Analazimisha watoto wote wasome shule moja wakati si yeye anayetoa huduma

Princess Zara

Senior Member
Dec 17, 2016
124
314
My best friend yuko dilemma.

Ameolewa mwaka jana mwanzoni yeye ana mtoto mmoja wa kiume miaka 5 alimpata katika harakati za ujana na shemeji ana mtoto mmoja wa kike ana miaka 6 naye alipatikana katika harakati hizo hizo; jumla watoto 2(na ana ujauzito wa miezi 5 sasa hivi).

Sasa tangu awali, baba wa mtoto wake anamhudumia mwanae kila kitu na walikubaliana na mumewe kuwa baba mtoto ataendelea kumhudumia mwanae maana uwezo anao na vyuma si mnavijua jamani

Mtoto huyu anasoma shule ya gharama kidogo(ukilinganisha na kipato cha kawaida cha mtanzania). Ndo shule anasoma tangu nursery hadi yuko primary sasa halikadhalika mtoto wa shemeji naye anasoma english medium nzuri tu lakini sio ya gharama kama ile ya kahandsome ka shogaangu.

Sasa mwezi uliopita shemeji kasema watoto wale ni wa familia moja lazima wasome shule moja. Rafiki yangu akasema sawa basi uongeze ada wakasome kule anakosoma huyu wangu sababu it is a better school. Akasema hapana watahamia anaposoma mwanangu akakubali kishingo upande.

Baba mtoto kufikishiwa taarifa akasema hapana, namsomesha mwanangu hivyo nina mandate ya kuamua anasoma wapi.

Kuambiwa shemeji akapanick akatema mitusi ya kutosha(sikuwepo sina uhakika) akamshutumu kutembea na huyo ex wake. Katika ugomvi akasema "hata Mama K aliniambia unaliwa tu huyo mwanaume wako wa Zamani."

Mama K ni mzazi mwenzie Shemeji baada ya uchunguzi wetu FBI tumegundua mama K ndo kashinikiza watoto wasome shule moja na hii ni baada ya yeye kuhoji iweje mwanae anasoma a cheaper school than yule mwingine? Alipoambiwa yule analipiwa na babaake ndo akamwaga sumu kibao.

Ninavyoongea hapa beste kamleta mwanae kwangu leo siku ya pili analala hapa anataka amrudishe mwanae kwa mamaake, mara anasema anavunja ndoa(najua ni hasira maana ana tumbo tayari).

Sasa akibaki na kale katoto ka kambo pekee si atakatesa tu kwa hasira maana bora wakiwa wawili.

Nimshauri nini arudi kwa mumewe aihandle hii situation? Mama Zara kashanichimba mkwara "Zara unashiriki kuvunja ndoa ya mwenzio".
 
Huyo baba K hajitambui, badala ajenge ukaribu na mwanaume mwenzake anaweza kumpiga tafu na kumtengenezea channel nzuri ya maisha mana kama kugongewa mke wake atagongwa tu na huyo mume mwenzake hata jirani pia aache ujinga.
 
Mambo haya ni magumu busara tu ndio inahitajika hapo ila huyo dada amsikilize mumewe kuoa single mother ni kipaji cha pekee nampongeza mwanaume mwenzangu kwa kukaza roho aachane na kusikiliza baba watoto aliyemtenda akamtelekeza kama huyo jamaa anataka achukue mtoto wake apambane na hali yake ni anajifanya ana hela ya kulipia shule za gharama!
 
Hivi kwanini huyo mwanamke alikubali kuolewa na mwanamme ( baba k) ambaye hana akili kiasi icho ? huyo mwaunaume ni bogus
 
Huyo baba K ndiyo fala yani mimi karo ya mwanangu nilipe mimi na umemkuta tayari anasoma shule nzuri leo eti nimuhamishe shule nyingine kisa mbwiga kasema?

Alipokuwa anamuoa alijua kabisa ana mtoto mwenye baba yake na anamhudumia mwanae so asilete ungese.
 
Huyo baba K ndiyo fala.
Yani mimi karo ya mwanangu nilipe mimi na umemkuta tayari anasoma shule nzuri leo eti nimuhamishe shule nyingine kisa mbwiga kasema?
Alipokuwa anamuoa alijua kabisa ana mtoto mwenye baba yake na anamhudumia mwanae so asilete ungese...
Huyo mbwiga ndo anaishi nae lakini baba mtoto hawezi kuishi na mwanae maana nae ni wale wakaka wa mjini umri mkubwa bado bachelor kutwa kuingia home na videmu tofauti daily hayo si mazingira ya kulelea mtoto kwahiyo amshukuru baba K kwa kumpa mwanae mazingira ya kifamilia.
 
Huyo mbwiga ndo anaishi nae lakini. Baba mtoto hawezi kuishi na mwanae maana nae ni wale wakaka wa mjini umri mkubwa bado bachelor kutwa kuingia home na videmu tofauti daily. Hayo si mazingira ya kulelea mtoto kwahiyo amshukuru baba K kwa kumpa mwanae mazingira ya kifamilia.
Huyo baba K atakuwa na inferiority complex, anahisi kushushwa kwa mtoto wa mwenzake kusoma shule ya gharama zaidi ya mtoto wake hakuna mtu ambaye anataka kupangiwa kuhusu elimu ya mwanaye wakati anayeigharamia ni yeye mwenyewe angekuwa anaenda kwa jamaa kufanya vurugu au kumfuata fuata mtoto hapo ningesema jamaa ana matatizo, ila yeye kamchagulia mwanae shule bora sasa mwenzake ananuna nini. Kama anataka ampeleke mwanaye kama uwezo hana atulie tu
 
Madhara ya kula makombo ndiyo hayo!mwanaume usipooa bikira ujiandae kwa lolote na ex s
 
Duh Hii iko so complicated!! Kwanini huyo mwanamke alikuja na mtoto kwenye ndoa? Si angemuacha kwa bibi yake au Kwa huyo Kidume? hii italeta shida saaana, halafu huyo boya nae atakua bado anakula Mama K off course hawezi kuacha!

Suluhisho, maisha yenu au mambo ya ndani yabaki ndani, hizi biashara za kuongea kila kitu hadi Kwa RC ni ujinga
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom