKA KWENU? Chuki zenu zinawaondolea integrity ya kumsema Magufuli kwa warevu.

Kabla ya kusema madudu hayo, Sisi tunahoji Uhalali wa hao watamkaji kwanza. Zitto, CAG, Wasomi, Wapinzani, Wastaafu, CCM, na wewe.

Wakati mwingine tutakuwa wakali kidogo, maana mnachosha.
 
Nilishawahi kukuuliza hapo nyuma, Kama wapo wanaokiuka Katiba ya Nchi ili kulinda matumbo yao, UPI ni Ubaya wa Kukiuka Katiba ya Nchi au taratibu zozote ili kulinda Ustawi wa Umma?
Kosa moja haliwezi kusahihisha kosa jingine. Tutengeneza mifumo isiyohitaji kurekebishwa kwa makosa. Tuangalie KATIBA kupitia maoni ya Tume ya Mzee Warioba.

Ukuu wetu katika kujitawala ni kuwasikiliza Wananchi wanasema nini, walishasema katika Tume ya Warioba. Tuepuka kutawaliwa na mtu au watu , somo la miaka 6 ni zuri na la wazi
Halafu kama unasema ni "entity huru" na bado unadai imeingiliwa, kwanini haikutumia Uhuru wake kutoingiliwa? Tunawaeleza kila siku ila hamsiki, Dhana ya Uhuru ni "KIINI MACHO" na bado mtaendelea kuhubiri huo Uhuru hewa.
Labda nisema haikuingiliwa iliporwa .
Kwamba, JPM alitaka kusikia alichokitaka si uhalisia wa kazi ya CAG
CAG akiwa na ripoti iliyokamilika, anaitwa kuitolea maelezo, wewe unadai Ameshtukizwa, HOW? Ilihitajika maandalizi gani kati huu ulimwengu wa kidigitali? Acha chuki Mkuu.
Kuna habari ima huzielewi au huna ufahamu nazo au hukuzifuatilia.

Tukio la Magufuli kumwita CAG Ikulu halikuhusu taarifa ya CAG.

Ilikuwa kuapisha viongozi . Katika hotuba Magufuli kwa makusudi akasema
'' ...Kuna wanaosema pesa 1.5T zimeibiwa, CAG yupo hapa tumuulize kama ni kweli ''.

Yaani Magufuli anatengeneza swali lenye jibu, anataka CAG amwambie kile anachotaka.

Ilikuwa ni ngumu kwa CAG kupingana na Rais hadharani, CAG akatumia busara ya hali ya juu sana kueleza ''... ripoti haisemi pesa zimeibiwa, inasema hazijulikani zilipo''

Magufuli alitaka kusikia neno ''hazikuibiwa'' ndipo alipokazia baada ya CAG kumaliza kujibu swali la kushtukizwa katika mkutano usiohusu ripoti ya CAG tena 'Live '

Katika mazingira ya kawaida kiongozi hawezi kumwita kiongozi mwingine na kumhoji hadharani kwa njia za malumbano! Magufuli alikuwa na nafasi ya kumwita CAG Ofisini

Tofauti na hilo Magufuli hakujibu Trilioni 1.5 zimekwenda wapi.
Hakutakiwa kupata kauli ya CAG, alitakiwa kujibu hoja ya upotevu wa 1.5T. Hakujibu
Bado ukweli unabali pale pale hatujui 1.5T alizosema CAG zimepotea zipo wapi!
Nafasi yako ilikuwa kuhoji ukiwa katikati ya Assad na Magufuli, lakini unapompa Usahihi wore Assad na kudai ni Chuki za Magufuli, inakufanya tukushangae sana na ndio maana wakati mwingine tunatumia maneno Makali kwa mitazamo ya aina yako.
Ninampa usahihi CAG Assad kwasababu ya taarifa yake kuna pesa 1.5T hazijulikani zilipo

Kuanzia wakati huo hadi leo hii hakuna! hakuna! yoyote aliyeahi kueleza zilipo 1.5T na imebaki siri kati ya Magufuli na Wasaidizi wake wa karibu. Kulikoni? hizi ni pesa za Umma
Kama Assad ailiweza kuingiliwa na Magufuli, Kichere pia, ni nini kinakufanya uone kuwa Kichere hawezi kuingiliwa na mhimili katika awamu hii? You keep no benefit of doubt, Je, wewe ndio Kichere mwenyewe au ndio Rais?
Hoja nzuri sana, ili tuwe na uhakika lazima tuangalie mifumo yetu- KATIBA Mpya
Kuna kundi linaonesha Chuki za wazi kwa Magufuli, na kila Siku linajaribu kumpaka matope (wewe ukiwemo).
Sijui kwanini mitazamo tofauti na wewe unaita chuki, hata hivyo hilo halijibu hoja

Nimekueleza mara nyingi onyesha chuki dhidi yaJPM , watuhumiwa watajibu, hujaweza!

Siku zote nimeeleza Magufuli atendewe haki, na kutendewa haki si kutaja SGR na JNHP tu, watu waangalie rekodi yake kwa ujumla. JPM akiwa kiongozi miaka 6 amefanya mengi mazuri na mabaya na hapo ndipo reko inahitaji. Kwa mema ashukuriwe na tuyaendeleze.
Kwa mabaya tujifunze yasijerudi au kujirudia tena kwenye Taifa hili Tukufu

Nipo katika rekodi nikisema katika mambo mazuri ni pamoja na kusimamia 'thamani ya pesa'' kwamba pesa ilikuwa na thamani hata kwa kazi ndogo. Jambo hilo lilisaidia sana kuzuia mfumuko wa bei (Inflation) na kumsaidia kila mtu

Hatuwezi kuchukua jambo moja tuka m-define Magufuli , si kumtendea haki lazima tuangalie rekodi ya Magufuli katika haya ;

Uchumi
Kuheshimu utu na ubinadamu
Demokrasia na haki za binadamu
Kukabiliana na majanga ya kitaifa na kimataifa
Mahusiano ya serikali na Wananchi aliyewaongoza
Uhusiano wa nchi na jirani na Mataifa
Ujenzi wa mshikamano na umoja wa Kitaifa bila kujali itikadi, dini au kabila


Ni kundi hilo hilo linalozunguka huku na huko kutoa Shutuma Hasi kwa Magufuli. SASA UTUSIDIE LABDA, TUNAWEZAJE KUTOFAUTISHA SHUTUMA ZA CHUKI NA ZILE HALISI KUTOKA KWENU? Chuki zenu zinawaondolea integrity ya kumsema Magufuli kwa warevu.
Maoni ya watu unayoyaita chuki hayajibiwi na chuki ambayo ni maoni yako.

Nimekuwekea mambo tunayotakiwa kuyajadili ili tutofautishe chuki, uhalisia na ukweli

Hatuwezi kuzungumzia chuki kama hatuna cha kujadili.

Chuki ni neno tu halisimami lenyewe bali husimamishwa na tukio au matukio.

Nimekuorodheshea mambo ya kujadili hapo juu
Kabla ya kusema madudu hayo, Sisi tunahoji Uhalali wa hao watamkaji kwanza. Zitto, CAG, Wasomi, Wapinzani, Wastaafu, CCM, na wewe.
Uhalali wa hao tu unapatikana katika ukweli mmoja tu, ni RAIA halali wa nchi hii na katiba ya 1977 pamoja na ubovu na uozo wake imewapa haki ya kushiriki shughuli za kijamii ikiwemo kutoa mawazo.

Uhalali wao ni sawa na ule walio nao watetezi wa Magufuli UKIWEMO wewe ambao wanataka azungumziwe wanavyotaka wao.

Kila mmoja ana haki katika nchi hii , hii si nchi ya mtu ni nchi ya Wananchi.

Tulipumbuzwa kwamba nchi hii ni ya mtu mmoja na kwa upumbavu huo wapo waliokumbatia na wanaokuumbatia hadi dakika hii, tuwasaidie hawa ni wenzetu !
Wakati mwingine tutakuwa wakali kidogo, maana mnachosha.
Kuwa mkali ni haki yako lakini ukali uambatane na facts.

Tujadili rekodi ya Magufuli A-Z

Hata wale wanaosema marehemu hasemwi ni wakali pia bila hoja, ingawa tunajua hawataki kujadili rekodi ya Magufuli kama tunavyojadili ya Nyerere na Mkapa ambao ni marehemu.

Nani kasema Magufuli ni marehemu tofauti na Nyerere au Mkapa?
 
Kosa moja haliwezi kusahihisha kosa jingine. Tunayo nafasi ya kutengeneza mifumo isiyohitaji kurekebishwa kwa makosa. Tuangalie utaratibu wetu wa KATIBA kupitia maoni ya Tume ya Mzee Warioba. Ukuu wetu katika kujitawala ni kuwasikiliza Wananchi wanasema nini, walishasema katika Tume ya Warioba. Tuepuka kutawaliwa na mtu au watu , somo la miaka 6 ni nzuri na la wazi

Labda nisema haikuingiliwa iliporwa na utawala wa JPM . Kwamba, JPM alitaka kusikia alichokitaka kutoka kwa CAG na si uhalisia wa matokeo ya kazi ya CAG

Kuna habari ima huzielewi au huna ufahamu nazo au hukuzifuatilia.
Tukio la Magufuli kumwita CAG Ikulu halikuhusu taarifa ya CAG, ilikuwa kuapisha viongozi
Katika hotuba yake Magufuli kwa makusudi akasema '' ...Kuna wanaosema pesa 1.5T zimeibiwa, CAG yupo hapa tumuulize kama ni kweli zimibwa''.

Yaani Magufuli anatengeneza swali lenye jibu halafu anataka CAG amwambie kile anachotaka.
Ilikuwa ni ngumu sana kwa CAG kupingana na Rais hadharani, CAG Assad akatumia busara ya hali ya juu sana kueleza kilichopo ndani ya taarifa ''... ripoti haisemi pesa zimeibiwa, inasema hazijulikani zilipo''

Magufuli alitaka kusikia neno ''hazikuibiwa'' na hapo ndipo alipokazia baada ya CAG Assad kumaliza shtukkizo la Ikulu.

Katika mazingira ya kawaida kiongozi hawezi kumwita kiongozi mwingine na kumhoji hadharani
Magufuli alikuwa na nafasi ya kumwita CAG kama alikuwa hajui nini kimetokea Ofisini kwake

Tofauti na hilo Magufuli hakujibu Trilioni 1.5 zimekwenda wapi. Hakutakiwa kupata kauli ya CAG, alitakiwa kujibu hoja na kama CAG alisema uongo angeweka wazi.
Magufuli alichofanya ni ''kuvizia'' CAG Assad kwa mshtukizo halafu amweke 'on the spot'

Bado ukweli unabali pale pale hatujui 1.5T alizosema CAG zimepotea zipo wapi!

Ninampa usahihi CAG Assad kwasababu ya taarifa yake kwamba kuna pesa 1.5T hazijulikani zilipo
Kuanzia wakati huo hadi leo hii hakuna! hakuna! yoyote aliwyeahi kueleza zilipo 1.5T na imebaki siri kati ya Magufuli na Wasaidizi wake wa karibu

Hoja nzuri sana, ili tuwe na uhakika lazima tuangalie mifumo yetu- Tutengeneze katiba Mpya

Sijui kwanini mitazamo tofauti na wewe unaita chuki, hata hivyo hilo halijibu hoja
Nimekueleza mara nyingi sana onyesha chuki dhidi ya Magufuli na watuhumiwa watajibu, hujaweza!

Siku zote nimeeleza kuwa Magufuli atendewe haki, na kutendewa haki si kutaja SGR na JNHP tu, lazima watu waangalie rekodi yake kwa ujumla kuhusu mambo mengi.
JPM akiwa kiongozi miaka 6 amefanya mengi mazuri na mabaya na hapo ndipo reko inahitaji

Kwa yale mema aliyofanya ashukuriwe na tuyaendeleze. Nipo katika rekodi nikisema katika mambo mazuri ni pamoja na kusimamia 'thamani ya pesa'' kwamba pesa ilikuwa na thamani hata kwa kazi ndogo. Jambo hilo lilisaidia sana kuzuia mfumuko wa bei (Inflation) na kumsaidia kila mtu

Hatuwezi kuchukua jambo moja tuka m-define Magufuli , si kumtendea haki lazima tuangalie rekodi ya Magufuli katika haya ;
Uchumi
Kuheshimu utu na ubinadamu
Demokrasia na haki za binadamu
Kukabiliana na majanga ya kitaifa na kimataifa
Mahusiano ya serikali na Wananchi aliyewaongoza
Uhusiano wa nchi na jirani na Mataifa
Ujenzi wa mshikamano na umoja wa Kitaifa bila kujali itikadi, dini au kabila



Maoni ya watu unayoyaita chuki hayajibiwi na chuki ambayo ni maoni yako.
Nimekuwekea mambo tunayotakiwa kuyajadili hapo juu ili tutofautishe chuki, uhalisia na ukweli
Hatuwezi kuzungumzia chuki kama hatuna cha kujadili. Chuki ni neno tu halisimami lenyewe bali husimamishwa na tukio au matukio. Nimekuorodheshea mambo ya kujadili hapo juu

Uhalali wa hao tu unapatikana katika ukweli mmoja tu, ni RAI halali wa nchi hii na katiba ya 1977 pamoja na ubovu na uozo wake imewapa haki ya kushiriki shughuli za kijamii ikiwemo kutoa mawazo. Uhalali wao ni sawa na ule walio nao watetezi wa Magufuli UKIWEMO wewe ambao wanataka azungumziwe wanavyotaka wao. Kila mmoja ana haki katika nchi hii , hii si nchi ya mtu ni nchi ya Wananchi. Tulipumbuzwa kwamba nchi hii ni ya mtu mmoja na kwa upumbavu huo wapo waliokumbatia na wanaokuumbatia hadi dakika hii, tuwasaidie hawa ni wenzetu !

Kuwa mkali ni haki yako lakini ukali uambatane na facts. Tujadili rekodi ya Magufuli A-Z
Hata wale wanaosema marehemu hasemwi ni wakali pia bila hoja, ingawa tunajua hawataki kujadili rekodi ya Magufuli kama tunavyojadili ya Mwalimu Nyerere na Mkapa ambao pia ni marehemu. Nani kasema Magufuli ni marehemu tofauti na Nayerere au Mkapa?
1. Kukiuka Katiba ili Kulinda Masilahi ya Umma SIO KOSA. Ustawi wa Umma upo juu ya Katiba au taratibu zozote ziwekwazo na binadamu. Hivyo Ukiukwaji huo si wa kuhalalisha kosa kwa kosa. Tunaposema Tutafakari zaidi, huwa ni hivyo. Yaani, kutoruhusu Fikra zako kutofungwa na chochote ila tu Ustawi wa Umma. Sio dini, Katiba, sheria, mazoea, usomi, chama, MTU, mlengo, nk....

2. Baada ya kuporwa hiyo ofisi ilichukuwa hatua gani kutetea Uhuru wake? Huoni dhana ya Uhuru wa CAG office unaodai ni wa makaratasi tu na haupo? Mfano hiyo tume ya Kijaji-Common Wealth, ilichukua hatua gani kumtetea mtanzania mnyonge aliyenyimwa haki ya kusemewa na CAG?
UHURU ni Kiini Macho, haujawahi kuwepo Kokote. Ni sisi tu tumepewa lidubwana la kupoteza muda kulijadili bila manufaa yoyote. Kimsingi kwangu Dhana ya Uhuru na Haki ni Upuuzi mkubwa kuwahi kutokea kwa wanyonge.

3. Unampa usahihi Assad kwa kuwa hakuna aliyesema 1.5T ziko wapi, JE, ULISHAWAHI KUJIULIZA USAHIHI WA UWEPO WA HIYO PESA? Aje kama ni Tuhuma Hewa na Mhimili ukaona ukengemfu wake, na kwa busara ukaamua kumstaafisha kwa lazima?

Je, umeshawahi kujiridhisha uwepo wake? Tuambie ni kwa namna gani!

4. Kama tunahitaji Katiba mpya ili kuwa na uhakika na usahihi wa CAG, Wewe usahihi unaodai kuwa nao juu ya ripoti ya Kichere umeutoa wapi halikuwa Katiba Yetu ni 77 bado? Huoni kuwa unatulisha mihemko has I tu pasipo facts unazodai?

5. Chuki zako ziko wazi unapotaka tuunge mkono Shutuma zusizo na Ushahidi juu ya Magufuli. Lakini hauko pekee yako, wenzako pia wameshaanza kujitaja hovyo, wanataka tukazikwe nae, wanaodai haikuwa rahisi kuishi nae, wanaotema nyongo, wenye nyuso za FURAHA, na wapigaji wengi tu. Huwezi kuturubuni, maandishi yako yanakuweka wazi, kama vile yangu yanavyojionesha uungaji mkono. Ajabu najiuliza, unachokwepa kusema wazi ni nini?

6. Najua unajua kuwa nililenga Uhalali wa Hoja zao. Lakini pia Si kila Mtanzania ana haki ya kuongelea Ustawi wa Umma. Huo ni Upuuzi mwingine uliolishwa kwa watumwa wa Fikra za Demokrasia. Wapumbavu hawana nafasi ya kusemea Taifa. Mifumo Batili inafanya Leo uwakute ofisini kabisa.

7. Umekuwa MTU wa kulaumu kuwa hatutaki mseme, sijui unatoa wapi hoja yako. TEMENI NYONGO MUWEZAVYO ndugu, hakuna wa kuwazuia Tmeni msibaki nazo ni sumu. Nasi tutazijibu tu, Tytazikosoa kila Leo, Na tunapozishangaa msitafsiri kwamva tunazuia, HATUNA UBAVU HUO. Acha woga ukiopitiliza, hili ni jukwaa LA wote.
 
1. Kukiuka Katiba ili Kulinda Masilahi ya Umma SIO KOSA.
Ni kosa kubwa sana! Katiba ni makubaliano na mwongozo wa jamii. Kwamba , kuna taratibu zinapaswa kufuatwa ili tuishi kama jamii. Katiba imetoa nafasi 'kukiukwa' katika msingi ya kikatiba. Mfano, Rais akapewa haki ya kumsamehe muuaji aliyethibitishwa na mahakama
Rais kapewa haki ya kuingiza nchi vitani kwanza lakini pia kuna utaratibu wa kufanya hivyo
Katiba imempa haki Rais juu ya umiliki wa ardhi ya MTU anaweza ku revoke hati ya mali ya mtu

Kwahiyo mfumo mzima wa katiba unatoa taratibu ikiwemo 'ukiukwaji wake'' lakini siyo open season kwamba anaibuka mwendawazimu anakiuka katiba tunajenga uhalali.
Uhalali wa ukiakwaji wa katiba upo ndani ya katiba siyo
Ustawi wa Umma upo juu ya Katiba au taratibu zozote ziwekwazo na binadamu. Hivyo Ukiukwaji huo si wa kuhalalisha kosa kwa kosa. Tunaposema Tutafakari zaidi, huwa ni hivyo. Yaani, kutoruhusu Fikra zako kutofungwa na chochote ila tu Ustawi wa Umma. Sio dini, Katiba, sheria, mazoea, usomi, chama, MTU, mlengo, nk....
Hata Simba na Tembo wanaishi kama jamii, tofauti baina yao na sisi ni weledi! Sisi tunaishi kwa taratibu ili kuepuka 'rule of the jungle'' . Kutofuata taratibu tulizojipangia kwa njia ya katiba ni kufuata mfumo wa rule of the jungle ambao 'tumeujaribu'' hivi karibuni na tunajua matokeo yake.
Unampa usahihi Assad kwa kuwa hakuna aliyesema 1.5T ziko wapi, JE, ULISHAWAHI KUJIULIZA USAHIHI WA UWEPO WA HIYO PESA? Aje kama ni Tuhuma Hewa na Mhimili ukaona ukengemfu wake, na kwa busara ukaamua kumstaafisha kwa lazima?
Siyo tuhuma hewa, tuhuma zilikuwepo na utawala wa JPM unajua hilo. Kilichotakiwa ni kueleza zipo wapi pesa za walipa kodi, hadi anaingia kaburini hakuwahi kujibu. Wasaidizi wake akiwemo mtoto wa Dada yake hakuna anayesema 'ni tuhuma za uongo'' . Kwavile hakuna anayekanusha basi aliyesema anabaki kuwa mkweli, hazijulikani zilipo 1.5T, CAG Assad
Ni sawa na anachosema Zitto hakuna maelezo ya 70B zilizokwenda Mwanza! CAG Kichere

Kumstaafisha kwa lazima ilikuwa kuondoa ''udhia'' ili asije ibua tena madudu mengine
Kumuondoa hakujibu hoja wapi zilipo 1.5T . Kabla ya jibu wapo wanaouliza 70 Bilioni zilikuwa za nini. Chuki haikuwahi kujibu tuhuma ndio maana siku za karibuni rekodi ya Magufuli inawekwa wazi na wapo wasiotaka kama wewe kwa kujua yapo mengi katika rekodi!!!
Kama tunahitaji Katiba mpya ili kuwa na uhakika na usahihi wa CAG, Wewe usahihi unaodai kuwa nao juu ya ripoti ya Kichere umeutoa wapi halikuwa Katiba Yetu ni 77 bado? Huoni kuwa unatulisha mihemko has I tu pasipo facts unazodai?
Kuna aina mbili za usomaji, kusoma maandiko kwasababu tunaziona herufi na kusoma maandiko kwa kuyaelewa. Nina shaka sijui upo wapi katika makundi hayo

Katiba haielengi kueleza usahihi wa taarifa za CAG. Katiba inalenga kuzuia upuuzi kama ule wa kumstaafisha CAG ili kuendelea kufanya watakavyo.
Tuliishi kwa mazoea ya viongozi waliotangulia wakiogopa taratibu tu kwa uadilifu
Tumejifunza kuwa kila 'kiingacho si dhahabu' . Tuipitie katiba ili kuzuia ubazazi usijitokeze tena
5. Chuki zako ziko wazi unapotaka tuunge mkono Shutuma zusizo na Ushahidi juu ya Magufuli.
Ndio maana nasema maoni ya watu hayawezi kuwa chuki na siwezi kukubaliana nawe eti nisiwe na chuki. Kwani shutuma nizitoa dhidi ya Magufuli ni zipi? Mbona huelezi ili tuweke ushahidi!
Siwezi kuweka ushahidi bila tuhuma, weka tuhuma mezani kwanza !
Lakini hauko pekee yako, wenzako pia wameshaanza kujitaja hovyo, wanataka tukazikwe nae, wanaodai haikuwa rahisi kuishi nae, wanaotema nyongo, wenye nyuso za FURAHA, na wapigaji wengi tu. Huwezi kuturubuni, maandishi yako yanakuweka wazi, kama vile yangu yanavyojionesha uungaji mkono. Ajabu najiuliza, unachokwepa kusema wazi ni nini?
Rekodi ya Magufuli ndicho kitu pekee kitakachosaidia legacy yake.

Watetezi wake wajikite kuieleza rekodi yake, wasiokubaliana naye wanajenga hoja zenye mantiki, zijibiwe kwa mantiki
Najua unajua kuwa nililenga Uhalali wa Hoja zao. Lakini pia Si kila Mtanzania ana haki ya kuongelea Ustawi wa Umma. Huo ni Upuuzi mwingine uliolishwa kwa watumwa wa Fikra za Demokrasia. Wapumbavu hawana nafasi ya kusemea Taifa. Mifumo Batili inafanya Leo uwakute ofisini kabisa.
Hakuna mtu mwenye mamlaka ya ustawi wa umma. Ustawi wa Umma ni jukumu la Umma na ni wajibu wa Umma na haki ya Umma. Kilichotokea kwa watu kujivika joho la Tanzania ulikuwa uzuzu 'imbecile'' . Tukatae uzuzu huo na hapa ndipo tunahitaji rekodi .
Rekodi ya kudhani Tanzania ni mtu na rasilimali za nchi za kikundi ni mbaya ndiyo inajadiliwa!

Kudhani ustawi wa jamii unahitaji kuigawa jamii katika misingi ya udini, ukabila na ukanda ni jambo la kulaaniwa na wenye akili timamu. Hilo haliondoi haki ya ' collective imbecilisation'
7. Umekuwa MTU wa kulaumu kuwa hatutaki mseme, sijui unatoa wapi hoja yako.
Kwamba Marehemu anasemwa kwa flyover, JNHP , SGR tu! hatusemi rekodi nyingine kwa kisingizo cha Marehemu hasemwi ili kuficha lundo la uchafu na uvundo linalonuka
Uvundo haupuuliziwi ubani unaondolewa na huwezi kuuondoa kama husemi upo wapi

Kuna watu wamedhulumiwa wanadai haki zao japo kuombwa radhi. Kuna watu hatujui wapo wapi, hakuna wa kuwasema isipokuwa tunaamini marehemu hasemwi.

TEMENI NYONGO MUWEZAVYO ndugu, hakuna wa kuwazuia Tmeni msibaki nazo ni sumu. Nasi tutazijibu tu, Tytazikosoa kila Leo, Na tunapozishangaa msitafsiri kwamva tunazuia, HATUNA UBAVU HUO. Acha woga ukiopitiliza, hili ni jukwaa LA wote.
Naam ni jukwaa la wote na tuwaache wenye nyongo zao wateme.
Wanotetea nyongo nao wana haki lakini tusijifiche chini ya kapeti linalovunda kwa kisingizio cha Marehemu hasemwi! Ni marehemu gani huyo ? Nyerere ? Mkapa? au Magufuli?
Kwanini Magufuli? nini kinafichwa !
 
Ni kosa kubwa sana! Katiba ni makubaliano na mwongozo wa jamii. Kwamba , kuna taratibu zinapaswa kufuatwa ili tuishi kama jamii. Katiba imetoa nafasi 'kukiukwa' katika msingi ya kikatiba. Mfano, Rais akapewa haki ya kumsamehe muuaji aliyethibitishwa na mahakama
Rais kapewa haki ya kuingiza nchi vitani kwanza lakini pia kuna utaratibu wa kufanya hivyo.
Ninyi ndio aina ya watu ambao hatuwataki kuwa serikalini, maana hamtashindwa kupeleka nchi Utumwani kwa hoja kwamba MNATII KATIBA. NI WASALITI.

Nitarudia tena... USTAWI WA UMMA UKO JUU YA KATIBA NA TARATIBU ZOZOTE KATIKA NCHI. Hakuna ubaya wa Kukiuka Katiba kulinda Umma. Na kwangu Magufuli alikuwa muumini mzuri wa hilo.

Ukishakuwa na conditioned mind to formalities huwezi kuona hayo. Ndio maana tunawasihi sana mvue ujuaji wenu na usomi wenu.

Unatuambiaje eti kuwa Katiba imeweka misingi ya ukiukwaji wake, na misingi hiyo ikawa nje ya Katiba? Hivi huwa unarudia unachokiandika na kukitafakari? Mifano yako ya Haki za Raisi haiko nje ya Katiba, wala haikiuki Katiba. Hiyo ndiyo Katiba yenyewe.

Kutetea Ubatili ni shida sana ndio maana huachi kujikanyagakanyaga. Pole sana. Ni chaguo la Hisia zako.
 
Back
Top Bottom