Nimekuwa nikifuatilia kwa makini maneno ya Dr Slaa na pia nilibahatika kufanya naye mahojiano na yeye anasema hivi:
1. Anataka haki ionekane ikitendeka. Kama A amepiga kura kituo B na kupata kura 20. Anataka Tume ya Uchaguzi ya Taifa ikitangaza matokeo, iseme A alipiga kura kituo B na amepata kura 20 na siyo 15 au 30. Kwa hili anataka kifanyike kile ninachokiita 'mathematical truth'.
2. Aliposema akishindwa atakubali kushindwa, alitumia 'analogy' ya timu ya mpira wa mguu. Alisema wachezaji wanapoingia uwanjani kucheza wanatakiwa wao na refa wao wafuate sheria za mpira. Mchezaji akifanya faulo au kufunga goli kwa kutumia mkono, refa aoneshe faulo iliyochezwa na pia aoneshe goli lilifungwa kwa mkono na siyo kwa mguu kwa kupuliza kipenga na si vinginevyo.
Alisema hana sababu ya kukataa goli liliofungwa kihalali. Kwa upande wa uchaguzi, anasema yuko tayarai kukubaliana na matokeo halali hata kama ameshindwa. Yaani, mchakato mzima wa uchaguzi uwe wazi wazi na wahusika watimize wajibu wao bila upendeleo. Lakini pale ambapo haki inakiukwa na matokeo yanabadilishwa ili kumpendelea mgombea fulani, hapo hakubaliani na matokeo yake kwani siyo halali.
3. Baadhi yetu tumekuwa tukitoa maoni na kusema viongozi wawe tayari kukubali matokeo lakini tunashindwa kuonesha ni matokeo ya namna gani tunatakiwa tuyakubali. Ni matokeo halali tu ndiyo tunapaswa tuyakubali na siyo ya kupikwa. Matokeo ya kupikwa ni lazima tuyapinge kwa nguvu zetu zote. Nawaomba Watanzania wenzangu tunapochangia hoja kama hizi tujaribu kuonesha ni kitu gani tunachoongelea na tuepuke ushabiki ambao hauna tija kwa taifa letu. Kwa kuendekeza uchakachuaji wa matokeo, tutakuwa tunakataa 'kuziba ufa' na ni wazi kwa baadaye tutaanza 'kujenga ukuta'.
4. Kwa hiyo, Dr Slaa ana haki ya kisheria ya kukataa matokeo pale anapoona haki haikutendeka. Inabidi asikilizwe na kasoro anazodai zimetokea ziangaliwe na zielezwe kwa nini zimetokea kuliko kukana na kuonesha kuwa anachosema ni uongo. The mentality of 'might is right' doesn't hold water in a democratic country like Tanzania.
1. Anataka haki ionekane ikitendeka. Kama A amepiga kura kituo B na kupata kura 20. Anataka Tume ya Uchaguzi ya Taifa ikitangaza matokeo, iseme A alipiga kura kituo B na amepata kura 20 na siyo 15 au 30. Kwa hili anataka kifanyike kile ninachokiita 'mathematical truth'.
2. Aliposema akishindwa atakubali kushindwa, alitumia 'analogy' ya timu ya mpira wa mguu. Alisema wachezaji wanapoingia uwanjani kucheza wanatakiwa wao na refa wao wafuate sheria za mpira. Mchezaji akifanya faulo au kufunga goli kwa kutumia mkono, refa aoneshe faulo iliyochezwa na pia aoneshe goli lilifungwa kwa mkono na siyo kwa mguu kwa kupuliza kipenga na si vinginevyo.
Alisema hana sababu ya kukataa goli liliofungwa kihalali. Kwa upande wa uchaguzi, anasema yuko tayarai kukubaliana na matokeo halali hata kama ameshindwa. Yaani, mchakato mzima wa uchaguzi uwe wazi wazi na wahusika watimize wajibu wao bila upendeleo. Lakini pale ambapo haki inakiukwa na matokeo yanabadilishwa ili kumpendelea mgombea fulani, hapo hakubaliani na matokeo yake kwani siyo halali.
3. Baadhi yetu tumekuwa tukitoa maoni na kusema viongozi wawe tayari kukubali matokeo lakini tunashindwa kuonesha ni matokeo ya namna gani tunatakiwa tuyakubali. Ni matokeo halali tu ndiyo tunapaswa tuyakubali na siyo ya kupikwa. Matokeo ya kupikwa ni lazima tuyapinge kwa nguvu zetu zote. Nawaomba Watanzania wenzangu tunapochangia hoja kama hizi tujaribu kuonesha ni kitu gani tunachoongelea na tuepuke ushabiki ambao hauna tija kwa taifa letu. Kwa kuendekeza uchakachuaji wa matokeo, tutakuwa tunakataa 'kuziba ufa' na ni wazi kwa baadaye tutaanza 'kujenga ukuta'.
4. Kwa hiyo, Dr Slaa ana haki ya kisheria ya kukataa matokeo pale anapoona haki haikutendeka. Inabidi asikilizwe na kasoro anazodai zimetokea ziangaliwe na zielezwe kwa nini zimetokea kuliko kukana na kuonesha kuwa anachosema ni uongo. The mentality of 'might is right' doesn't hold water in a democratic country like Tanzania.