Anataka akatambulishwe.

Husninyo

JF-Expert Member
Oct 24, 2010
23,723
9,188
Mpenzi anataka nikamtambulishe kwetu, tupo kwenye uhusiano mwaka wa saba sasa. Bado cjafikiria ndoa hata kidogo.
Naomba kujua umri mzuri kwa ke na me kuoana.
Pia nishaurini namna ya kumkatalia ili asijickie vibaya.
 
You better decide to continue with her or let her free. Naona unampotezea muda, miaka saba kwenye uhusiano ni mingi sana na inatosha wewe kufanya maamuzi ya kuoa. Kama una umeshafikisha miaka zaidi ya 18, unaweza kuoa. Suala hapa ni utashi. Je, ni kitu gani kinachokufanya usifanye uamuzi wa kuoa, je, ni uchumi au nini?

Kwa kuwa umekuwa naye kwa miaka 7, ana haki kabisa ya kutaka afahamike kwenu.
 
Duh miaka saba kwenye mahusiano bila kutambulishana! Hongera lakini kwa mtazamo wangu that may be too much. Kama hamtaki kutambulishana then kaeni tena chini mjadiliane lengo hasa la uhusiano wenu ni nini? Na lini mtafanya hicho anachoomba mwenzio na zipi sababu za msingi. Kumbuka kadri mnavyoendelea mbele ndio mtakavyoumia likitokea la kutokea (Siombei iwe hivyo). Umri ni miaka 18 (kisheria) na kuendelea but depending on other factors kama uchumi, masomo, umbali, etc
 
Duuh,

You're time waster, 7 years ??? vitukoz. You just set her free
 
I can say, your partner is the most patient person that's still left on earth..probably, u wont find any1 else who'll be ready to be treated like a concubine for 7 years..

Be serious, 7 years is way tooooo much..ana kila haki ya kutambulishwa kwenu.

Don't forget, binadamu tunaishi kwa expectation..kama umekaa naye all that time na huna clue kuhusu umuhimu wake kwako, chances are that she'll get tired and walk out on you when you least expect it..and you won't have anyone else to blame but yourself for keeping her waiting.

Good luck, Make a wise decision..!!
 
Kutokumtambulisha mpenzi wako miaka 7 ulimwengu wa leo si jambo la kujisifu mpeleke nyumbani haraka, tutakusindikiza.
 
umri usiwe chini ya miaka 25 kwa me na usiwe chini ya miaka 23 kwa ke. Ukitaka acchukie wewe mkubalie tu!
 
Miaka Saba???? Duh you are joking kijana? Nadhani wewe ndio una matatizo tena makubwa. Huyo Binti ni mvumilivu sana tena nampa big up kubwa sana. na ana haki kabisa ya kutaka kutambulishwa. Mimi nadhani mahusiano yenu may be hayana msimamo na mmependana tu na kuingizana chumbani basi huwa hamjadili nini malengo yenu ya baadae maana eeehhh 7yrs mmmhh hapana thats too much. Amua moja kama unamuoa au humuoi umpe muda mtoto wa watu usikae kumchezea kila siku halafu ukambwaga. Hebu kuwa na huruma kijana ungekuwa wewe unafanyiwa hivyo ungejisikiaje?? Kama huna mpango wa kumuoa sema kabisa mapema ajue nini cha kufanya.
 
Ahsanteni wote kwa ushauri ila wengi mnaojibu mnafikiri mimi ni mwanaume.
Mimi ni mwanamke, hebu wadau ifikirieni tena kwa upande wa pili.
 
Miaka Saba???? Duh you are joking kijana? Nadhani wewe ndio una matatizo tena makubwa. Huyo Binti ni mvumilivu sana tena nampa big up kubwa sana. na ana haki kabisa ya kutaka kutambulishwa. Mimi nadhani mahusiano yenu may be hayana msimamo na mmependana tu na kuingizana chumbani basi huwa hamjadili nini malengo yenu ya baadae maana eeehhh 7yrs mmmhh hapana thats too much. Amua moja kama unamuoa au humuoi umpe muda mtoto wa watu usikae kumchezea kila siku halafu ukambwaga. Hebu kuwa na huruma kijana ungekuwa wewe unafanyiwa hivyo ungejisikiaje?? Kama huna mpango wa kumuoa sema kabisa mapema ajue nini cha kufanya.

dena mimi ni msichana, boyfriend ndio anataka nikamtambulishe.
 
sasa siku zote hizo hutaki kumtambulisha kwa nn?au unamambo yako unafanya?kupotezeana mda si kwa wanaume tu,hata wanawake wanapotezea wenzao mda,kwann unampotezea kaka wa watu mda?una bahati anakupenda aza wise ungesoma vumbi lol,wenzio wanatambulisha ndani ya mwezi ww unaongelea miaka,duh,lkn mapenzi yanamsimu wake,subiri tu it will cme ur turn zen utajua wat goes around cmes around.
Ahsanteni wote kwa ushauri ila wengi mnaojibu mnafikiri mimi ni mwanaume.
Mimi ni mwanamke, hebu wadau ifikirieni tena kwa upande wa pili.
 
Ahsanteni wote kwa ushauri ila wengi mnaojibu mnafikiri mimi ni mwanaume.
Mimi ni mwanamke, hebu wadau ifikirieni tena kwa upande wa pili.

Miaka saba jamani kwani kaka yako huyo heheheh hebu mpe nafasi akatafute mke mwingine kama wewe hutaki
 
dena mimi ni msichana, boyfriend ndio anataka nikamtambulishe.

Siku hizi wanaume hawaombi kutambulishwa wenzako wanasubiri kama wataisikia hiyo kauli hawaisikii ng'o , Binti huyo wa kwako ni mstaarabu sana hebu mpe nafasi akatafute mwenza aliye tayari ... sawa mama
 
Back
Top Bottom