Candela
JF-Expert Member
- Aug 12, 2021
- 589
- 1,529
Habari wadau. Kuna mtu wangu wa karibu amenifuata akitaka ushauri juu ya mahusiano yake. Anajiuliza kama anaweza kumuacha mpenzi wake au aendelee nae.
Anasema alikutana na huyu binti miaka miwili iliyopita, wakati akimtongoza binti alisema anataka mtu siriaz amechoka kuchezewa ndio maana ameamua kukaa singo. Jamaa akakomaa mpaka akampata huyu binti lakini ndani ya miezi miwili ya mahusiano yao akabaini binti ana mahusiano na wanaume wengine wawili kwa takribani miaka 3 na mwingine miaka 5.
Anasema aliamua kukaa kimya kwa kuamini kama binti ameamua kuwa nae basi huenda hana mpango na hao jamaa labda hakupata tu mtu ataekuwa karibu.( hao jamaa wote ni waume za watu). Kwa imani hiyo jamaa akavumilia kuwa nae karibu huyu binti mpaka siku 1 alipomuaga anaenda kusalimia ndugu lakini kumbe alienda kwa mwanaume mwingine. akalala huko siku 2 kisha akarudi kwa jamaa.
Licha ya jamaa kugundua ukweli na mpaka aliongea na jamaa kwa simu alipoipokea simu ya binti wakati alipompigia saa 8 za usiku, bado hakuweza kumuacha, aliendelea nae. Kwa sasa anadai binti amesafiri tena kaenda kwa jamaa wa mwingine na amejaribu kumuuliza anaenda wapi anasema majibu hayamridhishi kabisa, binti anadai akifika anakoenda atamwambia lakini tangu amesafiri simu haipatikani tena.
Anasema anavumilia sana ameshindwa aamue nini kwani binti amwemwambia ana ujauzito wake hivyo anajikuta njia panda kumkataa asije sema kaikataa mimba.
Binafsi nimekosa cha kumshauri nimeona niwadondoshee wadau hapa tupate mitazamo tofauti.
Nawasilisha.
Anasema alikutana na huyu binti miaka miwili iliyopita, wakati akimtongoza binti alisema anataka mtu siriaz amechoka kuchezewa ndio maana ameamua kukaa singo. Jamaa akakomaa mpaka akampata huyu binti lakini ndani ya miezi miwili ya mahusiano yao akabaini binti ana mahusiano na wanaume wengine wawili kwa takribani miaka 3 na mwingine miaka 5.
Anasema aliamua kukaa kimya kwa kuamini kama binti ameamua kuwa nae basi huenda hana mpango na hao jamaa labda hakupata tu mtu ataekuwa karibu.( hao jamaa wote ni waume za watu). Kwa imani hiyo jamaa akavumilia kuwa nae karibu huyu binti mpaka siku 1 alipomuaga anaenda kusalimia ndugu lakini kumbe alienda kwa mwanaume mwingine. akalala huko siku 2 kisha akarudi kwa jamaa.
Licha ya jamaa kugundua ukweli na mpaka aliongea na jamaa kwa simu alipoipokea simu ya binti wakati alipompigia saa 8 za usiku, bado hakuweza kumuacha, aliendelea nae. Kwa sasa anadai binti amesafiri tena kaenda kwa jamaa wa mwingine na amejaribu kumuuliza anaenda wapi anasema majibu hayamridhishi kabisa, binti anadai akifika anakoenda atamwambia lakini tangu amesafiri simu haipatikani tena.
Anasema anavumilia sana ameshindwa aamue nini kwani binti amwemwambia ana ujauzito wake hivyo anajikuta njia panda kumkataa asije sema kaikataa mimba.
Binafsi nimekosa cha kumshauri nimeona niwadondoshee wadau hapa tupate mitazamo tofauti.
Nawasilisha.