Anayejua Rais Magufuli anatupeleka wapi atuambie, naona kama tumepotea

Status
Not open for further replies.
Watu wengi dhalimu Duniani hakuna walipoacha kumtaja Mungu kila walipotaka kutimiza uovu wao.

Ukiona mtu yeyote kila mara anamtaja Mungu katika maneno yake, weka mashaka ya juu. Wengi wao huwa ni waovu wanaotaka kuuficha uovu kwa kulitaja jina la Mungu.

Wenye kulitaja jina la Yehove kwa nia ya kuuficha uovu, kumbe mioyo yao imejaa kiburi, hila, jeuri, visasi, tamaa ya madaraka, walaaniwe. Laana ya Mungu wa haki iwe juu yao na vizazi vyao maana Mungu, si Mungu ww utakatishaji uovu.

Mungu ni Mungu wa wema, Mungu wa Upendo, Mungu wa Umoja, Mungu wa Msamaha. Mwenye kutenda kinyume chake ni zao la joka, joka lile la uovu yaani Ibilisi linalozunguka Duniani kuwatafuta wafuasi ili ufalme wake upate kutamalaki Duniani kote. Lakini hawatashinda maana Duniani, kila siku iitwayo siku, wapo watu wanyofu, watu wanyenyekevu, watu wenye upendo ambao usiku na mchana wapo kwenye madhabahu za Bwana wakiomba ufalme wa Mungu wa kweli, ufalme usitetereka wala kulegea, ukalitupe joka llile na wafuasi wake kwenye ziwa la moto maana kule ndiko wastahiliko.
 
Hizi ndio baadhi ya kauli zake katika maeneo na nyakati tofauti:

"Nataka upinzani uwepo..."

"Siasa mpaka 2020......."
 
  • Thanks
Reactions: PNC
Hapo kwenye siasa mpaka 2020 Uncle Magu apakaze sana
Mambo waliyokuwa wakiyafanya upinzani kwenye utawala wa JK wengi tulikuwa hatuyapendi
Migomo, Maandamano, Mara nchi haitatawalika
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom