Anguko la Ndugai: Somo la Katiba, viongozi na nchi

Soma hapo chini bandiko lako , na rudi bandiko 21 pia

Hapana hakuna mtu anayetaka kuchafua ukuu wake. Tunachosema hapa hatukubali ''collective imbecilisation'' tukiambiwa '' Marehemu hasemwi'' wakati huo huo tunahubiriwa uongo wa makubwa aliyofanya ambayo si makubwa ni marudio tu ya kawaida

Mfano ni wewe kueleza kuhusu Wami, wakati hakuna alichofanya zaidi ya kusimamia mradi wa JK
Kutetea kauli yake ya kuwasema watu wa kaskazini wakati ulikuwa ni kauli ya ajabu sana ya Rais wa nchi yoyote kuitoa! orodha inaendelea

Tunataka rekodi ya JPM isiishie flyover ya Tazara, twende kwenye rekodi yake ya haki za binadamu, kujali usalama wa raia, mahusiano ya kitaifa aliyobomoa na leo tunaongelea kanda ya kaskazini, mahusiano ya kimataifa n.k.

Hatuwezi kuficha rekodi katika mwamvuli wa '' Marehemu hasemwi'' halafu tunahubiriwa uongo

Hapa ndipo mjadala ulipo, kwamba, tuonyeshe basi nje ya urasimu Magufuli alifanya nini tofauti?
Hakuna jibu! hamkuweza kuonyesha hata kimoja
Nirudie mara ngapi kukuambia mimi si miongoni mwa hao waliokuzuia kumsema marehemu? Kwanza umezuiliwa lini na nani? Au unajipika lawama tu?

Ni Wami IPI hiyo iliyoanza na Jk? Unaishi wapi wewe, mbona kama unaishi kwa kusomuliwasimuliwa tu? Yaani hata kutafakari daraja la mtoni tu linajengwaje miaka 8 umeshindwa? Tanzanite limekamilika halafu la 2014 Lowe bado!

Embu tuambie wewe juu ya hayo ya Uhusiano wa Kimataifa na Umoja wa Kitaifa. Ameharibu UPI na kwa namna gani!?

Juu ya Haki na Demokrasia, mimi kwangu huo ni upuuzi kusikia unatetewa. Sitaujadili.

Juu ya UTU nikishakufundisha Utu ni nini, rudia kusoma kisha tafakari nyendo za Magufuli katika hilo.
 
Yes! hutajadili unajua rekodi ilivyo , tutasikia ''marehemu hasemwi''
Hili unalisema wewe. Unapenda kushikilia vihoja vya ajabuajabu. Nani amekuzuia kusema humu? Kama Rais tu anasema, nani asiseme?
Rekodi ya haki za binadamu, utu, demokrasia,
Hivi havipikiki chungu kimoja, kama umeviona mahali basi JITAFAKARI.
mahusiano ya kitaifa, kikanda na kimataifa hayasemwi kwasababu kwa mujibu wako! '' ukiukaji wa hayo umefanya afanye makuu''
Semea wewe, aliyaharibu wapi na kwa namna gani!
Kwamba ni haki kuvunja umoja wa kitaifa ili kufanya maajabu! yapi ! huwezi ku point out!
Thibitisha kuvunjika kwa huo umoja wa kitaifa, isije kuwa ni Hisia zako tu.
 
''Hatapeleka maendeleo maeneo waliochagua wapinzani'' wakati anachukua kodi maeneo hayo ni dhulma na ukiukwaji wa haki za binadamu.

Kutamka wazi ''nikupe gari halafu umtangaze mpinzani'' ni kukiuka misingi ya demokrasia na utawala bora.

Kuzuia wananchi kufanya shughuli 'wasubiri wengine'' kuwagawa wananchi, kupanda chuki, kunyima fursa ya kujiendeleza wakati wakilipa kodi

Utaratibu wa ''plea bargaining '' hauzingatia haki, ulijenga mwanya wa uonevu
CAG kasema hata pesa hazijulikani zilipo

Kuondoa wasio na vyeti ni zoezi halali, kuondoa kwa upendeleo ni kukiuka dhana ya haki

Sheria ya ' money laundering' ilitumika kubambikiza kesi na kuwanyima watuhumiwa dhamana
Unatulazimisha kuamini Hisia zako sasa.
 
Unatulazimisha kuamini Hisia zako sasa.
Hapana halazimishwi mtu kuamini , lakini, ukweli unajisemea
1. Je, JPM hakusema hatapeleka maendeleo maeneo waliochagua Wapinzani?

2.Je, Hakutamka wazi 'nikupe gari halafu umtangaze mpinzani'

3.Je, hakutamka '' Wakaskazini wasubiri' ? Kuna ushhuda umetoka alihamisha pesa zilizotengwa kwa mradi mmoja kaskazini akapeleka kwenye ule mradi wa nyumbani kwetu.

4. Je, si kweli pleas bargaining imetumia kama chanzo cha mapato ambayo leo hayajulikani yamekwenda wapi kwa mujibu wa CAG?

5. Je, si kweli aliondoa wenye vyeti fake na kuwaacha wapendwa akiwemo kijana wetu wa mkoa?

6. Si kweli maoney laundering ilitungwa ili kudhibiti watu kwa kuwanyima dhamana? Imetumika lini baada ya kwenda zake ?
 
Hapana halazimishwi mtu kuamini , lakini, ukweli unajisemea
1. Je, JPM hakusema hatapeleka maendeleo maeneo waliochagua Wapinzani?
2.Je, Hakutamka wazi 'nikupe gari halafu umtangaze mpinzani'
3.Je, hakutamka '' Wakaskazini wasubiri' ? Kuna ushhuda umetoka alihamisha pesa zilizotengwa kwa mradi mmoja kaskazini akapeleka kwenye ule mradi wa nyumbani kwetu.
Bado unahangaika na Urasimi/Formalities ambazo hazijawahi kuwa Tija kushinda Ukiukwaji wake.
4. Je, si kweli pleas bargaining imetumia kama chanzo cha mapato ambayo leo hayajulikani yamekwenda wapi kwa mujibu wa CAG?
Kwa mujibu wa CAG aliyebadilisha gia baada ya Magufuli kufa. Tuambie kwanini naye tusimjumuishe kwenye Team Haters kama wewe?
5. Je, si kweli aliondoa wenye vyeti fake na kuwaacha wapendwa akiwemo kijana wetu wa mkoa?
Mengine usiusemee moyo tu, uwe na ushahidi utuwekee hapa. Na Labda angeweza kuwaacha wengi wenye Ufanisi ila hakuweza kuwajua.
6. Si kweli maoney laundering ilitungwa ili kudhibiti watu kwa kuwanyima dhamana? Imetumika lini baada ya kwenda zake ?
Wapumbavu ni wale wanaoshindwa kuitumia.... Ndio maana tunakuambia mchwa wametamalaki upya.

Kama aliitumia vibaya(ulete ushahidi lakini) inazuiaje waliopo kuitumia vizuri?
 
Kwa mujibu wa CAG aliyebadilisha gia baada ya Magufuli kufa. Tuambie kwanini naye tusimjumuishe kwenye Team Haters kama wewe?
CAG Assad ulisema alikuwa hater, CAG Kichere naye hater!
Kichere kasema pesa za mradi wa barabara ya Aursha-Holili zilichotwa kujenga Airport ya Chat
Taarifa hiyo pia iliandikwa katika the citizen!
Mengine usiusemee moyo tu, uwe na ushahidi utuwekee hapa. Na Labda angeweza kuwaacha wengi wenye Ufanisi ila hakuweza kuwajua.
Zoezi likajengewa hoja ya ''wanasiasa'' hawahusiki na vyeti 'fake' kumlinda Bashite

Kuanzia hapo zoezi likakosa mashiko double standards zika demoralize watu kwa ubaguzi
Wapumbavu ni wale wanaoshindwa kuitumia.... Ndio maana tunakuambia mchwa wametamalaki upya.

Kama aliitumia vibaya(ulete ushahidi lakini) inazuiaje waliopo kuitumia vizuri?
Rugemalarila alikataa plea bargain. Sheria iliwekwa kama mkomoeni
Kila aliyekamatwa 'money laundering' ili akose dhamana

Ripoti ya CAG inaonyesha ubadhirifu uliokubuku tukiambiwa '' kuna uzalendo''

Uhusiano wa kimataifa, tuliambiwa JPM hana safari za nje ili kubana matumizi wakati anawatuma VP na PM katika capacity ya 'Rais' ! kupunguza gharama?

Mahusiano ya kimataifa yana umuhimu kwa nchi.

Mfano, mikutano ya SADC JPM alikuwa haudhurii, UNGA hakuwahi kwenda kwa kubana matumizi leo bilioni 70 bila maelezo- CAG.

Kutokuwepo kimataifa tulipoteza fursa. Dunia ya leo ni ya fursa, ushindani na networking

Katika viongozi waliopita ni JPM aliyepoteza nguvu ya Tanzania kimataifa
 
CAG Assad ulisema alikuwa hater, CAG Kichere naye hater!
Kichere kasema pesa za mradi wa barabara ya Aursha-Holili zilichotwa kujenga Airport ya Chat
Taarifa hiyo pia iliandikwa katika the citizen!
Jibu swali, Kwanini tusimuwekee shaka Kichere. Halafu usinilishe maneno, sijakuambia Kichere ni hater, ila nimehoji kwanini tusimtilie shaka!
Zoezi likajengewa hoja ya ''wanasiasa'' hawahusiki na vyeti 'fake' kumlinda Bashite

Kuanzia hapo zoezi likakosa mashiko double standards zika demoralize watu kwa ubaguzi
Shida ya Makonda ni Ujana mwingi tu, lakini ni mtendaji mzuri sana ambaye hata ingekuwa mimi nisingemuuza kwa njaa ya mtoto.
Rugemalarila alikataa plea bargain. Sheria iliwekwa kama mkomoeni
Kila aliyekamatwa 'money laundering' ili akose dhamana
Mtatetea mpaka Richmond, tunawajua. Ndio maana tunasema Wezi watumiao sheria kuiba, uhitaji Ukatili wa kisheria kudeal nao. Ukiwachekea wamekumaliza tayari. Leo nadhani mko nao viti virefu baada ya kuanza Kulipana.
 
Ripoti ya CAG inaonyesha ubadhirifu uliokubuku tukiambiwa '' kuna uzalendo''
Wanaosema Uzalendo ni kwa sababu hii...
Kwa miaka 5 Deni la Taifa limeongezeka kwa 32T, wastani wa mapato ya kila mwezi ni 1.5T.

Bado tukashuhudia Miradi kila kona ya Nchi; Bandari karibia zote zimeguswa, viwanja vya ndege, barabara, madaraja, reli, hospitals, shule, Elimu Bure, Vyuo, Masoko, Bus Terminals, Umeme, nk....

Kikubwa zaidi wahudumu walijitahidi kuwa na hekima katika ofisi za umma, na yalipotoea mengi yalikemewa bila haya. Wafanya biasharaha hawakujiropokea bei hovyo, na yalipotokea yalikemewa mengi.

Uzuri zaidi wengi Tuliona Fahari Kuitwa Watanzania, Tulitembea Kifua mbele.

Katika yote hayo mnataka tuamini poroja za Ubadhirifu mkubwa eti. Na use hivyo maana ulipokuwa mdogo hatukuona hata yakitendeka.

Leo mnataka kuturudisha kuzoea Ubatili kwa jina la msomi kasema, ripoti, mstaafu kasema, rais kasema, CCM au Upinzani umesema. MSITUFANYE WATOTO. Magufuli ameamsha wengi sana Kujitambua, mtahangaika na jina lake na hamtaliweza.

Uhusiano wa kimataifa, tuliambiwa JPM hana safari za nje ili kubana matumizi wakati anawatuma VP na PM katika capacity ya 'Rais' ! kupunguza gharama?
Unashangaza ndugu! Duuuuhh!
Mahusiano ya kimataifa yana umuhimu kwa nchi.

Mfano, mikutano ya SADC JPM alikuwa haudhurii, UNGA hakuwahi kwenda kwa kubana matumizi leo bilioni 70 bila maelezo- CAG.
Umerudi kwa Kichere tena. Usisahau na Assad.
Kutokuwepo kimataifa tulipoteza fursa. Dunia ya leo ni ya fursa, ushindani na networking
Kutokuwepo Kimataifa ndio Kupoje huko?
MindSlavery.
Katika viongozi waliopita ni JPM aliyepoteza nguvu ya Tanzania kimataifa
Nguvu ya Tz Kimataifa ilikuwa IPI na msaada gani kwa Umma!? Na tumekosa nini kutoka huko wakati wa JPM?

Wajomba zenu wamerudi sasa, hope Tutapiga hatua.
 
Jibu swali, Kwanini tusimuwekee shaka Kichere. sijakuambia Kichere ni hater, inimehoji kwanini tusimtilie shaka!
Unaweza kumwekea shaka wewe, haina maana wote wakubaliane nawe
Hoja hapa ni moja, CAG Assad alimyooshea kidole Magufuli kupitia ripoti yake, CAG Kichere kamnyooshea kidole kupitia ripoti yake, hivyo, tuangalie ripoti na si mtoa ripoti

Mifano
CAG Assad alihoji 1.5T zilipo, je, tunajibu zipo wapi?
CAG Kichere kahoji Bilioni 70, je, tunajua zilikwenda Mwanza kw autaratibu upi?
Majibu yanyotakiwa si Kichere bali madudu ya ripoti yake
Shida ya Makonda ni Ujana mwingi tu, lakini ni mtendaji mzuri sana ambaye hata ingekuwa mimi nisingemuuza kwa njaa ya mtoto.
Ni mtendaji mzuri kwa maana moja, unaweza kumtuma kufanya lolote na akafanya. Unajua tuhuma dhidi yake kuhusu upotevu na utekaji. Ni mtendaji mzuri kwasababu hiyo, hana muda wa kufikiri, kutathmini ili mradi ana zana za kazi mkononi, atapiga tindo kuwakomesaha sisimizi

Kwamba alitumwa ataje orodha (feki) ya wauza madawa, akawataja tu bila kujali haki zao
Orodha ile ipo waliotajwa wapo hakuna kilichotokea akaonekana mpumbavu tu.
Waliomtuma walimuona shujaa, kama ilivyokuwa kwa Sabaya.

Kimkakati si kiongozi mzuri kwa vigezo vyote. Hivi kampeni gani alianzisha ikafanikiwa?

Hivi kuna anayeweza kuzuia biashara ya madawa kwa mkakati wa mkoa mmoja tu!

Anashughulikia ndoa zao kwa misuli, makoleo na tindo bila kujua ndoa ni taasisi ya zamani duniani ikilindwa na sheria za dini au za secular. Aliangukia pua
Kama una agenda ya kusukuma isiyohitaji watu wanaofikiri Makonda anafaa sana!
Ndio maana tunasema Wezi watumiao sheria kuiba, uhitaji Ukatili wa kisheria kudeal nao. Ukiwachekea wamekumaliza tayari.
Naam! key word hapa ni ukatili. Imechukua siku nyingi hatimaye umetamka!
Ukatili ni silaha muhimu sana kwa wasio na maarifa wala elimu
 
Wanaosema Uzalendo ni kwa sababu hii...
Kwa miaka 5 Deni la Taifa limeongezeka kwa 32T, wastani wa mapato ya kila mwezi ni 1.5T.

Bado tukashuhudia Miradi kila kona ya Nchi; Bandari karibia zote zimeguswa, viwanja vya ndege, barabara, madaraja, reli, hospitals, shule, Elimu Bure, Vyuo, Masoko, Bus Terminals, Umeme, nk....
Hoja si ongezeko la deni la Taifa, hoja ni uongo ulioambatana na hilo.
Tuliambiwa pesa za makusanyo zikiwemo za mafisadi ndizo ziligharamia miradi.
Hatukuelezwa tunakopa Msingi wa hoja ni kuwa kwanini tulifichwa?
Tulikopa wapi kwa siri? Kwanini iwe siri kwa sisi walipaji?
Kikubwa zaidi wahudumu walijitahidi kuwa na hekima katika ofisi za umma, na yalipotoea mengi yalikemewa bila haya. Wafanya biasharaha hawakujiropokea bei hovyo, na yalipotokea yalikemewa mengi.
Ni kweli kabisa hayo unayosema, ningekukumbusha pia upande wa pili
Maiti zilipookotwa kwa makundi baharini na mitoni kimya kilitanda, ''yalipotokea hayakukemewa'
Ongezeko la watu wasiojulikana lilitishia kuliko panya road, 'yalipotokea hayakukemewa''
Kukawa na kesi ili wafanyabiashara waingine ' plea baragain, yalipotokea hayakukemewa''
Uzuri zaidi wengi Tuliona Fahari Kuitwa Watanzania, Tulitembea Kifua mbele.
Wengi kwa kigezo gani?
Katika yote hayo mnataka tuamini poroja za Ubadhirifu mkubwa eti. Na use hivyo maana ulipokuwa mdogo hatukuona hata yakitendeka.
Ubadhirifu ni neno, matendo ya ubadhirifu yanaonyeshwa na ripoti za CAG

Unachosema hapa ni kwamba, kwavile kuna miradi imeguswa ni halali milioni 70 zipotee tu
Kwavile kuna miradi imeguswa hakuna shida kama tutahamisha 1.5T kwenye vi account vyetu
Kwamba Tanroad wanajenga viwanda vya sukari, it's OK tusijiulize! mkubwa aliamua

Madudu yaliyorpotiwa taarifa ya CAG yanahitaji maelezo, hizi habari za flyover tutaongea lakini madudu kwanza.
 
Unaweza kumwekea shaka wewe, haina maana wote wakubaliane nawe
Hoja hapa ni moja, CAG Assad alimyooshea kidole Magufuli kupitia ripoti yake, CAG Kichere kamnyooshea kidole kupitia ripoti yake, hivyo, tuangalie ripoti na si mtoa ripoti

Mifano
CAG Assad alihoji 1.5T zilipo, je, tunajibu zipo wapi?
CAG Kichere kahoji Bilioni 70, je, tunajua zilikwenda Mwanza kw autaratibu upi?
Majibu yanyotakiwa si Kichere bali madudu ya ripoti yake
Ndio, shaka naweka mimi hasa kwa sababu ya nyendo za Makundi ya mchwa uliyoyataja. Hatuna imani nao.

Ila inachoshangaza ni wewe usie na shaka ukakosa Ushahidi ila tu kusemea imani yako.
Ni mtendaji mzuri kwa maana moja, unaweza kumtuma kufanya lolote na akafanya.
Na hakuna Kiongozi asiyetaka hilo kwa sarbodinates wake.
Unajua tuhuma dhidi yake kuhusu upotevu na utekaji.
Tuhuma. Kama una Ushahidi ulete. Kama huna usijengee hoja.

Ninachojua mimi Magufuli na timu yake hawakuwa wanapigana na mtandao dhaifu.
Ni mtendaji mzuri kwasababu hiyo, hana muda wa kufikiri, kutathmini ili mradi ana zana za kazi mkononi, atapiga tindo kuwakomesaha sisimizi
Unaowaita Sisimizi ni kina nani? Unafikiri kuna sisimizi anayehitaji tindo?

Alikuwepo Amina Chifupa, hao sisimizi wako ndio watuhumiwa.
Kwamba alitumwa ataje orodha (feki) ya wauza madawa, akawataja tu bila kujali haki zao
Ufake unautoa wapi? Ninakuuliza mara nyingine, Unaishi hapa Tz au nje ya Nchi?
Orodha ile ipo waliotajwa wapo hakuna kilichotokea akaonekana mpumbavu tu.
Waliomtuma walimuona shujaa, kama ilivyokuwa kwa Sabaya.
Hata wazazi walimuona Shujaa.
Kimkakati si kiongozi mzuri kwa vigezo vyote. Hivi kampeni gani alianzisha ikafanikiwa?
Wajibu wake haukuwa kuanzisha Kampeni tu. Hatupaswi kujitia upofu.
Hivi kuna anayeweza kuzuia biashara ya madawa kwa mkakati wa mkoa mmoja tu!
Ulitakaje kwahiyo, kwamba asifanye chochote au? Unaifahamu Dar na mahusiano yake ya Madawa ya Kulevya? Alipaswa kuungwa mkono, ila inatambulika Uzito wa Mtandao wa Madawa si kila mtu anaweza kuthubutu. Ajabu kufeli kwake mpo mnaoshangilia.
Anashughulikia ndoa zao kwa misuli, makoleo na tindo bila kujua ndoa ni taasisi ya zamani duniani ikilindwa na sheria za dini au za secular. Aliangukia pua
Umeamua kuona upande wake huo tu.
Kama una agenda ya kusukuma isiyohitaji watu wanaofikiri Makonda anafaa sana!
Ukifikiri hakuna agenda ya namna hiyo katika serikali, basi ujue Fikra zako ni Changa sana.
Naam! key word hapa ni ukatili. Imechukua siku nyingi hatimaye umetamka!
Ukatili ni silaha muhimu sana kwa wasio na maarifa wala elimu
Unachelewa sana kuelewa, hili nilishakuambia wakati umeparamia hovyo neno UTU.
Nilisema, "Itakapokupasa Kuua, UTAUA." Na Kuua kokote ni Ukatili, lakini si Kila Ukatili ni Kinyume cha UTU.

Unafikiria taratibu sana, halafu unaraka kusemea mambo makubwa, ni wazi utatia vituko tu.

Nilikuambia Uwe Mkomavu, Uaache moyo wa kulialia unaposemea Maslahi ya Taifa. Hata hao wanaowafundisha soft hearts katika Taifa, wenyewe hawaishi hivyo.

AMKA NDUGU!
 
Hoja si ongezeko la deni la Taifa, hoja ni uongo ulioambatana na hilo.
Tuliambiwa pesa za makusanyo zikiwemo za mafisadi ndizo ziligharamia miradi.
Hiki mlijiambia wenyewe, Magufuli hajawahi sema kila mradi ni pesa ya ndani.
Kiongozi wa AfDB aliwahi mpaka kuhojiwa juu ya mikopo mingi kufund miradi Tz, Why Tz.
Hatukuelezwa tunakopa Msingi wa hoja ni kuwa kwanini tulifichwa?
Ulijificha wewe.
Tulikopa wapi kwa siri? Kwanini iwe siri kwa sisi walipaji?
Huo Uhuru mwingine unaodai ni Tango Pori mlilomezeshwa. Lakini pia si kila mkopo ulikuwa siri, usitudanganye.
Ni kweli kabisa hayo unayosema, ningekukumbusha pia upande wa pili
Maiti zilipookotwa kwa makundi baharini na mitoni kimya kilitanda, ''yalipotokea hayakukemewa'
Bahati mbaya hatujui ni za nani na walifanya mini, tunaweza kuwaonea huruma tu kwa sasa. Lakini usikute walipaswa kusagwa kabisa wabakie majivuvkwa ufedhuli wao kwa umma.
Ongezeko la watu wasiojulikana lilitishia kuliko panya road, 'yalipotokea hayakukemewa''
Kukawa na kesi ili wafanyabiashara waingine ' plea baragain, yalipotokea hayakukemewa''
Wafanyabiashara! Hakika si kila ovu machoni ni la kukemea. Ibaki hivyo.
Wengi kwa kigezo gani?
Mimi na Mimi.
Ubadhirifu ni neno, matendo ya ubadhirifu yanaonyeshwa na ripoti za CAG

Unachosema hapa ni kwamba, kwavile kuna miradi imeguswa ni halali milioni 70 zipotee tu
Kwavile kuna miradi imeguswa hakuna shida kama tutahamisha 1.5T kwenye vi account vyetu
Kwamba Tanroad wanajenga viwanda vya sukari, it's OK tusijiulize! mkubwa aliamua

Madudu yaliyorpotiwa taarifa ya CAG yanahitaji maelezo, hizi habari za flyover tutaongea lakini madudu kwanza.
Unachelewa kuelewa. Hizo 70b na 1.5T nilikuomba Ushahidi wa uwepo wake.

Kwa yaliyofanyika hizo kelele zenu zinaonekana batili bado mpaka pale mtakapoleta Ushahidi.

Ndugu, T 1.5 hawezi jificha isionekane. Tena kwa hoja zenu za kwamba hako ni kasehemu tu, possible ni 4 T na bado haionekani.

EPA/Richmond/Gas, ZINAONEKANA.
 
Katika yote hayo mnataka tuamini poroja za Ubadhirifu mkubwa eti.
Nyaraka ndizo zinasema ubadhirifu wa serikali ya Magufuli.

CAG Assad alisema 1.5T haijulikani ilipo, kuna maelezo yaliyowahi kutolewa na kujibu hoja!

Sasa kuba Bilioni 70 ambazo hazijulikani zilikuwa zinasafiri vipi kwenda Mwanza

Kuna hoja ya TANROAD kujenga viwanda na si barabara

Ripoti ya CAG aliyesifiwa na JPM, madudu yanachefua yaliyofanywa na Wazalendo

Madudu hayasaifishwi kwa jiki bali hoja na majibu mujarabu
 
Hiki mlijiambia wenyewe, Magufuli hajawahi sema kila mradi ni pesa ya ndani.
Yupo katika rekodi akisema fedha ni za ndani
Bahati mbaya hatujui ni za nani na walifanya mini, tunaweza kuwaonea huruma tu kwa sasa. Lakini usikute walipaswa kusagwa kabisa wabakie majivuvkwa ufedhuli wao kwa umma.



M Hizo 70b na 1.5T nilikuomba Ushahidi wa uwepo wake.
Kamuulize CAG mimi siandiki ripoti, na nukuu. 1.5T alisema Assada akatibua nyongo ya JPM

Ukaitwa mkutano wa kuapisha viongozi CAG akaambiwa ''eti zimeibiwa''! mtu alifura sana

CAG anasimama na hoja ya madudu, B. 70 zinakwenda kutalii Mwanza halafu zitarudi hazina.
Kwa yaliyofanyika hizo kelele zenu zinaonekana batili bado mpaka pale mtakapoleta Ushahidi.
Haa! tumekuonyesha alichokifanya ni wajibu wa serikali yoyote , hakuna! hakuna! hakuna kipya watangulizi wake hawakufanya! In fact alichofanya ni juu ya !
Tulikuwambia hakujenga hata sentimita moja ya reli au Bandari
Turudi tena kwenye orodha?

 
Yupo katika rekodi akisema fedha ni za ndani
Lete, tuone wapi alisema kila mradi ni Fedha za ndani.
Kamuulize CAG mimi siandiki ripoti, na nukuu. 1.5T alisema Assada akatibua nyongo ya JPM

Ukaitwa mkutano wa kuapisha viongozi CAG akaambiwa ''eti zimeibiwa''! mtu alifura sana

CAG anasimama na hoja ya madudu, B. 70 zinakwenda kutalii Mwanza halafu zitarudi hazina.
Yes, CAG ndio mwenye majibu kamili na serikali ya Magufuli. Sasa wewe unaanzaje kusemea kwamba una majibu ya uhakika? Ndio maana unashangaza.
Haa! tumekuonyesha alichokifanya ni wajibu wa serikali yoyote , hakuna! hakuna! hakuna kipya watangulizi wake hawakufanya! In fact alichofanya ni juu ya !
Tulikuwambia hakujenga hata sentimita moja ya reli au Bandari
Turudi tena kwenye orodha?
Hiki ulichoandika hapa ni Utoto. Hivi ulitaka afanye nje ya wajibu wake au nini?
Eti hakuna alichojenga hata kimoja, kweli UNATAFAKARI HURU WEWE?

Mbona unapenda kujifariji kwa upepo?
 

Yes, CAG ndio mwenye majibu kamili na serikali ya Magufuli.
Na ndiye anayesema 1.5T hazijulikani zilipo, B 70 zibapelekwa Mwanza bila sababu kujulikana. Kuna Tanroad kujenga viwanda badala ya barabara.
Hivi zile cash za kununua ATCL zilidhinishwa na chombo gani!
asa wewe unaanzaje kusemea kwamba una majibu ya uhakika? Ndio maana unashangaza.
Hapana majibu ni kutoka kwa CAG
Eti hakuna alichojenga hata kimoja, kweli UNATAFAKARI HURU WEWE?
Mbona unapenda kujifariji kwa upepo?
Tuonyeshe sentimita (cm) moja ya reli aliyejenga!
Tuonyesha 'sq ft ' moja ya bandari aliyojenga
Tuonyeshe Daraja moja alilojenga nje ya yale ya awamu ya nne
Tuonyeshe barabara moja aliyojenga

Ukimaliza, tuonyeshe kitu kimoja ambacho hakikuwahi kuwepo au kufanywa kabla yake

**Kujenga na kukarabati ni vitu tofauti
 
Na ndiye anayesema 1.5T hazijulikani zilipo, B 70 zibapelekwa Mwanza bila sababu kujulikana.
Mwambie atuoneshe zilipo ili tusimuone muongo na mzushi. 1.5 T tena plus hakuna mahali zinaweza kukaa zisionekane.

Kama billions tu ambazo hazijawahi tajwa na CAG tunaziona, hiyo 1.5 T zinaweza kujificha wapi?
Kuna Tanroad kujenga viwanda badala ya barabara.
Hivi zile cash za kununua ATCL zilidhinishwa na chombo gani!
Usiwe MTU wa kuhamisha magoli. Imarisha ulinzi au mashambulizi.
Hapana majibu ni kutoka kwa CAG
Sasa Siku nyingine usitushawishi kuunga mkono tuhuma ambazo huna uhakika nazo. Kaa chini.
Hoja zako hapa chini ZINAKUDHARIRISHA, hivi ni wewe kweli wa kung'ania vihoja vya rafsiri za maneno?

Hivi tunaposema Wizara ya Ujenzi, shughuli za Ukarabati huo hazifanyiki ndani yake?

Halafu Kiswahili cha wapi hicho unachotaka kudanganya watu kuwa Kujenga ni Kuanzisha jambo jipya?

Umeishiwa hoja hakika, na inakuvua Nguo. Punguza chuki upunguze aibu yako.
Tuonyeshe sentimita (cm) moja ya reli aliyejenga!
SGR Dar-Moro Km 300, imekarabatiwa IPI? Mbona unatia aibu?
Tuonyesha 'sq ft ' moja ya bandari aliyojenga
Tunakuambia Ujenzi unaoendelea vandarini. Nipo Mtwara, karibu ujionee.
Tuonyeshe Daraja moja alilojenga nje ya yale ya awamu ya nne
Tanzanite, Wami, Busisi, nk...
Alilikuta la Mto Kilombero akamalizia, Kigamboni akalifungua tu, nk

UNAJICHETUA NDUGU, UNAKERA SASA. Wewe mtu mzima, usijidharaulishe.
Tuonyeshe barabara moja aliyojenga
Mtwara-Mnivata Km 50 Newala Road.
Za ndani ya miji, Kilakala To Nane Nane, to Mafiga, ndani ya Manispaa ya Morogoro.
Kwanini umeamua kujichetua hivyo?
Ukimaliza, tuonyeshe kitu kimoja ambacho hakikuwahi kuwepo au kufanywa kabla yake
Hili halina umuhimu wowote. Ila ukilitaka ni Electrified SGR Dar-Moro Km 300.
**Kujenga na kukarabati ni vitu tofauti
Usilazimishe Uongo zaidi ndugu. CHUTAMA, UNAAIBIKA.


***Hata tafsiri yako ingekuwa sahihi isingebadilisha kitu...

Hoja hapa ni Matumizi ya Kodi zetu na Mikopo aliyotuingiza, ZIMETUMIKAJE? Iwe ametumia Kujenga au Kakarabati, haiwezi kuwa hoja.
 
Mwambie atuoneshe zilipo ili tusimuone muongo na mzushi. 1.5 T tena plus hakuna mahali zinaweza kukaa zisionekane.
CAG Assad katueleza 1.5T hazijulikani zilipo, atakuonyesha nini?
CAG Kichere katueleza, Bilioni 70 zilikwenda Mwanza, hajui ni kwanini. Aeleze nini?

Mtuhumiwa ana dhima ya kuthibitisha uongo wa tuhuma, kwanini JPM amefariki hakuwahi kutueleza zilipo na sasa hivi hakuna anayetuambia B 70 zipo wapi
Kama billions tu ambazo hazijawahi tajwa na CAG tunaziona, hiyo 1.5 T zinaweza kujificha wapi?
Unakosea! pesa za umma hazifungwi kwenye mabunda. Zinaweza kuwa katika namna tofauti
Usitegemee kuona mabunda, kama zipo kwenye account bado ni account isiyofikika na kila mtu.

Taasisi kama Ikulu haikaguliwi na CAG sasa unawezaje kuona transaction?
Kumekuwepo na malalamiko kuhusu Ikulu kutokaguliwa na CAG kwa awamu zote !
Hoja zako hapa chini ZINAKUDHARIRISHA, hivi ni wewe kweli wa kung'ania vihoja vya rafsiri za maneno?
Nadhani ulikusudia kusema ''ZINAKUDHALILISHA'' kama hiyo ndio maana yako nitakujibu kama siyo samahani. katika kiswahili hakuna neno 'kudharirisha'' unless ni jipya

Ukarabati ( maintanance ) inalenga kutunza au kuhifadhi kilichopo. Kuna ukarabati wa kawaida halafu upo wa kuhuisha ( improvement).

Ukarabati wa kuhuisha huwa na ongezeko la kitu zaidi ya kilichokuwepo.

Ujenzi (construction) unalenga katika kupanga , kufanya tathmini na kueleza mipango inafanyikaje
Hivi tunaposema Wizara ya Ujenzi, shughuli za Ukarabati huo hazifanyiki ndani yake?
Yes, ukarabati unafanyika na mfano mzuri ni Barabara ya Chalinze Segera.

Miaka ya karibuni kampuni ya Kamphil ilipewa tenda ya kukarabati barabara hiyo ikiwa ni pamoja na kurekebisha madaraja na daraja la Wami linalotumika sasa ni mojawapo

Baada ya Uhuru barabara ya Chalinze-Segera haikuwepo. Nyerere aliijenga
Ujenzi (construction) ulianza na Feasibility studies ikiwa ni kuanza na wazo, kulitathmini, kuandaa mipango na kulitekeleza na mwisho tukawa na barabara.

Kwa maelezo hayo, Rais Ali H Mwinyi alifanya UKARABATI wa barabara ya Chalinze-Segera
Rais JK Nyerere ALIJENGA ( construct) barabara ya Chalinze-Segera
Halafu Kiswahili cha wapi hicho unachotaka kudanganya watu kuwa Kujenga ni Kuanzisha jambo jipya?
Kwa maelezo hayo ya ukarabati na ujenzi , chuki ipo wapi? au kuuliza wapi JPM kajenga ni chuki!
Umeishiwa hoja hakika, na inakuvua Nguo. Punguza chuki upunguze aibu yako.
Unatakiwa kutetea au kubomoa hoja, usihangaike na messenger hangaika na message
Sijaishiwa hoja, JPM alichofanya ni kukarabati (maintanance) reli ya kati na kuifanyia mahuisho (improvement).


JPM angeimarisha reli ya kati tu ingalikuwa 'repair au maintanance' kwavile ameihuisha kwenda SGR ikitumia umeme hapo amefanya improvement kwasabau kuna added value katika reli liyokuwepo.

Yaani usipokuwa na hasira au matusi nitakufahamisha vitu vingi kwakweli
SGR Dar-Moro Km 300, imekarabatiwa IPI? Mbona unatia aibu?
Imekarabatiwa kwasababu hakukuwepo na Feasibility studies'' imefuata njia ile ile iliyokuwepo kukiwa na mabadiliko ya madaraja au ''landscape' ili kuhimili mfumo wa SGR na umeme
Tunakuambia Ujenzi unaoendelea vandarini. Nipo Mtwara, karibu ujionee.
Yes ukarabati ni jambo jema. Tulizuia ujenzi wa bandari ya Bagamoyo
Tanzanite, Wami, Busisi, nk...
Alilikuta la Mto Kilombero akamalizia, Kigamboni akalifungua tu, nk
Ndugu yangu haya yalikuwa ya JK.
Mtwara-Mnivata Km 50 Newala Road.
Za ndani ya miji, Kilakala To Nane Nane, to Mafiga, ndani ya Manispaa ya Morogoro.
Kwanini umeamua kujichetua hivyo?
Ukarabati. Halafu uwe muangalifu maana ukitaja KM 50 sijui kwa Julius Nyerere tutasema nini
***Hata tafsiri yako ingekuwa sahihi isingebadilisha kitu...
Hoja hapa ni Matumizi ya Kodi zetu na Mikopo aliyotuingiza, ZIMETUMIKAJE? Iwe ametumia Kujenga au Kakarabati, haiwezi kuwa hoja.
Ndiyo maana tunauliza kodi zetu 1.5T na 70 B zipo wapi?
Hivi si JPM na MSD umesikia madudu yake! huko TANROAD ! yaani ni kama usikie kampuni ya IT inajishughulisha na ununuzi wa Korosho. By the way ya korosho vipi!
 
CAG Assad katueleza 1.5T hazijulikani zilipo, atakuonyesha nini?
CAG Kichere katueleza, Bilioni 70 zilikwenda Mwanza, hajui ni kwanini. Aeleze nini?

Mtuhumiwa ana dhima ya kuthibitisha uongo wa tuhuma, kwanini JPM amefariki hakuwahi kutueleza zilipo na sasa hivi hakuna anayetuambia B 70 zipo wapi
Waliofanya kazi na Magufuli wapo bado serikalini, Kichere au wewe utuhojie hao waoneshe 1.5 T zilipo, maana wengine bado tunaona Tuhuma zenu ni Propaganda.
Unakosea! pesa za umma hazifungwi kwenye mabunda. Zinaweza kuwa katika namna tofauti
Usitegemee kuona mabunda, kama zipo kwenye account bado ni account isiyofikika na kila mtu.
Unachelewa sana kuelewa.
Sijasema zinaonekana kwenye mabunda au bank. Tunaziona kupitia nyendo zao kiujumla wake na marafiki zao.

Kwamba kuwe na acc ambayo hata walioifungua washindwe kuifikia? Hizo bado zinabaki kuwaFikra za KUSADIKIKA.

Taasisi kama Ikulu haikaguliwi na CAG sasa unawezaje kuona transaction?
Kumekuwepo na malalamiko kuhusu Ikulu kutokaguliwa na CAG kwa awamu zote !
Umma hautegemei CAG pekee kujua ufanisi wa Taasisi ya Serikali. Hata CAG akinunuliwa, bado Umma unaweza kuwa na jicho huru la kuona.

JICHO HILO NDILO LINALOKATAA HOJA ZA UFISADI WA MAGUFULI.

Viongozi waliopita wengi waliimbwa ufisadi mpaka sokoni, Leo kapayuke hivyo juu ya Magufuli uone jicho la Umma kwake.

TUMEKATAA UNAFIKI WENU.
Nadhani ulikusudia kusema ''ZINAKUDHALILISHA'' kama hiyo ndio maana yako nitakujibu kama siyo samahani. katika kiswahili hakuna neno 'kudharirisha'' unless ni jipya
Vioja hivi.... Hakuna mkamilifu katika lugha humu. Usikimbie hoja kwa kuleta vioja.
Ukarabati ( maintanance ) inalenga kutunza au kuhifadhi kilichopo. Kuna ukarabati wa kawaida halafu upo wa kuhuisha ( improvement).
Ukarabati wa kuhuisha huwa na ongezeko la kitu zaidi ya kilichokuwepo.
Usihangaike sana ndugu, CHUTAMA.
Ujenzi (construction) unalenga katika kupanga , kufanya tathmini na kueleza mipango inafanyikaje
Kwahiyo unataka kusema Ukarabati hauna Tathimini? Hauna mipango? Umetokea wapi aisee?
Yes, ukarabati unafanyika na mfano mzuri ni Barabara ya Chalinze Segera.

Miaka ya karibuni kampuni ya Kamphil ilipewa tenda ya kukarabati barabara hiyo ikiwa ni pamoja na kurekebisha madaraja na daraja la Wami linalotumika sasa ni mojawapo
Baada ya Uhuru barabara ya Chalinze-Segera haikuwepo. Nyerere aliijenga
Ujenzi (construction) ulianza na Feasibility studies ikiwa ni kuanza na wazo, kulitathmini, kuandaa mipango na kulitekeleza na mwisho tukawa na barabara.
Katika Lugha ya Kiswahili hakuna tofauti hiyo ya msamiati wa Kujenga na Kukarabati.
Usidanganye. Katika Ukarabati kuna Ujenzi sawa na kwa maradi mpya.

Tusihangaikie vihoja vidogovidogo.
Kwa maelezo hayo, Rais Ali H Mwinyi alifanya UKARABATI wa barabara ya Chalinze-Segera
Rais JK Nyerere ALIJENGA ( construct) barabara ya Chalinze-Segera
Sasa ona unavyojichanganya, Yaani Mwinyi awe amekarabati, halufu JK awe amejenga kwa tafsiri hiyohiyo yako.

Kumbe u Team Msoga.
Kwa maelezo hayo ya ukarabati na ujenzi , chuki ipo wapi? au kuuliza wapi JPM kajenga ni chuki!
Unalazimisha dhana isiyokuwepo na hoja isisiyo na msingi. Tunachokuambia iwe amekarabati au amejenga, hoja kuu NI MATUMIZI YA FEDHA ZA UMMA. Wewe umeshikilia hakujenga amekarabati, hapo ndio tunapoona CHUKI YAKO.
Unatakiwa kutetea au kubomoa hoja, usihangaike na messenger hangaika na message.
Hoja hutafsiri aina ya messenger, usinizuie kufichua umbo lako sahihi. Je, umesahau?
Sijaishiwa hoja, JPM alichofanya ni kukarabati (maintanance) reli ya kati na kuifanyia mahuisho (improvement).
Reli ya Kati MGR ipo kama ilivyo, na imekarabatiwa pia na Magufuli.

SGR inajengwa alongside ya hiyo MGR na kuwepo kwa proposal za kufika Burundi,Rwanda ikiwezekana Uganda.

Hatujawahi kuwa na SGR ya kukarabati njia ya Dar-Mwanza,Dar-Kigoma.

WASHAURI WIZARA HUSIKA WABADILI NENO UJENZI WA SGR KATIKA MRADI. Pole sana, unaumizwa na kodi zako kutumika kwa faida yako. U wa ajabu sana.
JPM angeimarisha reli ya kati tu ingalikuwa 'repair au maintanance' kwavile ameihuisha kwenda SGR ikitumia umeme hapo amefanya improvement kwasabau kuna added value katika reli liyokuwepo.
Hiyo added value imekuwa Constructed ili kufikiwa.
Yaani usipokuwa na hasira au matusi nitakufahamisha vitu vingi kwakweli
Ni kweli unajua Vingi sana, natambua hilo. Shida IPO katika Tafakari yako, heri ya wavijuavyo vichache.
Imekarabatiwa kwasababu hakukuwepo na Feasibility studies''
Unayatoa wapi haya? Hivi unafikiri sisi tuko wapi?
Yaani Tilioni kadhaa zikose Upembuzi Yakinifu?
imefuata njia ile ile iliyokuwepo kukiwa na mabadiliko ya madaraja au ''landscape' ili kuhimili mfumo wa SGR na umeme
Muongo ndugu, hakuna daraja lililobadilishwa. Wala hakuna taruma la MGR lililong'olewa.
Ni reli mpya kuanzia Tuta mpaka hatua ya mwisho.

Hauko Bongo unalishwa uongo huko ulipo, au kama upo Bongo basi wewe ni mzembe kutokujua haya.
Yes ukarabati ni jambo jema. Tulizuia ujenzi wa bandari ya Bagamoyo
Ndio Tulisimamisha. Hasa kwa ujanjaujanja wenu katika mikataba kuumiza wananchi.

Hatukupewa mkataba tuuone, lakini uzoefu wa nyuma unatuonesha utapeli wenu.
Kumbuka Gas ya Mtwara ilisemewa na Magufuli kuwa sio Yetu, Samia nae anerejea mlemle. Hilo linaongeza shaka Juu yenu Team Msoga na miradi yenu.... Ina harufu ya Upigaji.
Ndugu yangu haya yalikuwa ya JK.
ACHA UONGO NA POROJO. Jisikie aibu kidogo.
Ukarabati. Halafu uwe muangalifu maana ukitaja KM 50 sijui kwa Julius Nyerere tutasema nini
Wewe ulitaka kuoneshwa hata sentimita moja, sasa unahamisha magoli.
Ndiyo maana tunauliza kodi zetu 1.5T na 70 B zipo wapi?
Hivi si JPM na MSD umesikia madudu yake!
Kamuulize Ummy aliliambia nini Binge juu ya Ufanisi wa MSD katika awamu ya Tano. Mengine yababaki kuchafuana tu.
huko TANROAD ! yaani ni kama usikie kampuni ya IT inajishughulisha na ununuzi wa Korosho.
Mimi sioni ajabu, kama tu Tija na Ufanisi utakuwepo. Kumbuka Mimi sio muumini wa Formalities za ajabuajabu.
By the way ya korosho vipi!
Mwaka wa Jana Tulimkumbuka Magufuli kwa kilio tena. Sauti ya wanunuzi ni kubwa kuliko ya serikali..... Mbaya zaidi kuna Tuhuma za Team yako kuchangamkia dili la wamarekani, kwa kuwanyonga RAIA.

Nipo huku tangu 2015, hakuna mwaka Korosho ilinuliwa bei ndogo kama msimu wa mwaka wa jana.

Bibi anasema, Mwamba angekuwepo haya yasingetokea.
 
Waliofanya kazi na Magufuli wapo bado serikalini, Kichere au wewe utuhojie hao waoneshe 1.5 T zilipo, maana wengine bado tunaona Tuhuma zenu ni Propaganda.
Hili nalo neno, nakubaliana nawe ingawa haliondoi ukweli kuwa shaka imetendeka wakati wa Mzalendo JPM. CAG anaweza kutusaidia zaidi kujua 1.5T na 70 B ilikuwaje wakati huo!
Sijasema zinaonekana kwenye mabunda au bank. Tunaziona kupitia nyendo zao kiujumla wake na marafiki zao. Kwamba kuwe na acc ambayo hata walioifungua washindwe kuifikia? Hizo bado zinabaki kuwaFikra za KUSADIKIKA.
Nashukuru umeelewa pesa 1.5T au 70 B haziwezi kufungwa katika mabunda.

Nikusaidie kuelewa zaidi, kwamba, pesa zinazochukuliwa kinyume na utaratibu haziachi 'trails' .

Kufungua account kutaacha trail katika transaction hivyo usitegemee kuiona acc

Ni kwa msingi huo wapo wanahoji pesa zilizopitia Ikulu kwa kuelewa hakuna audit
Kuhusu acc ninachosema ni kuwa hatuwezi kuzifikia ni account za watu au taasisi
Umma hautegemei CAG pekee kujua ufanisi wa Taasisi ya Serikali.
Ndio maana CAG wapo duniani, ni watalaam si kila Tom, Dick anbd Harry ni CAG
Kwahiyo unataka kusema Ukarabati hauna Tathimini? Hauna mipango? Umetokea wapi aisee?
Hapana hapa kuwa na utulivu unielewe. Construction, renovation , maintanance ni vitu tofauti na gharama zake zina vary pia.

Hapa kuna mahesabu kidogo nisingependa kukuumiza kichwa chako
Katika Lugha ya Kiswahili hakuna tofauti hiyo ya Masamiati wa Kujenga na Kukarabati.
Katika Ukarabati kuna Ujenzi sawa na kwa maradi mpya.
Mapungufu katika kiswahili hayabadili maana yake kama ilivyokusudiwa
Construction, renovation , maintanance.

Hapa sina ushauri zaidi ya kukutaka ufikiri katika umbali kidogo na ule wa pua, nina uhakika unaweza ! try. Anza na mita michache , km n.k.
Sasa ona unavyojichanganya, Yaani Mwinyi awe amekarabati, halufu JK awe amejenga kwa tafsiri hiyohiyo yako.
Yes Nyerere alifanya (construction) , AH Mwinyi akafanya ukarabati (maintanance)

Haya mambo ukiyasikia ghafla yanachanganya, kidogo kidogo nina uhakika utaelewa
Tunachokuambia iwe amekarabati au amejenga, hoja kuu NI MATUMIZI YA FEDHAZA UMMA. Wewe umeshikilia hakujenga amekarabati, hapo ndio tunapoona CHUKI YAKO.
Eeeh hapa ndipo hoja ilipo na ndio maana tunauliza 1.5T , 70 B na mauza uza tunayoyaona
Waziri Mkuu Majaliwa katueleza 'pesa zilivyotumika MSD' .
Of course kisicho na majibu kunazua ''chuki''.
Reli ya Kati MGR ipo kama ilivyo, na imekarabatiwa pia na Magufuli.
Well done! sasa unanena!
Hiyo added value imekuwa Constructed ili kufikiwa.
Added value katika SGR ipo, ni haraka na mzigo mkubwa kuliko mita reli.
Hatukupewa mkataba tuuone, lakini uzoefu wa nyuma unatuonesha utapeli wenu.
What? nawe unataka mkataba. Hivi si wewe uliyesema haya ''Kumbuka Mimi sio muumini wa Formalities za ajabuajabu''
Mimi sioni ajabu, kama tu Tija na Ufanisi utakuwepo. Kumbuka Mimi sio muumini wa Formalities za ajabuajabu.
Yes! watu wachote pesa tu ilimradi tuna ufanisi. Kwa mfano,tununue mfuko mmoja wa sementi 500,000 hakuna tatizo ilimradi tu daraja likamilike.
 
Back
Top Bottom