Anga la washenzi na Joana anaona kitu usiku

ANGA LA WASHENZI II --- 78


Simulizi za series



ILIPOISHIA


Wakatupiana mikono, ila wote wakafanya ustadi kujilinda. Wakakaa tenge kutazamana kana kwamba majogoo. Kamanda akauliza, “So you are the dangerous one?”


Jona hakujibu akamvamia. Alikuwa hana muda. Alikuwa anakimbizana na muda na mpaka muda huo alikuwa amebakiza dakika kumi na mbili tu.


ENDELEA


Wakatupiana makonde ya nguvu. Wote walikuwa wana nguvu za kupambana na ustadi wa aina yake. Ilikuwa ni mapambano ya mafahali wawili ambayo yaliumiza majani. Waliparangana kwa muda wa dakika kadhaa asionekane nani aliye mwamba. Wakasimama tena kutazamana.


“Anything left?” akauliza yule kamanda. Jona akatazamia muda. Sasa amebaki na dakika tano tu! Akapiga kelele kwanguvu na kumvamia kamanda kwa mashambulizi makali.


Kamanda akajizuiza, akatupa pia na yake, Jona akajikinga na upesi akambana kamanda miguu kumwangusha chini. Kabla kamanda hajafurukuta, Jona akawahi kunyanyua silaha na kumtwanga nayo risasi tatu kifuani! Kamanda akaenda na ubabe wake.


Jona akamkagua na kuchukua kila alichokiona kinastahili alafu akaanza kukimbia kwenda kuikuta boti waliyomo wenzake.


Kupiga hatua mbili, akadakwa mguu na kuanguka chini. Kumbe kulikuwa na adui mmoja aliyebakia na uhai. Aling’ang’ania mguu wa Jona na upesi akavuta silaha yake iliyokuwa pembeni apate kumuua, ila Jona kwa haraka akatumia mguu wake uliokuwa huru, akatengua mkono wa adui uliobebelea bunduki na kisha akammaliza mtu huyo kwa kummiminia risasi nne za uhakika.


Akanyanyuka na kuendelea kukimbia kwa kasi. Sasa alikuwa amebakiza dakika mbili tu kwenye muda wake. Hakutazama nyuma wala pembeni bali mbele aelekeapo!



**



“Tuondoke,” alisema Lee akimtazama Miranda aliyekuwa anaangalia msitu wa kisiwa.


“Hapana,” Miranda akatikisa kichwa. “Hatuwezi kuondoka tukamwacha.”


“Alisema ikifika daki ya arobaini na tano twende kama atakuwa hajafika,” Lee akakumbushia. Japo uso wake nao ulikuwa na huzuni kuyasema haya.


“Najua alisema hivyo, ila hatutaondoka pasipo yeye,” Miranda akasisitizia. Muda si mrefu macho yake yakaanza kujawa na machozi. Jicho lake la kushoto likadondosha maji.


“Najua atarudi,” akasema kwa sauti ya chini. Alikuwa anatazama miti kama vile mtu asomaye ramani. “Najua hatafia huko … atarudi tu.” akamtazama Lee na kumwambia, “Atarudi, si ndio?”


Lee akashusha pumzi ndefu. Akatazama saa ya mkono wake, ilikuwa ni dakika ya sitini sasa na Jona hajaonekana. Akakosa cha kusema.


“Atarudi, si ndio?” Miranda akauliza tena akiwa ameng’ata meno. “Na kama hatorudi, basi hapahapa nitawangoja waliomuua na kuwaadhibu.”


Wakakumbatiana Miranda akiegamisha kichwa chake kwenye bega la Lee. Machozi yaliendelea kumtoka. Hakuwa anataka kuamini kwamba msitu ule umemmeza Jona.


Basi punde wakiwa vivyo wamekumbatiana, wakasikia sauti, “Heey!”


Miranda akasema, “ni Jona!” akaangaza kule msituni na akamwona mwanaume akiwa anakuja akikimbia, mikononi mwake alikuwa amebebelea mwili wa Raisi. Akamtazama Lee kwa furaha kubwa na kumwambia tena. “Ni Jonaa!”


Basi wakaruka na kwenda kumlaki, Lee akapokea mwili wa Raisi na kuutanguliza botini. Miranda akafurahi sana kumwona Jona, hata akambusu mwanaume huyo shavuni na kumwambia, “Nilijua utarudi tu,” akasema akiwa na tabasamu pana. Akamkumbatia tena Jona kabla hawajakwenda botini.


“Umepata kitu?” Lee akamuuliza.


“Nimepata kila kitu,” Jona akajibu. “Sasa ni muda wa kwenda kumaliza kazi.”


Basi wakatia moto boti na kuondoka zao. Wakiwa njiani Jona akawasiliana na makao makuu na taarifa ikawa ni kwenda kwenye ‘bay’ kama ilivyokuwa awali. Huko watakutana na ‘helicopter’ ya kuwachukua na kuwarejesha makaoni.


Basi safari yao ikadumu kwa mwendo wa saa moja na nusu mpaka kufika ‘bay’ ya barafu kuu. Hapo kulikuwa na wanaume wawili ndani ya helicopter ambao walikuwa wanawangoja.


Basi kwakuwa haikutakiwa wanaume hao wagundue mapema kuwa si wenyewe waliokuja hapo, wakawataarifu kwa njia ya mawasiliano kuwa kuna majeruhi wa kuja kuwasaidia kuwabeba, hivyo waje kuwapatia mkono.


Wanaume wale wakashuka pasi na hiyana na kusonga kwenye boti. Tena walikuwa hawana hata silaha mikononi mwao. Wakajikuta wakiwekwa chini ya ulinzi na kuamriwa waanike mikono yao juu upesi! Kwa woga wakatii amri. Lee na Miranda wakawaswaga kwenda kwenye helicopter wakimwacha Jona peke yake na wale makomandoo.


“Nadhani sasa mtarudi nyumbani kupeleka mwili wa mheshimiwa. Sisi tunaenda England kumaliza mzizi wa yote haya,” Jona aliwaambia wale makomandoo, watatu kwa idadi, watano wakiwa waliuawa kule msituni.


“Tumekubaliana ataenda huko mmoja, na sisi wawili tutaongozana na nyinyi kwenda huko kupambana,” akasema yule kamanda wa kile kikosi cha makomandoo.


Basi kwakuwa tayari ndege yao iliyokuwa inawasiliana nayo ilikuwa njiani, wakawasiliana nayo kuwaelekeza walipo, kisha walipofanya hivyo makomandoo wawili wakaondoka na wakina Jona wakitumia ile helicopter waliyoiteka. Wakadaka anga kwenda kuwatafuta na kuwamaliza washenzi.



**



Saa tano asubuhi …



Baada ya mlango kufunguka, walitangulia wanaume wawili ambao ni wale waliokuwa madereva wa ile helicopter iliyotekwa. Wanaume hawa wazee waliokuwa wamevalia makoti meusi ya ngozi na jeans zilikoza kwa rangi ya bluu, walikuwa wamenyoosha mikono juu na nyuso zao zikiwa zimejawa na hofu.


Nyuma yao alikuwapo Jona na wenzake, Miranda, Lee na Makomandoo wawili. Basi wakaketi na Jona akawauliza wale mateka juu ya taarifa zao. Wakajitambulisha kuwa ni madereva waliokodiwa kwa ajili ya usafirishaji. Hakuna kingine wanachokijua.


Jona na wenzake wakafanya msako ndani ya makazi ya wanaume hao na wakabahatika kupata nyaraka na picha kadhaa ambazo zilithibitisha kuwa mateka walitoa taarifa za uongo. Walikuwa ni miongoni mwa wafanyakazi wa taasisi ya siri ya Uingereza, ila kwenye kitengo cha usafirishaji.


“So you were lying, unh?” Jona akamnyooshea mmoja wao tundu la bunduki kichwani. “So choose one, to speak or die?”


Mwanaume huyo akatetemeka kwa hofu. Jasho likamchuruza. Akabanwa na kigugumizi asijue nini aseme.


“I’m gonna count up to five seconds!” Jona akafoka kisha akafungua bunduki yake na kutoa risasi nne, akabakiza risasi moja tu ndani ya bunduki alafu akaifunga na kumwekea mateka wake kichwani.


“One …” Jona akahesabu kisha akafyatua kitufe cha bunduki. Bunduki ikalia kak! Kumaanisha imekosa risasi.


“Two …” akahesabu tena na kufyatua kitufe cha bunduki, bunduki ikalia kak! Kumaanisha imekosa tena tundu la risasi.


“Three! …” akahesabu tena na kufyatua kitufe. Tena, kak! Bunduki ikalalamika kwa kukosa risasi! Hapo mwanaume yule mateka akawa amelowana jasho ndembendembe. Alikuwa kwenye vuli la umauti. Pengine kwenye wakati mgumu zaidi tangu aingie duniani.


Jona aliposema “Four! …” kabla hajafyatua, mateka akapiga kelele, “I’ll speak! … damn! I’ll speak!”


Jona akafungua bunduki na kutazama, tundu lenye risasi ndilo lilikuwa limekaa tenge. Kwahiyo endapo angebonyeza kitufe basi mateka yule alikuwa anapasuliwa ubongo na kulazwa mfu!


“Okay, one after another,” akasema Jona akiketi. “Tell us about your boss.”


Mateka akamtazama na kumuuliza, “What do you want to know about him?”


“Important things,” akajibu Jona. “Let’s start with where he lives, where he likes to go and what he likes to do.”


Basi mateka akasema kila alichoulizwa, kwa ufasaha na kwa uoga. Ofisi za bosi ziko wapi, makazi yake yapo wapi na viwanja anavyopenda kutembelea. Pia pasipo kusahau nini huwa anapendelea kufanya.


Sasa Jona na wenzake wakawa wana kazi ya kuanza kusuka mipango ya kutekeleza na kumaliza. Ila Lee akapata wazo, akaita,


“Jona,” na kisha akasema kwa uhakika, “nadhani kuna mtu tunamhitaji kuturahisishia kazi yetu.”


“Nani huyo?” Jona akauliza.


“Mwanamke mmoja aitwa Glady,” Lee akajibu akimtazama Jona machoni.


“Glady? Ni nani huyo na atatufaa vipi?”



***
bro wewe nikiboko ur so creative
 
Aiseee! Ahsante sana Steve kwa riwaya murua namna hii. Nilianza kusoma kimya kimya katikati ya December hadi leo hii. Hakika imenikeshesha tangu zikiwa zote (Joana na Anga) hadi mwisho. Sijawahijutia muda wangu niliotenga kusoma hadithi hizi japo mostly ni usiku wa manani. Jana nimekalia tangu saa saba usiku hadi alfajiri hii na sasa imeisha najiandaa kwenda kwenye mihangaiko. A well spent night
 
Back
Top Bottom