anaumwa nini jamani

SAIZI YANGU

JF-Expert Member
Nov 8, 2013
381
83
Mke wangu alipatwa maralia na kupewa dawa Duo cotexin na panadol kwa siku tatu. Amemaliza dozi trh 17 Dec. Lakini ameendelea kutapika,kuumwa kichwa, kuharisha na joto kupanda. Kuona hali haibadiriki, tarehe 19 Dec alirudi hospital ambako alipimwa na kukutwa hana maralia na kuchomwa sindano za kuzuia kutapikan na vidonge vya kusafisha mkojo kwani ilionekana mkojo ni mchafu. Alikuwa hana typhod wala maradhi mengine (HIV).Alipewa pia vidonge vya kuzuia kutapika. Cha kushangaza anazidi kuumwa kichwa, kutapika na joto kupanda. Anaumwa nini na nifanyaje kumtibu?
 
Mpeleke hospitali nyingine tofauti na uliyompeleka mwanzo. Pili kama anatapika mara kwa mara na kuumwa kichwa basi mtengenezeeni juisi ya matunda na anywe kila mara asije akaishiwa maji.
 
Hebu mpeleke tena akaangalie tena 'UTI'

Sent from my BlackBerry 9900 using JamiiForums
 
asije akawa ana aleji na hiyo miduo cot ukisoma vuziri wanasema hayo ulioyasema hutokea kam zimekukataa..
 
kama yupo hospital tayari bas maombi yanaitajika dunia ya leo nayo inamengi
 
Wamemcheki mimba, coz mimba pia inawezekana ikaleta dalili kama hizo hasa wiki 12 za mwanzo. Pia kama hana mimba yawezekana typhoid inawezekana ikawa na dalili kama hizo. Na mwisho kabisa wamcheki BP nayo anaweza kuwa nayo.
 
Hapo kwenye maumivu ya kichwa napata la kusema. Hicho kichwa kinaumaje?Maana kuna aina 15 za maumivu ya kichwa. Pia mkeo ni mnene na anasumbuliwa na maumivu ya miguu mara kadhaa?Nategemea majibu yako mkuu.
 
Akapime tena vipimo vyote malaria ina tabia ya kujificha au pengine ana ujauzito
 
Mimba hana, ila kama hali inaendeleea hivi kesho J2 namrudisha tena hospital.
Wamemcheki mimba, coz mimba pia inawezekana ikaleta dalili kama hizo hasa wiki 12 za mwanzo. Pia kama hana mimba yawezekana typhoid inawezekana ikawa na dalili kama hizo. Na mwisho kabisa wamcheki BP nayo anaweza kuwa nayo.
 
Mke wangu ni mnene wa wastani (34yrs) na hasumbuliwi na miguu. Kichwa kinamuuma utosini.
Hapo kwenye maumivu ya kichwa napata la kusema. Hicho kichwa kinaumaje?Maana kuna aina 15 za maumivu ya kichwa. Pia mkeo ni mnene na anasumbuliwa na maumivu ya miguu mara kadhaa?Nategemea majibu yako mkuu.
 
Updates, joto limepungua na kutapoika tokea jana kaacha ila kaanza kuharisha na vichomi maeneo ya kiunoni. Nategemea kesho nimpeleke hospital.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom