ANC na CCM vyama vya ukombozi vilivyogeuka vichaka vya mafisadi. Vimesahau kutumikia wananchi

Muuza Kangala

JF-Expert Member
Jul 21, 2021
1,125
4,163
Namna viongozi wa Anc na CCM wanavyobehave ni namna moja.

Walijinyenyekeza kwa wananchi na kujionyesha kuwa wapo kwa ajili ya kutumikia wananchi wanyonge.

Lakini kumbe ni watu wakusahau na waiba mali za umma.

Leo hii ni magenge ya wafanyabiashara na wezi wa mali za umma wanaongoza viongozi wa vyama hivi kuibia mali za umma wananchi.

Anc wapo na matajiri wao kama akina Gupta. Ccm wapo na Rostam Azizi.

Watanzania tuikatae CCM.
 
Taja nchi mbili ambazo zimeondoa hivyo vyama vya ukombozi na kufanikiwa kutatua matatizo..

Kunatofauti gani ya Kenya ya KANU na hii ya wahuni wa mjini wa sasa.
Pale Zambia kuna tofauti gani baada ya kumtoa Kaunda na chama lake na sasa..
Mifano ni mingi Africa..

Tatizo la Africa na WaAfrica ni WaAfrica weusi wenyewe na si vinginevyo na kuleta utofauti ni pale waAfrica wote tutakapobadili tabia zetu..
 
You nailed it !! Tatizo kubwa kwetu ni SELFISHNESS !!! hiyo haina ubishi !!! Sijui tunawezaje kuibadili hii tabia !!
Taja nchi mbili ambazo zimeondoa hivyo vyama vya ukombozi na kufanikiwa kutatua matatizo..

Kunatofauti gani ya Kenya ya KANU na hii ya wahuni wa mjini wa sasa.
Pale Zambia kuna tofauti gani baada ya kumtoa Kaunda na chama lake na sasa..
Mifano ni mingi Africa..

Tatizo la Africa na WaAfrica ni WaAfrica weusi wenyewe na si vinginevyo na kuleta utofauti ni pale waAfrica wote tutakapobadili tabia zetu..
 
Namna viongozi wa Anc na CCM wanavyobehave ni namna moja.

Walijinyenyekeza kwa wananchi na kujionyesha kuwa wapo kwa ajili ya kutumikia wananchi wanyonge.

Lakini kumbe ni watu wakusahau na waiba mali za umma.

Leo hii ni magenge ya wafanyabiashara na wezi wa mali za umma wanaongoza viongozi wa vyama hivi kuibia mali za umma wananchi.

Anc wapo na matajiri wao kama akina Gupta. Ccm wapo na Rostam Azizi.

Watanzania tuikatae CCM.
UMesema kweli tupu
 
Taja nchi mbili ambazo zimeondoa hivyo vyama vya ukombozi na kufanikiwa kutatua matatizo..

Kunatofauti gani ya Kenya ya KANU na hii ya wahuni wa mjini wa sasa.
Pale Zambia kuna tofauti gani baada ya kumtoa Kaunda na chama lake na sasa..
Mifano ni mingi Africa..

Tatizo la Africa na WaAfrica ni WaAfrica weusi wenyewe na si vinginevyo na kuleta utofauti ni pale waAfrica wote tutakapobadili tabia zetu..
Kenya na Zambia
 
Taja nchi mbili ambazo zimeondoa hivyo vyama vya ukombozi na kufanikiwa kutatua matatizo..

Kunatofauti gani ya Kenya ya KANU na hii ya wahuni wa mjini wa sasa.
Pale Zambia kuna tofauti gani baada ya kumtoa Kaunda na chama lake na sasa..
Mifano ni mingi Africa..

Tatizo la Africa na WaAfrica ni WaAfrica weusi wenyewe na si vinginevyo na kuleta utofauti ni pale waAfrica wote tutakapobadili tabia zetu..
Haya ndugu mtaalam. Mwenzako amejitutumua kasema tatizo, ww umelikataa sasa tuambie wewe tatizo ni lipi?!
 
Bashite mkubwa wewe, budget ya Kenya ni 78T na wakati bongo ni 32T huoni tofauti hapo, maisha ya Zambia na bongo yanalingana?

nimeishi koote huko kabla na baada ya hizo tawala kubadirika..

unaposema budget ya Kenya 78T unajua thamani ya KSH ya Kenya vs TSH ya Tanzania..

Fedha ya kenya kuwa na thamani zaidi ya tsh ilianza toka enzi za KANU..

nimekwambia uniambie kilichobadirika kama impact ya mageuzi au upinzani kuingia ikulu...unaanza kuniita Bashite...( tetea hoja yaki then tufikie mahali tukubaliane)
 
Kwa upande wa Zambia kuna utofauti watu kwanza chama baadaye na ndiyo maana hawana mauaji ya kisiasa.
Taja nchi mbili ambazo zimeondoa hivyo vyama vya ukombozi na kufanikiwa kutatua matatizo..

Kunatofauti gani ya Kenya ya KANU na hii ya wahuni wa mjini wa sasa.
Pale Zambia kuna tofauti gani baada ya kumtoa Kaunda na chama lake na sasa..
Mifano ni mingi Africa..

Tatizo la Africa na WaAfrica ni WaAfrica weusi wenyewe na si vinginevyo na kuleta utofauti ni pale waAfrica wote tutakapobadili tabia zetu..
 
nimeishi koote huko kabla na baada ya hizo tawala kubadirika..

unaposema budget ya Kenya 78T unajua thamani ya KSH ya Kenya vs TSH ya Tanzania..

Fedha ya kenya kuwa na thamani zaidi ya tsh ilianza toka enzi za KANU..

nimekwambia uniambie kilichobadirika kama impact ya mageuzi au upinzani kuingia ikulu...unaanza kuniita Bashite...( tetea hoja yaki then tufikie mahali tukubaliane)
Nadhani utakuwa na shida sehemu, sisi tulio mipakani tunafuata bidhaa nyingi Kenya maanake wana viwanda vyao, natayari mwaka jana Rais Samia alizindua gari ambao limetengenezwa Kenya, kwanini hatuendi kuchukua Burudi?
 
Haya ndugu mtaalam. Mwenzako amejitutumua kasema tatizo, ww umelikataa sasa tuambie wewe tatizo ni lipi?!

Paragraph ya mwisho nimemueleza tatizo la Africa ni WaAfrica , Tatizo la Tanzania ni watanzania wenyewe...

Tunapokazana kuwanyooshea vidole waliopo madarakani basi tutambue wanatoka miongoni mwetu kwenye jamii zetu, Je huku kwetu kwenye jamii zetu tunawachukulia hatua gani maana Andrew chenge tunayemlalakia kule Bariadi kwa wanyantuzi ni Mtemi chenge na ndio mfalme wao..

Je sisi wengine ambao hatupo kwenye system Je sio wezi huko sekta binafsi, na mitaani, wote ni waaminifu?.... binafsi naona tabia zetu huku mitaani na wale waliopo madarakani hazina tofauti..
 
Nadhani utakuwa na shida sehemu, sisi tulio mipakani tunafuata bidhaa nyingi Kenya maanake wana viwanda vyao, natayari mwaka jana Rais Samia alizindua gari ambao limetengenezwa Kenya, kwanini hatuendi kuchukua Burudi?

Kwani hilo la Watanzania kwenda kuchukua bidhaa Kenya limeanza leo, mbona lipo toka enzi za KANU.. .. pale Taveta, Rombo, Sirali, Namanga na chocho nyingine kote huko magendo na watanzania kwenda kuchukua bidhaa ni toka enzi zile za miak 80's mpaka leo....

Naona unatoka nje ya maada, kaa kwenye mada yako..
 
Kwani hilo la Watanzania kwenda kuchukua bidhaa Kenya limeanza leo, mbona lipo toka enzi za KANU.. .. pale Taveta, Rombo, Sirali, Namanga na chocho nyingine kote huko magendo na watanzania kwenda kuchukua bidhaa ni toka enzi zile za miak 80's mpaka leo....

Naona unatoka nje ya maada, kaa kwenye mada yako..
Kwanini wasije kuchukua kwetu vitu kama sisi tumeendelea kuliko Kenya, siamini kama mtu anaweza kutoka Dar akafuata bidhaa Singida
 
Kwanini wasije kuchukua kwetu vitu kama sisi tumeendelea kuliko Kenya, siamini kama mtu anaweza kutoka Dar akafuata bidhaa Singida

"ANC na CCM vyama vya ukombozi vilivyogeuka vichaka vya mafisadi. Vimesahau kutumikia wananchi. Vinatakiwa kuondoka madarakani"

hapo juu hiyo ndio maada yako....nikakwambia huko ambapo wameshabadirisha vyama Kenya, Zambia nk nini kipya ? baada ya hayo madariko... sasa nashangaa unatoka nje ya maada....maana hiyo mifano yako kwa Kenya ni mambo yaliyokuwepo toka enzi za KANU....nataka utofauti Kenya baada ya KANU kutoka....ndio topic Chief..
 
Taja nchi mbili ambazo zimeondoa hivyo vyama vya ukombozi na kufanikiwa kutatua matatizo..

Kunatofauti gani ya Kenya ya KANU na hii ya wahuni wa mjini wa sasa.
Pale Zambia kuna tofauti gani baada ya kumtoa Kaunda na chama lake na sasa..
Mifano ni mingi Africa..

Tatizo la Africa na WaAfrica ni WaAfrica weusi wenyewe na si vinginevyo na kuleta utofauti ni pale waAfrica wote tutakapobadili tabia zetu..
Tofauti ipo... kwamba kumbe inawezekana kubadilisha vyama...
Mambo yanabadilika vyama navyo vibadilishwe!
Mbona rangi, viatu, nguo, injini, n.k mnabadilisha?
 
"ANC na CCM vyama vya ukombozi vilivyogeuka vichaka vya mafisadi. Vimesahau kutumikia wananchi. Vinatakiwa kuondoka madarakani"

hapo juu hiyo ndio maada yako....nikakwambia huko ambapo wameshabadirisha vyama Kenya, Zambia nk nini kipya ? baada ya hayo madariko... sasa nashangaa unatoka nje ya maada....maana hiyo mifano yako kwa Kenya ni mambo yaliyokuwepo toka enzi za KANU....nataka utofauti Kenya baada ya KANU kutoka....ndio topic Chief..
Hii siyo mada yangu mi nimchangiaji, kipindi cha KANU Kenya ilikuwa inatengeneza magari yake?
 
Back
Top Bottom