Nndu wa Selote
JF-Expert Member
- Jun 21, 2012
- 733
- 520
Ilianza kama utani, akanza kumlamba mke wa rafiki yake mpendwa. Rafiki yake, (Mwenye mke) kaanza mikwara ambayo haieleweki kwa mkewe akimwambia, ooh, mbona naona siku hizi mko karibu sana na rafiki yangu. Mikwara ilipozidi, mke akahisi mumewe anaweza kufuatilia na kugundua kinachoendelea. Akaamua kumweleza mumewe kuwa ni kweli huyu rafiki yako amekuwa akinitaka lakini nikamkatalia. Mume kashangaa, kakata mawasiliano na rafiki yake na kamtangaza kwa ndugu, amaa na marafiki kuwa huyo rafiki yake ana tabia mbaya sana kwa vile alikuwa anamtongoza mke wake. Baada ya miaka kadhaa wakarudisha urafiki lakini kimachalemachale huku mwenye mke akimsanifu rafiki yake kama vile anatamani kumwambia ''mshenzi ulitaka kutembea na mke wangu ukakuta yuko stable ukashindwa''. Ukweli ni kwamba alishatembea naye zaidi ya mara nne. Anatamani ampe jamaa live kwa vile sanifu zimezidi lakini anasita. Wewe ungefanyaje na alishakutangazia kwa watu kwamba ulikuwa ukimtongoza mkewe ? Kumbuka, hapo mke anaonekana ni shujaa kwa vile "alikukatalia" na akaamua kumweleza mumewe !