Beatrice Kamugisha
JF-Expert Member
- May 18, 2019
- 762
- 6,980
Familia ya Mbowe imethibitisha kupitia ukarasa wa tweeter kwamba baba yao amechanganywa na wafungwa wanaosubiri kunyongwa. Tunaamini waliofanya haya hawataweza kumnyonga ila wanaweza kumweka kigungoni milele. Lakini aishivyo Mwenyenzi Mungu alimweka huyu Condem pia anaweza akatwaliwa katika ulimwengu huu na mrithi wake akamtoa Mbowe.
Ila Jambo hili linakuwa gumu pale ambapo linafanywa na Watanzania wenzetu, waumini wenzetu wa dini na watu wanaolipwa mishahara na sisi kwa sababu tu wanaamini wao walizaliwa kututawala na iwavyo isivyo lazima tutawaliwe.
Haya yanafanyika katika Taifa ambalo linadai Lina viongozi wa dini lakini viongozi hao wa dini wameshindwa kabisa kufungu na kuomba ufunuo juu ya madhara ya uchungu unaosambazwa na watawala wetu.
Yanafanyika kipindi ambacho majirani zetu wanashangilia kuona na sisi tumegawanyika na wanajiandaa kututawala na kutwaa ardhi na rasilimali zetu Kama ilivyo Kongo. Naamini tunalo jukumu lakuwaamsha usingizini watu Hawa,viongozi wastaafu msione kama mpo salama Sana.
Mwisho niwaombe wenye Magereza wasikae kimya juu ya tuhuma hizi vinginevyo Kama ni za kweli na wao kwa utaratibu wao wanaamini hiki ndicho kinapaswa kufanyika.
Hatupo wamoja tena, nafsi zimeinama katika kila sekta. Naamini hata ndani ya nafsi za mawaziri na wakuu wa vyombo upo mgogoro mkubwa juu ya kesho ya watoto wao. Haiwezekani kila mtu alalamike, Kuna shida mahali na tunahijua japo atulazimishwi kuwalazimisha mfanye tuonavyo sisi.
Ila Jambo hili linakuwa gumu pale ambapo linafanywa na Watanzania wenzetu, waumini wenzetu wa dini na watu wanaolipwa mishahara na sisi kwa sababu tu wanaamini wao walizaliwa kututawala na iwavyo isivyo lazima tutawaliwe.
Haya yanafanyika katika Taifa ambalo linadai Lina viongozi wa dini lakini viongozi hao wa dini wameshindwa kabisa kufungu na kuomba ufunuo juu ya madhara ya uchungu unaosambazwa na watawala wetu.
Yanafanyika kipindi ambacho majirani zetu wanashangilia kuona na sisi tumegawanyika na wanajiandaa kututawala na kutwaa ardhi na rasilimali zetu Kama ilivyo Kongo. Naamini tunalo jukumu lakuwaamsha usingizini watu Hawa,viongozi wastaafu msione kama mpo salama Sana.
Mwisho niwaombe wenye Magereza wasikae kimya juu ya tuhuma hizi vinginevyo Kama ni za kweli na wao kwa utaratibu wao wanaamini hiki ndicho kinapaswa kufanyika.
Hatupo wamoja tena, nafsi zimeinama katika kila sekta. Naamini hata ndani ya nafsi za mawaziri na wakuu wa vyombo upo mgogoro mkubwa juu ya kesho ya watoto wao. Haiwezekani kila mtu alalamike, Kuna shida mahali na tunahijua japo atulazimishwi kuwalazimisha mfanye tuonavyo sisi.