Emc2
JF-Expert Member
- Sep 26, 2011
- 16,808
- 16,835
Kwa hakika nchi yetu imeanza kujikwamua tena kwa kasi sasa. Nataraji mda si mrefu nchi yetu itakuwa na maendeleo makubwa.
Nimekuwa nikijionea kwa macho yangu jinsi miradi mbalimbali hapa nchini inavyoenda kwa kasi. Hii ni dalili tosha kabisa kwamba viongozi wetu wameamka kutoka katika usingizi waliokuwa nao.
Nitajaribu kutaja baadthi ya miradi inayoendelea hapa nchini na italeta chachu kubwa sana ya maendeleo.
1. Ujenzi wa Hospitali ya kimataifa: Huu ni mradi ambao tayari umekwisha kuanza. Hospitali hiyo itajengwa maeneo ya kisarawe ambayo itakuwa na kiwanja cha ndege. vilevile kutakuwepo na chuo cha madaktari, wauguzi na wafamasia. Hospitali hiyo itarajiwa kumalizika mwaka 2014.
2. Ujenzi wa daraja la kigamboni: Huu mradi tayari umeshafunguliwa na tayari sasa daraja kwaajiri ya kuwasaidia wajenzi limeshawekwa. ni matumaini yangu mda si mrefu ujenzi wa daraja hilo utaanza.
3. Mabasi yaendayo kwa kasi: Katika kutatua tatiza la foleni kwa wenyeji wa dar es salaam nadhani wanajionea wenyewe jinsi shughuli za ujenzi wa njia za mabasi yaendayo kwa kasi inavyo enda kwa kasi.
4. Upanuzi wa barabara mbalimbali: Kila mmoja mwenye macho anaona jinsi miradi ya ujenzi na upanuzi wa barabara zetu unavyo enda kwa kasi.
5. Kupitiwa kwa mikataba mbalimbali: Mikataba mbalimbali ambayo ni mibovu inapitiwa na kurekebishwa. Mikataba ya madini na na mingine mingi tu.
6. Kuwa na umeme wa kudumu: Ujenzi wa bomba la gesi abao kwa uhakika utaondoa kabisa tatizo la umeme nchini.
7. Reli ya tazara: Ukarabati wa reli ya tazara utarahisisha usafiri wa watu waendao kusini mwa tanzania tayari sasa serikali ya Tanzania, Zambia na China wameshaanza utaratibu wa kuikarabati reli hiyo.
Kwa hayo machache tu na mengine yapo mengi. Hii ni dalili tosha kabisa nchi yetu inapiga hatua kwa kasi.
Tutambue kuwa kuna nchi hawataki kuona nchi yetu ikiendelea maana itakapoendelea watakuwa hawana chao kwetu.
Kwahiyo anayebeza maendeleo haya basi hana nia njema na nchi yetu.
Nimekuwa nikijionea kwa macho yangu jinsi miradi mbalimbali hapa nchini inavyoenda kwa kasi. Hii ni dalili tosha kabisa kwamba viongozi wetu wameamka kutoka katika usingizi waliokuwa nao.
Nitajaribu kutaja baadthi ya miradi inayoendelea hapa nchini na italeta chachu kubwa sana ya maendeleo.
1. Ujenzi wa Hospitali ya kimataifa: Huu ni mradi ambao tayari umekwisha kuanza. Hospitali hiyo itajengwa maeneo ya kisarawe ambayo itakuwa na kiwanja cha ndege. vilevile kutakuwepo na chuo cha madaktari, wauguzi na wafamasia. Hospitali hiyo itarajiwa kumalizika mwaka 2014.
2. Ujenzi wa daraja la kigamboni: Huu mradi tayari umeshafunguliwa na tayari sasa daraja kwaajiri ya kuwasaidia wajenzi limeshawekwa. ni matumaini yangu mda si mrefu ujenzi wa daraja hilo utaanza.
3. Mabasi yaendayo kwa kasi: Katika kutatua tatiza la foleni kwa wenyeji wa dar es salaam nadhani wanajionea wenyewe jinsi shughuli za ujenzi wa njia za mabasi yaendayo kwa kasi inavyo enda kwa kasi.
4. Upanuzi wa barabara mbalimbali: Kila mmoja mwenye macho anaona jinsi miradi ya ujenzi na upanuzi wa barabara zetu unavyo enda kwa kasi.
5. Kupitiwa kwa mikataba mbalimbali: Mikataba mbalimbali ambayo ni mibovu inapitiwa na kurekebishwa. Mikataba ya madini na na mingine mingi tu.
6. Kuwa na umeme wa kudumu: Ujenzi wa bomba la gesi abao kwa uhakika utaondoa kabisa tatizo la umeme nchini.
7. Reli ya tazara: Ukarabati wa reli ya tazara utarahisisha usafiri wa watu waendao kusini mwa tanzania tayari sasa serikali ya Tanzania, Zambia na China wameshaanza utaratibu wa kuikarabati reli hiyo.
Kwa hayo machache tu na mengine yapo mengi. Hii ni dalili tosha kabisa nchi yetu inapiga hatua kwa kasi.
Tutambue kuwa kuna nchi hawataki kuona nchi yetu ikiendelea maana itakapoendelea watakuwa hawana chao kwetu.
Kwahiyo anayebeza maendeleo haya basi hana nia njema na nchi yetu.