Anayeamini kuna vita ya kupambana na madawa ya kulevya nampa pole

hii vita tutashinda?


  • Total voters
    45

Salary Slip

JF-Expert Member
Apr 3, 2012
46,982
144,308
Sitaki kuamini na nitakuwa wa mwisho kuamini kuwa kuna vita ya kweli inaendelea kuhusu kinachoitwa kupambana na madawa ya kulevya bali nahisi kuna jambo nyuma ya zoezi hii.

Maswali ya kujiuliza kama kweli kuna dhamira ya dhati ya kupambana na hii biashara.

1.Unaweza kweli kuanika hadharani majina ya watu unaowatuhumu kabla hujawakamata /hujawafanyia uchunguzi?

2.Wakitoroka au kuharibu ushahidi sio wewe ulietangaza ndio utakuwa umewapa nafasi na muda wa kuharibu ushahidi au kutoroka?

3.Unawezaja kuanika hadharani majina ya watu unaotaka wakupe taarifa za kiuchunguzi?

3.Nani atakuwa tayari kutoa taarifa wakati umeshamuanika hadharani?

4.Huku si kuhatarisha maisha ya watu unaotaka wakupe taarifa?

5.Kama kweli uko serious,unaendaje kum-search mtu ambae tayari anajua leo au kesho atakuja kukaguliwa nyumbani kwake na isitoshe tayari ameshaona waliotangazwa kabla yake wamekaguliwa?

6.Unapoenda kum-search mtu kama huyo,unatarajia yeye awe mjinga kiasi gani asifiche au kuharibu ushahidi?

7.Mwisho wa zoezi hili si itakuwa tu ni kusafisha baadhi ya watuhumiwa(kwa kukosekana ushahidi)huku wengine wakichafuliwa?


Nina mashaka sana na zoezi hili zima na mwenendo wake.
 
me naona jamaa wanataka kupandisha bei ya unga! wanaouza ndo haohao wanaopiga vita. kuna teja mmoja jana kanambia bei imepanda maradufu kutokana na harakati za makonda.
 
Kama Tanzania imeshindwa kumdhibiti Mbu anaesambaza malaria!
Itaweza kumdhibiti, mtu anaesambaza madawa ya kulevya?
Mbu wapo Bonde la msimbaz hapo kama nzige kujenga mfereji Tu hakuna hata mmoja anaongelea sio mbal Na magogon lakin wameshindwa je ishu ya madaw ndo watafanyej?watu wanasubir waone mwisho Wa filam hii ya comedy mshind atajulikana
 
Mimi simshangai Makonda yeye tushamzoea ni mropokaji na mtu wa matamko ambayo utekelezaji sifuri nawashangaa Polisi hasa kamanda Sirro ambaye kwa suala hili la madawa ya kulevya kufanya kazi kinyume na taaluma ya Polisi.
Baada ya kupata majina polisi ilibidi wachunguze kwa kina wahusika wote wafanye upelelezi wa kina ndio wawakamate na kuwafikisha mahakamani.
Unamtaja mtu halafu baada ya siku mbili ndio unamfanyia upekuzi hiki ni kituko cha Karne.
 
Habari wanajamvi
Naomba kwanza kabla sijaanza chochote niweke kwanza swala moja sawa kwamba je Mkuu wa mkoa au wa wilaya wana haki au mamlaka ya kisheria kukamata MTU (Arrest) au kumuweka MTU under custody (chini ya ulinzi)

Kwa mujibu wa sheria ya tawala za mikoa ya mwaka 1997 The regional administration Act ambayo ndo inatoa mgawanyo na mipaka ya kimamlaka mwa mikoa na wakuu wa mikoa ukisoma kifungu cha 7(1) cha sheria hii kinatoa mamlaka kwa mkuu wa mkoa kuweza kukamata MTU yeyote aliyetenda kosa au ambaye mkuu wa mkoa naweza ona anahatarisha usalama wa eneo husika.

Pia ukisoma kifungu cha 7(4) pia kinatoa ukomo wa SAA 48 kwa MTU ambae amekuwa arrested kwa order ya mkuu wa mkoa kukaa ndani au kuwa under custody.
Nimeweka hili ili niweke kwanza sawa mamlaka aliyonayo kisheria mkuu wa mkoa katika kukamata MTU n.k.

Lengo la Uzi huu ni kuonesha sheria inasema nn kuhusu dawa za kulevya ,taratibu zipi za kufuatwa katika kudeal na tatizo hili na ni nani anapaswa kuhusika na utaratibu wa jumla wa kisheria wa kukabiriana na suala hili

.Sasa kwa mujibu wa sheria ya Dawa za kulevya [Sura ya 95] ukisoma vifungu vifuatavyo Kifungu cha 10(1) na kile cha 10(2) vipengele (a) (b) na (c) vifungu HV vinaeleza MTU au watu wnye mamlaka ya kukamata wahusika wa dawa za kulevya katika kifungu cha 10(1)

Kifungu cha 10(2) kinaeleza hatua ambazo serikali inabid izifuate katika kudeal na tatzo ikihusisha maofisa waliotajwa katika kifungu kidogo cha kwanza then kifungu cha 10(2)(a) hapo sheria inasema serikali itadeal na tatizo kwa kufanya coordination ya vyombo mbali mbali vya kiauslama na (b) inaeleza itashirikisha pia taasisi za kimataifa na jumuiya ya kimataifa katika kudeal na tatizo.

Ukienda kifungu vifungu vya 30 na 31 sheria inatoa mamlaka kwa officers waliotajwa katika kifungu cha 10(1) kufanya upekuzi na ukaguzi katka maeneo ya washukiwa.

Baada ya kuona vipengele hvyo vya kisheria apo juu tunarud katika uhalisia wa hii vita ya dawa za kulevya ambapo mpka sasa cjaona sheria iliyokiukwa mpka hatua na mchakato ulipofikia hapa ila nachokiona ni unafiki na mahaba ya kisiasa yaliyotamalaki katika nchi hii.

Kuna wakati 2013 waziri Lukuvi amewahi shinikizwa na bunge kutaja list ya wahusika wa dawa za kulevya na lbd kwa upande wao kipindi kile walikua sahh na walizngatia sheria ila Leo makonda kakiuka sheria...Hii ndio hatua tuliyofikia kama taifa ,kuleta unafiki na siasa hata kwa mambo yenye maslahi kwa taifa.

Nadhan n vema sasa ifike wakati kuwe na qualifications za kielemu za kuwa mbunge kama itashndkna BC uwekwe hata utaratibu wa wawakilishi wetu kuwa na utaratibu wa kusoma sheria hata kwa shuruti kwa sababu unashangaa anasimama mwakilishi KBS anahoji eti n wapi mkuu wa mkoa anapata mamlaka ya kumkamata MTU unabaki kujiuliza kama sheria ndg tu hii haijui n VP kuhusu hzo sheria tunazotarajia zitungwe kupitia yeye?

I'll be back badae

Stand to be corrected

Nkololo-(LLB)
 
Back
Top Bottom