The Analyst
JF-Expert Member
- Feb 26, 2011
- 464
- 246
Watu wengi tunapenda kusema yule mtoto au jamaa ananipenda sana a.k.a kanizimia ile mbaya nk. Naomba wanajamvi tujadili jambo hili kwa kina. Maadam kuna wasanii wengi sana ktk maisha ya siku hizi unaweza vipi kumtofautisha mtu anayekupenda kwa dhati na anayekusudia hasa (kwa dhati) kuonekana anakupenda kwa dhati japo siyo kweli?
Hadi kufikia muda huu naamini kwamba kama mtu ana lake jambo na amekusudia kwa nia moja anaweza kuigiza vizuri kiasi cha kuaminika kama anayependa kwa dhati wakati kumbe ana nia yake tofauti, na kupenda ni njia tu kufikia malengo. Mfano mzuri ni kijana anayempenda binti na kufanya mengi tu kama kubadili dini nk akidai anapenda lakini akishafaidi anachotaka huyoooo! anatimua. Hamjawasikia watu kama hao? Baadhi yao wanasema waziwazi kwamba iliwalazimu kujifanya wamependa ile mbaya ili wapate. Madada pia wapo wanaodai walijifanya wamependa ili kupata utajiri nk.
Hadi kufikia muda huu naamini kwamba kama mtu ana lake jambo na amekusudia kwa nia moja anaweza kuigiza vizuri kiasi cha kuaminika kama anayependa kwa dhati wakati kumbe ana nia yake tofauti, na kupenda ni njia tu kufikia malengo. Mfano mzuri ni kijana anayempenda binti na kufanya mengi tu kama kubadili dini nk akidai anapenda lakini akishafaidi anachotaka huyoooo! anatimua. Hamjawasikia watu kama hao? Baadhi yao wanasema waziwazi kwamba iliwalazimu kujifanya wamependa ile mbaya ili wapate. Madada pia wapo wanaodai walijifanya wamependa ili kupata utajiri nk.