Mzee Mwanakijiji
Platinum Member
- Mar 10, 2006
- 33,463
- 39,929
Tunataka kutetea demokrasia na utawala wa demokrasia, hivyo hatuwezi kuwa wa kwanza kupendekeza njia zisizo za kidemokrasia kushughulikia matatizo ya kidemokrasia. Tupo ambao tumechukizwa, kukerwa na kuumizwa na jinsi ambavyo matokeo ya uchaguzi mkuu katika ngazi zote yalivyotolewa na yanavyoendelea kutolewa na hasa mahali tulipofikia vijana wetu kulazimika "kulinda kura". Wapo ambao wanaona kabisa kuwa baadhi ya watu waliotangazwa au watakaotangazwa washindi wamekosa uhalali wa nafasi hizo.
Pamoja na ukweli wa hilo siku za karibuni kuanzia mvurugano wa Tume na Matokeo ya Uchaguzi nimefuatilia wapo watu wamejiunga ghafla ghafla au wengine wa muda kidogo ambao wamekuja na siasa kali za kutaka kutumia JF kama jukwaa la kuanzishia itikadi ya nguvu dhidi ya utawala wa kisiasa (violence against public officials).
Mimi binafsi nikiwa ni muumini wa nadharia ya nguvu ya hoja siungi mkono hoja za nguvu kwani katika kutumia hoja za nguvu kunathibitisha kuwa umeshindwa kutumia nguvu za hoja kuweza kuwashawishi watu wengine. Lakini ukweli ni kwamba, hadi hivi sasa tumeweza kwa kutumia hoja tu kujenga hoja na kuwashawishi mamilioni ya Watanzania kuchagua mabadiliko. Hatuna sababu ya kubadili mbinu hiyo sasa hata kama tunajisikia hasira kiasi gani.
Binafsi napinga na kulaani vikali kauli zinazotolewa aidha kama entrapment ya JF au kutoka moyoni kweli yenye kuashiria kuwa ni bora kutumia nguvu kuweza kupata matokeo ya kisiasa. Tulipoanza JF miaka michache iliyopita hatukujua kuwa uongozi wa kisiasa ungekuwa ulivyo, lakini tumeweza kupita katika misukosuko mingi ya kitaifa na tumeweza kufika leo tumeshuhudia mabadiliko makubwa na ushindi usiokadirika wa upinzani Tanzania na hivyo kusababisha malango yaliyofungwa kuachia. Huu ni ushindi wa hoja si vitisho.
Kama kundi ambalo baadhi yetu tunajiita au tunaitwa wasomi, ni lazima tuwe tayari kutetea hoja zetu nakutumia ushawishi wa hoja kuweza kupata matokeo ya kisiasa. Ninachosema ni kuwa tuwakatae kwa hoja wale wote wenye kujaribu kutushawishi au kutoa kauli za matumizi ya nguvu kama "laiti ningekuwa sniper", "tuwapige risasi"n.k ili waone kama kuna watu wataunga mkono - na inasikitisha wapo wanaounga mkono.
Kwa kufanya hivyo, tunaweka mtandao wetu tuupendao hatarini kwani kikiwa ni chombo kilichoandikishwa na licha ya watu kutumia majina mbadala endapo jambo fulani linatokea mtandao huu una wajibu wa kushirikiana na vyombo vya kiusalama kutekeleza amri halali ya mahakama kuweza kuwapata wahusika. Sasa tusichukulie kimzaha tunapotoa kauli zenye mfanano wa vitisho, kauli hizo hazilindwi na "uhuru wa maoni" kwani ni kama ilivyosema "kupiga kelele moto, kwenye ukumbi uliojaa".
Hivyo, kwa wale ambao tumekasirishwa sana na matokeo, tujitoe zaidi kujipanga katika vyama tunavyovitaka au kushiriki kuunga mkono au kuwasaidia wagombea waliochakachuliwa matokeo yao. Mtu akitoa kauli yenye mwelekeo wa vitisho kwa viongozi wa umma - haijalishi kama ni wa chama tawala au upinzani - nawaomba tuflag comment hiyo na kuwataarifu ma MOD mara moja. Tusidhania MODs wanasoma kila sentensi ya kila thread ya kila mtu kila siku. Tuwe walinzi wa forum yetu sisi wenyewe kwani ninaamini katika siku zijazo tutahitaji chombo hiki kuendelea kuwepo.
Tukumbuke kuwa ufisadi bado upo, mgongano ndani ya CCM upo na changamoto mbalimbali za kitaifa bado zipo. Hivyo, ni kwa maslahi yetu sisi wenyewe wanachama, wageni, na mashabiki kuulinda mtandao huu kutoka kwa watu ambao wengine naamini ni political operatives wa baadhi ya watu ambao kazi yao ni kupandikiza hoja za kichochezi ili JF itajwe (kama mnakumbuka Feb 2008) kuwa ni mtandao wa kighaidi au kichochezi. Maana ikifanyika hivyo wengi hutimka na kukaa pembeni huku wachache vichwa vyao vikiwekwa katika kamba za wanyongaji.
Tujiwajibishe wenyewe, tuilinde forum yetu..
Napendekeza.
Pamoja na ukweli wa hilo siku za karibuni kuanzia mvurugano wa Tume na Matokeo ya Uchaguzi nimefuatilia wapo watu wamejiunga ghafla ghafla au wengine wa muda kidogo ambao wamekuja na siasa kali za kutaka kutumia JF kama jukwaa la kuanzishia itikadi ya nguvu dhidi ya utawala wa kisiasa (violence against public officials).
Mimi binafsi nikiwa ni muumini wa nadharia ya nguvu ya hoja siungi mkono hoja za nguvu kwani katika kutumia hoja za nguvu kunathibitisha kuwa umeshindwa kutumia nguvu za hoja kuweza kuwashawishi watu wengine. Lakini ukweli ni kwamba, hadi hivi sasa tumeweza kwa kutumia hoja tu kujenga hoja na kuwashawishi mamilioni ya Watanzania kuchagua mabadiliko. Hatuna sababu ya kubadili mbinu hiyo sasa hata kama tunajisikia hasira kiasi gani.
Binafsi napinga na kulaani vikali kauli zinazotolewa aidha kama entrapment ya JF au kutoka moyoni kweli yenye kuashiria kuwa ni bora kutumia nguvu kuweza kupata matokeo ya kisiasa. Tulipoanza JF miaka michache iliyopita hatukujua kuwa uongozi wa kisiasa ungekuwa ulivyo, lakini tumeweza kupita katika misukosuko mingi ya kitaifa na tumeweza kufika leo tumeshuhudia mabadiliko makubwa na ushindi usiokadirika wa upinzani Tanzania na hivyo kusababisha malango yaliyofungwa kuachia. Huu ni ushindi wa hoja si vitisho.
Kama kundi ambalo baadhi yetu tunajiita au tunaitwa wasomi, ni lazima tuwe tayari kutetea hoja zetu nakutumia ushawishi wa hoja kuweza kupata matokeo ya kisiasa. Ninachosema ni kuwa tuwakatae kwa hoja wale wote wenye kujaribu kutushawishi au kutoa kauli za matumizi ya nguvu kama "laiti ningekuwa sniper", "tuwapige risasi"n.k ili waone kama kuna watu wataunga mkono - na inasikitisha wapo wanaounga mkono.
Kwa kufanya hivyo, tunaweka mtandao wetu tuupendao hatarini kwani kikiwa ni chombo kilichoandikishwa na licha ya watu kutumia majina mbadala endapo jambo fulani linatokea mtandao huu una wajibu wa kushirikiana na vyombo vya kiusalama kutekeleza amri halali ya mahakama kuweza kuwapata wahusika. Sasa tusichukulie kimzaha tunapotoa kauli zenye mfanano wa vitisho, kauli hizo hazilindwi na "uhuru wa maoni" kwani ni kama ilivyosema "kupiga kelele moto, kwenye ukumbi uliojaa".
Hivyo, kwa wale ambao tumekasirishwa sana na matokeo, tujitoe zaidi kujipanga katika vyama tunavyovitaka au kushiriki kuunga mkono au kuwasaidia wagombea waliochakachuliwa matokeo yao. Mtu akitoa kauli yenye mwelekeo wa vitisho kwa viongozi wa umma - haijalishi kama ni wa chama tawala au upinzani - nawaomba tuflag comment hiyo na kuwataarifu ma MOD mara moja. Tusidhania MODs wanasoma kila sentensi ya kila thread ya kila mtu kila siku. Tuwe walinzi wa forum yetu sisi wenyewe kwani ninaamini katika siku zijazo tutahitaji chombo hiki kuendelea kuwepo.
Tukumbuke kuwa ufisadi bado upo, mgongano ndani ya CCM upo na changamoto mbalimbali za kitaifa bado zipo. Hivyo, ni kwa maslahi yetu sisi wenyewe wanachama, wageni, na mashabiki kuulinda mtandao huu kutoka kwa watu ambao wengine naamini ni political operatives wa baadhi ya watu ambao kazi yao ni kupandikiza hoja za kichochezi ili JF itajwe (kama mnakumbuka Feb 2008) kuwa ni mtandao wa kighaidi au kichochezi. Maana ikifanyika hivyo wengi hutimka na kukaa pembeni huku wachache vichwa vyao vikiwekwa katika kamba za wanyongaji.
Tujiwajibishe wenyewe, tuilinde forum yetu..
Napendekeza.