Anayejua Rais Magufuli anatupeleka wapi atuambie, naona kama tumepotea

Status
Not open for further replies.

mpk

JF-Expert Member
Sep 26, 2012
3,115
3,862
Mwalimu Nyerere aliwahi kusema,"Hatuwezi kuwa na Rais ambaye hatujui kesho ataamka amefikiria nini au ameshauriwa nini na mke wake". Kwa wakati ule kilionekana ni kijembe kwa mzee Mwinyi lakini leo kauli yake inaonyesha maana.

Hatujui mwelekeo wa nchi kiukweli, hatujui kesho atafukuzwa na nani au ziara ya Rais au Waziri Mkuu itakuwa wapi. Hatujui kama tutaamka tunafagia barabara au tutaingia ofisini kwetu kama kawaida.

Hatujui tunaanza na nini, kujenga viwanda au kuboresha miundombinu na kuimarisha kilimo ili tupate malighafi.

Hatujui tatizo la sukari kwa mfano linaondoka kwa kurekebisha viwanda vyetu na kuongeza uzalishaji wa miwa au kuruhusu sukari ya nje au tuvamie magodauni ya watu.

Ukimuangalia usoni na ukasikia anachotamka unakiri ana nia kabisa ya kututoa hapa. Swali ni je, anajua jinsi ya kututoa? Anajua anakotupeleka?

Nimejitahidi kuangalia Bunge ili nione labda Mawaziri wake wanaweza kuonyesha mwelekeo, huko nikachanganyikiwa zaidi.

Mwanamtandao mmoja alisema unaweza kuwa na dereva mzuri anayefuata sheria zote za barabarani lakini hajui anaenda wapi!
 
Akupeleke kwani wewe umekuwa zombie? Raisi Magufuli hayuko hapa kukupeleka wewe popote pale, bali wewe ndiyo unatakiwa ujipeleke mahali kwingine, wewe ndiyo unatakiwa ujitoe hapo ulipo na kwenda sehemu nyingine, wewe ndiyo unatakiwa ujifungue minyonyoro uliyofungwa na fisadi Lowasa, Mbowe & Co. na kuwa mtu huru Raisi Magufuli hawezi kulifanya hilo na wala siyo kazi yake!
 
Kuna thread humu inaelezea ahadi za Magufuli nenda kaisome....

Halafu kuna Ilani ya CCM nenda kaisome pia.

Halafu rudi hapa uje kutuuliza ambacho hujakielewa....

HAYA ZUNGUSHAA ZUNGUSHAAA TENAA ZUNGUSHA MIKONOOO....MABADILIKOOOO!!!
Jamani mi niko serious, ninyi mnaleta siasa. Hii ni mada inayoweza kutusaidia na kumsaidia rais tukiondoa ushabiki
 
Tunakoelekea ni kazi tu.
Tulipoanzia ni kutumbua wafanyakazi hewa na kutengeneza afya bora kwa wafanyakazi wetu na Elimu bora .
Kwa sasa tuko na kazi ya kukusanya Kodi na kuweka taratibu sahihi wa matumizi sahihi ya Kodi .
 
Tunakoelekea ni kazi tu.
Tulipoanzia ni kutumbua wafanyakazi hewa na kutengeneza afya bora kwa wafanyakazi wetu. Elimu bora no.
Kwa sasa tuko na kazi ya kukusanya Kodi na kuweka taratibu sahihi wa matumizi sahihi ya Kodi .
Angalau wewe umejaribu kujibu, mkishakusanya fedha hizo zinaenda wapi? Halimashauri zinalia na mitaani ndo usiseme
 
Watanzania tuna akili fupi sana ndo maana hatusonge mbele kama taifa na mtu mmoja mmoja, maada ni nzuri inawweza kutusaidia kuibua njia mpya za kumsaidia rais kama ushauri, mtoa mada hana nia mbaya na rais bali anajaribu kutushirikisha tuangalie mwelekeo wa sisi kama taifa, kwa hiyo tuache kumkebehi tuchangie mada kwa mtazamo chanya kwa kutoa michango na ushauri wa kujenga taifa.
 
Tunakoelekea ni kazi tu.
Tulipoanzia ni kutumbua wafanyakazi hewa na kutengeneza afya bora kwa wafanyakazi wetu na Elimu bora .
Kwa sasa tuko na kazi ya kukusanya Kodi na kuweka taratibu sahihi wa matumizi sahihi ya Kodi .
Hivi mkuu makusanyo ya mwezi April yalikuwa trilioni ngapi? Na za mwezi May je?

Zamani tulikuwa tunatangaziwa mapato na matumizi ya serikali lakini kwa sasa ni kimya kabisa. Pia ukiongea na watumishi serikalini watakwambia hakuna hela ya DEVELOPMENT imetumwa mwezi wa nne na wa tano, pia hata hela ya kuendesha ofisi maarufu kama OC haijatumwa kwa miezi miwili. Hii ni dalili kuwa nchi haina muelekeo mzuri kiuchumi ingawa sisi wengine tunampa muda huyu nahodha wetu hadi atakapoanza kutekeleza bajeti yake mwezi July
 
Watanzania tuna akili fupi sana ndo maana hatusonge mbele kama taifa na mtu mmoja mmoja, maada ni nzuri inawweza kutusaidia kuibua njia mpya za kumsaidia rais kama ushauri, mtoa mada hana nia mbaya na rais bali anajaribu kutushirikisha tuangalie mwelekeo wa sisi kama taifa, kwa hiyo tuache kumkebehi tuchangie mada kwa mtazamo chanya kwa kutoa michango na ushauri wa kujenga taifa.
Nashauri moderators kama wapo na wanahitaji mijadala makini kwa maendeleo ya jukwaa wafanye kazi yao kwa kuondoa hizo hoja za nje ya mada na kebehi ili watu makini tujadiliane uelekeo wa nchi yetu.

Wengi tumeanza kuona nyota kwa vile serikali haijishugulishi na vitu vya kukuza uchumi, imetunga sheria ya kufanya usafi kila mwezi na faini zake, lakini imeshindwa kuifanyia marekebisho sheria ya kazi inayowapa wageni fursa za kupora ajira. Haijafanya chochote kuboresha mazingira ya kufanya biashara so far not so good
 
Hivi mkuu makusanyo ya mwezi April yalikuwa trilioni ngapi? Na za mwezi May je?

Zamani tulikuwa tunatangaziwa mapato na matumizi ya serikali lakini kwa sasa ni kimya kabisa. Pia ukiongea na watumishi serikalini watakwambia hakuna hela ya DEVELOPMENT imetumwa mwezi wa nne na wa tano, pia hata hela ya kuendesha ofisi maarufu kama OC haijatumwa kwa miezi miwili. Hii ni dalili kuwa nchi haina muelekeo mzuri kiuchumi ingawa sisi wengine tunampa muda huyu nahodha wetu hadi atakapoanza kutekeleza bajeti yake mwezi July
Haya wanayajua haya unayosema?
 
Muda mwingine unaweza kuonyesha uwerevu lakini kupitia uwerevu wako ujinga wako pia ukaonekana, hivi Dkt Magufuli tangu aingie madarakani alikua anaenda na bajeti aliyoiandaa au aloandaa Kikwete? Tabia za namna hii haitusaidii sisi kama watanzania, hata kama aumpendi jitahidi kupima kwa haki, nafikiri unafuatilia bunge la bajeti na kilichomo unakiona hapo ndo tuanzie, nchi haiendeshwi wewe unavyotaka bali Rais anavyoona inafaa muda wa kupima anafanikiwa au la bado aujafika kupitia bajeti hii tutaweza kupima ni kwa kiasi gani Rais anafanikiwa lakini hii tabia ya kumkatisha tamaa Rais haifai ni tabia za watu wenye husuda na zaidi wamejaliwa wanawake kuwa nazo nchi ikiyumba sio yeye Rais atakayeteseka bali ni sisi wananchi, ni jukumu letu kukosoa pale palikosewa na kuonyesha njia sahihi ya kupita lakini kukosoa tu bila kuonyesha nini kilitakiwa kifanyike hiyo ni tabia ya kike
 
Muda mwingine unaweza kuonyesha uwerevu lakini kupitia uwerevu wako ujinga wako pia ukaonekana, hivi Dkt Magufuli tangu aingie madarakani alikua anaenda na bajeti aliyoiandaa au aloandaa Kikwete? Tabia za namna hii haitusaidii sisi kama watanzania, hata kama aumpendi jitahidi kupima kwa haki, nafikiri unafuatilia bunge la bajeti na kilichomo unakiona hapo ndo tuanzie, nchi haiendeshwi wewe unavyotaka bali Rais anavyoona inafaa muda wa kupima anafanikiwa au la bado aujafika kupitia bajeti hii tutaweza kupima ni kwa kiasi gani Rais anafanikiwa lakini hii tabia ya kumkatisha tamaa Rais haifai ni tabia za watu wenye husuda na zaidi wamejaliwa wanawake kuwa nazo nchi ikiyumba sio yeye Rais atakayeteseka bali ni sisi wananchi, ni jukumu letu kukosoa pale palikosewa na kuonyesha njia sahihi ya kupita lakini kukosoa tu bila kuonyesha nini kilitakiwa kifanyike hiyo ni tabia ya kike
Nchi haiendeshwi kwa matakea ya rais ndiyo maana kuna miongozo kama ilani, mipango ya muda mrefu na mfupi, katiba, sheria, miongozo na nyaraka mbali mbali. Wananchi ni haki yetu kuhoji, kukosoa, kushauri na kulalamika kama mambo hayaendi vizuri. Tatizo linakuja pale anayehoji au kukosoa anapoonekana adui. Tabia hii siyo nzuri na haiwezi kutupeleka popote kama taifa
 
Muda mwingine unaweza kuonyesha uwerevu lakini kupitia uwerevu wako ujinga wako pia ukaonekana, hivi Dkt Magufuli tangu aingie madarakani alikua anaenda na bajeti aliyoiandaa au aloandaa Kikwete? Tabia za namna hii haitusaidii sisi kama watanzania, hata kama aumpendi jitahidi kupima kwa haki, nafikiri unafuatilia bunge la bajeti na kilichomo unakiona hapo ndo tuanzie, nchi haiendeshwi wewe unavyotaka bali Rais anavyoona inafaa muda wa kupima anafanikiwa au la bado aujafika kupitia bajeti hii tutaweza kupima ni kwa kiasi gani Rais anafanikiwa lakini hii tabia ya kumkatisha tamaa Rais haifai ni tabia za watu wenye husuda na zaidi wamejaliwa wanawake kuwa nazo nchi ikiyumba sio yeye Rais atakayeteseka bali ni sisi wananchi, ni jukumu letu kukosoa pale palikosewa na kuonyesha njia sahihi ya kupita lakini kukosoa tu bila kuonyesha nini kilitakiwa kifanyike hiyo ni tabia ya kike
Good point umeelezea vizuri.
Kwa fikra yangu ni kwamba watu hawawelewi kwa sababu mwanzoni mambo mengi yalifanywa wazi, yaani kutumbua Majipu etc.

Ila kwa sasa prezidaa yupo kimya sana. Sasa hilo pia linaweza kufanya wananchi wawe Na maswali.

Pia kwa siasa ya Tanzania ilipokuwa umefika mi sioni haja ya Raisi kuwa msiri kama alivyo huyu, kwa sababu unakuwa unaawacha njia panda.
Anaweza kuwa Na mkutano Na wazee kila Mwezi akawa anaelezea mambo muhimu yaliyotokea mwezi uliopita n.k au ateue mtu awe anasoma reports za mwezi.

Watanzania ni talkers Na Prezidaa ni Doer kwa hiyo hapo kunakuwa Na mgongano kidogo.

Mawazo yangu tu.
 
Status
Not open for further replies.
185 Reactions
Reply
Back
Top Bottom