Anayejua Rais Magufuli anatupeleka wapi atuambie, naona kama tumepotea

Status
Not open for further replies.
Ndio tunafika hivyo,
Wakuu wa upinzani wote vilema,
Vyama vya siasa, vinongelea kichochoroni,
Hakuna anayethubutu kuweka mkutanowa siasaTtanzania isipokuwa CCM.
Baki miezi 4 Uchaguzi, Hakuna Chaa hata kimoja cha upinzani kilichofanya maandalizi ya kisiasa.
Hata kampeni zikiruhusiwa,mashariti yake yatakuwa magumu mno na hakuna uwezekano kwa vyama kuzunguka nchi nzima kutangaza sera zao kwa kukosa Coodination kwa ufinyu wa budget na Muda.

Polisi nao wako pale tayari kusikiliza wapinzani,
ukimtaja Raisi tu au CCM kivibaya kwa kushindwa kwao kuleta maendeleo au ajira nk ,una kesi ya kujibu,unaishia korokoroni hadi uchaguzi unaisha.
MIMI NAONA

HAKUTAKIWI TENA SIASA WALA UPINZANI TANZANIA

Hivyo ndio tumeshafika huko.
Waarabu husema KHALAS
Wahindii husema KWISH NEHI
Wapemba husema YANSOZAAAAAAAA!!!!!!!!!!!!!
 
June 2020, still relevant!
Mwalimu Nyerere aliwahi kusema, "Hatuwezi kuwa na Rais ambaye hatujui kesho ataamka amefikiria nini au ameshauriwa nini na mke wake". Kwa wakati ule kilionekana ni kijembe kwa mzee Mwinyi lakini leo kauli yake inaonyesha maana.

Hatujui mwelekeo wa nchi kiukweli, hatujui kesho atafukuzwa na nani au ziara ya Rais au Waziri Mkuu itakuwa wapi. Hatujui kama tutaamka tunafagia barabara au tutaingia ofisini kwetu kama kawaida.

Hatujui tunaanza na nini, kujenga viwanda au kuboresha miundombinu na kuimarisha kilimo ili tupate malighafi.

Hatujui tatizo la sukari kwa mfano linaondoka kwa kurekebisha viwanda vyetu na kuongeza uzalishaji wa miwa au kuruhusu sukari ya nje au tuvamie magodauni ya watu.

Ukimuangalia usoni na ukasikia anachotamka unakiri ana nia kabisa ya kututoa hapa. Swali ni je, anajua jinsi ya kututoa?! Anajua anakotupeleka?

Nimejitahidi kuangalia Bunge ili nione labda Mawaziri wake wanaweza kuonyesha mwelekeo, huko nikachanganyikiwa zaidi.

Mwanamtandao mmoja alisema unaweza kuwa na dereva mzuri anayefuata sheria zote za barabarani lakini hajui anaenda wapi!
 
Kutoeleweka muelekeo wa safari inaweza kuwa tatizo la muongoza chombo au tatizo la kutoelewa tu la abiria mwenyewe.
 
Katupeleka kwenye uchumi wa kati.
Ahaaa ,uchumi ambao ajira zimeota mbawa, hela imetoweka ,na ukata umetamalaki, kw umasikini kuongezeka?
Uchumi wa kati ni fursa za Mabepari kujitanua,
pato la serikali limengezeka sana, lakini kwa gharama ya kuwabana mno masikini ambao tayari wengi wao walikuwa wanakula mlo mmoja kwa siku.
sasa hawanauhakika nahuo mlo mmoja kamwe.
Omba omba wameongezeka, utapeli, wizi, ubabaishaji nk.
 

Attachments

  • Nchi Masikini Haziwezi kulipa madeni yao kamwe.mp4
    6.4 MB
Sasa Tanzania iko grad ya Uchumi wakati bado hujafumbuliwa Mh JPM anatupeleka wapi?
Labda ludisha mkanda nyuma zilejee kumbukumbu kwa usahihi utaiona njia tunayoindea
 
Nawaomba muisikilize kwa umakini hii video.
Tanzania tunajigamba kuongeza kipato kwa kuongezeka kwa pato la nchi na kupanda GDP ,lakiniukija kwa watu wa kawaida ,umasikini unazidi kuwaelemea.
jibu lipo hapa.
Acha kukopa sana ili uondokane na madeni makubwa baki na uchumi unaolingana na msuli wako ''better late than never'' uharaka wa kuingia uchumi wa kati utatupasua msamba kwa kuwaridhisha Wazungu na Mabeberu wa IMF huku raia wako wanaangamia.
 

Attachments

  • Nchi Masikini Haziwezi kulipa madeni yao kamwe.mp4
    6.4 MB
Nawaomba muisikilize kwa umakini hii video.
Tanzania tunajigamba kuongeza kipato kwa kuongezeka kwa pato la nchi na kupanda GDP ,lakiniukija kwa watu wa kawaida ,umasikini unazidi kuwaelemea.
jibu lipo hapa.
Acha kukopa sana ili uondokane na madeni makubwa baki na uchumi unaolingana na msuli wako ''better late than never'' uharaka wa kuingia uchumi wa kati utatupasua msamba kwa kuwaridhisha Wazungu na Mabeberu wa IMF huku raia wako wanaangamia.
True mkuu, wanaangalia uchumi wa nchi tu, wakati raia hali ni mbaya huku mtaani kwa ujumla
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom