Umepata like zakutosha ila nizakinafiki. Umepotea mwenyewe.Mwl Nyerere aliwahi kusema "hatuwezi kuwa na rais ambaye hatujui kesho ataamka amefikiria nini au ameshauriwa nini na mke wake". Kwa wakati ule kilionekana ni kijembe kwa mzee Mwinyi lakini leo kauli yake inaonyesha maana.
Hatujui mwelekeo wa nchi kiukweli hatujui kesho atafukuzwa na nani au ziara ya rais au waziri mkuu itakuwa wapi. Hatujui kama tutaamka tunafagia barabara au tutaingia ofisini kwetu kama kawaida.
Hatujui tunaanza na nini, kujenga viwanda au kuboresha miundombinu na kuimarisha kilimo ili tupate malighafi.
Hatujui tatizo la sukari kwa mfano linaondoka kwa kurekebisha viwanda vyetu na kuongeza uzalishaji wa miwa au kuruhusu sukari ya nje au tuvamie magodauni ya watu
Ukimuangalia usoni na ukasikia anachotamka unakiri ana nia kabisa ya kututoa hapa. Swali ni je? anajua jinsi ya kututoa?
Anajua anakotupeleka? Nimejitahidi kuangalia bunge ili nione labda mawaziri wake wanaweza kuonyesha mwelekeo, huko nikachanganyikiwa zaidi.
Mwanamtandao mmoja alisema unaweza kuwa na dereva mzuri anayefuata sheria zote za barabarani lakini hajui anaenda wapi!
[HASHTAG]#Invisible[/HASHTAG] naomba hii iwe special thread mpaka hapo tutapopata jibu
Unga wenyewe hakuna,labda angechemsha mawe tukala na mikate ya barafuNije niwapikie?
Anataka kupikiwa huyuUna njaa!??
RAISI aje kupika siyo hiyo ndo Nazi yakeAnataka kupikiwa huyu
Ya mkwanjaUna njaa!??
Hata adolf hitler alikua chaguo la Mungu.wafalme wa pili sura ya sabaRAIS WETU NI CHAGUO LA MWENYE ENZI MUNGU. ....WAFALME WA PILI SURA YA SABA. ....