Wilson Gamba
JF-Expert Member
- Mar 1, 2013
- 777
- 749
Kama mada inavyojieleza hapo juu, huyu ndugu alikuwa askari magereza katika gereza la Musoma miaka ya 1980 na aliondoka Musoma mwaka 1983.
Anatafutwa na kijana wake anaitwa Matiku alimzaa na mama mmoja anaitwa Monika mwenyeji wa Musoma Vijijini,alizaliwa miaka ya 1981.Kwa mujibu wa mama Monika,mzee Michael Juma alikuwa na mke mnyilamba wa Singida ambapo kwa kipindi hicho walikuwa na mtoto wa kike jina lake Anna na huyu mama walikuwa wanamwita mama Anna.
Pia mzee Michael Juma alikuwa anasema wazazi wake walikuwa wanaishi Masasi na badae walihamia Mtwara Mjini kwa muda,bahati mbaya jina la babu yake mzeze Michael hatukuweza kulipata.
Kama huyu mzee bado yupo hai au kama kuna mtu anamjua au kama huyu binti yake yupo naomba sana kwani JF inaiunganisha Tanzania ,naomba tuwasiliane kwa namba 0789443404/0762364740.
Hii itasaidia huyu jamaa aweze kuwapata ndugu zake,kikubwa anataka tu amwone mzee wake na pia aweze kumsaidia hata kumjengea nyumba mbali na kwamba hakumlea lakini ni haki yake hafanye hivyo kwa baba yake.
ASANTENI
Anatafutwa na kijana wake anaitwa Matiku alimzaa na mama mmoja anaitwa Monika mwenyeji wa Musoma Vijijini,alizaliwa miaka ya 1981.Kwa mujibu wa mama Monika,mzee Michael Juma alikuwa na mke mnyilamba wa Singida ambapo kwa kipindi hicho walikuwa na mtoto wa kike jina lake Anna na huyu mama walikuwa wanamwita mama Anna.
Pia mzee Michael Juma alikuwa anasema wazazi wake walikuwa wanaishi Masasi na badae walihamia Mtwara Mjini kwa muda,bahati mbaya jina la babu yake mzeze Michael hatukuweza kulipata.
Kama huyu mzee bado yupo hai au kama kuna mtu anamjua au kama huyu binti yake yupo naomba sana kwani JF inaiunganisha Tanzania ,naomba tuwasiliane kwa namba 0789443404/0762364740.
Hii itasaidia huyu jamaa aweze kuwapata ndugu zake,kikubwa anataka tu amwone mzee wake na pia aweze kumsaidia hata kumjengea nyumba mbali na kwamba hakumlea lakini ni haki yake hafanye hivyo kwa baba yake.
ASANTENI