Huu uzi inabidi ubadilike heading sasa pale penye 'anatupeleka wapi?' isomeke 'ametufikisha wapi?'.
Mimi ni mmoja wa wanachama wa chama ambacho mwenyekiti wetu ni Jiwe, jiwe anatuumiza sana mioyo yetu. Msione kila mahali tunamsifu Jiwe lakini kiukweli mngejua mioyo yetu inavyoumia msingesema kitu, mioyo yetu inaumia kuliko mwanachama wa chama chochote kile hapa nchini lakini tunamsifu ili tupate hata sh. elfu saba siku isogee.
Jiwe anaumiza kuanzia viongozi wenzie mpaka wanachama wa kawaida, Jiwe amezungukwa na wanafiki wanaomsifia hata akifanya maamuzi yasiyo na faida kwa chama. Jiwe ametuondolea waliokijenga chama na kubaki na wasiojua chochote kuhusu chama ila kwakuwa wanamsifu.
Jiwe ukimkosoa wapambe wanampelekea taarifa, akizipata bila kufikiri anakuadhibu kwa namna yoyote ile. Wakati mwingine hata kama hujamkosoa ila mpambe akikuchonganisha nae basi imekula kwako, anapenda sana kusikiliza story za vijiweni.
Jiwe tuonee huruma wanachama wenzio, Jiwe umewamaliza wao sasa umeanza na sisi wenzio tuliokuwa pamoja kipindi chote cha kampeni. Tulikwenda porini pamoja, tulikwenda shinyanga pamoja, tukaenda bagamoyo pamoja lakini tulienda mpaka Tanga pamoja leo hii Jiwe umenitenda.
Asanteni sana Jiwe