Anayejua Rais Magufuli anatupeleka wapi atuambie, naona kama tumepotea

Status
Not open for further replies.
Sijui kama niko sahihi kuiweka na CCM au abaki mwenyekiti peke yake mtasahihisha wenyewe

Japo wengi hatuzijui sheria ila hatukuzoea kuona waziri anaapishwa kwenye makazi binafsi ya mtu

Japo mambo hubadilika hatukuzoea kuona Spika anapewa kiburi na Rais

Japo dunia inaenda kasi hatukuzoea kuona Rais anatoa kauli za kuchanganya wakati wa majanga

Japo kila mtu na tabia zake ila hatukuzoea kuona mtu akihamia CCM au akiwa mwana ccm anakuwa huru kufanya analolitaka

Bungeni sheria hazifuatwi,

Mahakamani mashauri ili kuamliwa yanasikiliziwa kwanza,

Watumishi wa umma hawana tena uwezo wa kunyanyua mdomo kudai haki zao

Mapolisi wanaamrishwa kufanya chochote na wakubwa zao,

Wapinzani wanajiongelesha ongelesha tu ila hawana wanachoweza kufanya,

Vyama vya wafanyakazi vinajiongelesha tu havina la kufanya,

Mawaziri wanajiongelesha tu hawana la kufanya wala la kushauri wapo kama bendera tu,

Spika wa bunge na hata Jaji nao wameshakuwa bendera

Kama sio kutuona mazwazwa ni nini?

Hebu niambieni kundi gani sasa hivi hata likifanyiwa uonevu gani linauwezo wa kujipigania na likashinda.

Sent using Jamii Forums mobile app
Chagueni mbadala. Mbona simple ila mwisho wa siku wengi watashinda.
 
Wabunge zaidi ya 30+ na wanasiasa kutoka upinzani ambao tayari wana vyeo ndani ya vyama vyao zaidi ya 200+ kutoka chama pinzani na kuja Katika chama chetu kwa kweli ni jambo ambalo sijawahi kulisikia popote duniani.
 
Sijui kama niko sahihi kuiweka na CCM au abaki mwenyekiti peke yake mtasahihisha wenyewe

Japo wengi hatuzijui sheria ila hatukuzoea kuona waziri anaapishwa kwenye makazi binafsi ya mtu

Japo mambo hubadilika hatukuzoea kuona Spika anapewa kiburi na Rais

Japo dunia inaenda kasi hatukuzoea kuona Rais anatoa kauli za kuchanganya wakati wa majanga

Japo kila mtu na tabia zake ila hatukuzoea kuona mtu akihamia CCM au akiwa mwana ccm anakuwa huru kufanya analolitaka

Bungeni sheria hazifuatwi,

Mahakamani mashauri ili kuamliwa yanasikiliziwa kwanza,

Watumishi wa umma hawana tena uwezo wa kunyanyua mdomo kudai haki zao

Mapolisi wanaamrishwa kufanya chochote na wakubwa zao,

Wapinzani wanajiongelesha ongelesha tu ila hawana wanachoweza kufanya,

Vyama vya wafanyakazi vinajiongelesha tu havina la kufanya,

Mawaziri wanajiongelesha tu hawana la kufanya wala la kushauri wapo kama bendera tu,

Spika wa bunge na hata Jaji nao wameshakuwa bendera

Kama sio kutuona mazwazwa ni nini?

Hebu niambieni kundi gani sasa hivi hata likifanyiwa uonevu gani linauwezo wa kujipigania na likashinda.

Sent using Jamii Forums mobile app
Haya nenda kwa Dj ukachukue mshahara wako.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hebu niambieni kundi gani sasa hivi hata likifanyiwa uonevu gani linauwezo wa kujipigania na likashinda.
Mimi nasubiri tu nione maajabu ya nchi yangu ya Tanzania.

Kama Coronavirus haitakuwa kikwazo cha kuvuruga ratiba yetu ya uchaguzi mkuu, au kufanywa kuwa kisingizio cha kuahirisha uchaguzi huo.

Nasubiri kuona maajabu ya waTanzania wakijitokeza kwa wingi kwenda kuwachagua viongozi hawa hawa wa CCM. Hili litanishangaza sana.

Na sio kuwa sijui kwamba CCM wanazo njia zao mbalimbali za kutulazimisha wabaki kwenye madaraka hata kama hatukuwapigia kura. Kukubali kulazimishwa huko pia itakuwa ni sehemu ya maajabu ninayosubiri kuyaona.

Wengi tunasema hatuoni mbadala wa kuwapa madaraka, isipokuwa CCM tu ndio wanaostahili madaraka hayo.
Kama hivyo ndivyo, basi tuwasihi CCM wasilazimishe, watuache tu sisi wenyewe tuendelee kuwaweka kwenye madaraka hayo.

Kutunyima haki ya kufanya hivyo hilo ndilo kosa lisiloweza kusameheka; na hiyo ndiyo sababu inayofanya baadhi yetu tuone ni bora kuwaweka wapinzani kwa muda ili tuone kama watafaa kuwa mbadala. Wasipofaa, tuwaondoe kabla hawajachukua tabia mbaya za kutulazimisha wao wabaki kwenye madaraka kwa nguvu kama wanavyofanya CCM sasa hivi.
 
Unashauri tufanyeje.

Mitandao ya kijamii imetuharibu. Tunakimbilia kulalamika basi. No action taken. Zaman watu walikuwa wanafikisha message zao kwa maandamano.

Sent using Jamii Forums mobile app
Nani wakuandamana! Kama vyombo vya habari vyenyewe vinachaguliwa cha kusema itakuwa maandamano.

Wala si kweli kwamba social media ndo zimezuia maandamano. Kilchozuia ni uzwazwa wa watanzania.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mimi nasubiri tu nione maajabu ya nchi yangu ya Tanzania.

Kama Coronavirus haitakuwa kikwazo cha kuvuruga ratiba yetu ya uchaguzi mkuu, au kufanywa kuwa kisingizio cha kuahirisha uchaguzi huo.

Nasubiri kuona maajabu ya waTanzania wakijitokeza kwa wingi kwenda kuwachagua viongozi hawa hawa wa CCM. Hili litanishangaza sana.

Na sio kuwa sijui kwamba CCM wanazo njia zao mbalimbali za kutulazimisha wabaki kwenye madaraka hata kama hatukuwapigia kura. Kukubali kulazimishwa huko pia itakuwa ni sehemu ya maajabu ninayosubiri kuyaona.

Wengi tunasema hatuoni mbadala wa kuwapa madaraka, isipokuwa CCM tu ndio wanaostahili madaraka hayo.
Kama hivyo ndivyo, basi tuwasihi CCM wasilazimishe, watuache tu sisi wenyewe tuendelee kuwaweka kwenye madaraka hayo.

Kutunyima haki ya kufanya hivyo hilo ndilo kosa lisiloweza kusameheka; na hiyo ndiyo sababu inayofanya baadhi yetu tuone ni bora kuwaweka wapinzani kwa muda ili tuone kama watafaa kuwa mbadala. Wasipofaa, tuwaondoe kabla hawajachukua tabia mbaya za kutulazimisha wao wabaki kwenye madaraka kwa nguvu kama wanavyofanya CCM sasa hivi.
Hapa ndo tunapokwama na wao ndio wanapotuona hatuwezi kuwafanya chochote!

Kwamba watuache tupige kura kihalali, kura zihesabiwe kihalali, na mshindi atangazwe kihalali! Kuwaza hivi ndo kunatufelisha

Nchi nyingi zilizofanikiwa kubadili uongozi zilijipanga kwa kuweka plan B. Wabongo plan B yetu iko wapi?

Wanajua hatuna plan B ndiomaana wanafanya wanavyotaka wao wala sio sisi

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom