Angalia nchi inavyoongozwa kwa freestyle na imla

moto wa maji

JF-Expert Member
Mar 25, 2016
4,077
2,882
Habari wakuu,

Siku zinavyokwenda katika nchi yetu ya Tanzania tunaona viongozi wetu wanavyokua wanachukua maamuzi mbalimbali ili nchi iweze kujikwamua ilipo na kupiga hatua kwenda juu zaidi ili wananchi wanufaike.

Lakini viongozi hao wengi wao hawajipangi kutatua tatizo ila wanazua tatizo lingine kwa kuongoza wananchi kwa mfumo wa Imla inayosomwa haraka haraka na hakuna muda wa marudio.

Yaani wananchi hawajui kinachoendelea kwani hata viongozi wanapokua wanaongea inaonyesha hawajajipanga kuongea wanakua wanafanya freestyle yani lolote linalokuja mdomoni wanaongea liwe baya twende au liwe zuri twende.
 
haijalishi umeanza kujua lini ila lini ulianza kuchukua hatua kujiondoa kwenye utumwa wa kifikra
 
Back
Top Bottom