Milton Makongoro Mahanga alipata anguko kali katika kinyang'anyiro cha NEC wilaya ya Ilala. Anguko hili limekuja miaka miwili baada ya ushindi uliojaa utata wa ubunge katika jimbo la Segerea. Kwa anguko hili, Mahanga amedhihirisha kwamba hakubaliki wilayani kwao na kuna kila dalili kwamba hata ubunge alichakachua na isingekuwa mahakama zetu uchwara, bwana huyu angekuwa keshang'olewa na sasa anashinda sebuleni kwa Lowassa kumuimbia nyimbo anapouguza jicho lake.