King Kong III
JF-Expert Member
- Oct 15, 2010
- 51,656
- 68,601
Jamani hili swala lipo mahakamni chonde chonde tusilizungumzie...
Atlantic Cleophance~Joshua Mulundi
Atlantic Cleophance~Joshua Mulundi
Taarifa ambazo bado nahangaika kuzithibitisha ni kwamba ndani ya jeshi la Polisi hakuna mtumishi mwenye jina hilo, hata kwenye data base yao, ila inasemekana viongozi wakuu wamezuia kwasasa data base ya orodha ya polisi wote waliopo kazini kwasasa imezuiwa isionyeshwe kwa mtu yeyote hata aliye kwenye Idara husika, inasemekana wanataka kuchomeka hilo jina hizi siku mbili tatu baada ya watu kuhoji kama ni kweli anaye hukumiwa ndiye aliyetenda mauaji ya Mwangosi. Kweli Polisi wanatumika vibaya sijapata kuona.
...Mkuu mbona hata NIDA walishasema kuwa miongoni mwa taasisi zenye watumishi vimeo wenye vyeti vyenye utata ni polisi? Huyo askari kwa umri wa 23 yrs kwa mazingira ya elimu ya Tanzania lazima atakuwa amemaliza Form 4 kati ya 2010 - 2011...Lakini kubebana huenda alipata kazi kwa cheti cha mnadani tu... Tanzania zaidi tuijuavyo.Kwa umri wa huyo askari ni dhahiri kaajiriwa juzi juzi tu! Jeshi la polisi halipokei vijana wenye elimu chini ya kidato cha nne kwa muda mrefu sasa.
Kiukweli huyu kijana hayupo kwenye list ya Necta mtandaoni!!! Wasituambie kijana amedanganya jeshi kwa vyeti feki! tunataka tumtambue huyu mshtakiwa maana hakuna haja ya siri while hili swala ni la public tuacheni mzaha kuna vitu havijakaa sawa kabisa!!!
Jina la kikagera au kanchi ka jiraniPACIFIUS CLEOPHACE SIMON Hakuna jina kama hilo kwa watanzania walio wengi, majina yakiwa matatu, utakutana la kienyeji duh! hii ni kali that why alifunikwa sura
Duu hii nayo ni kali aisee...Kwani hamjui ajira za polisi jamani? Jina Pasifius ila cheti cha kuingilia ni cha MwajumaNdalaNdefu
kwa hiyo unaamini hapo kwenye red kuwa hakuna mtu anaweza kubadilisha hii hali???huyu atakuwa sio Mtanzania
kakodiwa nje ya nchi na inawezekana hata aliepandishwa kizimbani ni kanyaboya tu
analala magereza mchana usiku anakuwa mitaani kama kawa
chezea serikali ya magamba wewe, kila kitu kinawezekana,
yawezekana analipwa huyu kucheza movie,iweje mtuhumiwa wa mauaji apakiwe katika gari la kifahari kama lile
na iweje azibwe sura? anaficha nini? why hawakutaka waandishi wajue siku ya kuletwa mahakamani?
Taarifa ambazo bado nahangaika kuzithibitisha ni kwamba ndani ya jeshi la Polisi hakuna mtumishi mwenye jina hilo, hata kwenye data base yao, ila inasemekana viongozi wakuu wamezuia kwasasa data base ya orodha ya polisi wote waliopo kazini kwasasa imezuiwa isionyeshwe kwa mtu yeyote hata aliye kwenye Idara husika, inasemekana wanataka kuchomeka hilo jina hizi siku mbili tatu baada ya watu kuhoji kama ni kweli anaye hukumiwa ndiye aliyetenda mauaji ya Mwangosi. Kweli Polisi wanatumika vibaya sijapata kuona.
wote hawa ni wauwaji wafikishwe mahakamani,
Wanajamvi naomba kuuliza huyu kijana anayetuhumiwa kumwua Mwangosi: PACIFIUS CLEOPHACE SIMON hajasoma sekondary? maana uki google jina lake na hata lile alilotajwa na Nchimbi (PASIFIOUS) halionekani NECTA. isije ikawa tunauziwa mbuzi kwenye gunia au kwa lugha rahisi kanyaboya.
Naomba habari za uchunguzi zichukue nafasi yake.