Wakati alipokuwa akisakamwa sana juu ya kuripotiwa kuwa anamiliki zaidi ya USD 1,000,000 nje ya nchi, Mh Chenge huku akiwa na hasira mbele ya waandishi wa habari aling'aka ni vp waandishi na watanzania kwa ujumla washangae hivyo vijisenti kiasi cha zaidi ya shs bilioni moja anavyomiliki? Na aliongeza kuwa iko siku ukweli utabainika.
Kama mwanasheria mahiri na kiongozi mkubwa tu wa taifa hili, Mheshimiwa Chenge hakuteleza na kwa kweli anayo siri na ufahamu mkubwa tu moyoni.
Toka kauli yake hiyo tumeshuhudia kugundulika kwa uchafu mwingi tu ndani ya Serikali kuanzia MEREMETA, EPA, UBADHIRIFU WA FEDHA ZA SERIKALI na mengine mengi.
Wiki hii nayo imefahamika kuhusu umilikaji wa fedha zaidi ya bilioni 300 zilizoibwa Serikalini na kutoroshewa mabenki ya nje!!
Hoja yangu:- Ni vipi Serikali hii inajipambanua kama inayojali watu wake inashindwa kuwakamata wahalifu hawa? Tatizo ni lipi? Tunao makachero wetu, Tunao watu wanaojua KILICHOTENDEKA kama Chenge n.k
Sasa niwapi tuna kwama viongozi wetu wa Serikali hii.
Kama mwanasheria mahiri na kiongozi mkubwa tu wa taifa hili, Mheshimiwa Chenge hakuteleza na kwa kweli anayo siri na ufahamu mkubwa tu moyoni.
Toka kauli yake hiyo tumeshuhudia kugundulika kwa uchafu mwingi tu ndani ya Serikali kuanzia MEREMETA, EPA, UBADHIRIFU WA FEDHA ZA SERIKALI na mengine mengi.
Wiki hii nayo imefahamika kuhusu umilikaji wa fedha zaidi ya bilioni 300 zilizoibwa Serikalini na kutoroshewa mabenki ya nje!!
Hoja yangu:- Ni vipi Serikali hii inajipambanua kama inayojali watu wake inashindwa kuwakamata wahalifu hawa? Tatizo ni lipi? Tunao makachero wetu, Tunao watu wanaojua KILICHOTENDEKA kama Chenge n.k
Sasa niwapi tuna kwama viongozi wetu wa Serikali hii.