GENTAMYCINE
JF-Expert Member
- Jul 13, 2013
- 56,073
- 107,563
Chama Kikongwe cha Afrika ya Kusini ANC ( African National Congress ) kinajipanga kubadili jina la nchi hiyo ambayo ni Afrika ya Kusini / South Africa kwa madai kwamba hilo jina haliakisi vilivyo nchi yao na kwamba wao kuendelea kuitwa South Africa ni muendelezo wa Sera zile zile za Wakoloni wao ambao wengi wao ni Makaburu.
Wanachama hao wa ANC walienda mbele na kujenga hoja kwa kusema kwamba kwa nchi yao kuitwa South Africa haielezi uhalisia wa nchi yao bali hilo jina linaelezea tu au linaelekeza Kijiografia kuwa wao wapo Kusini mwa Afrika hivyo wanajipanga kuipa nchi yao jina jipya kutoka hili la sasa la South Africa ambalo wanadai ni la Kikoloni zaidi na walipewa na hao hao Wakoloni.
Nini maoni yako juu ya Wanachama wa ANC kuamua kutaka kuipa nchi yao jina jipya?
Nawasilisha.
Wanachama hao wa ANC walienda mbele na kujenga hoja kwa kusema kwamba kwa nchi yao kuitwa South Africa haielezi uhalisia wa nchi yao bali hilo jina linaelezea tu au linaelekeza Kijiografia kuwa wao wapo Kusini mwa Afrika hivyo wanajipanga kuipa nchi yao jina jipya kutoka hili la sasa la South Africa ambalo wanadai ni la Kikoloni zaidi na walipewa na hao hao Wakoloni.
Nini maoni yako juu ya Wanachama wa ANC kuamua kutaka kuipa nchi yao jina jipya?
Nawasilisha.