#COVID19 Angekubali Chanjo na kuchukua tahadhari mapema, mpaka leo huenda tungekuwa naye

Umerudi mwanzo.

Maamuzi JPM: Kupima mapapai na kuyakuta na corona, kutangaza corona hakuna, kusisitiza umuhimu wa tiba mbadala n.k

Maamuzi samia: Kuchanja, kusisitiza watu wachanje.

Upimaji wa madhara na faida za maamuzi ya viongozi hawa wawili ni juu yako na uwezo wako wa upambanuaji mambo.
Sasa kama matokeo ya maamuzi yote ni the same kuna kipi kipya?
 
tangu aondoke nchi imekuwa shwari....limebaji tu bunge lake la ccm 100%
Nchi imekuwa shwari wakati tunaona watu wanaamua hadi kujitoa muhanga kama Hamza na wengine wapo jela kwa kesi za ugaidi, sasa sijui ushwari upi huo unaouzungumzia wewe?
 
Kumbe alikufa kwa huo ugonjwa mkakati wenu? Wenzio tulijua mmemuua ili mpore mali zetu, wizi na ugaidi virudi kwa kasi. Ili rushwa irudi, ili tusijione tunaweza bila mikopo ya "kifara" n.k kumbe hamkuwa nyie. Lakini mbona covid ilivyomuua ndo hvyo vitu navyo vikajitokeza ama ni coincedences tu? Kwa maneno tunawaelewa japo kidogo ila kwa matendo yenu hamfai kokote pale
 
Sasa kama matokeo ya maamuzi yote ni the same kuna kipi kipya?
Sijakuambia matokeo ya maamuzi ni the same, nimesema upimaji wa matokeo, madhara au faida inategemeana na uwezo wako wa kupambanua mambo.
 
Tupate funzo kupitia hili, Sio kwamba unapokua mkubwa kifedha/kimadaraka ni unaona kila mtu unamzidi akili, hapana Mungu alituumba akatupa akili akatubariki akatufanya tuishi kwa kutegemeana ili kutatua mambo mbali mbali ya duniani.

Mungu akawabariki wataalamu mbalimbali, watabibu, waalimu, wahasibu, wanajeshi, wanasayansi, wakulima, wafanyabiashara, wavuvi, wanamichezo nk.

Hawa wote tunaishi kwa kutegemeana ili maisha yasonge, mimi muhasibu nikiugua nitaenda kwa mtabibu, mwanajeshi akitaka kula ataenda kwa mkulima, mwanasiasa akitaka haki ataenda kwa wanasheria wamsaidie, mwalimu akipata tatizo la kiusalama ataenda polisi, polisi akitaka elimu atarudi kwa mwalimu, hivyohivyo kwa wote.

Inapotokea wewe umewadharau wenzio na kuona unaakili kuliko wote ndugu yangu unajidanganya.

Matabibu wamekwambia ukiwa na ugonjwa sugu tafadhari zingatia miongozo kwa usahihi maana upo kwenye risk kubwa, wewe kwa kiburi chako ukaona unacheo kikubwa na kuwadharau wengine ukijiona umewazidi akili matokeo yake utayaona.

Wewe mmoja huwezi kuwa mkemia, ukawa mtabibu, ukawa mwalimu, ukawa mchungaji, ukawa mfamasia, ukawa mwanasaikolojia tafadhali heshimu kada za wengine.

Ndugu yangu kufa kupo lakini na kufa kijinga kupo,
bibilia inasema usiwe mjinga kupita kiasi ukafa kabla ya siku zako

Mhubiri 7:17
Usiwe mwovu kupita kiasi;
Wala usiwe mpumbavu;
Kwani ufe kabla ya wakati wako?


Kwa maana hiyo ni kwamba sio kila mtu anaekufa basi ni wakati wake, wengine hufa kabla ya wakati kwa upumbavu.

Pengine ungeheshimu taaluma za watu ukachukua tahadhari mpaka leo tungekua pamoja tukiijenga Tanzania Mama,

Dharau na kibuli havijawai kumuacha mtu salama tangu kuumbwa kwa misingi ya ulimwengu huu

View attachment 1924317

mkuu na wewe unaamini meko alikufa corona?
 
Kama kipo kilichobadirika kwa nini usiweke hapa ili kunitoa ujinga?
Masuala ya ujinga mbona mm sijayazungumzia popote?
Nimesema uwezo wako wa kupambanua mambo ndo umekufanya uhitimishe kuwa samia na jpm hawana tofauti katika mtazamo wa covid. Sijatoa maoni yoyote juu ya kiwango cha uwezo wako wa kupambanua mambo.
 
Huu ndio ukweli na alisababisha wengi sana kufa kwa misimamo yake ya kijinga na kiwendawazimu.
waliochanjwa mpk saiv ni chin ya watu laki 4 kat ya mil 60,,ko hao watu laki tatu walio chanjwa ndo wamesababish watu wasife?.... mbona unandik upuuzi,,bila shaka na ww umechanja,, waliochanja tumeshaanza kuwashtukia,, kiufahamu wenu mnakurupuka tu..
 
Mkuu... huyu Mjomba alikua sahihi zaidi ya asilimia 70%! Na alikua na dhamira ya dhati kabisa na hii nchi.

Uchanga wa taifa ndio uliomuangusha, kuzielewa baadhi ya harakati hapa duniani inahitaji exposure na upeo wa kiwango cha maglev.

Sie wengine tusubili tu hadi wakati ufike, ni mapema sana kumjaji tutamuelewa tu.
 
Masuala ya ujinga mbona mm sijayazungumzia popote?
Nimesema uwezo wako wa kupambanua mambo ndo umekufanya uhitimishe kuwa samia na jpm hawana tofauti katika mtazamo wa covid. Sijatoa maoni yoyote juu ya kiwango cha uwezo wako wa kupambanua mambo.
Wewe uwezo wako wa kupambunua mambo umekufikisha kwenye hitimisho lipi?
 
Back
Top Bottom