Andy Ruiz atoa sababu za kufeli pambano na Antony Joshua

Course Coordinator

JF-Expert Member
Jul 27, 2019
1,681
3,065
Andy Ruiz Jr amesema kwamba miezi mitatu ya kusherehekea na ukosefu wa mazoezi ya kutosha kumemfanya kuwa na "uzito kupita kiasi" wakati wa shindano la kutetea taji lake dhidi ya Anthony Joshua.

Ruiz mwenye umri wa miaka 30, alishindwa kwa alama katika pigano hilo lililofanyika Saudi Arabia, ikiwa ni miezi sita baada ya kuutikisa ulimwengu pale alipomshinda bingwa wa ndondi katika uzani mzito Anthony Joshua kule Marekani.

Mwanandondi huyo wa Mexico amesema kwamba ingekuwa vizuri iwapo atapata pigano la tatu.

"Nilitakiwa kufanya mazoezi ya kutosha. Ningewasikiliza zaidi makocha na timu yangu," Ruiz amesema.

"Kwa pigano hili nilikuwa na uzito kupita kiasi. Sikufanikiwa kufanya mijongeo yangu kama nilivyotaka iwe."

"Hakuna sababu ya kujitetea ukweli ni kwamba nilisherekea zaidi. Lakini katika pigano jengine mambo yatakuwa tofauti."
Ruiz, anayeshikilia nafasi ya pili katika ubingwa wa dunia kwenye ndodi, aliongeza kilo 7 tangu alipomshinda Joshua, ambaye kwa sasa amekuwa mshindi mara mbili.

Wengi walikuwa wamehoji iwapo mtindo wake wa maisha ambao ni pamoja na kununua majumba mapya, magari na kufanya mikutano kadhaa na vyombo vya habari baada ya kushinda huenda ikawa sababu ya kujiachia.


Ruiz ameonekana mwenye kujutia na kuomba msamaha kwa makocha wake Manny Robles na babake Andres alipofanya mkutano na wanahabari baada ya pigano na mashabiki wake wakaashiria kumridhia kwa kumpigia makofi.

Mwandondi huyo aliyekuwa bingwa wa dunia anadai kwamba baada ya kupata ushindi alipunguza uzito lakini baadaye ukaanza kuongeza: "Niliongeza uzito na hilo lilikuwa kosa kubwa. Hakuna anayejua kuhusu mazoezi tuliyokuwa tunafanya. Tulijitihadi kadiri ya uwezo wetu.

"Kuwa bingwa kwa mara ya kwanza, kuwa hapa na pale na kukosa mazoezi, halikuwa jambo rahisi.

"Naahidi ya kwamba mambo yatakuwa mazuri na kwa sasa ninachotaka nikurejea nilivyokuwa hapa Saudi Arabia."

Kocha wake Robles aliongeza kwamba alikuwa na miezi mitatu ya kufanya mazoezi lakini ni mengi ambayo hayangeweza kufanywa katika kipindi cha miezi mitatu tangu alipomshinda Joshua na pale alipoanza kufanya mazoezi.

"Sitaki kusema kwamba miezi mitatu ya kusherehekea haikuniathiri", amesema Ruiz.

"Hakuna sababu ya kujitetea ukweli ni kwamba nilisherekea zaidi. Lakini katika pigano jengine mambo yatakuwa tofauti."

"Bado watu wanamashaka na mimi. Bado mimi ni mpiganaji mzuri katika uzani mzito na ukweli ni kwamba nina uwezo kumshinda yeyote duniani."

"Naomba muamini kwamba nitarejea katika nafasi yangu na kuwa tena bingwa wa ndodi dunia kwa kitengo cha uzani mzito .
 
Afisa Uchaguzi, Ruiz mpiganaji mzuri napenda aina ya upiganaji wake, AJ hawezi kukubali kurudiana muhimu ilikua kurudisha mikanda na ilo limetimia, AJ team ni businessmans,
Ruiz amshukuru AJ kumpa jina na utajiri, kuanzia now atakua akipata mapambano yenye fedha nyingi
All the best Ruiz
Umeongea point sana mkuu, nimependa pia Ruiz kutoa sababu za kitaalamu kushindwa kwake.!
 
Back
Top Bottom