Vitendo
JF-Expert Member
- Oct 23, 2009
- 582
- 103
FAULU wa kidato cha pili umeshuka kwa asilimia 8.3 mwaka jana, ikilinganishwa na mwaka juzi huku watahiniwa 671 wakifutiwa matokeo kwa udanganyifu.
Sababu zilizoelezwa kwa matokeo hayo mabovu, ni pamoja na uhaba wa walimu, ukosefu wa vitendea kazi na ubovu wa miundombinu ya kutolea elimu katika shule nyingi.
Naibu Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Mwantumu Mahiza alieleza hayo katika mkutano wake na waandishi wa habari uliofanyika ofisini kwake jijini Dar es Salaam jana.
Alisema idadi ya wanafunzi waliojisajili kufanya mtihani huo mwaka jana ilikuwa 394,508, kati yao wasichana walikuwa 167,961 sawa na asilimia 43 na wavulana 226,547 sawa na asilimia 57.
Alifahamisha kwamba, kati ya idadi hiyo; waliofanya mtihani walikuwa wanafunzi 364,957, wasichana 157,233 na wavulana 207,724, idadi ambayo ni sawa na asilimia 92.5.
Kwa mujibu wa Mwantumu, wanafunzi waliofaulu mtihani huo ni 238,267, wasichana 95,576 na wavulana 142,691.
Alisema wanafunzi walioshindwa mtihani huo ni 126,131 ambao ni sawa na asilimia 34.6. Wanafunzi ambao hawakufanya kabisa mtihani huo ni 29,547, wasichana 10,728 na wavulana 18,819.
"Kuna idadi kubwa ya wanafunzi ambao hawakufanya mitihani, hivyo tumewaagiza walimu wao kutoa taarifa juu ya wanafunzi hao ili tutafute njia ya kuwasaidia," alisema Mahiza.
Alisema wanafunzi wasichana walioshindwa mitihani hiyo ni 61,374 sawa na asilimia16.8 na wavulana ni 64,757 ambao ni sawa na asilimia 17.7.
Akilinganisha ufaulu huo na matokeo ya yaliyopita alisema: "Mwaka juzi matokeo yalionyesha kuwa watahiniwa 102,184 sawa na asilimia 26.5 ndio walioshindwa mitihani".
Alisema kutokana na matokeo hayo, ufaulu mwaka jana umeshuka na kufikia asilimia 65.3, ikilinganishwa na mwaka juzi.
Alisema katika mtihani wa mwaka jana kulikuwa na vituo 3726 ambavyo ni nyongeza ya vituo 218 ikilinganishwa na vituo vilivyosajiliwa mwaka juzi.
Waziri Mahiza alibainisha kwamba, wanafunzi waliofaulu kwa alama A, B na C walikuwa 88,636 na alama D ni 149,514.
Alieleza kuwa watahiniwa 671 sawa na asilimia 0.81, wamefutiwa mitihani kutokana na kufanya udanganyifu na uchunguzi juu ya tuhuma hizo bado unaendelea.
Alisema matokeo yameonyesha kuwa wanafunzi wengi wamefanya vizuri katika masomo ya Kiswahili, historia, uraia na jiografia na kufeli katika masomo ya Kiingereza na hisabati.
Alizitaja shule kumi bora katika mtihani huo kuwa ni Kibaha, Mzumbe, Ilboru, Tumaini, Msalato, Kilosa, Kilakala, Kwiro, Musoma Ufundi na Ihungo.
Mahiza alitaja shule za watu binafsi zilizofanya vizuri katika mitihani hiyo kuwa ni shule ya Feza ya Wavulana na Wasichana, St Francis, Thomas Moore, Don Bosco, Shule ya wasichana ya Marian, Sengerema, Qeen of Apostles, Mtakatifu Joseph Kilocha na Mafinga Seminari.
Alizitaja shule kumi za serikali zilizofanya vibaya zaidi katika mtihani huo kuwa ni Somangila, Uchindile, Tegetero, Mwanagati, Mole, Selembala, Mnolye, Igusule, Usunga na Kiningâila
Shule za watu binafsi zilizoingia kwenye orodha hiyo ni Ngateu,Olmotonyi, Tabata Wazazi, Nkuhungu, Dodoma Central, Africana, Uyui, Ujiji, Ali Hassan Mwinyi na Zunzuli.
Mahiza alisema kutokana na matokeo hayo, serikali imewaagiza wakuu wa shule zilizofanya vibaya katika mtihani huo kutoa maelezo ya sababu zilizohusishwa na tatizo hilo ifikapo Januari 31 mwaka huu.
Alisema wizara iko kwenye mchakato wa kutatua changamoto zinazoikabili sekta ya elimu ikiwemo ya kuongeza idadi ya walimu katika shule za kata, kutengeneza maabara za kisasa na kuboresha mazingira ya shule zake ili waweze kuongeza ufaulu, hasa katika masomo ya sayansi, hisabati ambayo wanafunzi wengi wanafeli.
Sababu zilizoelezwa kwa matokeo hayo mabovu, ni pamoja na uhaba wa walimu, ukosefu wa vitendea kazi na ubovu wa miundombinu ya kutolea elimu katika shule nyingi.
Naibu Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Mwantumu Mahiza alieleza hayo katika mkutano wake na waandishi wa habari uliofanyika ofisini kwake jijini Dar es Salaam jana.
Alisema idadi ya wanafunzi waliojisajili kufanya mtihani huo mwaka jana ilikuwa 394,508, kati yao wasichana walikuwa 167,961 sawa na asilimia 43 na wavulana 226,547 sawa na asilimia 57.
Alifahamisha kwamba, kati ya idadi hiyo; waliofanya mtihani walikuwa wanafunzi 364,957, wasichana 157,233 na wavulana 207,724, idadi ambayo ni sawa na asilimia 92.5.
Kwa mujibu wa Mwantumu, wanafunzi waliofaulu mtihani huo ni 238,267, wasichana 95,576 na wavulana 142,691.
Alisema wanafunzi walioshindwa mtihani huo ni 126,131 ambao ni sawa na asilimia 34.6. Wanafunzi ambao hawakufanya kabisa mtihani huo ni 29,547, wasichana 10,728 na wavulana 18,819.
"Kuna idadi kubwa ya wanafunzi ambao hawakufanya mitihani, hivyo tumewaagiza walimu wao kutoa taarifa juu ya wanafunzi hao ili tutafute njia ya kuwasaidia," alisema Mahiza.
Alisema wanafunzi wasichana walioshindwa mitihani hiyo ni 61,374 sawa na asilimia16.8 na wavulana ni 64,757 ambao ni sawa na asilimia 17.7.
Akilinganisha ufaulu huo na matokeo ya yaliyopita alisema: "Mwaka juzi matokeo yalionyesha kuwa watahiniwa 102,184 sawa na asilimia 26.5 ndio walioshindwa mitihani".
Alisema kutokana na matokeo hayo, ufaulu mwaka jana umeshuka na kufikia asilimia 65.3, ikilinganishwa na mwaka juzi.
Alisema katika mtihani wa mwaka jana kulikuwa na vituo 3726 ambavyo ni nyongeza ya vituo 218 ikilinganishwa na vituo vilivyosajiliwa mwaka juzi.
Waziri Mahiza alibainisha kwamba, wanafunzi waliofaulu kwa alama A, B na C walikuwa 88,636 na alama D ni 149,514.
Alieleza kuwa watahiniwa 671 sawa na asilimia 0.81, wamefutiwa mitihani kutokana na kufanya udanganyifu na uchunguzi juu ya tuhuma hizo bado unaendelea.
Alisema matokeo yameonyesha kuwa wanafunzi wengi wamefanya vizuri katika masomo ya Kiswahili, historia, uraia na jiografia na kufeli katika masomo ya Kiingereza na hisabati.
Alizitaja shule kumi bora katika mtihani huo kuwa ni Kibaha, Mzumbe, Ilboru, Tumaini, Msalato, Kilosa, Kilakala, Kwiro, Musoma Ufundi na Ihungo.
Mahiza alitaja shule za watu binafsi zilizofanya vizuri katika mitihani hiyo kuwa ni shule ya Feza ya Wavulana na Wasichana, St Francis, Thomas Moore, Don Bosco, Shule ya wasichana ya Marian, Sengerema, Qeen of Apostles, Mtakatifu Joseph Kilocha na Mafinga Seminari.
Alizitaja shule kumi za serikali zilizofanya vibaya zaidi katika mtihani huo kuwa ni Somangila, Uchindile, Tegetero, Mwanagati, Mole, Selembala, Mnolye, Igusule, Usunga na Kiningâila
Shule za watu binafsi zilizoingia kwenye orodha hiyo ni Ngateu,Olmotonyi, Tabata Wazazi, Nkuhungu, Dodoma Central, Africana, Uyui, Ujiji, Ali Hassan Mwinyi na Zunzuli.
Mahiza alisema kutokana na matokeo hayo, serikali imewaagiza wakuu wa shule zilizofanya vibaya katika mtihani huo kutoa maelezo ya sababu zilizohusishwa na tatizo hilo ifikapo Januari 31 mwaka huu.
Alisema wizara iko kwenye mchakato wa kutatua changamoto zinazoikabili sekta ya elimu ikiwemo ya kuongeza idadi ya walimu katika shule za kata, kutengeneza maabara za kisasa na kuboresha mazingira ya shule zake ili waweze kuongeza ufaulu, hasa katika masomo ya sayansi, hisabati ambayo wanafunzi wengi wanafeli.