ANALYSIS: CCM cadres’ new book revisits Mkapa’s troubled legacy

BAK

JF-Expert Member
Feb 11, 2007
124,790
288,009
ANALYSIS: CCM cadres' new book revisits Mkapa's troubled legacy
THIS DAY

IN our society, there is a group of people who felt relieved, perhaps, that the death of the country's founder Father and longest serving Chama Cha Mapinduzi (CCM) chairman, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere, meant also a death of courageous people who could take the bull by the horns and criticize high profile politicians and bureaucrats.

This group of people thought that Nyerere's demise paved way for a new era of leadership irresponsibility, greed and looting of public resources and that nobody would question, enquire or straight away criticize them in public for their irresponsible behaviour in public office.

But they have been proven wrong. A new book by veteran journalist, television talk show host and one-time CCM national executive committee (NEC) member, Makwaiya wa Kuhenga, in collaboration with one of Mwl. Nyerere's sons, Madaraka Nyerere and veteran politician- cum-former Mwalimu's closest aide, Joseph Butiku, indicates once again that CCM, and indeed Tanzania, has no shortage of courageous, visionary and upright men who can dare to challenge the system, be it a former president and CCM national chairman.

In the book titled: 'CCM na mustakabali wa nchi yetu,' which literally means, 'CCM and our nation's destiny', deals blow after blow to the immediate former president and CCM national chairman, Benjamin William Mkapa.

The authors in unison condemn the era of the former party national chairman; his avoiding to meet and talk over issues of interest to the party and nation as a whole; his disdain of his peers and the sudden usurpation of party by a class of filthy rich people, often with questionable character. The chairman's behaviour gave rise to a culture of gossip and bad mouthing among the top brass of the party, signifying a major rift within the party.

The authors also question why the ruling party under former chairman Ali Hassan Mwinyi silently abolished the Arusha Declaration, including its leadership code of conduct, which resulted into free-wheeling accumulation of ill gotten wealth, with the rich vying for leadership positions through bribery, deceit and other dirty tricks.

The book accuses Mkapa of entertaining hearsays and gossips which led to divisions within the top hierarchy of the party which was once revered and respected across Africa and the world. The party leadership sometimes trampled on members' rights by changing important procedures and regulations. When those disenchanted asked for clarification, during meetings, they got jeered off by other members.

The book also mentions the fraudulent deletion of immediate former CCM vice chairman for the Mainland John Malecela, from the list of presidential aspirants in 2005 just because the former prime minister had not conferred with Mr Mkapa as chairman prior to his picking presidential nomination forms.

The veteran CCM members and Mwl. Nyerere's son question CCM�s loss of vision and direction in terms of formulating the five years development rolling plan, which was last done in 1981, hence impacting negatively on the part of the government. The authors wonder whether the party is any longer in charge and holding the government accountable.

Because of lack of a visionary leadership that sidelined some critical voices, CCM under Mkapa did sow seeds of racial discrimination especially during internal party nominations and primaries. The authors cite examples of former Prime Minister Dr Salim Ahmed Salim, who was opposed by some Zanzibar caucus members as being of Arab origin, and having played a role in the slaying of former Zanzibar President Abeid Karume.

It condemns a new culture of stage managed public rallies convened by the party and often addressed by senior party leaders including the national chairman and secretary general, to issue party membership cards to opposition cross-overs and wonders whether such people share a strong belief in CCM's ideals.

The book, the first of its kind to be written by the ruling party's members in the past ten years or so since the late Mwl . Nyerere wrote, 'Uongozi wetu na hatima ya Tanzania,' in 1995, ends with a number of suggestions to current President Jakaya Kikwete , who is also the party's national chairman:- avoid entertaining gossip, rediscover the Arusha Declaration and preside over the writing of a new constitution to replace the one party 1977 Constitution.

The authors advise Mr Kikwete to take the leadership in enacting a new constitution that will also reduce excessive powers of the presidency, which has routinely been abused by some individuals to advance personal rather than national interests while at Ikulu.
 
Mungu ampe siha njema na subira Mh.Ben William Mkapa lakini siku yake ikifika kutuacha au kuiacha dunia Sintawaelewa Hawa Jamaa Kama Watatoa Maoni Tofauti Ya Ktk Kitabu Chao;

Niseme Tu Kuwa Mkapa Aliongoza Nchi Na Chama Ktk Namna Aliyoiona Yeye Inafaa,kinachoangaliwa Hapo Ni Chama Kipo Na Bado Kipo Madarakani,ana Mapungufu Yake Lakini Sikubaliani Na Ufundi Huu Wa Makwaiya Na Jose Butiku Na Ndg Madaraka Kuwa Unai6tendea Haki Mkapa's Legacy,tanzania Na Watakaoturithi.

Nimpongeze Tu Ben W.mkapa Kwa Kuiongoza Nchi Kadri Ya Uwezo Wake Na Si Kadri Ya Mapenzi Ya Mwalimu Nyerere,nyerere Was Founder-mwinyi Second ,mkapa Was The Third ..cha Kushukuru Huyu Bwana Hakuwahukumu Julius Na Mwinyi Kwa Umaskini Wa Tanzania,wote Wawili Wanamuabudu Mungu,na Kwa Mungu Umaskini Ni Chukizo Lakini Si Kwa Mzee Nyerere,alikuwa Na Misimamo Yake Na Zama Zake Ilionekana Inafaa ,mwinyi Akaishi Ktk Zama Zake Naye Aliyaona Yake Sasa Iweje Mkapa Kuishi Kwa Mujibu Wa Zama Zake Imekuwa Kesi Kwelikweliiii,viongozi Ni Watu Kama Butiku Na Makwaiya,sipendi Kuamini Kuwa Butiku Na Makwaiya Ni Watakatifu Ktk Jamii Ya Watanzania,sipendi Kuwazuia Wao Kusema Wanaloliona Ni Faida Kwa Umma Lakini Sipendi Kukiuka Haki Na Fasiri Sahihi Ya Uandishi Kwa Style Kukuza Mambo.

Kitabu Hiki Hakikulenga Kuijenga Ccm Bali Kumbomoa Mkapa Machoni Pa Walimwengu Lakini Baya Zaidi Ni Kuibomoa Tanzania Hiyo Ya Nyerere Mnayoihubiri,kumbukeni Butiku Alivyoshangilia Mkapa Kuikosa Tuzo Ya Mo Ibrahimu !!!! Binafsi Nimekwama Kumuelewa Huyu Mtu Butiku Mpaka Sasa.
 
Labda kuna watu wanataka waongozwe na malaika kutoka mbinguni! Hiyo itatokea lini? Hakuna siku atapatikana kiongozi akakosa upungufu fulani wa kibinadamu, iwe katika kauli zake, mahusiano na wenzake, mambo anayosikiliza ama kutosikiliza, na hata mambo ya ndoa na ngono. Pengine ingefaa tukaweka mizani (ambayo sidhani kama tutaweza kuepuka subjectivity), kuona kiongozi awe na positive ngapi na negative ngapi ili tuone kwamba hizi zinavumilika? Maana kiongozi mwenye positives tupu tupu hatutampata kamwe, hajawahi kupatikana popote duniani. Na suala la kipi ni positive na kipi ni negative bado ni mtazamo wa mtu binafsi, ndio maana hata wale manabii maarufu hawakuaminiwa na kila mtu. Kwa hiyo nasema tujadili lakini tusihukumu, tujadili hoja mojamoja kama inavyokuja, lakini si sawa kutumia hoja kama hizo kutoa general conclusions kwamba mtu ni mbaya kijumla (angalao iwe hivyo hadi tutakapokubaliana juu ya kipimo kinachofaa kutumika).
 
preside over the writing of a new constitution to replace the one party 1977 Constitution.

Kwangu mimi haya tu ndio maoni muhimu kwenye hicho kitabu, the rest ni malalamiko ya walioachwa nje ya mlo, Butiku aliwahi kuwamo ndani, so is Makwaiya, walifanya nini cha maana? Majungu yalikuwepo toka enzi za Mwalimu, mbona Butiku hakuyapigia kelele?

Azimio La Arusha, ili litusaidie nini? tunazo sheria ngapi za maadili ya uongozi na hazifuatwi leo kuna anyelilia Azimio La Arusha, lililowafanya kina Msuya, Bomani, na Kahama wawe matajiri, huku kina Sozigwa, wakiwa masikini tena under Butiku's na Mwalimu's watch?

Butiku, tunajaribu kumuheshimu kwamba angalau anajaribu kumpigia tembo kelele, lakini barua na ile hotuba yake ya majuzi, vinatosha sana, kwa sababu Mkapa, akiamua kuzitoa habari zake chafu ataweza kuzijibu? Yaaani Butiku ameona matatizo ya nchi pale tu mgombea wake Salim, aliposhindwa? Kabla ya hapo hakuona kitu? Na Makwaiya naye baada tu ya rafiki yake Ulimwengu, kupigwa chini kwenye ulaji na Mkapa, basi ndio wameanza kuona mwanga sasa?

Butiku, angekuwa mkweli angeongelea CDA under Mwalimu na yeye akiwemo, na sasa tofauti yake ni nini? kuna kinachofanyika? hela ngapi zimatumika so far nini cha kuonyesha? Aongelee Gapex, what happened to it? Halafu Madaraka, mbona baba yake alipokuwa madarakani hakusema kitu wakati ule akipewa malori ya bure ya Mama Mtakatifu Maria, je hakujua kuwa walikuwepo wananchi waliokuwa wakisota kutokana na siasa za baba yake na Azimio La Arusha?

I mean, binafsi ningewaheshimu kama wange-stick na ishu muhimu za taifa, kama vile kutueleza ukweli wa mali za Mkapa, maana kwa muda mrefu alikuwa akijificha nyuma ya mkewe, ni sasa tu ndio inagundulika kuwa mkewe ni mkewe, na yeye ni yeye maana mkewe sie aliyefungua biashara na Yona, ila ni Mkapa mwenyewe, CCM ilianza kukosa muelekeo toka Mwalimu akiwepo, lakini kwa sababu alijiamini kuwa ni semi-God hakutaka kukubali mbele ya taifa, na hasa makosa makubwa aliyolifanyia hili taifa baada ya kutoka urais, kwanza alituchagulia Mwinyi, baadaye yeye mwenyewe akaanza kumtukana Mwinyi, bila hata kutuomba samaahani wananchi kwamba alikosea kutupa Mwinyi, baadaye akatupa Mkapa na kayaona madudu ya Mkapa, na ubinafsishaji lakini akanyamaza kimyaaa, halafu aliyaona madudu ya Salmin na hata yeye binafsi Mwalimu, kumuunga mkono kuiba kura za CUF, yes maana ilishatngazwa rasmi kuwa CUF imeshinda, na katibu wa CCM kule then Ameir, alishatangaza kuwakilisha malalamiko yake rasmi mahakamani kuwa ushindi wa CUF utenguliwe, lakini within hours tukaambiwa CCM ndio iliyoshinda, baada ya mikutano mingi ya siri kati ya Mwalimu, Salmin, na Mkapa, na hata Seif mwenyewe pia alishiriki, sasa haya mbona hawakuyasema kwenye hicho kitabu fake?

Sijakiona hicho kitabu, lakini nina-sense kuwa kuna kutaka kujifanya kuwa CCM ilikuwa clean isipokuwa imeharibiwa na Mkapa, taht is nonesense, Mwalimu alipokuwa anaharibu katiba za CCM na kuwaamuru wampe Mwinyi, na Mkapa urais, ndipo alipokuwa anapanda mbegu chafu ambazo wanacholalamikia hawa kina Butiku sasa ni matunda yake, mbona Butiku hazungumzii ile Foundation zile shillingi millioni mia tatu alizokuwa akipewa na Mkapa, walipokuwa bado washikaji zilikuwa zinatoka kwenye mfuko upi?

Alipokuwa akizitumia hizo hela kwa kusafiri na vimada wadogo wadogo kama binti zake kwenda UN, mbona hakuna aliyepiga kelele? Yeye alipokuwa akimpora Mzee Kamba mkewe, ambaye then alikuwa ubalozini Belgium, yale yalikuwa ni maadili mazuri sana ya uongozi?

Wananchi tumechoshwa na hawa watu vinyonga, wanaotaka ushujaaa tu wakiwa na nzala, Msekwa nzala imempiga kidogo tu alikuwa analia lia na katiba mpya, sasa tungetegemea hotuba yake ya kwanza kama makamu wa CCM irudie yale machungu yake ya katiba, lakini wapi na wala hakuna wa kumuuliza, Mangula naye analialia huko pembeni ngoja wampe kula kidogo tu utaona kimyaaa, hawa kina Butiku wanasubuliwa na nzala,

Ninawaambia one thing kina Butiku, wajifunze maana ya kutesa kwa zamu ndicho hasa wanacholilia, lakini sio taifa!
 
Mungu ampe siha njema na subira Mh.Ben William Mkapa lakini siku yake ikifika kutuacha au kuiacha dunia Sintawaelewa Hawa Jamaa Kama Watatoa Maoni Tofauti Ya Ktk Kitabu Chao;

Niseme Tu Kuwa Mkapa Aliongoza Nchi Na Chama Ktk Namna Aliyoiona Yeye Inafaa,kinachoangaliwa Hapo Ni Chama Kipo Na Bado Kipo Madarakani,ana Mapungufu Yake Lakini Sikubaliani Na Ufundi Huu Wa Makwaiya Na Jose Butiku Na Ndg Madaraka Kuwa Unai6tendea Haki Mkapa's Legacy,tanzania Na Watakaoturithi.

Nimpongeze Tu Ben W.mkapa Kwa Kuiongoza Nchi Kadri Ya Uwezo Wake Na Si Kadri Ya Mapenzi Ya Mwalimu Nyerere,nyerere Was Founder-mwinyi Second ,mkapa Was The Third ..cha Kushukuru Huyu Bwana Hakuwahukumu Julius Na Mwinyi Kwa Umaskini Wa Tanzania,wote Wawili Wanamuabudu Mungu,na Kwa Mungu Umaskini Ni Chukizo Lakini Si Kwa Mzee Nyerere,alikuwa Na Misimamo Yake Na Zama Zake Ilionekana Inafaa ,mwinyi Akaishi Ktk Zama Zake Naye Aliyaona Yake Sasa Iweje Mkapa Kuishi Kwa Mujibu Wa Zama Zake Imekuwa Kesi Kwelikweliiii,viongozi Ni Watu Kama Butiku Na Makwaiya,sipendi Kuamini Kuwa Butiku Na Makwaiya Ni Watakatifu Ktk Jamii Ya Watanzania,sipendi Kuwazuia Wao Kusema Wanaloliona Ni Faida Kwa Umma Lakini Sipendi Kukiuka Haki Na Fasiri Sahihi Ya Uandishi Kwa Style Kukuza Mambo.

Kitabu Hiki Hakikulenga Kuijenga Ccm Bali Kumbomoa Mkapa Machoni Pa Walimwengu Lakini Baya Zaidi Ni Kuibomoa Tanzania Hiyo Ya Nyerere Mnayoihubiri,kumbukeni Butiku Alivyoshangilia Mkapa Kuikosa Tuzo Ya Mo Ibrahimu !!!! Binafsi Nimekwama Kumuelewa Huyu Mtu Butiku Mpaka Sasa.

Kiongozi ni lazima afuate maadili ya uongozi na kuhakikisha hatumii nafasi aliyopewa kujitajirisha yeye na familia yake. Kiongozi ni lazima pia ahakikishe maamuzi mbali mbali anayoyafanya akiwa madarakani ni yenye maslahi na nchi yake. Huyu Mkapa kuna ushahidi wa kutosha kwamba alitumia wadhifa wake kujitajirisha na alifanya maamuzi mbali mbali ikiwemo kuwaleta makaburu wa Net Group problems, ununuzi wa rada, mikataba ya madini ambayo maamuzi hayo hayakuweka mbele maslahi ya nchi bali ya yeye Mkapa. Halafu alivyokuwa na kiburi, alipoombwa ajibu tuhuma hizo alidai, "niacheni nimeshastaafu." Kwa nini yeye aogopwe huyu!? Sasa kwa nini Watanzania wasiandike vitabu na na kujadili yale aliyoyafanya akiwa madarakani!? Nyerere kang'atuka miaka 22 iliyopita mpaka leo hii kuna watu wanamjadili na pia kuandika vitabu, hivyo sioni kosa lolote la Butiku na Makwaia wa Kuhenga kuandika kitabu au Mtanzania mwingine yeyote yule.

Kwenye demokrasi ndani ya vyama ni lazima kuwe na kutofautiana. Tunaona katika vyama vya Republicans na Democrats jinsi viongozi mbali mbali na hata wanachama wanavyotofautiana kimawazo na wanazijadili tofauti zao peupe bila kuficha kwa madhumuni ya kuimarisha vyama vyao. Vivyo hivyo kama CCM inataka kuwa imara lazima wanachama na viongozi wa chama hicho wawe huru kujadili na hata kuandika mabaya na mazuri ndani ya chama hicho. Kuna wana CCM wanamuona Mkapa alifanya mazuri na kuna wengine wanamuona hakufanya chochote cha kuinufaisha Tanzania bali kujilimbikizia mali yeye na familia yake. Kuyaficha mabaya ndani ya chama hicho ni kosa kubwa sana ambalo linaweza kabisa kuangamiza chama hicho. Kumbuka mficha ugonjwa kifo kitamuumbua!
 
preside over the writing of a new constitution to replace the one party 1977 Constitution.


Alipokuwa akizitumia hizo hela kwa kusafiri na vimada wadogo wadogo kama binti zake kwenda UN, mbona hakuna aliyepiga kelele? Yeye alipokuwa akimpora Mzee Kamba mkewe, ambaye then alikuwa ubalozini Belgium, yale yalikuwa ni maadili mazuri sana ya uongozi?
[/U][/B]

Mkuu FMES, hiyo umepiga chini ya belt boss! Ila hii tabia ya kuwahamisha waume za watu, whether kuwapeleka ofisi za kibalozi nje ya nchi au kuwapeleka mikoani, ili wenyewe wawe wanatesa na wake za hao waliohamishwa ni tabia chafu inayotakiwa kukemewa kwa nguvu zote!
 
preside over the writing of a new constitution to replace the one party 1977 Constitution.

Kwangu mimi haya tu ndio maoni muhimu kwenye hicho kitabu, the rest ni malalamiko ya walioachwa nje ya mlo, Butiku aliwahi kuwamo ndani, so is Makwaiya, walifanya nini cha maana? Majungu yalikuwepo toka enzi za Mwalimu, mbona Butiku hakuyapigia kelele?

Azimio La Arusha, ili litusaidie nini? tunazo sheria ngapi za maadili ya uongozi na hazifuatwi leo kuna anyelilia Azimio La Arusha, lililowafanya kina Msuya, Bomani, na Kahama wawe matajiri, huku kina Sozigwa, wakiwa masikini tena under Butiku's na Mwalimu's watch?

Butiku, tunajaribu kumuheshimu kwamba angalau anajaribu kumpigia tembo kelele, lakini barua na ile hotuba yake ya majuzi, vinatosha sana, kwa sababu Mkapa, akiamua kuzitoa habari zake chafu ataweza kuzijibu? Yaaani Butiku ameona matatizo ya nchi pale tu mgombea wake Salim, aliposhindwa? Kabla ya hapo hakuona kitu? Na Makwaiya naye baada tu ya rafiki yake Ulimwengu, kupigwa chini kwenye ulaji na Mkapa, basi ndio wameanza kuona mwanga sasa?

Butiku, angekuwa mkweli angeongelea CDA under Mwalimu na yeye akiwemo, na sasa tofauti yake ni nini? kuna kinachofanyika? hela ngapi zimatumika so far nini cha kuonyesha? Aongelee Gapex, what happened to it? Halafu Madaraka, mbona baba yake alipokuwa madarakani hakusema kitu wakati ule akipewa malori ya bure ya Mama Mtakatifu Maria, je hakujua kuwa walikuwepo wananchi waliokuwa wakisota kutokana na siasa za baba yake na Azimio La Arusha?

I mean, binafsi ningewaheshimu kama wange-stick na ishu muhimu za taifa, kama vile kutueleza ukweli wa mali za Mkapa, maana kwa muda mrefu alikuwa akijificha nyuma ya mkewe, ni sasa tu ndio inagundulika kuwa mkewe ni mkewe, na yeye ni yeye maana mkewe sie aliyefungua biashara na Yona, ila ni Mkapa mwenyewe, CCM ilianza kukosa muelekeo toka Mwalimu akiwepo, lakini kwa sababu alijiamini kuwa ni semi-God hakutaka kukubali mbele ya taifa, na hasa makosa makubwa aliyolifanyia hili taifa baada ya kutoka urais, kwanza alituchagulia Mwinyi, baadaye yeye mwenyewe akaanza kumtukana Mwinyi, bila hata kutuomba samaahani wananchi kwamba alikosea kutupa Mwinyi, baadaye akatupa Mkapa na kayaona madudu ya Mkapa, na ubinafsishaji lakini akanyamaza kimyaaa, halafu aliyaona madudu ya Salmin na hata yeye binafsi Mwalimu, kumuunga mkono kuiba kura za CUF, yes maana ilishatngazwa rasmi kuwa CUF imeshinda, na katibu wa CCM kule then Ameir, alishatangaza kuwakilisha malalamiko yake rasmi mahakamani kuwa ushindi wa CUF utenguliwe, lakini within hours tukaambiwa CCM ndio iliyoshinda, baada ya mikutano mingi ya siri kati ya Mwalimu, Salmin, na Mkapa, na hata Seif mwenyewe pia alishiriki, sasa haya mbona hawakuyasema kwenye hicho kitabu fake?

Sijakiona hicho kitabu, lakini nina-sense kuwa kuna kutaka kujifanya kuwa CCM ilikuwa clean isipokuwa imeharibiwa na Mkapa, taht is nonesense, Mwalimu alipokuwa anaharibu katiba za CCM na kuwaamuru wampe Mwinyi, na Mkapa urais, ndipo alipokuwa anapanda mbegu chafu ambazo wanacholalamikia hawa kina Butiku sasa ni matunda yake, mbona Butiku hazungumzii ile Foundation zile shillingi millioni mia tatu alizokuwa akipewa na Mkapa, walipokuwa bado washikaji zilikuwa zinatoka kwenye mfuko upi?

Alipokuwa akizitumia hizo hela kwa kusafiri na vimada wadogo wadogo kama binti zake kwenda UN, mbona hakuna aliyepiga kelele? Yeye alipokuwa akimpora Mzee Kamba mkewe, ambaye then alikuwa ubalozini Belgium, yale yalikuwa ni maadili mazuri sana ya uongozi?

Wananchi tumechoshwa na hawa watu vinyonga, wanaotaka ushujaaa tu wakiwa na nzala, Msekwa nzala imempiga kidogo tu alikuwa analia lia na katiba mpya, sasa tungetegemea hotuba yake ya kwanza kama makamu wa CCM irudie yale machungu yake ya katiba, lakini wapi na wala hakuna wa kumuuliza, Mangula naye analialia huko pembeni ngoja wampe kula kidogo tu utaona kimyaaa, hawa kina Butiku wanasubuliwa na nzala,

Ninawaambia one thing kina Butiku, wajifunze maana ya kutesa kwa zamu ndicho hasa wanacholilia, lakini sio taifa!

Kila mtu apewe yake kwa nafasi yake,maana tunawaona ma-FALSE PRETENDERS wanajitokeza sana,why!!!!!!!!!!
 
Labda kuna watu wanataka waongozwe na malaika kutoka mbinguni! Hiyo itatokea lini? Hakuna siku atapatikana kiongozi akakosa upungufu fulani wa kibinadamu, iwe katika kauli zake, mahusiano na wenzake, mambo anayosikiliza ama kutosikiliza, na hata mambo ya ndoa na ngono. Pengine ingefaa tukaweka mizani (ambayo sidhani kama tutaweza kuepuka subjectivity), kuona kiongozi awe na positive ngapi na negative ngapi ili tuone kwamba hizi zinavumilika? Maana kiongozi mwenye positives tupu tupu hatutampata kamwe, hajawahi kupatikana popote duniani. Na suala la kipi ni positive na kipi ni negative bado ni mtazamo wa mtu binafsi, ndio maana hata wale manabii maarufu hawakuaminiwa na kila mtu. Kwa hiyo nasema tujadili lakini tusihukumu, tujadili hoja mojamoja kama inavyokuja, lakini si sawa kutumia hoja kama hizo kutoa general conclusions kwamba mtu ni mbaya kijumla (angalao iwe hivyo hadi tutakapokubaliana juu ya kipimo kinachofaa kutumika).

Naam,ifike wakati waTZ tuwe wakweli mioyoni mwetu kabla ya kuwaharibu wenzetu.
 
Nyerere kang'atuka miaka 22 iliyopita mpaka leo hii kuna watu wanamjadili na pia kuandika vitabu, hivyo sioni kosa lolote la Butiku na Makwaia wa Kuhenga kuandika kitabu au Mtanzania mwingine yeyote yule.

Mkulu Bubu,

Heshima mbele, kama kweli Tanzania, tunataka kutatua matatizo yetu ya maadili ya uongozi, basi tuanzie pale yalipoanzia na Mwalimu mwenyewe, kuwasingizia kina Mkapa, hatuwezi kutatua anything ila itabakia a witchunt, Mwalimu was the greatest, lakini pia alikuwa na mapungufu ndio haya baadhi yake wanayoyalilia kina Butiku,

George Washington, kule US aliweka misingi imara ya ungozi ambayo imeota mizizi mpaka leo, ukiona kiongozi anaondoka kama Mwalimu, alivyoondoka halafu nyuma yake system aliyoijenga ya uongozi inatka ku-collapse, basi huyo kiongozi alikuwa ni selfish, uongozi wake ulikuwa ni wa me! myself! and I, hata kama alikuwa na sifa kiasi gani ni bure, mfano ni Keeenja, sifa nyingi kule City, alipotoka tu ile City system almost collapsed, ndio maana ya viongozi wa me! me! me! look at me! me! kina Mwalimu,

Wa-Tanzania tuamuke na hawa viongozi nzala, ambao siku zote wanajaribu kutumia ujinga wetu wa kuelewa mambo yetu ya kisiasa kujitafutia umaarufu, Butiku alikuwa akipewa na Mkapa, shillingi millioni mia tatu annually walipokuwa washikaji, je uliwahi kusikia zile hela zilikuwa zinatoka kwenye mfuko upi? Je ulikuwa unajua kuwa alikuwa akipewa hizo hela kule Nyerere Foundation? Mbona asiseme kwenye hicho kitabu? Tanzania kuna foundation ngapi ambazo ni more important kwa jamii kuliko Nyerere Foundation mbona hazijawahi kupewa pesa na serikali?

Matatizo yetu ya uongozi hayakuletwa na Mkapa, huo ni uongo tena uzandiki, yaliletwa na Mwalimu, mwenyewe the greatest, ni haki ya Butiku na wenziwe kuandika anything they want, lakini pia ni haki yetu wananchi kukataa kudanganywa, wasitudanganye wananchi tumedanganywa vya kutosha, hakuna kitu chochote Mkapa, alichokuwa akikifanya kwenye uongozi wake ambacho ni kipya yote alikuwa akiiga ya Mwalimu, isipokuwa ulimbikizaji wa mali tu, lakini kama ni ubabe ni ule ule wa Mwalimu, kama kumtoa Malecela na kumharibu Salim, alijifunza kwa Mwalimu, na Butiku binafsi anahusika sana na kumpiga vita Malecela enzi za Mwalimu, tatizo la taifa letu sasa ni viongozi mafisadi, ambao walikuwa wakibembelezwa toka enzi za Mwalimu, sasa ndio matokeo yake haya wanazaliwa mpaka leo, maadili ya uongozi Butiku hana kabisaa hawezi zungumzia ya wengine, that is my point, anasumbuliwa na nzala lakini hana uchungu wowote na taifa!

Sasa akae pembeni, maana kutesa ni kwa zamu, ya kwake ilipita sasa ni ya wengine, FULL STOP!
 
Mkuu FMES, hiyo umepiga chini ya belt boss! Ila hii tabia ya kuwahamisha waume za watu, whether kuwapeleka ofisi za kibalozi nje ya nchi au kuwapeleka mikoani, ili wenyewe wawe wanatesa na wake za hao waliohamishwa ni tabia chafu inayotakiwa kukemewa kwa nguvu zote!

Hapana mkuu, alikuwa akitumia hela za Foundation kusafiri na girlfriends zake, huu akiharibu ndoa ya Mzee Kamba, ofisa mdogo wa ubalozi ambayo aliishia kuiua kabisa, sasa haya ni maadili? Alipoambiwa atoe mahesabu kule Foundation wacha apige kelele mpaka wakmfukuza Warioba, lakini here he is antaka kutudanganya, come on! hawa watonee huruma wabongo kidogo, hivi kweli unajua yakisemwa yote ya Butiku, ya abuse of power aliipokuwa madarakani mkuu wangu utalia machozi kama mtoto na usiamini kuwa ni huyu sasa anyeandika wengine!
 
Mkulu Bubu,

Heshima mbele, kama kweli Tanzania, tunataka kutatua matatizo yetu ya maadili ya uongozi, basi tuanzie pale yalipoanzia na Mwalimu mwenyewe, kuwasingizia kina Mkapa, hatuwezi kutatua anything ila itabakia a witchunt, Mwalimu was the greatest, lakini pia alikuwa na mapungufu ndio haya baadhi yake wanayoyalilia kina Butiku,

George Washington, kule US aliweka misingi imara ya ungozi ambayo imeota mizizi mpaka leo, ukiona kiongozi anaondoka kama Mwalimu, alivyoondoka halafu nyuma yake system aliyoijenga ya uongozi inatka ku-collapse, basi huyo kiongozi alikuwa ni selfish, uongozi wake ulikuwa ni wa me! myself! and I, hata kama alikuwa na sifa kiasi gani ni bure, mfano ni Keeenja, sifa nyingi kule City, alipotoka tu ile City system almost collapsed, ndio maana ya viongozi wa me! me! me! look at me! me! kina Mwalimu,

Wa-Tanzania tuamuke na hawa viongozi nzala, ambao siku zote wanajaribu kutumia ujinga wetu wa kuelewa mambo yetu ya kisiasa kujitafutia umaarufu, Butiku alikuwa akipewa na Mkapa, shillingi millioni mia tatu annually walipokuwa washikaji, je uliwahi kusikia zile hela zilikuwa zinatoka kwenye mfuko upi? Je ulikuwa unajua kuwa alikuwa akipewa hizo hela kule Nyerere Foundation? Mbona asiseme kwenye hicho kitabu? Tanzania kuna foundation ngapi ambazo ni more important kwa jamii kuliko Nyerere Foundation mbona hazijawahi kupewa pesa na serikali?

Matatizo yetu ya uongozi hayakuletwa na Mkapa, huo ni uongo tena uzandiki, yaliletwa na Mwalimu, mwenyewe the greatest, ni haki ya Butiku na wenziwe kuandika anything they want, lakini pia ni haki yetu wananchi kukataa kudanganywa, wasitudanganye wananchi tumedanganywa vya kutosha, hakuna kitu chochote Mkapa, alichokuwa akikifanya kwenye uongozi wake ambacho ni kipya yote alikuwa akiiga ya Mwalimu, isipokuwa ulimbikizaji wa mali tu, lakini kama ni ubabe ni ule ule wa Mwalimu, kama kumtoa Malecela na kumharibu Salim, alijifunza kwa Mwalimu, na Butiku binafsi anahusika sana na kumpiga vita Malecela enzi za Mwalimu, tatizo la taifa letu sasa ni viongozi mafisadi, ambao walikuwa wakibembelezwa toka enzi za Mwalimu, sasa ndio matokeo yake haya wanazaliwa mpaka leo, maadili ya uongozi Butiku hana kabisaa hawezi zungumzia ya wengine, that is my point, anasumbuliwa na nzala lakini hana uchungu wowote na taifa!

Sasa akae pembeni, maana kutesa ni kwa zamu, ya kwake ilipita sasa ni ya wengine, FULL STOP

Very Good FieldMarshall
Naungana na wewe moja kwa Moja dhidi ya wale wanaotaka kumfanya Mwalimu Nyerere(RIP) kama kitu gani sijui.

Nyerere huyu huyu si ndo alimpiga kwanja Muungwana Mwaka 95 na kumuweka mkapa ,mbona kina Butiku hawalisemi hili. mbona hawakuandika kitabu kueleza kuwa Nyerere anaipeleka peleka CCM.

Nyerere hakuwa mtakatifu( japo inawezekana alikuwa si mbaya). na wala Nyerere si kwamba alikuwa ni Mwenye Hekima peke yake katika ile nchi, yeye alishika mpini tu toka mapema, ndo maana aliwawahi wenzie. lakini matendo yake ni yenye kuhojika kabisa. na kizazi alichokiongoza nyerere si kama kizazi cha sasa, hakuna kiongozi katika Tanzania ya leo atakayethubutu kufanya baadhi ya mambo aliyoyafanya Nyerere katika utawala wake watu wakamuachia hivi hivi.

Halafu wamemuingiza na Mtoto wa Nyerere ndani,lengo sijui ni kutafuta legitimacy au kitu gani,Huyu Madaraka angekuwa na shukrani angekaa pembeni, fadhila alizozilipa Mkapa kwa familia ya Nyerere ni nyingi sana. Nadhani Makongoro ana akili atamshauri ndugu yake akae pembeni katika hii ishu.

Besides, kama kitabu kinalenga kuipa faida jamii basi ni jambo jema, lakini kuandika kitabu kumchonganisha mtu na watu pamoja na vizazi vinavyofuata ili aonekane yeye mbaya ,si jambo jema.

Ni matumaini yangu kwamba iwapo wataamua kuandika legacy ya mkapa, waandike na Mazuri pia ambayo Ben aliifanyia Tanzania.
 
WanaJF,

Ukitaka kujua watanzania walivyo some hii thread, then compare watu hao hao na thread waliokuwa wanacomment kuhusu Butibu kusema waziwazi kuhusu sisiem kabla ua chaguzi,then soma thread ya Tuhuma kuhusu mkapa na BoT. Utaona tuna lack consistency, tunapenda kucritisize tuuu. Mfano wengi wamelalamika kuhusu BWM kufanya biashara ikulu haijawahi kuwa na kiongozi mfanya biashara lakini hapa mnamtetea BWM safiiiiii, Kashindwa kuzuia Scam in Bot leo BWM saaaaafiiii, Ameonyesha kiburi chake cha kukataa kuzungumzia maswala na tuhuma zinazomkabili wakati wa utawala eti kastaafu siasa wakati aikua dodoma few weeks leo BWm saaaaaaaaafiiii. Swali Je mbona hakupata tuzo aliyokuwa anaitarajia? Tuache unafiki tujadili yaliyoandikwa kwenye kitabu na kulinganisha na ukweli ambayo bado uko kwenye memories zetu.
 
WanaJF,

Ukitaka kujua watanzania walivyo some hii thread, then compare watu hao hao na thread waliokuwa wanacomment kuhusu Butibu kusema waziwazi kuhusu sisiem kabla ua chaguzi,then soma thread ya Tuhuma kuhusu mkapa na BoT. Utaona tuna lack consistency, tunapenda kucritisize tuuu. Mfano wengi wamelalamika kuhusu BWM kufanya biashara ikulu haijawahi kuwa na kiongozi mfanya biashara lakini hapa mnamtetea BWM safiiiiii, Kashindwa kuzuia Scam in Bot leo BWM saaaaafiiii, Ameonyesha kiburi chake cha kukataa kuzungumzia maswala na tuhuma zinazomkabili wakati wa utawala eti kastaafu siasa wakati aikua dodoma few weeks leo BWm saaaaaaaaafiiii. Swali Je mbona hakupata tuzo aliyokuwa anaitarajia? Tuache unafiki tujadili yaliyoandikwa kwenye kitabu na kulinganisha na ukweli ambayo bado uko kwenye memories zetu.

Bowbow
Nikiziangalia post zote katika Thread hii na nikicompare na Tread nyingine zilizopita kuhusu Mkapa, natofautiana na wewe kimtazaomo kuhusu maoni ya wachangiaji.

Uzuri ni kwamba watu hawashabikii Unazi, siyo kwa sababu Mkapa alisemwa vibaya kutokana na baadhi ya matendo yake, basi ataendelea kusemwa vibaya hata kwa yale Mazuri aliyoyafanya.
Watu wanaangalia mabovu ni yapi, wanayaponda na pia wanaangalia upande wa pili wa shilingi wenye kusifia wanasifia,wenye kuacknowldege wana acknowledge,watu hawataki uzandiki wa kujifanya wao ni wasafi sana kwa expense ya kuwatia "masingi" wenzao usoni

Au kwasababu Mkapa alitofautiana kisiasa na baadhi ya watu ndani ya CCM basi eti tutaunga mkono juhudi zao za kumponda(si kwa misingi ya mabaya aliyoyafanya)bali kwa sababu tu ya visasi ,choyo na chuki binafsi huku wakichukulia makosa ya mkapa kama kichaka cha kutupia mashambulizi yao.

Mimi Binafsi ninaunga mkono mjadala wa kumtaka bwana Mkapa aelezee ni kwa vipi alitumia madaraka yake kujinufaisha(kama inavyodaiwa) na kwa vipi alikubali mikataba mibovu ya nchi,lakini wakati huo huo siungi mkono exageration eti Mkapa kaiua Tanzania ile nzuri iliyojengwa na Nyerere,.Mimi ninapinga unafiki.
 
Nyerere kang'atuka miaka 22 iliyopita mpaka leo hii kuna watu wanamjadili na pia kuandika vitabu, hivyo sioni kosa lolote la Butiku na Makwaia wa Kuhenga kuandika kitabu au Mtanzania mwingine yeyote yule.

Mkulu Bubu,

Heshima mbele, kama kweli Tanzania, tunataka kutatua matatizo yetu ya maadili ya uongozi, basi tuanzie pale yalipoanzia na Mwalimu mwenyewe, kuwasingizia kina Mkapa, hatuwezi kutatua anything ila itabakia a witchunt, Mwalimu was the greatest, lakini pia alikuwa na mapungufu ndio haya baadhi yake wanayoyalilia kina Butiku,

George Washington, kule US aliweka misingi imara ya ungozi ambayo imeota mizizi mpaka leo, ukiona kiongozi anaondoka kama Mwalimu, alivyoondoka halafu nyuma yake system aliyoijenga ya uongozi inatka ku-collapse, basi huyo kiongozi alikuwa ni selfish, uongozi wake ulikuwa ni wa me! myself! and I, hata kama alikuwa na sifa kiasi gani ni bure, mfano ni Keeenja, sifa nyingi kule City, alipotoka tu ile City system almost collapsed, ndio maana ya viongozi wa me! me! me! look at me! me! kina Mwalimu,

Wa-Tanzania tuamuke na hawa viongozi nzala, ambao siku zote wanajaribu kutumia ujinga wetu wa kuelewa mambo yetu ya kisiasa kujitafutia umaarufu, Butiku alikuwa akipewa na Mkapa, shillingi millioni mia tatu annually walipokuwa washikaji, je uliwahi kusikia zile hela zilikuwa zinatoka kwenye mfuko upi? Je ulikuwa unajua kuwa alikuwa akipewa hizo hela kule Nyerere Foundation? Mbona asiseme kwenye hicho kitabu? Tanzania kuna foundation ngapi ambazo ni more important kwa jamii kuliko Nyerere Foundation mbona hazijawahi kupewa pesa na serikali?

Matatizo yetu ya uongozi hayakuletwa na Mkapa, huo ni uongo tena uzandiki, yaliletwa na Mwalimu, mwenyewe the greatest, ni haki ya Butiku na wenziwe kuandika anything they want, lakini pia ni haki yetu wananchi kukataa kudanganywa, wasitudanganye wananchi tumedanganywa vya kutosha, hakuna kitu chochote Mkapa, alichokuwa akikifanya kwenye uongozi wake ambacho ni kipya yote alikuwa akiiga ya Mwalimu, isipokuwa ulimbikizaji wa mali tu, lakini kama ni ubabe ni ule ule wa Mwalimu, kama kumtoa Malecela na kumharibu Salim, alijifunza kwa Mwalimu, na Butiku binafsi anahusika sana na kumpiga vita Malecela enzi za Mwalimu, tatizo la taifa letu sasa ni viongozi mafisadi, ambao walikuwa wakibembelezwa toka enzi za Mwalimu, sasa ndio matokeo yake haya wanazaliwa mpaka leo, maadili ya uongozi Butiku hana kabisaa hawezi zungumzia ya wengine, that is my point, anasumbuliwa na nzala lakini hana uchungu wowote na taifa!

Sasa akae pembeni, maana kutesa ni kwa zamu, ya kwake ilipita sasa ni ya wengine, FULL STOP!

Mkuu, Nyerere hakujilimbikizia mali alipokuwa madarakani. Nyerere hakusaini mikataba mibovu ya madini yetu. Nyerere hakuuza nyumba za serikali kiholela. Nyerere hakununua rada ambayo bei yake ilipigiwa kelele kila kona ya Tanzania na hata baadhi ya nchi za nje. Nyere hakuwaleta makaburu ili waendeshe TANESCO na kulipwa mabilioni ya pesa na hakuna chochote walichofanikiwa! Nyerere siku zote aliweka mbele maslahi ya Tanzania tofauti.

Tuchukulie mfano Mkapa alitamba kwamba aliongeza makusanyo ya kodi kwa kiasi kikukwa, hili anastahili pongezi, akaleta 'wachukuaji' yeye aliwaita wawekezaji akasaini mikataba mbali mbali na 'wachukuaji' ya kuchimba madini. Lakini pamoja na yote hayo Watanzania hawakuona tofauti yoyote katika maisha yao ya kila siku. Ajira bado zilikuwa ni adimu na vipato vyao viliendelea kuwa vidogo ambavyo havikulingana na hali halisi ya gharama za maisha, lakini bado wa kulaumiwa kutokana na kushindwa kuwakomboa Watanzania katika hali ngumu ya kimaisha ni NYERERE! (Mwenyezi mungu amlaze mahali pema peponi).

Mwacheni Mwalimu apumzike kwa amani jamani hastahili lawama zozote kwa madudu aliyoyafanya Mkapa maana hata kabla hajafariki alishaanza kutofautina na sera nyingi za Mkapa. Mnaelekeza lawama zenu za matatizo ya Tanzania mahali ambapo hazistahili kabisa kupelekwa. Mtu alin'gatuka miaka 22 iliyopita na baada ya kung'atuka kwake wamekuja marais watatu tofauti, lakini bado wa kulaumiwa kwa matatizo yetu ni Nyerere tu! Duh!kazi kweli kweli!
 
Very Good FieldMarshall
Naungana na wewe moja kwa Moja dhidi ya wale wanaotaka kumfanya Mwalimu Nyerere(RIP) kama kitu gani sijui.

Nyerere huyu huyu si ndo alimpiga kwanja Muungwana Mwaka 95 na kumuweka mkapa ,mbona kina Butiku hawalisemi hili. mbona hawakuandika kitabu kueleza kuwa Nyerere anaipeleka peleka CCM.

Nyerere hakuwa mtakatifu( japo inawezekana alikuwa si mbaya). na wala Nyerere si kwamba alikuwa ni Mwenye Hekima peke yake katika ile nchi, yeye alishika mpini tu toka mapema, ndo maana aliwawahi wenzie. lakini matendo yake ni yenye kuhojika kabisa. na kizazi alichokiongoza nyerere si kama kizazi cha sasa, hakuna kiongozi katika Tanzania ya leo atakayethubutu kufanya baadhi ya mambo aliyoyafanya Nyerere katika utawala wake watu wakamuachia hivi hivi.

Halafu wamemuingiza na Mtoto wa Nyerere ndani,lengo sijui ni kutafuta legitimacy au kitu gani,Huyu Madaraka angekuwa na shukrani angekaa pembeni, fadhila alizozilipa Mkapa kwa familia ya Nyerere ni nyingi sana. Nadhani Makongoro ana akili atamshauri ndugu yake akae pembeni katika hii ishu.

Besides, kama kitabu kinalenga kuipa faida jamii basi ni jambo jema, lakini kuandika kitabu kumchonganisha mtu na watu pamoja na vizazi vinavyofuata ili aonekane yeye mbaya ,si jambo jema.

Ni matumaini yangu kwamba iwapo wataamua kuandika legacy ya mkapa, waandike na Mazuri pia ambayo Ben aliifanyia Tanzania.

Nyerere alipomweka Mkapa kama Rais mwaka 95 hakumwambia akafanye madudu aliyoyafanya na hata kabla hajafariki alishaanza kutofautina na sera za Mkapa na hata mambo yalivyokuwa ndani ya CCM na ushahidi wa hili upo. Nyerere hakuwa perfect, lakini kutaka kumtwisha lawama za madhambi aliyoyafanya Mkapa siyo sawa kabisa!

Ndio demokrasia hiyo Baba! vizazi vinavyofuata Tanzania vina haki ya kujua mabaya na mazuri ya viongozi waliowahi kuiongoza Tanzania. Tukitaka kuyaficha madhambi waliyoyafanya na kuandika mazuri tu eti tusiwagombanishe na vizazi vijavyo itakuwa ni kichekesho cha hali ya juu. Kama viongozi wanataka wakumbukwe kwa mema waliyotenda basi wanapokuwa madarakani wafanye hivyo vinginevyo historia itachukua mkondo wake na kuandika hata yale mabaya waliyoyafanya
 
1. Bubu ataka kusema
JF Senior Expert Member

ANALYSIS: CCM cadres' new book revisits Mkapa's troubled legacy

-----------------------------------------------------------------

ANALYSIS: CCM cadres' new book revisits Mkapa's troubled legacy
THIS DAY

IN our society, there is a group of people who felt relieved, perhaps, that the death of the country's founder Father and longest serving Chama Cha Mapinduzi (CCM) chairman, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere, meant also a death of courageous people who could take the bull by the horns and criticize high profile politicians and bureaucrats. This group of people thought that Nyerere's demise paved way for a new era of leadership irresponsibility, greed and looting of public resources and that nobody would question, enquire or straight away criticize them in public for their irresponsible behaviour in public office.


Mkuu Bubu na Bowwow,

Heshima mbele wakuu, Wa-Tanzania sasa tumechoshwa na hawa viongozi mashujaa uchwara, Makwaia, was never in any high position, ingawa rafiki yake mpenzi ambaye ndiye hasa chanzo cha yeye kuandika hii kitabu, Ulimwengu, alikuwa, yeye na Butiku wame-enjoy too the spoil sasa huu ushujaa wameupata lini? Irresponsible behavior ilianza toka Mwalimu akiwa mdarakani, na Butiku akiwa the number two, exactly alifanya nini kinachoweza kumpa the power ya kusema sasa baada ya kukatiwa mrija wa kula?

2. But they have been proven wrong. A new book by veteran journalist, television talk show host and one-time CCM national executive committee (NEC) member, Makwaiya wa Kuhenga, in collaboration with one of Mwl. Nyerere's sons, Madaraka Nyerere and veteran politician- cum-former Mwalimu's closest aide, Joseph Butiku, indicates once again that CCM, and indeed Tanzania, has no shortage of courageous, visionary and upright men who can dare to challenge the system, be it a former president and CCM national chairman.

Calling spade a spade, Tanzania leo tuna viongozi wawili tu kwa maoni yangu ambao ni courageous, nao ni Dr. Slaa na Zitto, kwa sababu hawa wawili ndio peke yao wameonyesha ujasiri wa kusimama imara kwa manufaa ya taifa, na sio ya Chadema au yao binafsi. Hawa wengine wanajaribu tu kudandia treni, hao Butiku, Makwaiya, na Madaraka, hapana, ninasema kuwa hawana credibility waliojipa hapo juu kwa sababu in one way or another waliwahi kufaidika na system wanayoitukana sasa, cha muhimu tunchaoweza kuwakubali ni pale tu wanapogusa interest za taifa letu, so far kwenye hizo passage mbili juu hakuna walipogusa taifa, isipokuwa ni mwandishi wa article anajaribu kuwapamba kuwa ni mashujaaa, ukweli ni kwamba of nothing, ila tu kama kawaida wanajaribu ku-play na uwezo mdogo wa wananchi ku-comprehend mambo ya siasa za taifa letu, tabia ambayo sasa inaazna kugeuka kuwa kama sheria, lakini hatimaye wananchi tumeanza kuamuka mashujaa wa taifa hili so far ni Zitto na Dr. Slaaa tu!


3. In the book titled: 'CCM na mustakabali wa nchi yetu,' which literally means, 'CCM and our nation's destiny', deals blow after blow to the immediate former president and CCM national chairman, Benjamin William Mkapa. The authors in unison condemn the era of the former party national chairman; his avoiding to meet and talk over issues of interest to the party and nation as a whole; his disdain of his peers and the sudden usurpation of party by a class of filthy rich people, often with questionable character. The chairman's behaviour gave rise to a culture of gossip and bad mouthing among the top brass of the party, signifying a major rift within the party.

Mwalimu, hakuwahi kukaa chini na kujadili interest za CCM, na wanachama wake, siku zote ilikuwa wanachama kukubali tu anayosema yeye Mwalimu, and that is exactly what Mkapa did sasa hawa kina Butiku, wanajaribu kumshambulia Mkapa kwa tabia ambayo aliirithi toka kwa Mwalimu? I mean no question Mwalimu was the greatest, lakini haina maana kuwa alikuwa malaika, na ukiangalia kwa undani zaidi matatizo wanayolilia hawa kina Butiku, yalianzia kwa Mwalimu, na hili la kutowasikiliza wanachama wa CCM, linaaniza kwake Mwalimu, sio Mkapa, halafu walihitaji ku-define kwa maelezo zaidi kama kweli hilo ni tatizo la taifa zima.

Mambo ya gossip, aliyaanzisha Mwalimu from Kambona, Kawawa, Mwinyi, Mzee Masha, mpaka Malecela, hawa ni victims first hand wa hiyo tabia mbaya ya gossip ya Mwalimu, na Butiku anajua sana hili maana ni yeye aliyehusika sana na kuwapiga vita hawa kwa kupeperusha ujumbe kutoka kwa Mwalimu, sasa ninam-hold responsible Butiku zaidi kwenye hawa walioandika hiki kitabu kwa sababu yeye anajua better kuliko hao wengine aliowavuta tu kama mabehewa, na huenda nao pia hawajui machungu yake ni kutokana na kukosa mlo. Kama alikuwa hapendi hizo tabia za ubabe wa Mkapa na gossip, basi angeanza kukasirika na Mwalimu kwanza, maana ni huko ndiko Mkapa, alikoyatoa hayo, na Butiku anajua kuwa siku alipokwenda kumuomba Malecela,amsaidie mgombea wake wa urais alimwambia exactly ninayoyasema kuwa ni mnafiki mkubwa na hakujibu kitu. Mkapa, tunamlaumu kwa kujilimbikizia mali nyingi kwa muda mfupi sana, na kama magazeti yetu yalivyosema tunadhani kuna sheria zetu zimevunjwa somewhere kwenye yeye kujilimbikizia mali, otherwise hakuna lolote baya jipya alilolianzisha, mengine yote aliiga kwa Mwalimu, period!

4. The authors also question why the ruling party under former chairman Ali Hassan Mwinyi silently abolished the Arusha Declaration, including its leadership code of conduct, which resulted into free-wheeling accumulation of ill gotten wealth, with the rich vying for leadership positions through bribery, deceit and other dirty tricks.

Azimio La Arusha, had to go anyways kwa sababu halikuwa na maana yoyote kwa kuruhusu viongozi wachache kujilimbikizia mali, huku wengi wanyonge kina Sozigwa na Manuye, wakifa nzala, it was just unfair ndio maana viongozi wetu walipopata the first opportunity, bila ya Mwalimu aliyekuwa akiwalazimisha ishus kuwepo, wakalivunjilia mbali. Hiyo ilikuwa dalili tosha kuwa wanachama wa CCM wangekuwa wanapewa nafasi na Mwalimu, wasingekubali mengi aliyokuwa akiwalazimisha tu bila ridhaa zao, na kuvnjwa kwa Azimio ni mfano tosha wa hilo la kuvutwa kama magunia, Please hatulihitaji tena hilo Azimio, kwenye sheria zetu tunazo sheria za kutosha katika kulinda madili ya viongozi tatizo ni enforcement, sio maazimio zaidi ya Arusha, NONESENSE!

5. The book accuses Mkapa of entertaining hearsays and gossips which led to divisions within the top hierarchy of the party which was once revered and respected across Africa and the world. The party leadership sometimes trampled on members' rights by changing important procedures and regulations. When those disenchanted asked for clarification, during meetings, they got jeered off by other members.


Here we go Mwalimu, ndiye aliyekuwa kiongozi wa kwanza kubadilisha the rules of the game, Kikwete alishinda, lakini yeye akampitisha Mkapa, 1995, sasa Butiku anaweza kusema alikuwa hajui haya? Kama kweli Butiku ana uchungu huo mpaka wa kuandika kitabu ilikuwaje akawa RC wa Musoma under Mkapa, bila ya kupiga kelele kuwa hawezi kufanya kazi kwenye utawala usiokuwa wa halali uliopitishwa na Mwalimu? Baaada ya u-RC akaingia Nyerere Foundation, ambako pia akiwa mshikaji wa Mkapa, tena wa karibu akaendelea kutanua tu na mahela chungu nzima ya taifa ambayo hayakuwa yakiripotiwa mahali popote waka kuombewa kwenye bajeti, mbona hakupiga kelele? WHY NOW? Baaada ya kuachwa nje na msaaaada kukatwa kule Foundation sasa ndio Mkapa amekuwa mbaya?

6. The book also mentions the fraudulent deletion of immediate former CCM vice chairman for the Mainland John Malecela, from the list of presidential aspirants in 2005 just because the former prime minister had not conferred with Mr Mkapa as chairman prior to his picking presidential nomination forms.

Hili lilianzia na Mwalimu, wasimsingizie Mkapa, we all know this hivi kuna mbongo anayehitaji kuandikiwa kitabu kuwa hivi vita dhidi ya Malecela, vilianzishwa rasmi na nani kati ya Mkapa na Mwalimu, na Butiku mwenyewe akishiriki tena kwa karibu sana kumpiga vita Malecela? I mean pleaseee!

7. The veteran CCM members and Mwl. Nyerere's son question CCM�s loss of vision and direction in terms of formulating the five years development rolling plan, which was last done in 1981, hence impacting negatively on the part of the government. The authors wonder whether the party is any longer in charge and holding the government accountable. Because of lack of a visionary leadership that sidelined some critical voices, CCM under Mkapa did sow seeds of racial discrimination especially during internal party nominations and primaries. The authors cite examples of former Prime Minister Dr Salim Ahmed Salim, who was opposed by some Zanzibar caucus members as being of Arab origin, and having played a role in the slaying of former Zanzibar President Abeid Karume.

Again, kama CCM ilikuwa na vision under Mwalimu, akisaidiana na Butiku then why as a nation tuko hapa tulipo? Ni lini CCM iliwahi kuwa na vision? Ukweli ni kwamba haikuwahi hata siku moja isipokuwa ilikuwa ina shamiri kiutokana na time, sasa time has changed ndio maana hata Mwalimu aliondoka bila kusema ukweli kinachomuondoa, maana alishagundua kuwa time has changed na kwamba sasa wananchi wameanza kuamuka haitakuwa rahisi tena kuwadanganya, na that is exactly kinachotokea sasa. Kama ni kuwa-silence viongozi waulizaji maswali wao wanajua kuwa Jumbe, Seif Bakari, na Seif Hamadi walitolewa uongozi kinyemela na Mwalimu ili kukwepa hoja zao za msingi kwa taifa, sasa leo wanashangaa Mkapa kuzirudia tabia hizo? Salim, alishakataliwa na wajumbe wa visiwani mwaka 1985, kwa sababu hizo hizo alizokataliwa nazo majuzi, sasa hawa wanashangaa kitu gani kama sio unafiki?

8. It condemns a new culture of stage managed public rallies convened by the party and often addressed by senior party leaders including the national chairman and secretary general, to issue party membership cards to opposition cross-overs and wonders whether such people share a strong belief in CCM's ideals.

Another big lie, hizi tabia zina tofauti gani na kukimbiza mwenge? Exactly faida za kukimbiza mwenge ni zipi? Na yale mambo ya halaiki Butiku kweli aanaamini kuwa sisi wanachi tulikuwa tunayataka au kuyapenda? Mambo ya kusindikiza rais airport yalianzia na nani? Mambo ya mikutano siku za sherehe za wakulima na saba saba yalianzishwa na nani? Yana tofauti gani na hayo wanayolilia kina Butiku?


9. preside over the writing of a new constitution to replace the one party 1977 Constitution. The authors advise Mr Kikwete to take the leadership in enacting a new constitution that will also reduce excessive powers of the presidency, which has routinely been abused by some individuals to advance personal rather than national interests while at Ikulu.

This is it, hii ndio point muhimu katika kitabu chao kizima, walipaswa ku-dwell on hii point tu, mengine yote ni uongo wa mchana kweupee maana wanakwepa responsibility tu kwa kumsingizia Mkapa, mambo ambayo wanajua kuwa aliyaiga tu toka kwa the greatest ever Mwalimu, Mkapa tunamlaumu kwa kulimbikiza mali nyingi kwa muda mfupi sana, lakini the rst aliyaiga tu toka kwa Mwalimu, otherwise our national mashujaa wanabaki kuwa Zitto, na Dr. slaaa, kwa kusimamia hoja muhimu kwa wananchi wote bila ya kujali nafsi zao, wala vyma vyao vya siasa, na in one stike wameweza kubadili mambo mengi ambayo hayatarudiwa tena na viongozi wetu, kwa mfano ya kwenda kusaini mikataba ya taifa mahotelini, na mikataba ya uhuni wa madini, Butiku na wenziwe ukweli ni kwamba no credibility, kama vile ambavyo tunshindwa kumpa heshima Mtikila.

Butkiu na wenziwe walitakiwa kuki-dedicate kitabu chao kizima kwenye ishu ya mwisho ya uchache wa katiba yetu, ni ishu ambayo ni nzito na ni pana sana, kuliko kupoteza muda wao mwingi na songi songi, yaani udaku, hatuwezi kuanzisha sheria za kuzuia gossip! In the absence ya mashujaa wa taifa ni lazima tuwe macho na wale wanaoutaka ushujaa kwa njia za uchwara, ndio maana ninawaita Zitto na Slaa, kuwa watakwenda chini ya historia yetu kama mashujaa wa kweli kwa ku-strike at the right time, na kwa kuweka their everything on line bila kuogopa, huo ndio ushujaaa, sio mpaka ukose mlo! Ninarudia kuwa Mwalimu, was the greatest, lakini matatizo wanayoyasema kina Butiku, kwanza sio ya taifa, na pili yalitokea kwa Mwalimu, ambako Butiku alikuwa the right hand man, sio Mkapa.

Wa-Tanzania tumechezewa vya kutosha, sasa tunasema enough!

Wakuu great debate na tuendelee kumkoma nyani hapa mpaka kileleweke!
 
Mkuu, Mkapa aliiga kila kitu kwa Nyerere sasa ilikuwaje Mwalimu alikuwa ameshaanza kuonyesha kupinga sera za Mkapa? Je Mkapa aliiga hata kujilimbikizia mali, kusaini mikataba mibovu, kufanya biashara akiwa Ikulu kwa Mwalimu Nyerere!?

Nimeshasema mara nyingi hapa ukumbini Nyerere hakuwa perfect hata yeye mwenyewe aliwahi kutamka hivyo, lakini kumlinganisha na fisadi Mkapa, kwa maoni yangu Nyerere ni malaika bila wasi wasi wowote. Ufisadi alioufanya Mkapa kwa miaka 10 aliyokaa madarakani huwezi kabisa ukaulinganisha na mabaya yote aliyoyafanya Nyerere alipokuwa madarakani kwa miaka 24
 
Mkuu FieldMarshall, naona Umeamua kumkoma Nyani bila huruma.
Nakupa Tano Mkuu.

Mtu anayeandika kitabu kwa lengo la kumkomoa mtu, na si kwa lengo la kuipa faida jamii, sijui anakuwa anakusudia nini haswa!
Kibaya zaidi pale mlipokuwa marafiki ulikuwa huyaoni matendo yake, leo hii mmetofautiana au kukorofishana ,mtu unaanza ooh huyu yuko hivi, mara ooh fulani alifanya hivi. mambo gani!
 
Mkuu, Mkapa aliiga kila kitu kwa Nyerere sasa ilikuwaje Mwalimu alikuwa ameshaanza kuonyesha kupinga sera za Mkapa? Je Mkapa aliiga hata kujilimbikizia mali, kusaini mikataba mibovu, kufanya biashara akiwa Ikulu kwa Mwalimu Nyerere!?

Nimeshasema mara nyingi hapa ukumbini Nyerere hakuwa perfect hata yeye mwenyewe aliwahi kutamka hivyo, lakini kumlinganisha na fisadi Mkapa, kwa maoni yangu Nyerere ni malaika bila wasi wasi wowote. Ufisadi alioufanya Mkapa kwa miaka 10 aliyokaa madarakani huwezi kabisa ukaulinganisha na mabaya yote aliyoyafanya Nyerere alipokuwa madarakani kwa miaka 24

Hoja yako dhidi ya Legacy ya 3 Tanzania especially Ben imejibiwa kiustadi sana na kwa kuzingatia maslahi ya nchi yetu; itoshe kusema kuwa pengine mwenzetu una agenda ya siri dhidi ya Mkapa maana 90% wamekuwa wakweli na hawa waandishi watatu pamoja wewe Bubu usiyetaka kusikia; We do acknowledge all Ben's disappointments to TZ but tunatambua pia kuwa naye ni muhanga wa msingi tuliojijengea watanganyika the Tz.

Kwa zama za Mwalimu na maono yake kwake Utajiri halikuwa jambo la msingi kabisa tofauti na watu kama Oscar na ndg yake Wambura kibaya zaidi mambo aliendesha ktk utaratibu wa imani hiyohiyo,na ili udumu ktk siasa ilikuwa ni wajibu wako kufa na tai shingoni,lakini niseme tu kuwa mwalimu hakuwa na masikini kwani kwa elimu yake especially kwa zama zile + maisha ya utawala aloishi toka 50s-90s ilitosha kwake kuridhika. Mkapa mwenye watoto wawili ambaye si mwanasiasa wa aina ya Mwalimu kimaono ndiye kiongozi ambaye alishawahi au kuthubutu kuunga mkono mageuzi ya kiuchumi kabla ya vita ya kagera(kumbuka kuwa mwalimu alichukizwa na maono hayo ya akina Mkapa na ndio safari yake Nigeria)aliamini kuwa umasikini si sifa ya kiongozi bora; sisi tunasema hapo alikosea na ametufadhaisha lakini pia ni wajibu wetu sasa kutambua kuwa si kila alilosema mwalimu ni dira ya Tanzania yenye Neema ,vivyo hivyo kwa Mwinyi,Mkapa na one day JK maana ni kwa njia hiyo tu historia yetu itazidi kuimarika na kuijenga nchi yetu; hoja yetu hapa ni kwanini Jose B,Makwaiya na Mada waandike kitabu kwa ajili ya mtu mmoja tu?? Hilo halihitaji pHD Bubu,why??? Ni haki yetu watz kuifahamu historia yetu,viongozi wetu na chimbuko lao lakini kuwepo na muunganisho; Mwalimu always atadumu mioyoni mwetu kwa % 70 + lakini pia ni haki ya vizazi kujua kuwa mwalimu atadumu % 30 -; na ndicho tunachotaka kurithi toka kwa waandishi hawa especially Butiku.

Kila mtu ana mazuri yake lakini ni dhahiri ana mabaya yake,why Mkapa anazungumzwa ktk mabaya yake tu daima hasa na wewe Bubu lakini hamuipi nafasi chanya ya Mkapa ktk jamii ?? Lakini hata kama huyu bwana ni the dirtiest Presidaa ever kwa nchi kama asemavyo Jenerali basi kwanini Nyerere avuliwe dhambi ya kutupatia rais wa aina hii,na leo unataka akapumzike amani huko aliko!!!!

Ben was in Mwal.'s cabinet,Mwinyi also but JK wasnot; Now we have a president who is Mwinyi's product,2premiers also but still some of Nyerere's products are stil there; some of them ni matajiri kabla ya Mkapa,lakini wako wapi leo wazao wa Oscar Kambona??? Nchi hii ni ya nani Bubu??

Hakuna ambaye anaweza kujinasua kutoka ktk connection ya Mwalimu kwani hata JK akiwa anapata unaibu M/kiti wa CCM alikuwa Mwalimu hivyo unaweza kuona hawa wote ni product yake ila wewe na mimi tunayohaki ya kujifunza toka kwao kwa namna ya walivyojipambanua ktk mamlaka walizoziongoza.

Hatujawahi kuwa maraisi wa nchi hivyo ni vema tujiandae tukitambua kuwa Mkapa always ni Mkapa,Mwinyi,JK ila ni dhahiri
kuwa hata kama Mkapa amenilimbikizia mali,Kikwete kumlinda na Mwinyi ruksa ukweli unabakia palepale " Kuna urithi wa Mwalimu viongozi wetu kama si pia basi meno na si meno angalia nywele lakini ni lazima wamerithi kimoja au viwili toka kwa mwalimu"

Alikiri" Siwezi tena kuifanyia jambo jingine Tz zaidi kile nilichofanya kwa 24 yrs as president hata kama watanipa 10 yrs ingine" Siku alipokuwa anawaaga jumuiya ya Madola alipohojiwa na wana habari.

Ninakutakia heri na usikivu mwema Bubu a.k.a Yuri Orbida (The long wait -TVT)
 
Mkuu, Mkapa aliiga kila kitu kwa Nyerere sasa ilikuwaje Mwalimu alikuwa ameshaanza kuonyesha kupinga sera za Mkapa? Je Mkapa aliiga hata kujilimbikizia mali, kusaini mikataba mibovu, kufanya biashara akiwa Ikulu kwa Mwalimu Nyerere!?

Nimeshasema mara nyingi hapa ukumbini Nyerere hakuwa perfect hata yeye mwenyewe aliwahi kutamka hivyo, lakini kumlinganisha na fisadi Mkapa, kwa maoni yangu Nyerere ni malaika bila wasi wasi wowote. Ufisadi alioufanya Mkapa kwa miaka 10 aliyokaa madarakani huwezi kabisa ukaulinganisha na mabaya yote aliyoyafanya Nyerere alipokuwa madarakani kwa miaka 24

Hoja yako dhidi ya Legacy ya 3 Tanzania especially Ben imejibiwa kiustadi sana na kwa kuzingatia maslahi ya nchi yetu; itoshe kusema kuwa pengine mwenzetu una agenda ya siri dhidi ya Mkapa maana 90% wamekuwa wakweli na hawa waandishi watatu pamoja wewe Bubu usiyetaka kusikia; We do acknowledge all Ben's disappointments to TZ but tunatambua pia kuwa naye ni muhanga wa msingi tuliojijengea watanganyika the Tz.

Kwa zama za Mwalimu na maono yake kwake Utajiri halikuwa jambo la msingi kabisa tofauti na watu kama Oscar na ndg yake Wambura kibaya zaidi mambo aliendesha ktk utaratibu wa imani hiyohiyo,na ili udumu ktk siasa ilikuwa ni wajibu wako kufa na tai shingoni,lakini niseme tu kuwa mwalimu hakuwa na masikini kwani kwa elimu yake especially kwa zama zile + maisha ya utawala aloishi toka 50s-90s ilitosha kwake kuridhika. Mkapa mwenye watoto wawili ambaye si mwanasiasa wa aina ya Mwalimu kimaono ndiye kiongozi ambaye alishawahi au kuthubutu kuunga mkono mageuzi ya kiuchumi kabla ya vita ya kagera(kumbuka kuwa mwalimu alichukizwa na maono hayo ya akina Mkapa na ndio safari yake Nigeria)aliamini kuwa umasikini si sifa ya kiongozi bora; sisi tunasema hapo alikosea na ametufadhaisha lakini pia ni wajibu wetu sasa kutambua kuwa si kila alilosema mwalimu ni dira ya Tanzania yenye Neema ,vivyo hivyo kwa Mwinyi,Mkapa na one day JK maana ni kwa njia hiyo tu historia yetu itazidi kuimarika na kuijenga nchi yetu; hoja yetu hapa ni kwanini Jose B,Makwaiya na Mada waandike kitabu kwa ajili ya mtu mmoja tu?? Hilo halihitaji pHD Bubu,why??? Ni haki yetu watz kuifahamu historia yetu,viongozi wetu na chimbuko lao lakini kuwepo na muunganisho; Mwalimu always atadumu mioyoni mwetu kwa % 70 + lakini pia ni haki ya vizazi kujua kuwa mwalimu atadumu % 30 -; na ndicho tunachotaka kurithi toka kwa waandishi hawa especially Butiku.

Kila mtu ana mazuri yake lakini ni dhahiri ana mabaya yake,why Mkapa anazungumzwa ktk mabaya yake tu daima hasa na wewe Bubu lakini hamuipi nafasi chanya ya Mkapa ktk jamii ?? Lakini hata kama huyu bwana ni the dirtiest Presidaa ever kwa nchi kama asemavyo Jenerali basi kwanini Nyerere avuliwe dhambi ya kutupatia rais wa aina hii,na leo unataka akapumzike amani huko aliko!!!!

Ben was in Mwal.'s cabinet,Mwinyi also but JK wasnot; Now we have a president who is Mwinyi's product,2premiers also but still some of Nyerere's products are stil there; some of them ni matajiri kabla ya Mkapa,lakini wako wapi leo wazao wa Oscar Kambona??? Nchi hii ni ya nani Bubu??

Hakuna ambaye anaweza kujinasua kutoka ktk connection ya Mwalimu kwani hata JK akiwa anapata unaibu M/kiti wa CCM alikuwa Mwalimu hivyo unaweza kuona hawa wote ni product yake ila wewe na mimi tunayohaki ya kujifunza toka kwao kwa namna ya walivyojipambanua ktk mamlaka walizoziongoza.

Hatujawahi kuwa maraisi wa nchi hivyo ni vema tujiandae tukitambua kuwa Mkapa always ni Mkapa,Mwinyi,JK ila ni dhahiri
kuwa hata kama Mkapa amejilimbikizia mali,Kikwete kaamua kumlinda na Mwinyi alitoa ruksa ukweli unabakia palepale " hawa wote wanaandamwa,Kuna urithi dhahiri wa Mwalimu kwa viongozi wetu kama si pia basi meno na si meno angalia nywele lakini ni lazima wamerithi kimoja au viwili toka kwa mwalimu"

Alikiri" Siwezi tena kuifanyia jambo jingine Tz zaidi kile nilichofanya kwa 24 yrs as president hata kama watanipa 10 yrs ingine" Siku alipokuwa anawaaga jumuiya ya Madola alipohojiwa na wana habari.

Historia itajiandika kwa yenyewe pasipo kushurutishwa na ghiliba,chuki,njaa na husuda. Abrahamu Lincoln ndiye the best man mpaka leo kwa wamarekani lakini Washington anebakia kuwa the founder. Nyerere pia atabaki ktk line hiyo time will tell Bubu.
Ninakutakia heri na usikivu mwema Bubu a.k.a Yuri Orbida (The long wait -TVT)
 
Back
Top Bottom