ANGOLA: Mwili wa Jonas Savimbi kufukuliwa ili upate maziko mazuri

Influenza

JF-Expert Member
Jul 1, 2018
1,445
3,403
Mwili wa aliyekuwa kiongozi wa waasi nchini Angola Jonas Savimbi utafukuliwa kabla ya mwisho wa mwaka huu ili apate kupewa maziko mazui, kwa mujibu wa chama chake cha Unita kilichonukuliwa na shirika la habari la AFP.

Savimbi aliuawa na vikosi vya serikali tarehe 22 Februari mwaka 2002 na kuzikwa siku iliyofuatia kwenye mkoa ulio mashariki wa Moxico.

Wiki sita baadaye Unita walisaini makubaliana ya amani na serikali na kumaliza vita vya wenyewe kwa wenyewe vya miaka 27.

Kiongozi wa sasa wa chama cha Unita Isaias Samakuva, alitangaza kuwa mwili wa Savimbia utafukuliwa baada ya kukutana na rais Joao Lourenco kwenye mji mkuu Luanda siku ya Jumatano.

Mapema mwezi huu aliilaumu serikali kwa kumnyima Savimbi maziko Mazuri.

Jonas Savimbi ni nani?

Jonas Savimbi alizaliwa tarehe 3 Agosti mwaka 1934 huko Munhango mkoa wa Bié, mji mdogo kwenye reli ya Benguela na kulelewa Chilesso mkoani humo.

Alikuwa kiongozi wa siasa kisa kwa siaia na jeshi mabaye laizniajsa na kuongoza chama cha cha National Union for the Total Independence of Angola (UNITA).

UNITA kwanza waliendesha vita vya msituni dhidi ya utawala wa wareno kati ya mwaka 1966 na 1974 na kisha kikapigana na chama cha People's Movement for the Liberation of Angola (MPLA) wakati wa vita vya wenyewe kwa wenyewe hadi wakati wa kifo cha Savimbi kwenye mapigano na vikosi vya serikali mwaka 2002.

Utotoni mwake Savimbi alisemea shule za kiprotestanti lakini pia na kwenye shule za kikatoliki.

Akiwa na umri wa miaka 24 alipata msaada wa kwenda kusomea nchini Ureno. Huko alimaliza masomo ya sekondari.

Baadaye alikuja kuwa na uhusino na wanafunzi kutoka Angola na koloni zingine za Ureno ambao walikuwa wanajiandaa kuanzisha vita dhidi ya ukoloni na kufanya pia urafiki na chama cha kikomunisti nchini Ureno.

Alijuana na Agostino Neto ambaye wakati huo alikuwa akisomea udaktari na ambaye alikuja kuwa kuwa rais wa chama cha MPLA na rais wa kwanza wa Angola.

Chanzo: BBC Swahili
IMG_20180817_082540.jpg
IMG_20180817_082436.jpg
 
Hao ndio walikua wanaume. na upinzani wa tanzania ujifunze kwa watu kama wakina savimbi. Waachane ule ujinga ujinga wakusema mandela alikaa miaka 27
Gerezani na akatoka akaja kuwa rais. Na wakati huo juzi tu hapo mbowe pasaka alichezea gerezani alinvyotoka sio kwa kulalamika kule. na akaacha kujiuliza je mandela ktk hiyo miaka 27 alipitwa na siku kuu ngapi?
 
Hao ndio walikua wanaume? na upinzani wa tanzania ujifunze kwa watu kama wakina savimbi. Waachane ule ujinga ujinga wakusema mandela alikaa miaka 27
Gerezani na akatoka akaja kuwa rais. Na wakati huo juzi tu hapo mbowe pasaka alichezea gerezani alinvyotoka sio kwa kulalamika kule. na akaacha kujiuliza je mandela ktk hiyo miaka 27 alipitwa na siku kuu ngapi?

Duuuh kipindi kile Kulikuwa na Vita Baridi alipata Back up kutoka kwa USA wakati ule Utawala wa Angola ulikuwa chini ya USSR kwa sasa HAIWEZEKANI!
 
Hao ndio walikua wanaume? na upinzani wa tanzania ujifunze kwa watu kama wakina savimbi. Waachane ule ujinga ujinga wakusema mandela alikaa miaka 27
Gerezani na akatoka akaja kuwa rais. Na wakati huo juzi tu hapo mbowe pasaka alichezea gerezani alinvyotoka sio kwa kulalamika kule. na akaacha kujiuliza je mandela ktk hiyo miaka 27 alipitwa na siku kuu ngapi?
mwisho wake aliuawa na kuburuzwa barabarani
 
Hao ndio walikua wanaume? na upinzani wa tanzania ujifunze kwa watu kama wakina savimbi. Waachane ule ujinga ujinga wakusema mandela alikaa miaka 27
Gerezani na akatoka akaja kuwa rais. Na wakati huo juzi tu hapo mbowe pasaka alichezea gerezani alinvyotoka sio kwa kulalamika kule. na akaacha kujiuliza je mandela ktk hiyo miaka 27 alipitwa na siku kuu ngapi?
mwisho wake aliuawa na kuburuzwa barabarani
 
mwisho wake aliuawa na kuburuzwa barabarani
Hata kama alibuluzwa sio mbaya cha msingi yeye alitimiza malengo yake. na huenda hapa tanzania angetokea mtu kama savimbi labda tanzania ingekuwa mbali sana. Kwa sababu hata mandela mwenyewe amewahi kuitwa gaidi.
 
Ahsante mno mtoa uzi huu,tatizo kubwa tunalokabiliwa nalo sisi wachangiaji ni uvivu wa kusoma upande wa pili wa story(every story ina side mbili),au ushabiki wetu tuliokuwa nao wa kuuona ukweli bali tunapinga for the sake ya kupinga tu,kulishwa taarifa zisizo za ukweli na wanasiasa wetu uchwara kwa masilahi yao binafsi,JONAS MALHEIRO SAVIMBI alikuwa mmoja wa mwanasiasa,mwanajeshi mahiri sana aliyetoa mchango mkubwa kwa uhuru wa nchi yake ya Angola,alikuwa jemedari mzuri katika uwanja wa medani and he died fighting kwa kitu alichokiamini,mara baada ya uchaguzi mkuu kufanyika baada ya mapatano na vyama vingine including MPLA ,na uchaguzi ule kugubikwa na mizengwe(HILI LIPO WAZI KWA VYAMA HIVI TAWALA),aliamua kuendeleza mapamabano hadi alipouawa kwenye mapambano,kumbuka alileta mgawanyiko wa kiitikadi katika vita ya Angola kati ya president Kaunda na president Nyerere;msome zaidi kwenye kitabu cha JONAS SAVIMBI,A KEY TO AFRICA by Fred Bridgland(the story behind the battle of Angola).
 
Jonas Savimbi, alikuwa msomi wa udaktari Doctor of Medicine aliyesomea kule Ureno enzi hizo. Pamoja na ukweli kuwa akina Savimbi na Unita yao ndio haswa waliopigania uhuru wa Angola kutoka kwa mkoloni Mreno lkn, Unfortunately, wakati wa kutolewa uhuru ni MPLA ndio walioukwaa utawala kwani wao walikuwa mji mkuu Luanda wakati akina Savimbi walikuwa mbali porini.

Kitendo hicho kiliwaudhi Unita na matokeo yake wakaanzisha vita vikali dhidi ya serikali ya Mpla iliyodumu kwa miongo kadhaa.

Savimbi alikuwa mwanasiasa mahiri na jasiri sana na pia "Very articulate orator", na alikuwa na kipaji cha kushawishi akiwa pia na uwezo wa kuongea kwa ufasaha lugha kuu nne za Ulaya.

Savimbi pia alikuwa ni mtu asiyependa kuburuzwa na ukweli huo ndio ulifanya wakosane na serikali ya Mpla pale alipokuwa makamu wa rais kwa muda mfupi mwanzoni mwa miaka ya tisini kabla hajarejea tena msituni.
 
Ahsante mno mtoa uzi huu,tatizo kubwa tunalokabiliwa nalo sisi wachangiaji ni uvivu wa kusoma upande wa pili wa story(every story ina side mbili),au ushabiki wetu tuliokuwa nao wa kuuona ukweli bali tunapinga for the sake ya kupinga tu,kulishwa taarifa zisizo za ukweli na wanasiasa wetu uchwara kwa masilahi yao binafsi,JONAS MALHEIRO SAVIMBI alikuwa mmoja wa mwanasiasa,mwanajeshi mahiri sana aliyetoa mchango mkubwa kwa uhuru wa nchi yake ya Angola,alikuwa jemedari mzuri katika uwanja wa medani and he died fighting kwa kitu alichokiamini,mara baada ya uchaguzi mkuu kufanyika baada ya mapatano na vyama vingine including MPLA ,na uchaguzi ule kugubikwa na mizengwe(HILI LIPO WAZI KWA VYAMA HIVI TAWALA),aliamua kuendeleza mapamabano hadi alipouawa kwenye mapambano,kumbuka alileta mgawanyiko wa kiitikadi katika vita ya Angola kati ya president Kaunda na president Nyerere;msome zaidi kwenye kitabu cha JONAS SAVIMBI,A KEY TO AFRICA by Fred Bridgland(the story behind the battle of Angola).
Mhhh. Are we talking about the same Savimbi? The leader of UNITA? Au tunaongelea mtu mwingine? Savimbi huyu ambae aliongoza majeshi yake kutokea South Africa, ambapo waafrika walikuwa wanaishi kwenye zile Bantustans? Na Papa Mandela kafungwa kwa zaidi ya miaka 30? Makaburu walikuwa wanalaaniwa na kutengwa na dunia nzima, lakini Savimbi ndio alikuwa kibaraka wao. Ndio unasema alikuwa great leader?
 
Back
Top Bottom