Mimi ni kijana wa miaka 30, sijaoa lakini niko kwenye mahusiano na Dada mmoja ni mwaka wa nne sasa. Nina kazi nzuri tu na kipato kizuri na kwakweli najitahidi kumhudumia huyu Dada kwa kila kitu. Yeye anafanya kazi lakini hata siku moja sijawahi kumuulizia kuhusu pesa yake. Hatuishi pamoja, yeye bado anaishi kwao lakini matumizi yote ya nyumbani kwao mimi ndiyo natoa.
Anaishi na wazazi wake wote ila ananiambia kuwa kwakua mimi ni mpenzi wake natakiwa kumhudumia na kwakua anaishi kwao basi ni lazima kuwahudumia na wazazi wake kwani hawezi kujinunulia chakula peke yake. Basi mimi hilo sina shida nalo kwani kama mwanaume naona kama ni majukumu yangu. Sababu ya kuja kwako Kaka ni hivi, huyu mwanamke bado hajamsahau X wake.
X wake ameoa lakini kila akigombana na mke wake anamtafuta mpenzi wangu wanaongea, nikimuuliza kwanini unaongea naye ananiambia ni urafiki tu kisha ananinunia hata wiki mpaka mimi ndiyo nimuombe msamaha. Niliamua kumpigia X wake na kumuambia kuwa yeye si anandoa basi aniachie mwanamke wangu lakini aliniambia kuwa hana mpango naye alishamuacha ila mimi ndiyo niongee na mtu wangu.
Shida inakuja hivi, baada ya mimi kuongea na X wake basi amebadilika, amekua mtu wa hasira na kila siku ananiambia kuwa tuachane. Ananiambia kuwa nimemdhalilisha kuwa kwa mimi kumpigia X wake ni kama nimemuita yeye malaya kuwa anarudia matapishi ili tuachane. Alilazimisha sana tuachane, akakata mawasiliano kabisa na mimi, kwakua nampenda basi niliamua kwenda kwa wazazi wake na kuwaambia ili waongee naye.
Niliwaambia kuwa nipo tayari kumuoa wakati wowote, wazazi wake waliongea naye na kweli alinisamehe. Basi niliona ili nisimpoteze na kumziba X wake nitoe mahari moja kwa moja, nilitoa mahari ingawa ishu ya ndoa aliniambia kuwa yeye bado hajajipanga lakini niliona kwa kutoa mahari basi atakua wangu.
Lakini haikua hivyo Kaka, pamoja na kutoa mahari ndiyo alibadilika zaidi, yaani amekua mtu wa hasira, amekua mtu wa kununa nuna sijui hata nifanyeje. Kuna wakati nilijikuta nakasirika na kumuambia kuwa bora tuachane kwani nimechoka, nikamtafuta mshenga na kumuambia ukweli kuwa nimechoka nataka aende kuwaambia wazazi wake kuwa nimechoka nataka kuachana naye, kweli nilikua nimechoka na nilipanga kumuacha.
Lakini baada ya kuona nimemtafuta mshenga aliniambia kuwa namdhalilisha kumtolea mahari kisha kumuacha. Alinizimia simu, nilikuja kupigiwa simu baadaye na X wake kuwa anataka kujiua na kanywa sumu wako hospitalini. Nilikua na hasira lakini nilienda na kwelia likua kalazwa hospitalini, alinilaumu mimi kuwa nimemdhalilisha kwani nikimuacha nisipomuoa hatapata mwanaume mwingine wa kumuoa.
Ana mika 32, kusema kweli nampenda na nipo tayari kumuoa, lakini nashindwa kujua kama ananipenda kweli au la. Ananiambia ananipenda ni mimi tu sijiamini yeye hana chochote na X wake ni marafiki tu lakini nilishawahi kuona anamtumia mpaka picha za uchi X wake, nikimuuliza ananiambia kwani kuna ubaya gani kama ni kumuona alishamuona kila kitu hakuna jipya, nimechanganyikiwa.
Kuna mambo mengi sana ambayo nashindwa kuyaongea, ubaya nikuwa, kila mtu sasa hivi ananilaumu mimi kwakua nimemuacha lakini hawajui mambo ninayopitia. Mimi kama mwanaume kuna mambo siwezi kuwaambia ndugu zangu wala ndugu zake, wao wanajua nimemuacha tu namharibia maisha yake lakini ukweli nashindwa kuamua kuwa huyu mtu ananipenda au vipi, nisaidie ushauri wako.
Nimeikuta sehemu nami nawasilisha.
Anaishi na wazazi wake wote ila ananiambia kuwa kwakua mimi ni mpenzi wake natakiwa kumhudumia na kwakua anaishi kwao basi ni lazima kuwahudumia na wazazi wake kwani hawezi kujinunulia chakula peke yake. Basi mimi hilo sina shida nalo kwani kama mwanaume naona kama ni majukumu yangu. Sababu ya kuja kwako Kaka ni hivi, huyu mwanamke bado hajamsahau X wake.
X wake ameoa lakini kila akigombana na mke wake anamtafuta mpenzi wangu wanaongea, nikimuuliza kwanini unaongea naye ananiambia ni urafiki tu kisha ananinunia hata wiki mpaka mimi ndiyo nimuombe msamaha. Niliamua kumpigia X wake na kumuambia kuwa yeye si anandoa basi aniachie mwanamke wangu lakini aliniambia kuwa hana mpango naye alishamuacha ila mimi ndiyo niongee na mtu wangu.
Shida inakuja hivi, baada ya mimi kuongea na X wake basi amebadilika, amekua mtu wa hasira na kila siku ananiambia kuwa tuachane. Ananiambia kuwa nimemdhalilisha kuwa kwa mimi kumpigia X wake ni kama nimemuita yeye malaya kuwa anarudia matapishi ili tuachane. Alilazimisha sana tuachane, akakata mawasiliano kabisa na mimi, kwakua nampenda basi niliamua kwenda kwa wazazi wake na kuwaambia ili waongee naye.
Niliwaambia kuwa nipo tayari kumuoa wakati wowote, wazazi wake waliongea naye na kweli alinisamehe. Basi niliona ili nisimpoteze na kumziba X wake nitoe mahari moja kwa moja, nilitoa mahari ingawa ishu ya ndoa aliniambia kuwa yeye bado hajajipanga lakini niliona kwa kutoa mahari basi atakua wangu.
Lakini haikua hivyo Kaka, pamoja na kutoa mahari ndiyo alibadilika zaidi, yaani amekua mtu wa hasira, amekua mtu wa kununa nuna sijui hata nifanyeje. Kuna wakati nilijikuta nakasirika na kumuambia kuwa bora tuachane kwani nimechoka, nikamtafuta mshenga na kumuambia ukweli kuwa nimechoka nataka aende kuwaambia wazazi wake kuwa nimechoka nataka kuachana naye, kweli nilikua nimechoka na nilipanga kumuacha.
Lakini baada ya kuona nimemtafuta mshenga aliniambia kuwa namdhalilisha kumtolea mahari kisha kumuacha. Alinizimia simu, nilikuja kupigiwa simu baadaye na X wake kuwa anataka kujiua na kanywa sumu wako hospitalini. Nilikua na hasira lakini nilienda na kwelia likua kalazwa hospitalini, alinilaumu mimi kuwa nimemdhalilisha kwani nikimuacha nisipomuoa hatapata mwanaume mwingine wa kumuoa.
Ana mika 32, kusema kweli nampenda na nipo tayari kumuoa, lakini nashindwa kujua kama ananipenda kweli au la. Ananiambia ananipenda ni mimi tu sijiamini yeye hana chochote na X wake ni marafiki tu lakini nilishawahi kuona anamtumia mpaka picha za uchi X wake, nikimuuliza ananiambia kwani kuna ubaya gani kama ni kumuona alishamuona kila kitu hakuna jipya, nimechanganyikiwa.
Kuna mambo mengi sana ambayo nashindwa kuyaongea, ubaya nikuwa, kila mtu sasa hivi ananilaumu mimi kwakua nimemuacha lakini hawajui mambo ninayopitia. Mimi kama mwanaume kuna mambo siwezi kuwaambia ndugu zangu wala ndugu zake, wao wanajua nimemuacha tu namharibia maisha yake lakini ukweli nashindwa kuamua kuwa huyu mtu ananipenda au vipi, nisaidie ushauri wako.
Nimeikuta sehemu nami nawasilisha.