Mnyamahodzo
JF-Expert Member
- May 23, 2008
- 1,932
- 985
Unapotafakari kuhama kwa The Nyalandu kuyoka CCM kwenda CHADEMA na Yale yanayomsibu kuna mambo mengi utang'amua.
Kwasasa tunasheria ya Uhalifu/makosa ya kimtandao, mbona haifanyikazi pale Nyalandu anapozushiwa mambo lakini inataka kufanya kazi kwa wale wenye kumtetea? maana kauli za vitisho zinayylewa dhidi yao.
Wanaomshambulia Nyalandu, je ndiyo haohao wanaomchukia Lissu?
Tuanze kwa maswali rahisi ili tutakapoingia kwenye maswali magumu, tusiachwe midomo wazi kwa mshangao.
- Mwl Nyerere akiwa Mwenyekiti wa TANU na CCM wako waliotoka katika TANU kwa sabbu tofauti ikiwa ni pamoja na Oscar Kambona, Kasanga Tumbo, n.k.
- Alhaji Mwinyi akiwa Mwenyekiti wa CCM, wako waliotoka CCM kwasababu mbalimbali ikiwani pamoja na Barongo, Augustine Mrema, Mabele Marando, Kighoma Malima, Maalim Seif S Hamad, n.k.
- Mzee Mkapa akiwa Mwenyekiti wa CCM, wako waliotoka CCM kwasababu mbalimbali ikiwa pamoja Dr W. Slaa, Mzee Tumbo,
- Kanali Kikwete akiwa Mwenyekiti was CCM, wako waliotoka CCM kwasababu mbalimbali ikiwa pamoja na Mpendazoe, Shibuda, Kingunge Mwiru, Lowasa, n.k.
- Mwl Magufuli akiwa Mwenyekiti wa CCM, kiongozi aliyehama CCM kwasasa ni Lazaro Nyalandu.
- Nani anawatuma kumshambulia Nyalandu?
- Wanaomshambulia Nyalandu wanamsukumo wa dhati toka ndani mwao au ni maagizo au wanafanya kumfurahisha MTU.
- Ni nani anayechukizwa zaidi na kuhama kwa Nyalandu, hao wenye kuzumngumza au Mwenyekiti wa Chama?
- Unafikiri sababu alizozitoa Nyalandu juu ya kuihama CCM, zinamuathiri zaidi mwanachama au Mwenyekiti?
Kwasasa tunasheria ya Uhalifu/makosa ya kimtandao, mbona haifanyikazi pale Nyalandu anapozushiwa mambo lakini inataka kufanya kazi kwa wale wenye kumtetea? maana kauli za vitisho zinayylewa dhidi yao.
- Juu ya Mhe Waziri Kigwangala kumshambulia Nyalandu, ambaye anaweza akafikia kiwango cha kutoa siri za Baraza la Mawaziri, je kutamjenga Kigwangala na kumchafua Nyalandu tu au hadi Kikwete?
- Kitendo cha Kigwangala kumshambulia Nyalandu unafikiri kina faida ya kuwaonyesha wote walokuwa nyuma yake, kwamba mheshimiwa haogopi kitu au lugha ya mtu muoga kushindwa kupambana nao mwenyewe isipokuwa kwa mgongo wa Nyalandu anapiga kelele?
- Kwanini Kigwangala hamtaji Mhe Maige au Maghembe au Zakhia Meghji bali Nyalandu?
Wanaomshambulia Nyalandu, je ndiyo haohao wanaomchukia Lissu?
Tuanze kwa maswali rahisi ili tutakapoingia kwenye maswali magumu, tusiachwe midomo wazi kwa mshangao.