Anataka kumroga hadi kumuua aliyeachana naye

Black hermit

JF-Expert Member
Mar 20, 2017
658
945
Habari za Eid pili, bila kuchelewa niingie moja kwa moja kwenye jambo lenyewe, nina rafiki yangu ambaye nilisoma naye Tabora TC (2011) baada ya kumaliza hatukuwahi kuonana tena kwani yeye yupo Dodoma mimi Tanga lakini tuna mawasiliano ya mara kwa mara,

juzi kanipigia simu ananiambia alifanikiwa kumpata binti na akaoa wakawa wanaishi pamoja na kufanikiwa kupata mtoto mmoja ghafra mkewe akabadilika ghafra na hataki tena kuendelea naye na ameondoka yuko kwa dada yake Babati jamaa anasema hadi sasa kesharudishiwa na mahari kabisa na kinachomuumiza zaidi hadi anishirikishe ni kwamba wamemkata pesa kibao wakidai za mtoto na mkwe anamtusi na kumtishia atakujwa kuchukua vitu wagawane wakati binti kaondoka mwenyewe,

kibaya zaidi binti ana jamaa na anamrusha fb ili kumuumiza mshkaji wangu hasira zaidi kwa msela wangu ni kwamba alichukua kamkopo sasa maisha kidogo yanakuwa havy na anapata wakati mgumu akikumbuka baadhi ya pesa alitumia kumsomesha mkewe hadi akamaliza nursing,

sasa ameamua liwalo na liwe kaniambia anataka kuja kwangu nimpeleke pangani madanga kuna mzee makata ni shida sana akamalize kabisa biashara bora wakose wote maba akimuona hajisikii vizuri,

bado sijamjibu natafakari sijui nimwambieje kuua siyo mchezo wakuu, nipeni mawazo nimshauri.
 
Waambie vita ya uchawi haina mshindi
Atamuua huyo x wake, ndugu wa x wake wataagua na kujua aliyeua nao watalipa kisasi upande wa pili. Ndugu wa upande wa pili wataagua na kulipa kisasi. Utakua ni mwendo wa kuuana na kugeuzana mandondocha. Mshauri tu kuwa asiwe na shingo ngumu, amalize hilo kwa mazungumzo hata kama atapata hasara akubali tu maana wahenga tunasema " hasara roho, pesa makaratasi".
 
Waambie vita ya uchawi haina mshindi
Atamuua huyo x wake, ndugu wa x wake wataagua na kujua aliyeua nao watalipa kisasi upande wa pili. Ndugu wa upande wa pili wataagua na kulipa kisasi. Utakua ni mwendo wa kuuana na kugeuzana mandondocha. Mshauri tu kuwa asiwe na shingo ngumu, amalize hilo kwa mazungumzo hata kama atapata hasara akubali tu maana wahenga tunasema " hasara roho, pesa makaratasi".
Swadakta
 
Machungu yamemjaa ndo mana
Amshkr tu Mungu ni mitihani hiyo anapewa,Mwenyez Mungu anapenda watu wenye kusubir mshauri atulize akili na amuombe Mungu saaaaana huenda ikawa kunajingine kubwa ameepushwa nalo yaaan tena akienda huko ndo atazidi kuona matatizo yanaongezeka

Mali na watoto ni mapambo ya dunia tu(mtihani) akaze buti na kumuomba Mungu wake
 
Nilidhani mnapofunga mnatubu dhambi na kuziacha, kumbe ndiyo mnarecharge uovu? Shetani haondoki kwa kushinda njaa!. Mtafuteni Mungu kwa njia ya Yesu Kristo nanyi mtaokolewa pamoja na nyumba zenu. ELOHIM awarehemu.


Habari za Eid pili, bila kuchelewa niingie moja kwa moja kwenye jambo lenyewe, nina rafiki yangu ambaye nilisoma naye Tabora TC (2011) baada ya kumaliza hatukuwahi kuonana tena kwani yeye yupo Dodoma mimi Tanga lakini tuna mawasiliano ya mara kwa mara, juzi kanipigia simu ananiambia alifanikiwa kumpata binti na akaoa wakawa wanaishi pamoja na kufanikiwa kupata mtoto mmoja ghafra mkewe akabadilika ghafra na hataki tena kuendelea naye na ameondoka yuko kwa dada yake Babati jamaa anasema hadi sasa kesharudishiwa na mahari kabisa na kinachomuumiza zaidi hadi anishirikishe ni kwamba wamemkata pesa kibao wakidai za mtoto na mkwe anamtusi na kumtishia atakujwa kuchukua vitu wagawane wakati binti kaondoka mwenyewe, kibaya zaidi binti ana jamaa na anamrusha fb ili kumuumiza mshkaji wangu hasira zaidi kwa msela wangu ni kwamba alichukua kamkopo sasa maisha kidogo yanakuwa havy na anapata wakati mgumu akikumbuka baadhi ya pesa alitumia kumsomesha mkewe hadi akamaliza nursing, sasa ameamua liwalo na liwe kaniambia anataka kuja kwangu nimpeleke pangani madanga kuna mzee makata ni shida sana akamalize kabisa biashara bora wakose wote maba akimuona hajisikii vizuri, bado sijamjibu natafakari sijui nimwambieje kuua siyo mchezo wakuu, nipeni mawazo nimshauri.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom